Ally Kessy awashukia Zanzibar, Awataka Wabunge wa Zanzibar watoke nje kwa mambo yasiyo ya Muungano

Ally Kessy awashukia Zanzibar, Awataka Wabunge wa Zanzibar watoke nje kwa mambo yasiyo ya Muungano

Kwahapo kuna Nahodha wakinyamaza bila kuhoji ndani ya bunge nawaona kama yatima waishio kwa mama wa kambo mnyanyasaji
 
kwenye bunge la katiba ni alipiga makelele hayo hayo na baadae kwa sauti kubwa akaunga mkono ule uvundo wao. aache unafiki kama kweli ana la maana asingeunga mkono ule uvundo walioupitisha. Msitusimange wazanzibari hatuna haja wala shida ya centi zenu...wenye haja na hizo centi ni hao hao vibaraka wanaotumiliwa na ccm... mbona tunadai uhuru wetu siku nyingi mmegoma kutuachia...?
Kwa kweli wengi walisema hawautaki muungano jinsi ulivyo.
 
Poleni wabunge kutoka znz hasa wa ccm
Huo ndio ukweli
Ni ukweli mtupu. Huyu kessy aliwahi kusema bungeni kwamba baraza la wawakilishi linatakiwa kujumuisha na wabunge wa bara kama bunge la bara linavyowahusisha wajumbe wa baraza la wawakilishi(kumbuka baraza la wawakilishi ni kama bunge la znz linalojuimuisha wabunge wa ccm&cuf)
 
Kuwaponda Wazanzibar Bungeni hajaanza leo.
Linalo nishangaza ni kuwa Mbunge akiishambulia Zanzibar kama mnufaika wa muungano wabunge wa ccm na kiti cha spika wanafurahi sana na kushangilia.

Lakini Mbunge akizungumzia Zanzibar ijitenge na kujitegemea anaitwa mhaini na kiti cha spika kinaweza kumshughulikia kwa kutaka kuvunja muungano.

Sasa nini hasa msimamo wa ccm kuhusu Zanzibar?
 
Kama hawana asili ya tanganyika basi ni wanatumiwa na serikali ya tanganyika kwa manufaa ya tanganyika.
ok! hapo unaendeleza uchotara bila kujua.

Ni hivi, wznz wanalalamika mgonjwa kapelekwa na SMZ kutibiwa wanataka bili alipe Mtanganyika, hivi hawa wenzetu wanafikiri nini kuhusu muungano?

Halafu wanataka mgao wa mawaziri sawa, come on, mzanzibar wizara ya kilimo, mali asili, maji na mifugo inamhusu vipi. Huko halmashauri za miji wapo kwa kuhurumiwa sasa wanataka kufanya haki yao. Wizara za muungano zinajulikana na ndizo watapata fursa.period

Gharama za kuihudumia znz ni kubwa kuliko majjiji Zaidi ya Tanganyika yenye eneo kubwa, uchumi mkubwa, na mchango mkubwa kwa Taifa. Hali hii hadi lini?

Wapewe wanachostahili siyo wanachotaka. Wawajibike kwa watu wao, inapofikia mahali hata wagonjwa wao wanataka bili za walipa kodi wa Tanganyika inakera sana.

Wahudumie watoto wao kwa kuwapa mikopo ya masomo si kutafuta nafasi za ubalozi
Kessy kawapa ukweli, znz inaweza kuhudumia ubalozi hata mmoja! Wanajua gharama za ubalozi.

Wabunge wa znz wanakuja kwa uzanzibar wao na SMZ ishapewa mgao wake, ihudumie watu wao wanaokuja kutetea znz si kutuletea kauli za maudhi wakitumia kodi zetu

Hongera Kessy, unayosema ndiyo tunayoyaona. Hongera sana kwa uchungu wa kodi zetu

Tunataka kuona mchango wa znz kwa namba, na kwamba muungano si maneno ni ushiriki wa kitu mkononi.
 
Hapaana! anawaambia ukweli
Hao wznz wako Dodoma hawajui gharama za uwepo wao
Huku bara wanakuja Zaidi ya 80, BLW wapo 50.

Wanataka nafasi za ubalozi, hivi SMZ inachangia nini katika kuendesha balozi 21 zilizopo.

Kama wanataka nafasi za ubalozi, basi waombe kugharamia balozi watakazokuwa na balozi mzanzibar. Siyo watake vyeo wakimbie gharama

Kessy kaongea ukweli, mambo yasiyowahusu wanayaongelea yanawahusu nini?

Wanalalamika mgonjwa hakutibiwa na JMT, kwani wizara ya afya ni suala la muungano!

Wanadai nafasi za muungano sawa, hivi znz yenyewe inatoa ajira za muungano ngapi
Halafu wamejazana katika maeneo yasiyowahusu kama wizara zisizo za muungano

Wanataka mgao wa 4.5 wakati huo huo wanataka na kile kisicho cha muungano

Kessy kawaambia ukweli, wakati umefika tuwaambie ukweli.
Muungano ni gharama tushirikiane, si eneo la kuzalisha ajira au kutoa mafao kwa znz.

Znz ili iwe na heshima ni wakati sasa wakiongelea muungano wasidai tu watuambie na eneo gani wanasaidia. Tumechoka kusikia madai tuu hakuna mchango wowote

Hiyo 4.5 ni pato la Tanganyika, bado wanataka na inasikitisha wanataka kugawana sawa
Wakiambia wenzetu mnaleta nini mezani, wanakimbiaa. Utegemezi huu unachosha

Kwakweli afadhali amepatikana mwenye uchungu na kodi zetu

Watu milioni wanachukua sehemu kubwa sana ya kodi zetu. Hivi Dar na znz zina ulinganifu kwa jambo gani kiasi znz ipate takribani mara 20

Ahsante Kessy, Ahsante sana. Wakiwa Dodoma watulie na kusubiri watakacho zawadiwa,
kwenye bunge la katiba ni alipiga makelele hayo hayo na baadae kwa sauti kubwa akaunga mkono ule uvundo wao. aache unafiki kama kweli ana la maana asingeunga mkono ule uvundo walioupitisha. Msitusimange wazanzibari hatuna haja wala shida ya centi zenu...wenye haja na hizo centi ni hao hao vibaraka wanaotumiliwa na ccm...

mbona tunadai uhuru wetu siku nyingi mmegoma kutuachia...?
 
Hiyo ni kweli unaweza kuzunguka kwa baiskeli isipokuwa utatumia muda mrefu, mimi na rafiki yangu tulizunguka zanzibar yote kwa gari tulitumia saa mbili na robo tukamalizia kwenda Tumbatu na boti

Wewe na mwenzio mlikuwa mnakusudia nini kuizunguka Zanzibar?
 
Huyu Mbunge alishawahi kusema unaweza kuizunguka Zanzibar yote kwa kutumia Baiskeli..


Hawa Wabunge kwanini wasitulie kwao????
Kuna siku alisema unaweza kuwakusanya wazanzibar wote kwa kupiga filimbi
 
ok! hapo unaendeleza uchotara bila kujua.

Ni hivi, wznz wanalalamika mgonjwa kapelekwa na SMZ kutibiwa wanataka bili alipe Mtanganyika, hivi hawa wenzetu wanafikiri nini kuhusu muungano?

Halafu wanataka mgao wa mawaziri sawa, come on, mzanzibar wizara ya kilimo, mali asili, maji na mifugo inamhusu vipi. Huko halmashauri za miji wapo kwa kuhurumiwa sasa wanataka kufanya haki yao. Wizara za muungano zinajulikana na ndizo watapata fursa.period

Gharama za kuihudumia znz ni kubwa kuliko majjiji Zaidi ya Tanganyika yenye eneo kubwa, uchumi mkubwa, na mchango mkubwa kwa Taifa. Hali hii hadi lini?

Wapewe wanachostahili siyo wanachotaka. Wawajibike kwa watu wao, inapofikia mahali hata wagonjwa wao wanataka bili za walipa kodi wa Tanganyika inakera sana.

Wahudumie watoto wao kwa kuwapa mikopo ya masomo si kutafuta nafasi za ubalozi
Kessy kawapa ukweli, znz inaweza kuhudumia ubalozi hata mmoja! Wanajua gharama za ubalozi.

Wabunge wa znz wanakuja kwa uzanzibar wao na SMZ ishapewa mgao wake, ihudumie watu wao wanaokuja kutetea znz si kutuletea kauli za maudhi wakitumia kodi zetu

Hongera Kessy, unayosema ndiyo tunayoyaona. Hongera sana kwa uchungu wa kodi zetu

Tunataka kuona mchango wa znz kwa namba, na kwamba muungano si maneno ni ushiriki wa kitu mkononi.

nimewaelewa pamoja na uchotara wangu...point yangu ni kwamba wazanzibari tulio wengi hatuutaki huu muungano wa kulalamikiana laiti kama ccm wasingekuwa wanawabeba hawa wahafidhina kwa manufaa yao binafsi, tungekuwa tumefika mbali sasa hivi na wala kusingekuwa na ugomvi wala shida yoyote kwani kila upande ungejua mipaka yake.

tusilaumiwe wazanzibari la kufanya ni mtusaidie tupate uhuru wetu basi tutawaachia salama usalimin na tanganyika yenu.
 
Watu hawamuelewi huyu Kessy, anazungumza total 360 degree opposite na CCM wanashangilia bila kujijua, hapo ndio unapima akili ya nani muelewa, swali itakuaje, mwarabu, somehow ana asili ya huko Zanzibar aishambulie zanzibar

kifupi anchosema Muungano haupo nynyi CCM mnamdanganya nani na hawa jamaa wawakilishi wanafanya nini hapa?
 
kwenye bunge la katiba ni alipiga makelele hayo hayo na baadae kwa sauti kubwa akaunga mkono ule uvundo wao. aache unafiki kama kweli ana la maana asingeunga mkono ule uvundo walioupitisha. Msitusimange wazanzibari hatuna haja wala shida ya centi zenu...wenye haja na hizo centi ni hao hao vibaraka wanaotumiliwa na ccm... mbona tunadai uhuru wetu siku nyingi mmegoma kutuachia...?
Kwani mlinyimwa uhuru na nani? Uhuru unaweza kupatikana kirahisi.
Tushaeleza sana.

Ukweli kuwa mnataka kutibiwa nje na bili kuleta Tanganyika, inasikitisha
Hakuna namba unzoweka hapa kuonyesha mchango. Nikupe namba kidogo tu, miezi 3 tu znz imepewa bilioni 29. Hapo hakuna gharama zingine unazozijua wewe huku watoto wakisomeshwa bure.

Nipe namba miezi 3 znz imechangia kiasi gani katika muungano

Tmechoka na kulalama tuu hakuna mawazo ya mapya hakuna kitu mkononi.

Mkitaka mabaozi 10 kati ya 21 basi mulipie gharama zake, siyo vyeo gharama Tanganyika

Mnapewa ajira na sasa PAYE , mnataka nini Zaidi

Ukweli kuwa hamna mchango wowote katika muungano. Mnadai usawa ,mbona humhudumii wabunge wenu. Usawa una wajibu siyo vyeo tu.

ZNZ iwajibike kwa taasisi zake, watu wake na utegemezi sasa ufike kikomo.
 
Kessy kwa njia ya pekee kabisa anawaamsha Wazanzibari wenye uelewa.

Historically, Kessy ana asili ya Uzanzibari.

Simshangai.
 
nimewaelewa pamoja na uchotara wangu...point yangu ni kwamba wazanzibari tulio wengi hatuutaki huu muungano wa kulalamikiana laiti kama ccm wasingekuwa wanawabeba hawa wahafidhina kwa manufaa yao binafsi, tungekuwa tumefika mbali sasa hivi na wala kusingekuwa na ugomvi wala shida yoyote kwani kila upande ungejua mipaka yake. tusilaumiwe wazanzibari la kufanya ni mtusaidie tupate uhuru wetu basi tutawaachia salama usalimin na tanganyika yenu.
Kwani ukiwa CCM unapoteza uzanzibar? Sikiliza unposema vibaraka wa znz au wenye asili ya Tanganyika tayari unaleta uibaguzi kama ule wa uchotara. Angalia shilingi pande zote ndugu yangu

Wznz walio wengi kinawashinda nini? Mwiteni makamu wa Rais arudi nyumbani, na wale wa Dodoma wasije. Walioko taasisi za uungano warejee nyumbani. kipi kigumu
 
...... hapo ndo huwa naamini ili uwe mfuasi wa chama cha kijani lazima uwe na ubongo wa kuku, hoja au mchango huo angeutoa lissu, ungesikia jenessta kaomba mwongozo, ungewaona vilaza wa zbar kuomba atelewe yeye nje kisa kawabagua....... ila kwa kuwa kasema mwenzao hapo hawaoni impact na mbegu ya chiki aliyonayo kwa wenzetu wa zbar...... SHAME
 
Hiyo ni kweli unaweza kuzunguka kwa baiskeli isipokuwa utatumia muda mrefu, mimi na rafiki yangu tulizunguka zanzibar yote kwa gari tulitumia saa mbili na robo tukamalizia kwenda Tumbatu na boti
Itakuwa mlizunguka unguja tu,ila Pemba hamkufika na visiwa vidogo vidogo.Hiyo ndo tafsiri ya Zanzibar.
 
Back
Top Bottom