Aliyekuwa Mrakibu wa Polisi, Kinondoni akata rufaa dhidi ya hukumu yake ya kunyongwa hadi kufa

Tume maalum iliundwa chini ya Jaji....
 
Namba 3 hakuna cheo kama hicho
 
Nikurekebishe kidogo ni kwamba baada ya zombe and Co kutekeleza hilo tukio mwanzo kabisa ilijulikana wale wafanya biashara walikuwa majambazi hvyo askar wote waliokuwa zamu hyo siku walirudisha silaha zao salama bila tatzo ila sekeseke likaanza siku tatu au nne baada ya tukio baada ya baadhi ya wananchi Ku rise hoja kwamba wale hawakuwa majambazi Bali wafanyabiashara, na ndipo wakaamuliwa askar wote waliokuwa zamu wakamatwe na kuwekwa mahabusu huku tume ya uchunguzi ya Kipenka ikienderea .. Hapo ndipo yule askar aliyefyatua risas akapata mwanya Wa kutokomea mpaka Leo hii
 
sawa mkuu ila fanya kautafiti kadogo ndani ya nchi yetu,je adhabu hii imepunguza hayo makosa uliyoyaorodhesha hapo juu?na elewa hizi adhabu mara nyingi zinakuja na makosa mengi ya kunyonga watu wasio na hatia
Hiyo ya kunyonga watu wasio na hatia haihusiani..

Ukisema kufanya utafiti, sio kuangalia kama adhabu imesaidia kupunguza uhalifu, unatakiwa uchukua kipindi ambacho hakukuwa na hiyo adhabu kisha ulinganishe na kipindi ambacho kuna adhabu hiyo.. Wewe umefanya utafiti gani?

Kwa saikolojia ya kawaida tu, kama nikiua watu kwa kukusudia halafu mimi siuwawi, siwezi kuogopa kuua, maana najua mimi nitaendelea kuishi, nitaendelea kuonana na familia yangu na ndugu zangu na washkaji watakuwa wananilitea fegi naendelea kupuliza, wewe na familia yako mmezikwa.

Labda nirudi kwenye hoja ya kunyonga watu wasio na hatia; kwa namna yeyote ile, suluhisho sio kuondoa adhabu, ni sawasawa na kuondoa adhabu ya kifungo gerezani kwa sababu kuna watu wanafungwa bila hatia, nadhani mfano umejitosheleza.

Tuendelee, naona sijachoka kuandika, mkuu wewe una umri gani? Unauelewe mpana wa wahalifu na aina za uhalifu unaofanywa na binadamu?
Kuna binadamu huwa wanafanya uhalifu ambao ukiusikia au kuuona utakubali mtu kama huyo adhabu ya kunyongwa ni sawa, kuna mtu ana historia ya uhalifu na ukatili tangu mdogo, uporaji wa kutumia silaha na kuua, mtu kama huyo, anahukumia kukaa gerezani, lakini mtu huyohuyo, anamuua mfungwa mwenzie, mhalifu kama huyo wamfanyeje? Tayari wameshamfunga kifungo cha maisha lakini anaua wafungwa wenzake..

Wamuongezee kifungi kingine cha maisha ili aendelee kuwaua wenzie au wafanyaje?
 
Hivi askari kurudisha silaha jioni ikiwa na idadi ile ile ya risasi alizokabidhiwa asubuhi inaweza kuwa utetezi tosha kwamba askari huyo hakutumia silaha yake kuua? Maana kama askari mwenyewe kama ana tabia ya kushiriki kwenye matukio machafu ya mauaji ili kujinufaisha si kazi ngumu kwake yeye kuwa na risasi zake za pembeni za kufanyia kazi na unapofika muda wa kurudisha silaha ofisini anarudisha na risasi kwa idadi ile ile aliyokabidhiwa.
 
Ngoja ndugu yako auwawe!
 
The world is not Fair.

Anayeua auawe tu
 
Tuliza munkari dada

Kuna uzi kule uliletwa juu ya wanao kamatwa kwa kwenda Pm ,ukasema mtu wa Jf ukamatwe kwa lipi

Ukisoma katikati ya mistari hii comment yako ni sababu ya wewe kukamatwa

Ndio uzuri tu wa kuwa na ID feki
 

Tafiti za adhabu ya kifo zinasemaje?

Studies zinaonesha kwamba leading criminologists (crime experts) overwhelmingly do not believe the death penalty is an effective deterrent to crime. Huu ni ukweli; murder rates katika nchi zilizo na capital punishment aren’t necessarily lower than zile za nchi zisizo na capital punishment!
 
Huyu Bageni ni mfano wa Polisi wengi tu wanaofanya matukio kwa kutumia kivuli cha upolisi.
Mwisho wa siku haya ndiyo uwa yanawakuta.
 
kuna wadau kuelewa ni wagumu,aliyerudisha silaha ikiwa haina risasi ndie aliyewafyatulia wale marehemu wote risasi,namaanisha wote waliokuwa Doria walikuwa na silaha,but silaha iliyotumika ni moja tu ya huyo aliyekimbia
Ingekuwa vizuri ungemtaja kwa majina huyo mfyatua risasi ili akionekana popote pale akamatwe.
 

Adhabu ya kifo ipo tu lakini sidhani na sina hakika kama wahukumiwa huwa wananyongwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…