Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Ukiona Rais anaanza kuzungurukwa na majeshi na mabunduki, ujue Rais huyo ameanza kuhisi wananchi hawampendi na kinachofuatia ni kwa Raisi huyo kuanza hotuba za vitisho na pia kuanza kutoa amri za papo kwa papo.

Unajua watu walijenga imani kubwa kwake na kuona sasa wamepata Raisi msikivu ambae atakuwa anaenda sambamba na uwajibikaji kwa wananchi wake, picha inayoongezeka ni mvinyo wa madaraka na wakujiaminisha kuwa sasa anamiliki nguvu zote,tutaona mengi.

lakini sasa kinachoonekana ni style ambazo hazipatikani kwengine kokote hapa Duniani, ile kusimama na gari akatokeza kichwa na kuhutubia wananchi barabarani style ya Marehemu iron Man Magufuli.
 
Sisi wananchi tunasubiri mtekeleze ahadi ya kuimarisha uchumi wa nchi,

Hayo mengine ni yenu.
 
Japo I hope Samia hawezi kufikia level za ukatili, uonevu na kutojali kama Magufuli, lakini upo uwezekano akapata shinikizo na ushauri mbovu kutoka kwa wahafidhina wa CCM kuendesha nchi kwa staili ya kuonea wapinzani, kuvunja haki za wapinzani na hata ikibidi kuiba na kuvuruga chaguzi kama mwenzie aliyemtangulia.

Sasa Magufuli yeye alikuwa na long game, nadhani ni kubaki madarakani baada ya moaka 10, kwa hiyo kila alichofanya alilenga kimsafishie njia hiyo, kwa hiyo alinyamazisha vyombo vya habari, kuingilia mahakama, bunge, kununua watu influential, kuhonga vyeo etc Je Samia anaweza kuafford kufanya ubandidu huu? —Hatoweza umma utamkatalia sana, Kutakuwa na Sauti yenye mwangwi mkali sana wa kumkatalia

The only way ya kumsaidia Samia asikataliwe na Umma kwa kasi ya kutisha ni kufanya mabadiliko (Reforms), Mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kihaki. Haya Mambo lazima yaende sambamba, kimoja hakiwezi kusubiri kingine.

Samia awe macho na washauri wake hao wanaomshauri afanye mambo Kimagufulimagufuli katika masuala ya haki za kijamii za wananchi zikiwemo haki za kisiasa za makundi ya kisiasa. Hao watampoteza, watasababisha achukiwe sana.
 
Ukiwa kiongozi huwezi kumridhisha kila mtu au kila kundi
ukitaka kumridhisha kila mtu au kila kundi unaweza kukumbwa na mambo makubwa mawili:
1. utachelewa sana kufikia malengo.
2. Unaweza kupoteza mwelekeo.

Kinacho takiwa ni kufanya maendeleo yanayo wagusa wananchi wengi.
Madai ya katiba mpya ni madai ya kikundi kidogo cha wanasiasa wachache.
wananchi walio wengi mijini na vijijini wanataka kasi ya maendeleo iongeze, tunamuomba Rais wetu asicheleweshwe na kelele za watu wachache, wananchi wengi ambao hawapigi kelele wanamatumaini makubwa na yeye.
Kanyaga twende mbele kwa mbele.
 
Ukiwa kiongozi huwezi kumridhisha kila mtu au kila kundi
ukitaka kumridhisha kila mtu au kila kundi unaweza kukumbwa na mambo makubwa mawili:
1. utachelewa sana kufikia malengo.
2. Unaweza kupoteza mwelekeo.

Kinacho takiwa ni kufanya maendeleo yanayo wagusa wananchi wengi.
Madai ya katiba mpya ni madai ya kikundi kidogo cha wanasiasa wachache.
wananchi walio wengi mijini na vijijini wanataka kasi ya maendeleo iongeze, tunamuomba Rais wetu asicheleweshwe na kelele za watu wachache, wananchi wengi ambao hawapigi kelele wanamatumaini makubwa na yeye.
Kanyaga twende mbele kwa mbele.


Sent using Jamii Forums mobile app
Huwezi kupata hayo maendeleo unayoyataka bila siasa safi na uongozi bora
Ni katiba bora pekee inayoweza kuguarantee vitu hivyo!
 
Huwezi kupata hayo maendeleo unayoyataka bila siasa safi na uongozi bora
Ni katiba bora pekee inayoweza kuguarantee vitu hivyo!
Mbona kenya pamoja na kuwa na katiba bora haija "guarantee mambo hayo unayo yasema?
hivi sasa wanasiasa wamekimbilia mahakamani kudai mabadiliko ya katiba tena(BBI).
Siku zote wanasiasa wanataka kutimiza malengo yao tu ya madaraka na kugawana vyeo sio kuwaletea maendeleo wananchi.
Tanzania pamoja na kuwa na katiba ya zamani lkn bado imekuwa nchi bora zaidi ktk kuheshimu haki za binaadamu, Amani na utulivu, maendeleo n.k kuliko hata mataifa yenye katiba mpya.
kwa sasa hitaji la katiba mpya kwa Tanznaia ni upotezaji wa muda na rasilimali, jambo la msingi kwa sasa tujenge uchumi wa nchi yetu.
 
Mimi naongea tu kwa mfano kuna Marais duniani yaani wao hakuna wanachoweza kufanya kwa ufasaha!

Rais hawezi kudhibiti mfumuko wa bei
Rais hawezi kupambana na ufisadi
Rais hawezi kupambana na Rushwa
Rais hawezi kukuza democracy
Rais hawezi kuacha watu na vyombo vya
Habari kuwa huru kwenye nchi yao
Rais hawezi kutatua hata matatizo ya maji yaani maji yanakatika yeye yupo yupo tu na watendaji wa chini wala hawachukulii hatua.
Rais hawezi hata kutatua matatizo ya umeme yaani umeme unakatikakatika tu mpaka ikulu wanawasha Generator wala hashutuki kuwatumbua wahusika anacheka Cheka nao tu.

Rais anazungukwa na wezi na wapigadili ila hawezi kuwaondoa kwenye nafasi zao

Rais wa namna hii anapataje nafasi ya kuongoza nchi hata kwa wiki moja?

Wapo marais wa namna hii duniani yaani yeye hana anachoweza kila kitu "Maziganyanga"

Yaani kuna Marais hata akianza kuongea tu unaona hana chochote anachoweza kufanya bila chawa wake kutaka

Rais wa nchi unakuwa mnyonge umekata tamaa je wanachi watakuwaje?

Yaani ukimface tu unaona kwamba hapa tumepigwa hamnamo rais hapa

Rais wa nchi kuacha Ilani ya chama chako lazima uwe na self vision! Kama ni Ilani kila mtu akiwa pale anaweza kuitekeleza.

Kitu cha ziada ndio kinakufanya uwe Rais

Tusiruhusu tena kuwa na Marais type hii tufanye vetting ya kutosha.
 
Rais akiwa na self vision kama unavyosema wewe inasemekana hafati sheria na taratibu.

Vinginevyo nakubaliana na wewe kabisa kwamba nchi ikipata kiongozi mwenye uwezo wa kutatua changamoto ulizozisema anakuwa ni lulu kwa taifa.
 
Rais akiwa na self vision kama unavyosema wewe inasemekana hafati sheria na taratibu.
Vinginevyo nakubaliana na wewe kabisa kwamba nchi ikipata kiongozi mwenye uwezo wa kutatua changamoto ulizozisema anakuwa ni lulu kwa taifa.
Good
 
Back
Top Bottom