Kama aliivyonena Mwanabodi
Saint Ivuga ,
Kuhusiana na maswala kadha wa kadha kuhusiana na demokrasia na utawala wa sheria kwa awamu hii ya Sita. WANAHARAKATI WENGI NA WANASIASA walikuwa wakijaribu kumuasa Mama afanye kadha wa kadha wa kadha ama aaeche hili na lile. Mwanzoni ni kama alikuwa msikivu kwao lakini baada ya siku 100 za ubatizo hatimaye upepo ukabdili uelekeo na kuwapeleka mchakamchaka kwelikweli.
Kinachofuata ni kukimbiza malalamiko nje ya nchi na kweli tumeanzakuona wiki hii Jumuiya za kimataifaama wajumbe katika mikutano yao wakisema hili na lile kuhusuiana na hali ya Demokrasia, Haki za kukusanyika na utawala wa sheria kwa ujumla katika nchi hiyo. Taasisi hizo ni kama:
-Tume ya haki za binadamu na utawala bora Africa,
-Umoja wa Ulaya
-Canada kupitia Ubalozi wake
-USA
-Vyombo vya habari vya kimataifa kama Aljazeera, CNN ,BBC , N.K
Achilia hivyo hata hapo nchini Vyama vya siasa kama CUF, ACT , CDM; Kituo cha Haki zaBinadamu, Chama cha wanasheria (TLS),N.K nacyo vimekuwa vikipiga kelele hali hii.
Ukimya wa Mama na uimara anaounesha katika hili ni kipimo tosha kuwa wanaharakati na wanasiasa wasihadaike na upole, ukarimu au muonekano wake. Ni wakati sasa wa kufahamu kuwa Mama ameshajua ukubwa wa Power aliyonayo, ameshatambua nguvu ya kinga alizonazo so hasira, wivu ,adhabu na kuonya anaweza kuumia kuendana na Hulka yake. Si sahihi kusema labda anashawishiwa sana.
Tukikumbuka ukimya huu licha ya matamko ya jumuiya hizo , tunapata mrejeo wa kaka Meko alipoamua kufunga Masikio na kugawa dozi kwa wanaharakati kadha wa kadha wanaojaribu kupingana naye.
Ukimya wa Mama ni
Dalili tosha kuwa ameshakomaa, Yupo Imara kama ama zaidi ya Mtangulizi wake. Ni wakati sasa ya wanaharakati hao kubadili Strategy kwani Mama amehsafikia Level ya Meko na anaelekea kuipita, She does not care Anymore