Ally Kamwe msemaji wa Yanga afungwe break, Haya sasa Mzee wa watu kakujibu kiutu uzima

Ally Kamwe msemaji wa Yanga afungwe break, Haya sasa Mzee wa watu kakujibu kiutu uzima

Kakosea
Ameomba radhi
Yameisha
Ni utani wa jadi tu mtu hachaguliwi Cha kutaniwa Wala sio tusi
Yanga na Simba Ni watani wa jadi
Utani hauchagui mtu, jinsia, Wala Rika
Au nyie Makolo mseme hadharani Kama hamtaki utani
Young Africans
Bingwa cafcc
Mkuu ww ni show Gah na unatafunwa nyuma...... HAHAHAHAA USIHOFU MKUU SISI NI WATANI WA JADI
 
Halafu utasikia vijana hatuna ajira, wakipewa wanaharibu kama hivi.

Enzi za JPM aliwaamini vijana akawapa nafasi lakini mambo ndio kama haya. Hao wazee waendelee tu kukaa madarakani.

Sio wote ila wengi hatujui mipaka yetu. Binafsi angemtania Ahmed Ally ningemuelewa matani ya ujana na wale wanajuana.

Huu usemaji wa vilabu ni kacheo flani hakana maana yoyote, kwa mpira ulipofikia sasa hivi.
Huu usemaji unakuwa timamu ukiwa nje ukishaingia ni kama unapewa vidonge vya kufyetua akili.
 
BAADA YA KUDHIHAKIWA NA ALIKAMWE, JUMA MGUNDA AMPA JIBU

🗣️"Yanga ni Club yetu pekee Tanzania inayotuwakilisha kwenye fainaly hii ya CAF na kwa bahati iliyonjema inacheza na Club Inayotoka nje ya nchi yetu.

🗣️Sijui kinachopelekea mimi kuwa miongoni mwa kampeni hii ya matusi na kunidhalilisha Nilidhani kampeni itakuwa ni kushinda fainally, kuliko hiki alichokifanya Mwanangu Ally Kamwe.

🗣️Namuombea kwa Mungu awe na mwisho mzuri, mimi nimeshuhudia watu wengi wakifanya kazi Yanga na Simba na sasa wapo nje ya mfumo.

🗣️Kama nilipaswa kutukanwa ili Yanga ishinde basi nimekubali ili Taifa langu lijivunie .

🗣️Tusiposhinda kesho nitashangaa sana kwanini tumefungwa wakati kilichotakiwa kifanywe kimefanywa juu yangu na familia yangu" Kocha Juma Mgunda.

Akiwa ktk kampeni za mechi ya tarehe 28/05/2023 huko Zakhiem Mbagala aliwauliza mashaabiki kati ya "Mgunda na andazi" utachagua nini. Mashaabiki wakaitikia "andazi" . Hakutosheka akauliza tena"kati ya wasimamizi wa Feisal na andazi utachagua nini. Mashaabiki tena wakajibu "andazi".

Sasa mimi kama mtu mzima naona Ally Kamwe alichofanya ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa malezi na makuzi ya wazazi wake. Huwezi kumlinganisha mtu mzima mwenye umri sawa na baba yako na "andazi".

Mgunda amekuwa Hana utani wa Simba na Yanga hata ktk media sjawahi kumskia akitoa maneno ya shobo kwa Wana Yanga. Iweje leo mbele ya watu tena wa rika tofauti tofauti umlinganishe na andazi.

Haya sasa kakujibu kiutu uzima kama baba. Kazi kwako.
Ally Kamwe aombe radhi kwa huo ujinga
 
Vitu vingine ni vya kawaida na watu kutaka kukuza Jambo tu....!, Kipindi manara yupo Simba alivyosema yanga wenye akili ni 2 Kuna aliyemwona kakosea?.
Ahmad Ally majuzi Kati alitamka watu wa Yanga ni sawa na MAITI Kuna aliyemnyooshea kidole?, Utamaduni huu wa kipuuzi umeasisiwa na watu wa Simba. BTW kwani mbona aliyesema Andazi ni bora kuliko CCM hajaonekana kuwa na dharau kwa CCM na Rais wa Nchi?.
 
Akiwa ktk kampeni za mechi ya tarehe 28/05/2023 huko Zakhiem Mbagala aliwauliza mashaabiki kati ya "Mgunda na andazi" utachagua nini. Mashaabiki wakaitikia "andazi" . Hakutosheka akauliza tena"kati ya wasimamizi wa Feisal na andazi utachagua nini. Mashaabiki tena wakajibu "andazi".

Mgunda amekuwa Hana utani wa Simba na Yanga hata ktk media sjawahi kumskia akitoa maneno ya shobo kwa Wana Yanga. Iweje leo mbele ya watu tena wa rika tofauti tofauti umlinganishe na andazi.

Haya sasa kakujibu kiutu uzima kama baba. Kazi kwako.
huo ndio utani wa jadi wenyewe, haina tofauti na aliyebeba jeneza kuingiza uwanjani.
 
Mgunda kaongoe maneno mazito sana. Kwani Ali Kamwe alianza vipi hadi kufikia kwa Mgunda? Mbona mechi ni Yanga vs USM Alger na bora hata angekuwa kamtupia madongo Ahmed Ally tungesema labda karudisha madongo. Sasa huyu baba wa watu kamuanzia nini?
Ukisha kuwa mke wa boss unasahau majukumu yako, unaona ushavuka level za kazi yako.
 
Aly ameomba radhi , amejua kama amekosea na atamuomba radhi kadri siku zinavyoenda mbele.

Lakini sasa ajenda itabadilika na kumshambulia Aly Kamwe .

Tunakula kakisea lakini kaomba asamehewe kuna binadamu ambaye hafanyi makosa?

Naomba Tu Kesho yanga tushinde kwa sababu tukifungwa watu wataanza kusema ni laana za Mgunda na Aly atakuwa kwenye kikaango kikubwa Sana.

Kila la kheri YANGA , Muungwana akivuliwa nguo huchutama Aly kachutama kesi iishe.
Muulize Manara atakuambia alivyopelekewa moto na Karia baada ya kuchutama.

Kuna muda namna nzuri ya kumfundisha mtu ni kupitia adhabu. Sio kila kichwa kina uwezo wa kujifunza kupitia msamaha. Ukifuatilia mfululizo wa matamshi ya huyo jamaa utagundua sio msamaha unaomfaa.
 
BAADA YA KUDHIHAKIWA NA ALIKAMWE, JUMA MGUNDA AMPA JIBU

🗣️"Yanga ni Club yetu pekee Tanzania inayotuwakilisha kwenye fainaly hii ya CAF na kwa bahati iliyonjema inacheza na Club Inayotoka nje ya nchi yetu.

🗣️Sijui kinachopelekea mimi kuwa miongoni mwa kampeni hii ya matusi na kunidhalilisha Nilidhani kampeni itakuwa ni kushinda fainally, kuliko hiki alichokifanya Mwanangu Ally Kamwe.

🗣️Namuombea kwa Mungu awe na mwisho mzuri, mimi nimeshuhudia watu wengi wakifanya kazi Yanga na Simba na sasa wapo nje ya mfumo.

🗣️Kama nilipaswa kutukanwa ili Yanga ishinde basi nimekubali ili Taifa langu lijivunie .

🗣️Tusiposhinda kesho nitashangaa sana kwanini tumefungwa wakati kilichotakiwa kifanywe kimefanywa juu yangu na familia yangu" Kocha Juma Mgunda.

Akiwa ktk kampeni za mechi ya tarehe 28/05/2023 huko Zakhiem Mbagala aliwauliza mashaabiki kati ya "Mgunda na andazi" utachagua nini. Mashaabiki wakaitikia "andazi" . Hakutosheka akauliza tena"kati ya wasimamizi wa Feisal na andazi utachagua nini. Mashaabiki tena wakajibu "andazi".

Sasa mimi kama mtu mzima naona Ally Kamwe alichofanya ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa malezi na makuzi ya wazazi wake. Huwezi kumlinganisha mtu mzima mwenye umri sawa na baba yako na "andazi".

Mgunda amekuwa Hana utani wa Simba na Yanga hata ktk media sjawahi kumskia akitoa maneno ya shobo kwa Wana Yanga. Iweje leo mbele ya watu tena wa rika tofauti tofauti umlinganishe na andazi.

Haya sasa kakujibu kiutu uzima kama baba. Kazi kwako.
Katika watu ambao kabla ya kuongea napima maneno yangu ni watu wazima.

Hawa watu wazima wamepita vingi na wameona vingi bado tuna mengi ya kujifunza kwao..
 
Back
Top Bottom