Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Mkuu technically Samia unayemuona ni yuleyule aliyekwenda kumuona Tundu Lissu Nairobi mwaka 2017. Ni muungwana, mpole, mcha Mungu na anapenda utawala wa sheria. Amejutanabaisha kuwa hapendi hata kodi ya TRA ya dhuluma.

Tatizo liko kwa akina Tundu Lissu na Mbowe wenyewe. Pamoja na kuwa walikuwa wanufaika wakubwa wa siku 100 za kwanza za Samia sijui walipatwa na pepo gani.

Kwenye mkutano wa Barccuda wakampandisha yule MDUDE CHADEMA mtukana matusi maarufu aliyekuwa rumande kuanzia mwaka jana na akawa ametoka recently na akatoa matusi mapya dhidi ya Rais. Kuwa atamnyoa kwa wembe aliomnyolea mtangulizi wake.

Na akina Mbowe hawakumchukulia hatua kumkanya, wakaona ni sawa tu.
Kwenye namna ya kudeal na watu kama hawa nasema Samia yuko SAWA. NJOONI MUNIUE
 
Ulishaambiwa na Wahenga kwamba Wapambe ni Nukusi
 
Maza tunamwelewa sana, kamwaga ajira zaidi ya elf 1 huko tra,

Wazanzibar wakichukua asilimia zao 21 za muungano, huku zinabaki nafasi kama 800 hivi, kiukweli si haba, ni nafasi nyingi hizi
 
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Madame Samia Suluhu Hassan
Mtemi Wa Watemi Chifu Hangaya



Anaupiga Mwingi Sana
 
Ipo siku tu wote tutaongea lugha moja! Bado miaka michache. Dalili zinaonekana.
 
Kama ni rangi ya Muangaza basi muangaza wa Raisi Samia ni wa rangi nyeusi,Black light hatuoni mbele wala hajatupa matumaini,zaidi tuna matumaini ya teuzi na kubadilisha wachezaji .

Atokee mpinga maendeleo yeyote wa CCM atueleze kuwa kabla ya mwaka wa uchaguzi 2025, jambo gani atakuwa amelifanya na kuonekana kuwa limetimia ? Nini amekamilisha aliyoyaacha Mh.Magufuli ?

Hata wasaidizi wa mikakati na agenda za CCM nao wamevurugika nini wakifanye ,hawana !! Kinachoonekana ni uzinguaji ,bungeni kule ndio kumezidi miujiza watu wanatia siku,kinachojadiliwa na kuamuliwa hakionekani hata wanachokiamua hurudi wakakijutia,tuseme wamebabaika ,wapo wapo tu ,mtu aseme hapa atokee CCM atueleze wameleta faida hii,wamepinga hili kwani halina faida na Taifa.

Nafikiri Tanzania haijawahi kupata bunge lililopotea njia kama hili lililopo,are they history maker?

Sasa bunge limekuwa kama sanaa au usanii tena wa uchekeshaji maana unaweza vunja mbavu ukibahatika kuliangalia kwenye runinga.

Amekosekana yule wa Mtwara, Mh.Bwege angalau akichekesha kimantiki na akifahamika.Ila hawa wa sasa unaweza kuvunja tv.

CCM mnaipeleka wapi Nchi hii?
 
Bibi bado anapambania jinsia kwanza

Aachane na mambo ya jinsia sasa akazane na kuonesha mafanikio ya uongozi wake. Asione aibu kutumbua watu ambao ni kikwazo kwa yale anayotaka kufanikisha hasa hasa kuleta mabadiliko kwenye baraza lake la mawaziri. Hakuna mtu anayependwa na watu wote duniani. Aepukane na kuangalia jinsia,dini na sura za watu anapofanya uteuzi bali weledi wao.
 
"mimi ni mama"
"mimi ni mwanamke"
"mimi ni bibi"
"mimi ni dada"
"mimi ni shangazi"
"mimi ni raisi mwanamke"
 
Mh: bwege ni wa mkoa wa Lindi wilaya ya Kilwa. ( mivinjeni ).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…