Anaitwa Roma: Wimbo mpya wa Roma Mkatoliki

Anaitwa Roma: Wimbo mpya wa Roma Mkatoliki

maramla,
Acha ujinga wa Nanjilinji na ushamba juu. North Korea ambao wana mpaka silaha za nyuklia achilia mbali "daraja" kama Tazara wasingelalamikiwa kukosa demokrasia kama vitu ndio vinapimwa.

Halafu kwa vile nyie hamfanyi vitu kwa niaba ya akili zenu mnadhani kila mtu anatumwa? Roma ni sina ya wasanii wachache sana duniani wanao tumia sanaa kuwasemea wengine mfano kama alivyokuwa Bob Marley.

Sio vijana kama Harmonize wanaimba nyimbo za kusifu ndege sijui na nini lakini kijiji alichotoka watu wanakunywa maji machafu, kuugua na kufa kwa maradhi ya kimasikini yeye anafurahia kuitwa kuimba kwenye sherehe kama katuni.
 
Kwa usomi wako demokrasia inapimwa kwa fiesta na kuzunguka vijiwe nongwa? Wewe ni miongoni mwa wasomi wanaotumia tumbo kutafuta teuzi
Mwambie kabisa bila kumremba kuwa ni mtu mpuuzi katika jamii iliyo elimika.
 
typo disregard as long as the msg is home and dry!
Oooh sorry mate, I didn't know You can't Swahili..

Acha kuikinajisi lugha ya Taifa, angalia kamusi kabla hujaandika au kama huna uhakika wa unachokiandika..
 
Mzalendo.... "Mange ni TBC ya wanyonge, TBC taifa imetekwa na wenye mapembe"
 
Oooh sorry mate, I didn't know You can't Swahili..

Acha kuikinajisi lugha ya Taifa, angalia kamusi kabla hujaandika au kama huna uhakika wa unachokiandika..
you can't swahili ndio nini?
 
Habari ya muda huu Wakuu,

Mnamo mapema wiki iliyopita niliandika uzi nikihoji nafasi ya sanaa ya Tanzania (Muziki) katika kuelezea na kuonesha uhalisia wa jamii yetu (Tanzania yetu). Nilipata wazo la kuandika uzi ule kutokana na kukithiri kwa nyimbo mbalimbali zenye mlengo wa kusifia pekee (kusifia awamu ya tano).

Unaweza kujikumbushia kidogo hapa chini:

Je, ni ipi nafasi ya wasanii wa kizazi kipya kumulika uhalisia wa jamii yetu?


Nikirudi kwenye mada, nimeridhishwa sana kuona jambo lililokuwa linaniumiza katika sanaa ya Tanzania limefanyiwa kazi. Naona kama sanaa imerudisha uhai wake kwa kuwa na maudhui yanayogusa pande zote. Leo katika pitapita zangu Mjini, nimepata bahati ya kuusikia wimbo mpya wa msanii Roma unaoitwaAnaitwa Roma”. Aidha, katika wimbo huo Roma ameonesha mtazamo tofauti na wasanii wengine (wasanii wanaosifia pekee) kwa kujaribu kugusia na kukosoa matukio mbalimbali yanayotokea Tanzania. Aidha, uzi huu hautazama sana kuchambua maudhui ya wimbo huo, isipokuwa uzi huu utaeleza kwa ufupi namna ambavyo nimefurahishwa kuona sanaa ya Tanzania inasawazishwa (imebalance) kwa kuwa na wasanii wanaosifia na wengine wanaokosoa.

Wakuu, kuwa na sanaa ya aina hii ni muhimu sana katika ustawi wa Nchi yetu kwa sababu, wasanii wanaposifia wanawapa nafasi wananchi (wanajamii) kuona mema yanayofanywa na viongozi. Ama pale wanapokosoa, wanaipa nafasi jamii kuona udhaifu na maovu yanayofanywa na viongozi. Kimsingi, mimi ni muumini wa dhima ya ukosoaji katika sanaa kwa sababu naamini dhima hiyo husaidia kumulika mabaya ya viongozi na kuwafanya wawe na uoga wa kufanya maouvu na kuwa makini katika kutekeleza majukumu yao. Kwa upande wa dhima ya kusifia sio mbaya, lakini kwa mtazamo wangu naona sehemu kubwa ya masuala yanayosifiwa ni sehemu ya majukumu ya viongozi kwahiyo si lazima sana kuyasifia na kuyatangaza (mtazamo wangu).

Kongole Roma Mkatoliki kwa kuonesha mfano, sanaa ili iwe hai lazima iwe hivyo. Wakuu kazi ya sanaa sio kusifia peke yake, sanaa inatakiwa ikosoe pia. Hakika nitasikitika sana kama ikatokea wimbo huu wa Roma ukafungiwa. Viongozi watakuwa wameonesha udhaifu wa hali ya juu. Unapokubali kusifiwa lazima ukubali kukosolewa pia. Naamini Roma atakuwa amewasaidia watu wengi wenye mtazamo wake kuyasema yale ambayo hawawezi kuyasema

Naomba kuwasilisha.
 
Nenda ukajifungue kwanza mimba uliyonayo I nakupa kichaa,, kipi cha uongo Roma kaimba ??? Yaani wimbo aimbe yeye, anandike yeye, akarekodi yeye then useme hata mwenyewe hajui alichoimba??? Hivi wafuasi wa jiwe mmelishwa nini??? Au mmelishwa sumu kama ambavyo boss wenu alilishwa?
 
Back
Top Bottom