Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

Ameniomba Msamaha lakini ameniwekea Masharti

Ufa
Binti anajiingiza kwenye mateso makubwa sana
Mapenzi ni upofu lkn Mungu ataenda kumfungua aepuke hili janga.. bora aumie kwa muda mfupi kwa kumkosa kuliko mateso yanayo msubiria kama ataingia kwenye hii ndoa 🚮🚮
 
Mkuu...mwanaume ni simba, kiongozi na mshawishi.

Inategemea na aprochi yake.
Angemwita amwambie....my love plz naomba tuahirishe kwani nilitegemea kupata pesa lakini nimeahirishiwa nami aitaki nikuaibishe kwa wazazi wako.
Naomba tusogeze mbele kidogo...binti asingekataa lakini kutamka wazi unamsaidia rafiki na aio ndg ilikuwa dharau mkuu
Hili ndio neno,kuhusu kumsaidia rafiki yake sikatai,angemsaidia lkn alichokosea ni the way alivyomfikishia mwenziwe taarifa,kwa maana kwamba alikuwa ameshaamua tayari,lkn pia hakutoa taarifa ukweni hapo ndo shida ilipoanzia.
 
Sahihi kabisa! Ukiwa kapuku tegemea kuwa mtu wa kudharirika ukweni, kwa kuomba misamaha mara kumi kumi bila sababu za msingi,
Ila hapa kakosea,tuache masihara wangekuwa wamekutana tu wawili hakuna utambulisho kwa pande zote mbili ingekuwa sio kesi,lkn ni watu walitambulika officially,it's not right for what he has done
 
Kwahiyo kwa mawazo yako binti ndo kakosea!?!?..... Aisee walio kwenye mchakato wa kutafuta wachumba kwasasa Mungu awasaidie.. sio kwa vichwa hivi 🚮🚮
Barikiwa mwenye kichwa kizuri.


Toa ushauri uachane na sisi vichwa maji
 
Miezi michache iliyopita, nilitengana na mwenzi wangu wa muda mrefu baada ya kusitisha kuota mahari nyumbani kwao na kuamua kumsaidia rafiki yangu ambae alikuwa kwenye changamoto fulani za kimaisha.

Nilipomjulisha kwamba nitaahirisha kutoa mahari, hakukubali na aliniomba tuachane. Nilikubali na kumtakia kila la kheri lakini pia nikamsihi kwamba kama atafikiria uamzi wa tofauti basi nitakuwa tayari kumpokea.

Jana alinipigia simu na kuomba msamaha. Alijutia sana, hatimae, nikaamua kumsamehe. Jambo gumu ambalo bado linaniumiza kichwa, ni yeye kutaka mimi niwaombe ndugu zake na wazazi wake msamaha kwa kutokupeleka mahari kwa muda tuliopanga.

Kabla sijatoa maamuzi, naombeni ushauri. Hili jambo ni sawa?
Kama uliahidi kuitoa hadi na wazazi wakajua kuna siku utafika utatoa, wewe nenda tu kaombe msamaha, ahadi ni deni na kufanya ukauzu kabla hata ndoa yenyewe kuanza basi msiiwaze kabisa achaneni nayo, mtashindwana.
 
Umemkosea na umempa fedheha kwa familia yake, na Umevunja Ahadi..!!!

Kama ni mimi ningeshakublokilia mbali everywhere kuanzia kwenye Moyo,nafsi,akili etc

Unaonekana hauna msimamo wala clear vision, Mwanaume mwenye Vision habadili plans zake kwa changamoto za ghafla, huyo Dada ningemjua ningemshauri akusahau angaalie maisha yake
[emoji23][emoji23] kuna mipango yako na kuna mipango ya Mungu, wewe unawaza panga hili na Mungu kakupangia lile so maisha hayana formula. Angekuwa hana msimamo kama angemwacha kabisa ila aliahirisha kwaemergence iliyotokea ila hakuacha msimamo wake kuwa atatoa mahali sema binti alishindwa uvumilivu. Ni vitu viwili tofauti. Binti alisusa na kuzira, mipango hupangwa ila jua Mungu anamipango yake. Kukosa msimamo ni kitu kingine kabisa.
 
Jamaa ulichemka Sana

We endekeza tu maneno ya watu kukataa ndoa na kuleta ujana. Kitu unasahau ni kuwa Hao unaowaona marafiki zako leo hutakuja kuwaona kesho ukiwa unaumwa unavaa pampers.

Ujana huwa unawasumbua Sana, stori nyingiiiii ila hamjui ya mbele yenu.

Wewe ulijitolea kuacha kutoa mahali na kujenga familia yako ambayo kimsingi ndio rafiki wako wa kweli na kumsaidia mshkaji, subiri sasa utakuja kuona Nani Atakuwa upande wako katika maisha yako.
Very true
 
Jamaa ulichemka Sana

We endekeza tu maneno ya watu kukataa ndoa na kuleta ujana. Kitu unasahau ni kuwa Hao unaowaona marafiki zako leo hutakuja kuwaona kesho ukiwa unaumwa unavaa pampers.

Ujana huwa unawasumbua Sana, stori nyingiiiii ila hamjui ya mbele yenu.

Wewe ulijitolea kuacha kutoa mahali na kujenga familia yako ambayo kimsingi ndio rafiki wako wa kweli na kumsaidia mshkaji, subiri sasa utakuja kuona Nani Atakuwa upande wako katika maisha yako.
Hii ya kumtisha mtu ili iweje[emoji23][emoji23][emoji23]. Yaani hata kilichomfanya ahairishe mahari na kumsaidia kwanza mwenzake hukijui ila tayari ushakuwa judge jury na executioner [emoji23][emoji23][emoji23]. Mtu anaweza kufa hivihivi, wewe ukasema mahari kwanza wakati mahari ni zawadi. Mtu hajaikataa ndoa, wewe ushamlabel kuwa mpinga ndoa, mwana tumia busara kwanza kukurupuka hakujawahi kumuacha mtu salama na kama umeoa basi jitaidi kulikabili hilo jambo
 
ujue maisha ni safari ndefu sana!
Mleta uzi ni type ya wale watu wana overconfidence
watu wenye kujiskia flani hivi kwamba maisha wameyapatia kwahiyo huyo mwanamke ni kama kuwa nae ulikua unamsaidia tu. ( ndio mana maamuzi yako ni sheria)
Wewe ndo wewe yani ...
matendo ya huyo dada yanakuongezea utukufu zaidi...[emoji1]

ni jamii ya watu wenye shida kwenye makuzi yao, inayopelekea upungufu wa Busara
 
Mbona simple man

"Jaman samahani mambo yangu yalikaa vibaya ndo maana sikuja na masmahanini zaidi Kwa kushindwa kuja kuwajulisha kama nimekwama ila leo nimefika rasmi tulimalize hili swala"

Jifunze ku-lower ego

Vitu kama samahan, naomba, nilikosea, nisamehe, ahsante vinasaidia sana kujenga uhusian mzuri na wengine

Wengi IQ kubwa alafu Emotional intelligence ipo chini sanaaaaa..

Kwenye ule Uzi wako nilikashauri kitu Kwa ulivojibu nikajua tu you have na ku-deal na emotions za wengine
 
Back
Top Bottom