Akizungumza Kamanda wa Polisi mkoani humo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Richard Abwao amesema tukio hilo limefanyika Januari 30 mwaka huu saa 11 jioni likihusishwa na imani za kishirikina.
Kamanda Abwa amesema baada ya mtuhumiwa kumpasua mke wake, alitoa watoto pacha kisha kumpika mmoja huku mwingine pamoja na mwanaye mwingine aliyekuwa na miaka miwili, akiwazika.