TANZIA Aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar, Willson Kabwe afariki dunia

TANZIA Aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar, Willson Kabwe afariki dunia

Status
Not open for further replies.
RC Makonda alisema hawezi kufanya kazi na Mr Kabwe, itashangaza wengi endapo ataudhuria msibani. Kwani utampendaje mtu baada ya kufariki? Huo utakuwa unafiki mkubwa sana.
Kwani umesikia Makonda akisema kuwa ataenda msibani?
 
Bado liko tumaini! La ufufuo na uzima wa milele kwa waliolala katika kristo. Mungu awape amani, faraja na tumaini ndugu wote wa marehemu.
 
Unafki mbaya Sana.Malaika wa mwenge watahudhuria nakumwabia mjane"Kabwe was good man".
Siku zote kifo cha binadamu mmoja ni huzuni kwa waliosalia. Siamini kama kuna binadamu, tena aliyepewa majukumu mengi katika utumishi wake kwa miaka mingi, akakosa jambo jema katika utumishi wake.

Mungu mwenye uweza wote awajalie wanafamilia, ndugu na marafiki zake moyo wa kuyapokea mapenzi yake kwa unyofu na upole.
 
Tenda wema Duniani nawe utapata dhawabu mbingunii..

RIP..
 
haya maisha haya..mahoteli yake,,viwanja vyake , nyumba zake zote ameziacha dah,,,tutendeni mema hapa duniani mali, pesa, zote tutaziacha..R.I.P

Bigonzo umenena na lakuongezea tuna tukanana,dhalilishana na kuchezeana rafu
Kisa ushabiki wa vyama vyetu.Mwisho tunafukiwa futi sita.
 
wilson%2Bkabwe.JPG


Inadaiwa amefariki dunia akiwa nchini India alikokuwa kwa matibabu.

Aidha, inasemekana tangu siku ile wamtumbue jipu ktk Daraja la Kigamboni (Nyerere Bridge) alikuwa shocked sana alikuwa kalazwa India akipatiwa matibabu.

=====
UPDATE: Naithibitisha taarifa hii
Naomba kuuliza tu, hivi Makonda ataenda msibani? Maana marehemu alikuwa colleague wake!!!! Nauliza tu naomba nisimsemee mkulu
 
Taarifa zaweza kuwa kweli. Lkni vp hawa wezi wanapokuwa wakiondoka kwenda hatujui tunajua wakisha rejea. mara nyingi utasikia amerejea kutoka India alipokuwa kwenye matibabu!!! Kama kafa kweli. Nisomo kuwa hata tukikimbia kwenda India nakwengineko Umauti utatukuta popote kwa saa dakika na sekunde husika. Muumba habadilishi ahadi na ajali ya mtun
 
Ninaomba tuache habari za uchochezi. Huyu mzee baada ya tangazo la kufukuzwa kazi, iliwekwa bayana kwamba alikuwa ameomba kustaafu kwa ajili ya afya yake. Iweje leo tusingizie watu wameua ikiwa likuwa dhaifu kwa muda mrefu kiasi hata cha kushindwa kufanya kazi?

Ni vyema tukamheshimu Mungu jamani.
Halafu pia, mtu akifanya makosa akaumiza watu au kuharibu hatima zao makusudi kwa jinsi isiyohalali, makosa hayo hayafutwi na kifo kwa sababu kufa kwake hakubadilishi automatically maumivu ya watu aliowatesa na wengine kuwapotezea maisha. Ndiyo sababu Biblia inasema kufa ni mara moja na baada ya kufa ni hukumu. Hakuna toba wala nini baada ya kufa bali matendo ya kila mtu yanamfuata.

Lakini huyu mzee wetu hajawahi kufanya jema lolote katika maisha yake? Katika kipindi hiki, ninaomba turejee ubindamu wote. Tujengemsiba wake katika heshima ya mazishi bora. Kwamba tuache kulaumiana kwa ushabiki wa kukomoana, lakini pia tutafakari kama kuna jema lolote alilowahi kutenda huyu ndugu, na hilo ndilo tulitaje. Ni binadamu huyu.

Maisha yake baada ya hapa sasa yanakuwa chini ya Hukumu ya Mungu kwa ajili ya roho yake, na sheria za nchi kwa ajili ya matumizi ya mamlaka aliyokuwa nayo.

Ninashukuru kwa walionielewa.
Yawezejana alikuwa mgonjwa lakini siyo kweli kuwa alikuwa mgonjwa kiasi cha kushindwa kufanya kazi. Hata siku alipokuwa anasimamishwa alikuwa kazini. Na waliokuwa naye siku akisimamishwa wanasema alionesha utulivu mkubwa tofauti na walivyotegemea.

Hadithi ndefu hazisaidii lakini kilicho muhimu ni kuwa Kabwe kafariki wakati jina lake likitajwa kila mahali kuanzia magazetini, bungeni mpaka vinywani mwetu tulio wengi. Kilichokuwa kikitamkwa zaidi ni kuwa aliondolewa kazini kwa namna ambayo ni kinyume na kanuni za utumishi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom