Anahitajika msichana/mwanamke kwa ajili ya IVF

Anahitajika msichana/mwanamke kwa ajili ya IVF

Mkuu umeleta uzi wako so tegemea kuulizwa maswali mengi....ungekuwa hutaki maswali ungeita watu pm uwaelezee hilo tatizo lako

Nashangaa unakuwa mkali[emoji848]
Niliemjibu alishanielewa na akakaa kimya,
Pia nakukumbusha kwamba sijaja hapa kueleza tatizo bali nimekuja kutoa fursa yenye malipo kwa mwanamke mwenye sifa nilizotaja pia mwanamke huyo awe tayari kwa hiari yake.
Hakuna sehemu niliyoonesha ukali ila nimekua najaribu kuwaelekeza watu kadiri ninavyoona inafaa.
Jambo lingine unatakiwa kujua kwamba hata kama hii ni forum huru ila unapoona jambo lina hiari unaweza kushiriki au kuacha sababu halikupunguzii kitu, ila endapo jambo lingekuwa ni lazima ndio hiyo mijadala ingekuwepo.
 
Asante kwa maoni ndugu, ila huo ni mtazamo wako.
Kuna vitu vingine viko juu ya uwezo wako penda kujifunza vitu usivyofaham.
Pia usipende kushinikiza na kukisema uongo kitu usichokifaham vizuri.
Wenzio hawahapa
The point sio IVF lasivyo angebebana na mkewe kimya kimya wakafanya,
The point is mtu atoe mtoto wake (yai lake) tena eti amlee mwaka mzima halafu amuachie,
People just have questions which he refuses to answer so tunabaki na viulizo wengine tumejiundia majibu yetu,
Mfano kakataa kusema kama hata ana huyo mke ndomana me nimewaza labda ni mwana upinde anataka mtoto sa sijui watu wanatoa wapi huruma kwani kasema ana shida!
Kumbe na wewe umeligundua hilo,simple tu huyu jamaa anavunjiwa mayai na magudume
 
IVF kirefu chake ni In Vitro Fertilization.
IVF ni jambo la kurutubisha kwa kuunganisha mbegu za uzazi za mwanamme na yai la uzazi la mwanamke maabara, baada ya hapo zoezi linalofatia ni kupandikiza ujauzito kwa mwanamke kwa njia ya sindano kisha ujauzito utaendelea kukua kama kawaida kwa mda wa miezi tisa kisha mwanamke atajifungua kawaida.

IVF haihusishi kukutana kimwili kati ya mwanamke na mwanaume bali mwanaume anatoa mbegu kwa kujichua au punyeto na mwanamke anatolewa yai lililopevuka maabara na wataalamu baada ya hapo ndio ujauzito unapandikizwa kwa mwanamke,
Ni njia safi na salama na haihusishi operation kubwa na haina hatari yeyote kwa mwanamke.

Sasa anahitajika mwanamke au msichana katika zoezi hilo,

MALIPO
Moja malipo ni milioni 25 ambayo yatasainiwa kisheria mahakamani na ustawi wa jamii.
Pili kila mwezi atalipwa milioni moja kama malipo ya motisha kwa mda wa miezi tisa ya ujauzito, malipo hayo ni nje ya ile milioni 25.
Tatu kila siku atalipwa elfu ishirini kama gharama ya chakula kulea mimba kwa mda wa miezi tisa ya ujauzito.
Nne atalipwa shilingi elfu hamsini kila siku kama gharama ya chakula baada ya kujifungua kwa mda wa mwaka mmoja kipindi ananyonyesha.
Tano gharama zote za hospital kwa mama kipindi cha ujauzito, mama na mtoto baada ya kujifungua zitagharamiwa na baba wa mtoto/watoto

MASHARTI
Moja ujauzito utalelewa sehemu aliyopo baba wa watoto.
Mbili hauruhusiwi kisheria kutangaza kwa mtu yeyote kama una ujauzito labda wazazi wako tu, na wazazi wakiambiwa nao wataelimisha kuhusu hili sharti.
Tatu baada ya kujifungua, mtoto/watoto wakifikisha mwaka mmoja utawakabidhi kwa baba yao.
Nne baada ya kukabidhi mtoto/watoto hautoruhusiwa kisheria na kibinadam wewe ndugu zako au rafiki zako kuwaona mtoto/watoto kwa namna yeyote kipindi chote cha maisha yenu hapa duniani.
Tano hautoruhusiwa kuwa na mahusiano ya aina yoyote na baba wa watoto kabla na baada ya kujifungua mtoto/watoto.
Sita awe tayari kulea ujauzito akiwa jijini dar es salaam.

SIFA ZA MWANAMKE/MSICHANA ANAEHITAJIKA.
Moja awe na afya nzuri, asiwe na magonjwa ya akili, pili asiwe na magonjwa ya zinaa ikiwemo ukimwi.
Pili awe mtanzania kutoka kabila na dini yeyote.
Tatu awe mrefu, mrefu sana atapewa upendeleo.
Nne awe mwembamba, akiwa mnene isiwe unene mkubwa sana.
Tano awe na umri wa kati ya miaka 25 hadi 35.
Sita awe mweupe au maji ya kunde asiwe mweusi sana.

Asanteni.
Pia kwa mwana Jamii Forum mwenye ndugu, rafiki au jirani mwenye hizo sifa naomba mnisaidie kusambaza hili tangazo.
Asante tena.

Vigezo na masharti kuzingatiwa
mbegu atatowa huyo mwanaume kwa kujichuwa?Kama ndiyo kwanini hadi kupandikiza kwanini wasifanye mapenzi?
 
Kila mtu yupo huru kufanya anachoona kinamfaa, hasa kama havunji sheria kwako na kwa ujumla.
Tusiwe wepesi kuhukumu, aliye mtakatifu ni Mwenyezi Mungu pekee.
Mkuu wewe si ulisema jana usiku ungefunga dirisha na kujibu watu ?
Be a man of your own words...
 
Back
Top Bottom