Kajiarashid
Member
- Jun 2, 2021
- 69
- 27
ADUI?Ndo mkome kupapatikia watu haraka haraka!
Tuliwaambia adui yenu ni CCM. Siyo Magufuli.
Lakini hamkusikia.
Adui sio Magufuli, wala sio Samia na wala sio CCM; bali ADUI ni sisi wenyewe, tumekuwa wavivu wa KUFIKIRI.
TAFAKURI:
Neno hili TAFAKARI ndani ya Qur'ani, limetumika Mara 37.
"Je! Hamfikiri"?
Leo tuna miaka 60, baada ya uhuru wa BENDERA. Muda kama huu ni mrefu sana. Mbona hatujiulizi shida iko wapi?
SHIDA NI WANASIASA!!!!
WANASIASA kivipi?
Ilikuwa ni ada ukitoka form two kwenda form three, tunachaguliwa MASOMO. Wale wenye akili ya darasani hupangwa msomo ya sayansi. Na wale feliyaz (wenye kupata alama za sifuri masomoni), hupangwa masomo ya arts. {Nakumbuka mwenzetu mmoja tulisoma naye. Alipata F Tisa mtihani ule wa Kembriji miaka ile. Lakini wakati wa serikali ya Mkapa, alikuwa namba tatu kwenye usalama wa taifa}.
Weee bwana! Kumbe hii ni janja ya mkoloni. Kwani mkimaliza shule na kutoka vyuoni, wale feliaz, ndio huwa WANASIASA viongozi wa nchi, mikoa, wilaya n.k. Wao ndio wakuu wa majeshi, wakurugenzi, Mameneja kwenye maofisi hata benk na ndio Waalimu mashuleni. Wao ndio wapanga sera n.k. Wakienda ulaya hutandikiwa red kapet. Wao ni kuanguka saini bila hata kusoma kilichoandikwa, eeee. Huku anapigwa mabega wakimdhihaki -una akili!
Wale waliokuwa wana uwezo mkubwa wa KUFIKIRI darasani, wanaishia kuongozwa na hawa mbumbu Muzungu wa reli. Hawana lao, ila kufuata ukoloni mambo Leo. Ndio mainjinia, madoktari, waalimu, wahasibu n.k.
TAFAKURI:
Sasa tufanyeje? Kwani mbinu hii ya wakoloni ikikiukwa na akaingia MWEREVU IKULU, wanamuua directly au indirectily, bila hofu wala kizuizi chochote.
MUNGU TUMEMWACHA, NAYE AMETUACHILIA:
Wameweza hayo kwa kututenga mbali na Mungu wetu watu WEUSI. Kwa hiyo tukaibwaga dini yetu (UNYENYEKEVU), na kushikishwa dhehebu, taasisi na au shirika. ELIMU ikafichikana. Tumo kwenyeMKOROGO. Tumekorogwa ajabu Q50:5 . Humo, tukaingizwa kwenye uadui na faraka baina yetu. Na ndipo wakatutwanga rungu kuubwa kwa kuwakabidhi FELIAZ wetu vyama pinzani. Leo wengine wako ulaya, wanabwata ya kuwafurahisha wakoloni, hata kama anayosema ni kweli. Wazungu Hawahitaji kupambana nasi tena bali sisi wenyewe kwa wenyewe. Wao wazungu walicholenga ni KUTUFISIDI.
UFISADI:
Wameturithisha serikali iliyoundwa kuenzi wizara Mji mkuu 23. Wizara hizi, zikarudiwa kama idara mikoani na wilayani. Kwa hiyo bajeti humwagwa wizani mji mkuu kwa mabilioni. Pesa hizi kupitia idara ya MANUNUZI huishia ulaya for shopping. Manunuzi ya vifaa vya maofisini, magari n.k. Miaka sitini Leo pesa ambayo angepewa MJASIRIA MALI MMOJA, angefanya maajabu. Mwone Bahkhresa. Leo tungekuwa na Mabakhresa wangapi?
Lakini pesa ya nchi hutokomea Mji mkuu wizarani kwa mabook kipaz (makatibu wakuu), mikoani na walayani kwa wakurugenzi. Na yote inaishia shopping EEU, USA NA BRICS.
Tell me HUU SI NDIO UFISADI? Yuda 1:4
Wao WANASIASA wetu, wanaamini kuwa, manunuzi hayo wanayofanya ni ili WAJENGE NCHI Q2:11-12 kumbe wanaharibu.
ADUI YETU NI NANI?
ADUI yetu ni wewe na mimi tusio TAFAKARI juu ya mustakabali wa UMMA wetu. Na tumewaachia kikundi kidogo kilichopitia shule zilizo tayarishwa na wazungu kwa malengo yao wazungu na FAIDA kwao. Mitaala wakaisementi, Leo miaka 60 baada ya uhuru, vyuo vyetu vinazalisha wasaka AJIRA. UZALISHAJI MALI wameachiwa MAMANTILIE. Huu ni ufukara wa AKILI.
Oh!?!?!?