Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Mimi mwenyewe ,nimeshtuka, kumbe kuna watu 10000/= wanapata unit 73[emoji1787][emoji1787]
Ndio... Umeme wa REA ukinunua elfu 10 unapita units 70+ na una masharti.. ikitokea hizo units 70+ zimeisha kabla ya mwezi ukinunua units tena unapata units chache below 70
 
Mwanzoni ulipoingia madarakani, ulikuwa ukienda vyema. Kwa hilo pongezi ulizipata na matumaini mema yakaanza kurejea.

Pote palipokwenda kombo kukiwemo:

1. maongezeko ya kodi na tozo mbalimbali katikati ya janga la Corona,
2. kutozingatiwa kikamilifu kwa mapendekezo yakiwamo ya tume mbalimbali na wenye dhamana akiwamo CAG,
3. kuwepo kwa ubaguzi mbele ya sheria ambapo vigogo ni daraja tofauti, kodi hamlipi, chanjo mmepata, sheria nyingi haziwahusu,
5. kutokuzingatiwa kwa utawala wa sheria.

Ikiaminishwa kuwa hayo yalikuwa ni mapungufu ya watendaji wako tu. Ukisifiwa kwa kuyaweka maslahi zaidi ya taifa mbele dhidi ya mengine yote.

Wapo waliokuwa na mashaka nawe wakikuelezea mithili ya mama wa kambo:



Ni wazi kuwa vitimbi vyote vya polisi Mwanza na ukimya wako, ni kwa sababu yote ni kwa maelekezo yako.

Umeonyesha katika wanao kumbe kuna yatima pia.

Leo mnakamata watu na kuwapekua mkitafuta vifaa vya kutengenezea katiba mpya.

Yaani mnatafuta computer, karatasi, kalamu na vichwa vya watu.

Ujumbe utakuwa umefika.

Yatima hawako salama tena.
 
Huyu dada ametoa kauli iliyonishangaza sana.

Chadema bado ina tatizo la viongozi makini. Hawaelewi hata wanasimamia kitu gani.

Juzi tu hapa Mama Samia alikuwa anaupiga mwingi...Leo wameanza kumkumbuka Magufuli.

Chadema bado sana kuaminiwa kupewa hata majimbo....Mama Samia shikilia hapo hapo naona walikuwa wanapima kama muziki wako upoje.
 
Political prostitutes ndo walivyo
Say anything mradi uweze Ku trend hata kama si kweli
 
Hukustuka pale chama kilichotumia miaka 20 kuuaminisha umma kuwa fulani ni fisadi halafu kikatumia mwezi kuwaaminisha watanzania kuwa anafaa kuwa rais?

Wenye akili tulishajua hapa hakuna chama cha siasa, hii ni NGO.
 
Mama anaupiga mwingiπŸ˜‚.
 
Anatupeleka pale tunapostahili, huyu Mama kichwa kweli haki ya Mungu.
 
Wakuu,

Kama mtaniita mzee wa kukurupuka ni sawa tu maana niliyataka mwenyewe. Nilimuunga mkono Rais Samia bila kufanya uchunguzi wa kina, kiukweli kiongozi yeyote anaetumia uongozi wake kuumiza wengine kwa namna yeyote ile mimi hua sipo upande wake na kamwe simuungi mkono.

Nilifanya hivo kwa mwendazake na kwa huyu ni hivo hivo kwahiyo najitokeza hadharani kusema kua kwa matendo machache tu na yanayoumiza watu aliyofanya toka kaingia madarakani nasema mimi sipo upande wake kabisa hivo waliodhani vinginevo hapana nimeshtuka nimeshtuka nae ni walewale tu.
 
Utahangaika sana kaka.
 
Ukishaunga umeunga tu hakuna kupingulua mpaka mitano ipite.
Asubiri mitano iishe.

Si walikua wanashangilia, ooh mama amefungua nchi, nchi inaenda vizuri, sijui ujinga gani. Tuliokua tunapiga tulipewa matusi sio ya nchi hii, mara sukuma gang, mara tufe tumfuate Magu, mara tukubali Magu keshakufa na kashfa kadha wa kadha.

Leo hii mnakuja kujifanya eti mnajitoa, hakuna kujitoa hadi miaka 5 iishe.

Mama endelea kuupiga mwingi.
 

Usikonde mkuu. Kumwunga mkono mtu hakuna maana ya kuwa chawa.

Nilimwunga mkono na wengi tulimwunga mkono lakini hatukuwa vyawa wake (aione hii taslimu bwana Jumbe Brown Mzanzibara wa pale Mkunazini).


Mama Samia kabadilika baada ya zile sifa za siku 100. Akapandisha mabega na kuona kumbe yeye alifaa zaidi kuwa ndiye mnene mwenyewe hata enzi za uwepo wa mwendazake. Kwamba kumbe mwendazake alipaswa kuwa kidampa tu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚!

Hiiiiii bagosha
 
Nahisi Makonda amerudi kwenye himaya yake, zile picha hazikuwa za bure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…