Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Kila mtu anafuraha,ajira,biashara,kazi za ujenzi,ukulima.Leo ukiwa na biashara yoyote hulali njaa.Wapo wanaouza bidhaa za madukani,bidhaa za kilimo,wote wanapata pesa.Ni mvivu wa kazi tu,ndio anayelalamika.
 
Mungu ampe Afya,uzima,umri mrefu,Rais wetu Samia Suluhu Hassani.Kila mwananchi,anayefanya kazi halali,anafurahi,kwa mzunguko wa pesa,uliopo.
 
Mimi naomba nikurekebishe usitumie neno "kumpuuza" ni neno kali sana kulitumia kwa kiongozi wa Nchi.

Pengine ungesema ni vitu gani ambavyo hujavipenda katika uongozi wa Serikali hii ya awamu ya sita au vitu ambavyo ungependa itekeleze serikali hii ya awamu ya sita.

Kwa upande wangu mimi ningependa Serikali hii ya awamu ya Sita iendelee msimamo wa Serikali ya awamu ya tano kuhusu mambo yafuatayo

Mosi, Corona 19

PILI,Kutokujenga bandari ya Bagamoyo.Maana nisawa na kuuza kipande cha nchi kwa wachina.

Tatu,Mafisadi kutolewa gerezani kiholela.

Nne,Kusisitiza kujitegemea,Badala ya kusafiri nje kuomba mikopo na misaada.Hiyo sipendi

Lakini pia serikali hii ya awamu ya sita kuna mazuri yapo imefanya

Mosi,Kidogo kuna uhuru wa vyombo vya habari.

Ningependa serikali ifanye marekebisho kidogo kwenye uhuru wa vyama vya siasa.Wapinzani waruhusiwe kufanya mikutano ya hadhara ili waonyeshe ufisadi kwa baadhi ya watendaji wasio waaminifu kwenye majukumu yao.

Yangu ni hayo tu.
 
Ni pale alipoongeza mapato ya serikali, kuvutia wawekezaji wengi, kuongeza pesa kwenye halmashauri zetu, kupandisha madaraja watumishi, kufuta kesi 400 za kubambikia, na kusimamia vizuri miradi yote ya kimkakati...nikaanza kumchukia
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Walimu wa msingi kusimamia mitihani sekondari na walimu wa sekondari kusimamia msingi. Walimu wa vyuo kusimamia darasa la NNE. Hii ni hatari sana.
MAMBO MENGINE SIO RAIS NI NDALICHAKO NA UMMY MWALIMU.

MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI.
 
Mimi sijampuuza, kimbuka amepokea Serikali katika mazingira magumu na hakutegemea, anahitaji muda wa kurekebisha.
Ila kuna jambo moja natamani kushauri: Ndani ya chadema hakuna mtu anayeweza kuwa mvumilivu kama Mbowe, ikitokea Mbowe akafungwa, akawa si Mwenyekiti wa Chadema, tutengemee kuja watu wapya wenye misimamo mikali, wasiotaka mijadala na hii itamgharimu Mama, huyu Mbowe anaweza kumfaa.
 
4. kujidhihirisha yupo team mafisi waloifisadi nchi na kuitia hasara kubwa.
giphy (2).gif
 
Wakuu salaam,

Mwanzoni mwa utawala wa rais samia nilimkubali sana, na niliamini ataliponya taifa, bt mambo yafuatayo yalipodhiri nilianza kumpuuza rais samia

1. kumbambikia mbowe kesi ya ugaidi ajili ya kudai katiba mpya.

2. kupanda ghafla kwa bidhaa alafu kakaa kimya bila kutoa tamko lolote.

3. kuminya demokrasia kama mtangulizi wake.

4. kujidhihirisha yupo team mafisi waloifisadi nchi na kuitia hasara kubwa.

je, kwako wewe ni yapi yalokufanya umpuuze rais samia?
Kudemka mkuu ndio kulinifanya nikaanza kumpuuza
 
"Mimi ni raisi haswa haswa" "jicho langu legevu lakini linaona mbali" Nani kasema 2025 sigombei"
 
4. Udini na ukanda( kufuta mawaziri 90% wa kanda ya ziwa, ilihali alishiriki kuwapendekeza Enzi za kwenda zake
5.Kuzunguka akiomba, omba pesa utafikiri tumekumbwa na mafuriko na sunami
6.Kutetea masilahi ya kina Makamba(deni NSSF), Kinana( mkataba na OBC kuuza wanyama kutoka ngorongoro),Riz na mkataba wa kuingia mafuta
7.kumpa hawara take airtime utazani ni waziri OR
 
Wakuu salaam,

Mwanzoni mwa utawala wa rais samia nilimkubali sana, na niliamini ataliponya taifa, bt mambo yafuatayo yalipodhiri nilianza kumpuuza rais samia

1. kumbambikia mbowe kesi ya ugaidi ajili ya kudai katiba mpya.

2. kupanda ghafla kwa bidhaa alafu kakaa kimya bila kutoa tamko lolote.

3. kuminya demokrasia kama mtangulizi wake.

4. kujidhihirisha yupo team mafisi waloifisadi nchi na kuitia hasara kubwa.

je, kwako wewe ni yapi yalokufanya umpuuze rais samia?
Alipokataa umuhimu wa katiba mpya nikajua hana tofauti na Kagame wala M7
 
Back
Top Bottom