Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sheria TFF amaliza utata: Asema Fei Toto amekosea, mkataba hauvunjwi kienyeji vile

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sheria TFF amaliza utata: Asema Fei Toto amekosea, mkataba hauvunjwi kienyeji vile

Nadhani huyu hajamaliza utata bali katoa mawazo yake kulingana na uelewa wake. Kwani wewe huyu ndo unamuamini sana ktk sheria za mpira kuliko watu wote Tanzania au Duniani waliosomea sheria za mchezo huo. Au kuwa mkurugenzi wa sheria hiyo title ndio inakufanya kuamini kuwa anajua Kila kitu
Mtu kama ameajiriwa kuwa Mkurugenzi wa Sheria na chombo kikubwa kama TFF hiyo inakupa ujumbe gani kuhusu uelewa wake wa masuala ya sheria? Huyo sio layman
 
We ndio huna akili, kununua kitu lazima muuzaje aridhie vinginevyo na vurugu. Ndio maana ya mkataba(pande mbili kukubaliana) na pia mnaweza kukubaliana kutokukubaliana(hii hutaelewa).

Kajifunze upya
Umeongea vyema ndo maana Kuna jamaa nimemwambia swala sio kipingele kinakuruhusu huwez vunja mkataba kihuni ndo maana ndege tatu za ATCL zimekamatwa kwa mambo haya haya ya kihuni, swala sio haki kwenye mkataba ufuate taratibu ndo kitu Cha muhimu
 
Ila mwamba nilikua nakuonaga una akili Ila unatabia za upiga debe, mkataba hauvunjwi lazima pande mbili zikae zikubaliane sababu Feisal alikua Mali ya Yanga, anahaki ya kuondoka lakin alichofanya ni uhuni
Mtu kutimiza sharti la mkataba wake sio uhuni, ni upeo wenu tu ndio mdogo, mnaongozwa na mahaba.

Kuna kipengele kinachombana Fei kwenye mkataba aliosaini na Yanga SC? Kama unacho weka hapa..

Fei keshafanya part yake kulingana na makubaliano yao kimkataba, sasa ni zamu ya Yanga kutimiza part yao, wakigoma kama walivyofanya, Fei ana uwezo wa kwenda kushtaki TFF.

Msikariri sheria na matukio yake bila kujua mambo kwa undani.
 
Sehem ya mkataba inasema hv, Fei n mchezaj huru wala sio mali ya YangaView attachment 2457681
Usitake kudanganya kwanza ni kosa kuweka huu mkataba (kama ni wa kweli) wenye haki hiyo ni pande husika. Unaweza kushitakiwa.

Hakuna mchezaji mwenye mkataba hai halafu awe huru. Haipo, ila mchezaji asiyekuwa na club anaposajilia anaitwa mchezaji kwa maana huko atokako. Anapoingia mkataba anakuwa mali ya club husika mpaka itakapomwachia.

Kasome tena
 
Kuna kipengele kinachombana Fei kwenye mkataba aliosaini na Yanga SC? Kama unacho weka hapa..
Lazima yanga washirikishwe ambao yanga na Feisal kwa pamoja waliweka hiko kipingele, sasa kwainin kwenye kuvunja unataka uvunje peke yako acha ushabiki, yaani kipingele tuweke wote kwa pamoja alafu kwenye kuvunja uvunje peke yako hizo ni akili au matope
 
Usitake kudanganya kwanza ni kosa kuweka huu mkataba (kama ni wa kweli) wenye haki hiyo ni pande husika. Unaweza kushitakiwa.

Hakuna mchezaji mwenye mkataba hai halafu awe huru. Haipo, ila mchezaji asiyekuwa na club anaposajilia anaitwa mchezaji kwa maana huko atokako. Anapoingia mkataba anakuwa mali ya club husika mpaka itakapomwachia.

Kasome tena
Umeongea vyema na Ili uvunje mkataba lazima uongee na mwajiri wako mkubaliane, tatizo la watanzania tunapenda sana shortcut
 
Kama katika mkataba wake kuna kipengele cha release clause, mchezaji anaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu itakayolipa kiasi kilichomo kwenye hiyo clause bila kuhusisha klabu yake. Ila hataruhusiwa kuhama mpaka msimu wa uhamaji unapokuja. Klabu iliyo na release clause inatakiwa kuanza mazungumzo na mchezaji ambae wanaona thamani yake imepanda ili kuongeza kiasi kilichomo na wakati huo huo kumuongezea maslahi yake binafsi. Wasipofanya hivyo, ruksa kwa klabu nyingine kuingia MOU na huyo mchezaji mara watakapolipa lile dau. Na hiyo klabu mpya inaweza kumuuza tena kwa bei ya juu zaidi bila ya klabu ya awali kupata chochote.

Aidha, kama kuna buyout clause, mchezaji anaweza kulipa kiasi kilichopo na kuingia mkataba mpya na klabu nyingine msimu unaofuata. Tatizo la buyout clause ni kuwa mara nyingi hizi pesa mchezaji anapewa na klabu inayomtaka na hivyo inaweza kuwaingiza katika matatizo ya kodi ( ametoa wapi hizo pesa?) na hoja kuwa alianza mazungumzo na klabu nyingine kabla ya kuifyatua hiyo clause, kitu ambacho hakiruhusiwi.

Amandla...
-una nakala ya huo Mkataba uuweke maCPA (T) Tuuchambue vizuri?
 
Mkuu, ukisitisha mkataba unakuwa free, hakuna haja ya mazungumzo tena. Sasa kama ni mali ya Yanga siku zote hata baada ya kufanya termination, hicho kipengele kina maana gani hapo?
Uelewa wako mdogo sana nikusaidie kwa mfano huu.

Ukimwacha mke pasipo na talaka bado ataendelea kuitwa mkeo au mumeo hadi pande mbili zitakapo kubali kuvunja ndoa hiyo.

Ingekuwa kirahisi hivyo hakuna team duniani ingewanunua wachezaji kwa gaharama kubwa hivyo kwani wachezaji wangelipa cluba ada ya uasajili na mishahara kadhaa. Kisha anaenda timu nyingine.

Kikichofanyika ni uhuni ingawa bado Feisal na Azam wanayo nafasi ya kurekebisha
 
Lazima yanga washirikishwe ambao yanga na Feisal kwa pamoja waliweka hiko kipingele, sasa kwainin kwenye kuvunja unataka uvunje peke yako acha ushabiki, yaani kipingele tuweke wote kwa pamoja alafu kwenye kuvunja uvunje peke yako hizo ni akili au matope
Unaniita mimi shabiki wakati kimsingi wewe ndie shabiki, unaposema "lazima Yanga washirikishwe" hapa unasukumwa na mahaba tu, sio logic.

Mtambue, mtu kutimiza sharti lake kimkataba haitaji ruhusa ya upande wa pili, ni uamuzi wake binafsi, kazi inabaki kwako wewe wa upande wa pili kufanya alichofanya mwenzio, ukigoma kama Yanga walivyofanya, Fei ana uwezo wa kwenda TFF kushtaki.

Sijui kwanini mnataka Yanga SC washirikishwe maamuzi binafsi ya Fei, sioni logic yako hapa.
 
Uelewa wako mdogo sana nikusaidie kwa mfano huu.

Ukimwacha mke pasipo na talaka bado ataendelea kuitwa mkeo au mumeo hadi pande mbili zitakapo kubali kuvunja ndoa hiyo.

Ingekuwa kirahisi hivyo hakuna team duniani ingewanunua wachezaji kwa gaharama kubwa hivyo kwani wachezaji wangelipa cluba ada ya uasajili na mishahara kadhaa. Kisha anaenda timu nyingine.

Kikichofanyika ni uhuni ingawa bado Feisal na Azam wanayo nafasi ya kurekebisha
Umeongea vizuri, watanzania wanapenda ujanja, mkataba tumeingia wote wawili, mkataba ukivunjwa lazima tukubaliane pande mbili sio pande moja inajiamulia inavyotaka, ndo maana ndege tatu za ATCL zimekamatwa kwa mambo haya haya ya kuvunja mkataba kihuni pasipo kushirikisha pande zote mbili
 
Unaniita mimi shabiki wakati kimsingi wewe ndie shabiki, unaposema "lazima Yanga washirikishwe" hapa unasukumwa na mahaba tu, sio logic.

Mtambue, mtu kutimiza sharti lake kimkataba haitaji ruhusa ya upande wa pili, ni uamuzi wake binafsi, kazi inabaki kwako wewe wa upande wa pili kufanya alichofanya mwenzio, ukigoma kama Yanga walivyofanya, Fei ana uwezo wa kwenda TFF kushtaki.

Sijui kwanini mnataka Yanga SC washirikishwe maamuzi binafsi ya Fei, sioni logic yako hapa.
We ushaona wapi mkataba niingie mim na wewe, alafu kwenye kuuvunja uvunje pekee yako unavyojisikia bila kunishirikisha ulishaonaga wapi

mfano ulaya wachezaji kibao wana release clause ingekua rahisi Kama unavyotaka kuaminisha watu si wangekua wanalipa release clause Yao kirahisi alafu waende timu nyingine, usipende kuchukulia mambo kirahisi rahisi
 
Sasa wewe si ndiyo ungeileta ili uprove point yako?
Ni prove kweni nabishana na mtu hapa
Mi nimesema huyo aloleta alete na kipande Cha chini yake maana hicho ni kipande kidogo sana alicholeta.
 
Back
Top Bottom