Pre GE2025 Amos Makalla Mwenezi mpya CCM Taifa, Ally Hapi Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi

Pre GE2025 Amos Makalla Mwenezi mpya CCM Taifa, Ally Hapi Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana leo tarehe 03 April, 2024 jijini Dar Es Salaam, katika kikao chake maalum, chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na masuala mengine, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, imefanya mabadiliko madogo ya Sekreteriet ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kuwachagua wajumbe kama ifuatavyo:
  • Ndugu John Mongella kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, akichukua nafasi ya Anamringi Macha ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga,
  • Ndugu Amos Gabriel Makalla kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, akichukua nafasi ya Ndugu Paul Makonda ambaye ameteulia kuwa Mkuu wa Mkoa Arusha.
  • Ndugu Ally Salum Hapi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania, akichukua nafasi ya Ndugu Gilbert Kalima ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga,
  • Ndugu Jokate Urban Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM akichukua nafasi ya Ndugu Fakii Raphael Lulandala ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro.
Aidha katika kikao hicho, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, chini ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi, ambaye pia ni Mwenye kiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa kazi kubwa na nzuri ya kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 – 2025.

IMETOLEWA NA IDARA YA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO 03 APRIL, 2024
Ally Hapi ni mfano mzuri kwa kufanya kilimo baada ya kutenguliwa ukuu wa mkoa. Ameonesha kwa vitendo kwamba siyo lazima apate cheo cha kisiasa ili aishi.
Kwa uzoefu aliopata kwenye kilimo, atakuwa kiongozi anayejua shida za wakulima.
 
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana leo tarehe 03 April, 2024 jijini Dar Es Salaam, katika kikao chake maalum, chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na masuala mengine, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, imefanya mabadiliko madogo ya Sekreteriet ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kuwachagua wajumbe kama ifuatavyo:
  • Ndugu John Mongella kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, akichukua nafasi ya Anamringi Macha ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga,
  • Ndugu Amos Gabriel Makalla kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, akichukua nafasi ya Ndugu Paul Makonda ambaye ameteulia kuwa Mkuu wa Mkoa Arusha.
  • Ndugu Ally Salum Hapi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania, akichukua nafasi ya Ndugu Gilbert Kalima ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga,
  • Ndugu Jokate Urban Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM akichukua nafasi ya Ndugu Fakii Raphael Lulandala ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro.
Aidha katika kikao hicho, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, chini ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi, ambaye pia ni Mwenye kiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa kazi kubwa na nzuri ya kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 – 2025.

IMETOLEWA NA IDARA YA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO 03 APRIL, 2024
Kilasiku hahahaha wanabadirishana nafasi tu, that means Chama hakuna workforce ya kutosha. Wanachama wajitathmini
 
Happi amerudi kwenye cake ya taifa?? Km namuona kidampaa akifurahi kututambia wenzie, basha wake kapata teuzi.

Tutakomaaaa mwaka huu, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Happi amerudi kwenye cake ya taifa?? Km namuona kidampaa akifurahi kututambia wenzie, basha wake kapata teuzi.

Tutakomaaaa mwaka huu, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Duuuuuh upande wa mwenezi sijaona mtu mwenye kujipamba ccm na kuwafanya watanzania waiamini na kuweza kuipa kura tena
 
sijawahi mwelewa makala, zaidi ya kuona midomo ikicheza cheza tu. Ila salute sana kwa Mongera, Hapi...kazi naimani itapigwa sana kama ushirikiano utakamilika toka kwa mkuu wa nchi
 
Kwa hiyo Ali Happy alikuwa analima na drones? Mbona tulikuwa tunamuona anabeba kwenye mandoo machakavu na sio kutumia scavator?
Ngumu kuelewa

Ukishafika level ya juu au kati wkenye kilimo, hulazimiki kuwa na mundu, singe na ndoo site

Unatakiwa kuwa na strong team on the ground
 
CCM ni Chama kinachofuata ushauri wa wanachama wake,nadhani ni vizuri kwa vyama vingine kuiga mfano huu.
Yawezekana Mbinu ya kufuata ushauri ni mojawapo ya sababu ya CCM kuendelea kubaki madarakani.
Nawapongeza wote walioaminiwa na kuteuliwa na Chama,lakini ni muhimu kwao kuona teuzi hizo sio za kudumu bali ni Chama kinachopaswa kudumu.
Muda wowote nafasi zao zinaweza kuwa za wengine kwa nyakati ambazo Chama kitahitaji kujibalidisha kutokana na maoni ya wanachama.
 
" afadhali angebaki tu Makonda" ndio sentensi inayotamba mitandaoni usiku huu

Sijajua Wana CCM walitaka ateuliwe nani? Pascal Mayalla au nani?!!!

Mlale Unono 😀😀
 
Back
Top Bottom