Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Marais upatwa na Nini wanapoingia Ikulu?

Uwa najiuliza hili swali nashindwa kuelewa.

Hivi Samia aliyeenda Nairobi kumuona Lissu amepigwa risasi ndio huyu wa sasa ninayemuona?

Bado najiuliza madaraka Yana Nini kuwafanya watu wabadilike na kuwa Kama wanyama.

Samia Leo ndio wa kutaka kumfunga Mbowe kuhuni ? Na watu wake kumtishia Lissu asirudi nyumbani kisa madaraka.

Hakika natafakari sipati jibu Ikulu uwa zina Nini!!

Lakini nawaambia Malipo ni hapahapa duniani mtalipa kila kitu before mfe.

Tuendelee kuwepo muda utaongea.
 
change is the only law which is permanent and that law will never change.
 

Hata Idd Amini mwanzoni alionekana mkombozi.

Madaraka ni matamu na hulevya ndiyo maana waliotutangulia walitambua umuhimu wa kuwa na katiba madhubuti.

Tungali tuna safari ndefu.
 
Namuona wa siku hizi hadi sura anaikunja sijui hiyo tabia kafundishwa na nani?

Tunachotaka utawala wake ufuate sheria, sio kuvunja sheria makusudi halafu kututisha kwa kutukunjia sura na kubambikia wengine kesi, mambo hayaendi hivyo.
 
Sidhani kama alienda kwa ajili ya kumtaka hali Lissu. Kulikuwa na shughuli nyingine Nairobi ambapo alikuwa anamwakilisha Mheshimiwa Marehemu Rais. Ilibidi aende kumtazama kwa sababu wenyeji wake wasingemuelewa.

Kwa sababu hiyo sidhani kama amebadilika ila wengi tulimvisha joho ambalo sisi tulilipenda lakini sio yeye.

Amandla...
 
Samia wa leo ni rais na yule alikuwa makamu. Na ikimbukwe nyakati hizo hukuweza kwenda nchi za nje isipokuwa kwa kibali cha mtukufu. Nani aliyemtuma?
 
Tena huyu mama anaweza kuwa na roho mbaya kuliko jiwe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…