Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Jamaa kapigwa BAN lakini nasemaa TUMEPOTEA KWELIIIII...!! Yani mama anaendeshwa na JK wiziii juu ya wiziiii
 
Mtu anaetoa 1M kamapuni husika inakata 8,000 Halafu tozo ya serikali ni 9400!! Serikali ya WANYONGE.
 
Huyu mwanamke sijui anaongozwa na watu wangapi? Kila anaemwambia kitu anakubali aisee haya ni mambo ya ajabu sana.

Wizi wa mali za taifa wameona haitoshi sasa ni kumbana mwananchi.
 
Report ya uchunguzi wa BoT haijawekwa wazi kwa umma halafu unaanza kukata watu hela kwa lazima.

Kwahiyo mtoa huduma anatukata halafu anamlipa tax man kodi wakati huohuo maCCM yanachukua hela kinguvu kwenye same transaction? Huu sio wizi ni ujinga kabisa...
Tuamke Kumekucha
 
Kwenye pombe wateja ni wachache na wasingekusanya zaidi
Issue (JAMBO KUU) sio waziri au Raisat Samia, bali shida iko kwenye KATIBA. Basi!

Tukiishika KATIBA yetu kutokana Mbinguni,makato na kodi yatakuwa hakuna. Ila RAIA watapewa ruzuku. Mbona Nyerere na Karume Baba walifanya hayo. Na hata Magufuli alipambana kwa ajili ya hayo.

Mama una uwezo. Mbona Malkia wa UK, amemudu? Nchi yake haina mafuta, wala gesi, wala madini, wala misitu, shamba hawana. Nusu mwaka nchi ni barafu. Mbona ni matajiri.

Ah!! Wanayo centre of gravity imara - mihimili ya ta taifa lao mi3~
MAJUMBA HAYA MATUKUFU MATATU:
1) Buckingharm palace, alipo Malkia, nchi ni yake na ndiye mkuu wa dini ya taiafa lake.
2) Lumbath Palace alipo askofu mkuu wa Kantibury. Yeye ndiye mkuu wa kanisa LA anglikan. Na ni namba mbili kutoka kwa Malkia.
3) Jumba LA Bunge -10 DOWN STREET (yaani amrisha kumi zifuatwe chini mitaani) alipo Waziri mkuu.

KWA UTATU HUU UTAJIRI WETU UNAMWAGIKIA KWAO, WAKITAKA WASITAKE. Na Mama akakinga kapu lenye kudumisha mfumo huo. Jumba LA nne
4) Jumba LA CW {COMMONWEALTH [UTAJIRI WA PAMOJA] -waliloliita jumba la jumuia ya madola}

Wazungu wakoloni walituvua nguo (MILA, DESTURI NA JADI), tuko uchi. Hatuna maadili. Kizuri kwetu ndicho kibaya na vibaya ndivyo kwetu wametuhalalishia. Serikali kuu ni mradi wao wazungu. Bajeti ikipitishwa wao hufungua maduka yao kusubiri order za idara za manunuzi kutoka mawizarani mwetu.

Mbaya zaidi elimu waliyotufunza imetupa upofu, uziwi na ububu.

Jamani uraisi ni taasisi. KITABU cha uongozi hakipo. Kila aingiaye Ikulu anatumia bongo yake, ila Magufuli. Tutegemee nini?

Magufuli alikuwa na KITABU chake. Akanadi Mungu awekwe MBELE. Ukatuunganisha kwa salamu -SALAMALEKO (Amani iwe nanyi). Anageuka upande huu mwingine anasalimu -BWANA ASIFIWE.

Tunashauri Taasisi ya urais ilione hili Salamu iwe hii~ KWA JINA LA MUNGU WA BABA ZETU NYERERE NA KARUME NA BABU ZETU MKWAWA, KIMWERI NA HOROMBO MUNGU MMOJA, TUMEJISALIMISHA KWAKO; KAZI IENDELEE Q2:133.

HUYU tunayejisalimisha kwake, ndiye MUNGU, katuandikia KATIBA.

KATIBA hii imefichwa MADRASA. Inaitwa KANUNI YA IHSANI PAMOJA NA JUZ'U 3 1) AMMA {Mambo yaweje}, 2) TABARAKA {Tubarikiwe} NA 3) QADSAMIA {Watu wawe Wasikivu}. Ina jumla ya sura 58. Ina Ibara 1139.

Huu ni uchunguzi nimeufanya kwa muda wa miaka 53.

JAMBO NI HILI:

Hela tunazo, lakini mipango tumebaki shule ya Mzungu ~Mihimili angamizi mi3
1) SERIKALI
2) BUNGE na
3) MAHAKAMA.
UTATU HUU NDIO UNA TUTAFUNA. Hiki ndicho kidudu mtu.

Nalia mama NALIA. RAISAT SAMIA TUPO. JAHAZI HALIENDI MRAMA, ISIPOKUWA LIKIPAKIWA VIBAYA.

NCHI YAKO INAHITAJI CENTRE OF GRAVITY KWANZA IJULIKANE IKO WAPI.
 
Mwacheni mama aijenge nchi, atafute kodi kwa njia halali, sio kama lile dubuwasha lililokuwa linatafuta kodi kwa kubambikizia matajiri makesi ya uhujumu uchumi ili lipate pesa. Uchumi utajengwa na sisi wenyewe, hutaki weka ndani majambazi waje wazichukue au usafirishe kwa kukwepa gharama ya 20,000 upate ajali ufe au korona ukajitibu kwa milioni 10
 
Kuna muda nafsi ya kishetani inakuvaa mpaka unasema natamani mtu flani afe, waliofurahia naniiiiiiiiiiii kufa inawezekana wana sababu za msingi
 
Ila mimi nataka kujua ni wananchi wa jimbo gani waliomwambia mbunge wao kuwa wanataka gharama za juu kwenye miamala
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, KODI IENDELEE.
 
Magufuli alipowaambia anatetea wanyonge hamkumuelewa. Wengine mkadiriki kukanusha unyonge wenu. Haya sasa, fanyeni miamala hiyo mtume na ya kutolea, ninyi si siyo wanyonge bhana.
Wale wezi waliokuwa wanatuma sms za "ile pesa tuma kwa namba hii," sasa wameamia Ikulu
 
Ila mimi nataka kujua ni wananchi wa jimbo gani waliomwambia mbunge wao kuwa wanataka gharama za juu kwenye miamala
Wananchi hawajampa hoja mbunge wao ambae ni Zungu wa Ilala, isipokua Africa viongozi wetu wengi wabinafsi
 
Kwa mambo yanavoenda kuhusiana na kuongezeka kwa Kodi mbalimbali na hivo hii hali itapelekea Hali ya maisha kuwa ngumu sana huko mbeleni.Hali hii itaongeza wakosoaji kwenye utawala wa huyu mama .swali langu je atavumilia kukosolewa na watu wenye njaa?.

Naona mama atatumia nguvu ya Dola ili audumishe utawala wake,kwa ufupi mama anaenda kuwa dikiteta kwa hizi sera zake mbovu za uchumi.

Hali ya maisha ngumu Bado katiba mpya hivi vitu viwili vitampa Hali ngumu kwenye utawala wake na itabidi ajihami.
 
Back
Top Bottom