#COVID19 Al-Jazeera: President Magufuli claims, without evidence, that vaccines against COVID-19 are dangerous

#COVID19 Al-Jazeera: President Magufuli claims, without evidence, that vaccines against COVID-19 are dangerous

Siku zote Aljazeera ni wachonganishi: media houses nyingi zimeripoti athari ambazo waliopata chanjo wamezipata including VIFO, na technical team nyingi zimekiri kuwa uwepo 20% or so wanaopata athari ni jambo dogo, why Magufuli aonekane kituko wakati akisema ukweli. Natamani kufanya compilation ya unexpected outcome ya vaccination, none the less, haiwezekani u develop chanjo na ndani ya miezi sita ianze kutumika, definately yale mabaya ya chanjo yanakuwa hayajajionesha na kupatiwa ufumbuzi
 
Ametumia neno inawezekana na mfano katolea chanjo ya kansa ya kikazi
 
Mkuu kuhusu data, zimewasaidiaje USA, UK, Italy, France etc. Je, vifo nchini mwao vimepungua kwa sababu ya kuweka data? Au unaweka data kuweka hofu tu?
Mbona Data za kipindupindu na ukimwi tunaweka na tulikuwa tunasema au vitisho tu?? Data zinasaidia kujuwa mko wapi na mnaenda wapi je hatua mnazochukuwa zinasaidia au hapana ili kurekebisha makosa. Nchi duniani zili sign makubaliano ya kuwa na uwazi katika mambo kama haya na sababu kuu ili kumfanya yule ambaye hajaathirika kuchukuwa hatua. Kwenye mtaa kama kuna mtu kavamiwa au anaibiwa na vibaka mara nyingi atawaambia jirani zake jamani kuna vibaka wanakuja kwangu hebu kuweni makini au jamani kuna watu wanakuja kugonga mlango lakini ni matapeli ili tahadhari iwepo sasa kila mtu akikaa kimyaa ngoja na jirani limpate tusichekane haileti maana. ndio maana kuweka Data wazi ili watu wajue serious ya janga.
 
Watulie hatutaki chanjo, hizo chanjo nyengine ni hormones [emoji2359]
Bahati nzuri hujafikwa. Not infected neither affected. Siku ikikufika utacomment kwa kutumia mdomo na akikili siyo kinyeo.
 
Siku zote Aljazeera ni wachonganishi: media houses nyingi zimeripoti athari ambazo waliopata chanjo wamezipata including VIFO, na technical team nyingi zimekiri kuwa uwepo 20% or so wanaopata athari ni jambo dogo, why Magufuli aonekane kituko wakati akisema ukweli. Natamani kufanya compilation ya unexpected outcome ya vaccination, none the less, haiwezekani u develop chanjo na ndani ya miezi sita ianze kutumika, definately yale mabaya ya chanjo yanakuwa hayajajionesha na kupatiwa ufumbuzi
Waziri mkuu wa UK kasema jana wazi kuwa na chanjo na matokeo ni mambo mawili tofauti, amesema hivi, ikifika kati ya Feb tutapata picture nzuri huko tunakoenda kwa maana tukiona level ya wagonjwa mahospitalini inashuka na chanjo zikiwa zinaendelea itatupa picha halisi ya huko mbeleni ili by March 8 watoto wetu warudi mashuleni. chanjo zimeanza kutolewa inachukuwa muda kufikia watu wote haya ndio maneno aliyosema. Sasa chanjo haikufanyi kutopata corona ila hutaumwa itakuwa kama mafua ya kawaida tu. Case ya Rais wetu siku ikifika halafu chanjo wamechoma sana lakini bado Hosp zinajaa hapo Magufuli atakuwa kashinda lakini sasa Data zikija kuthibitisha kuwa kila chanjo zinavyotolewa number hosp zinashuka wagonjwa wanapungua hapo ndio aibu yetu tuje tuanze na mambo ya kinadharia tu hawa hawatupendi basi hawataki tuzae.....bla bla
 
Rais ashauriwe aache kuropoka. Hivi mtu gani asiye na aibu? Sasa hivi watanzania wote tunaonekana machizi, majuha, mahayawani yasiyojielewa sababu ya upumba.vu wa mtu mmoja
 
Nimemsoma Magufuli akizungumzia ujio wa Corona mpya nchini kwanz amekiri ipo akidai imeletwa na watu walioenda kutafuta chanjo nje, hapa naamini lile tamko lake la kusema Corona hakuna Tanzania ndio kalifuta rasmi.

Lakini pia amekazania watanzania wasitumie kinga kwasababu wazungu hawatupendi, hiyo kinga anadai inaweza kusababisha tusizaliane kwa mtazamo wake anadai wazungu hawapendi tuzae.

No research, no right to speak; huyu mtu aliemtumbua yule mtoto wa Malecela NIMR kwasababu alitimiza majukumu ya kazi yake kwa kutoa taarifa ya kitaalamu nitamwamini vipi kwenye hii sababu yake ya wazungu hawatupendi? sio yeye ndio hapendi matokeo ya kazi za kitaalamu?

He is not a doctor or a pharmacist, but kwanini hupenda kuingilia taaluma za watu kwa kutoa majibu mepesi kwenye maswali ya msingi? hapa nikisema yeye ndio hawapendi wazungu ndio maana huwasingizia vitu asivyo na uthibitisho navyo nitakuwa nakosea?

Nikiri hapa, mtazamo wa Rais wetu kwenye hili jambo ni wa kushangaza na kusikitisha, sasa kama Rais hataki watu wake wajikinge kwa chanjo ambayo naamini ametumia hisia kusema hiyo chanjo sio salama kwa raia, na kusisitiza watu wajifukize.

Sasa huku kujifukiza kulithibitishwa na maabara ipi hapa kwetu wakati maabara ile ya mwanzo iliyopima mapapai walidai ilikuwa mbovu? na mtaalamu wake akatumbuliwa?
hivi hawa waliokaribu nae kwanini wasitusaidie kutu.... tuanze upyaaaaaaaaaaa
 
chanjo zinavyotolewa number hosp zinashuka wagonjwa wanapungua hapo ndio aibu yetu tuje tuanze na mambo ya kinadharia tu hawa hawatupendi basi hawataki tuzae.....bla bla
Kuna hoja ya msingi na ya kitaalam juu ya chanjo: ni pale ambapo wanapewa chanjo watu kadhaa, 10% wanakufa immediately, hii ndo hoja ya msingi. Hii ni kielelezo kuwa chanjo haijawa na sifa lengwa, wengine wamesema kuwa baada ya kupewa chanjo walitest +ve kwa HIV, si taarifa njema hizi na haya ndo mambo ya msingi ya kuzungumzia badala ya ;
Wanataka kutupunguza so, so, so
 
Mabeberu na wanaotuonea husuda wameiandika na kuitangaza sana hii habari!Washington post, AFP,BBC.RFA,.Hapa kazi tu.Wahenga walisema mti wenye matunda hurushiwa mawe!
 
Nilikua nasoma hii post nikisubiri kwenye kile kipande alichosema "wizara ya afya usikubali chanjo bila wao kama wataalamu kujiridhisha"

Uko wapi weledi wa uandishi hapo mkuu?
 
Kwenye hii mapambano ya Covid19, probably makosa pekee ya Magufuli ni kuficha data na kuruhusu wageni wavuke mipaka yetu na kuingia nchini bila haja ya kuonyesha negative test certificates.

Mtu hahitaji kuambiwa na Magufuli avae barakoa au anawe mikono kwa sabuni na kusanitize as many times as possible

Hakuna success story yoyote kutoka kwa Nchi zilizo impose lockdowns, kufunga mipaka na hata hizo chanjo zenyewe

Utalock down nchi au miji until when? Unalock down then unafanya nini - kusubiri beberu apate tiba then akupe msaada?
Hakuna anayepinga Magufuli anayethubutu kujibu hizi hoja. Ni makelele tu yasiyo na mpangilio na kutusi na kushutumu Rais. Mpaka sasa bro Magu ndiye kiongozi pekee aliyeweza kui-outstand corana hapa duniani.
 
Mkuu kuhusu data, zimewasaidiaje USA, UK, Italy, France etc. Je, vifo nchini mwao vimepungua kwa sababu ya kuweka data? Au unaweka data kuweka hofu tu?
Msingi wa hizo data na vinavyoitwa tahadhari dhidi ya corona lengo lake kubwa ni kujaza watu hofu na hivyo kuufanya ugonjwa kuendelea kuwa tishio. Lengo ni kuendelea kustimulate demand ya chanjo kwa njia yoyote ile.

Wanaotaka chanjo wajiorganize waagize chanjo zao maisha yaendelee. Dundur heads wengi wanaotaka chanjo hawajui hata hizo pesa za kununulia hiyo chanjo zitatoka wapi.

Wiki chache tu zijazo hali itatulia kama awali. Wataleta kirusi kipya then with time tutakuwa immune tena. Acha tuendelee kucheza ngoma yetu nao wacheze ya kwao.
 
..sasa kwanini mitishamba tunayotumia serikali haiuzi kwa mabeberu ile tuongeze mapato?

..badala yake bwana mkubwa anatushauri tulime sana ili tuwauzie walioko kwenye lockdown.
Mabeberu wanapinga tiba yoyote ile isiyo kwenye project yao. Nikuulize swali kiongozi. Chukulia serikali ingekurupuka kuagiza chanjo kama nchi zingine. Sasa kimekuja kirusi kipya kutoka SA ambacho chanjo zilizopo hafui dafu! Ikiwa myororo huo utaendelea kama ambayo ilikwisha kuwekwa wazi miaka kibao iliyopita, je tutaagiza chanjo mara ngapi?
 
Mh. Rais kaongea kweli kabisa kama wao ni mabingwa wa kutengeneza chanjo waje na chanjo ya ukimwi kwanza. Tuko pamoja na wewe Mh. Rais piga kazi
 
uchafu tu, Madgascar watu wanapukutika sana pamoja na hayo maji anayokunywa wa Jalalani. Wasted our resources to send people and hire ATCL aircraft kwenda Madagascar kuchukua hizo takataka. Acheni papara kufanyia kazi vitu ambavyo havijawa proved ni effective. Hivi Loliondo jiwe lilienda?
Ngoja tukuwekee picha yake akipiga mafunda
 
Back
Top Bottom