Hahaha pls hajafikia huko loh..[emoji23]Mama hana jeuri ya kubana mianya,kwake kila kitu ruksa ili tu apate sifa binafsi ndio maana wasaidizi wake wanampinga. Leo hii si ajabu ata ukitaka kiwanja national stadium unaweza kupata[emoji23][emoji23][emoji2089]
Umeadimika sana ukumbini humu, natumai ni majukumu tu yamezidi.Ndio tunachotaka atekeleze miradi tutampa kura tofauti na hapo tutamfurusha yeye na CCM yake.
Rest In Peace JPM, Kazi iendelee.Mama Samia achana na cheap popularity haitakusaidia lolote unatakiwa usiwe muongeaji sana maana naona unaanza kutoboa matundu ya hela wakati huo ukiwa umewekwa kwenye mtego mgumu na mzito sana wa ilani yenye kurasa 300 ya kutekeleza miradi yote iliyoko kwenye ilani.
Yaani kumbuka sasa hivi hauko kwenye meli mpya uko kwenye meli ileile sema tu imepata mawimbi katikati ya safari.
Mama nimekushangaa sana unaposema kuna miradi mingine iko kwenye makaratasi wakati wewe na Hayati Magufuli ndio mliotembea nchi nzima kuinadi kwa hiyo tunataka ahadi zilizoko kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi.
Tofauti na hapo hatutakuelewa tutanyima kura 2025 kama ukitaka kuomba ridhaa ya kugombea tena.
Jitahidi sana kwenye suala la kodi usiwalaumu tu TRA waonye hata wafanyabiashara pia maana ni wakorofi.
Vyuma kumbe havijawahi kukaza enzi za Magu.Nikiwa sebleni kwa shemeji yangu na king'amuzi ameshakilipia huku na subiri dada apike ugali na nyama nile...Jana katika pitapita zangu kwenye kituo cha mafuta nimeona bei imeshapanda lita 2600 petrol..bidhaa nyingi zimepanda bei kuanzia vyakula, sabuni, gas migao ya umeme na maji vifurushi vimeminywa tena hali imekua mbaya sana..hali hii imekuja baada ya Rais wawanyonge kufariki sasa Mabeberu yanatawala yameamua kutuminya Wanyonge ili warudishe pesa zao walizobanwa na Rais wetu wawanyonge. RIP Magufuli...
Una jipyaWe utakuwa Sukuma Gang, nyie mna chuki za waziwazi na serikali ya mama...
Mama ameifungua nchi na sasa pesa zimejaa mtaani... Acha uchochezi na chokochoko muacheni mama arudishe furaha iliyotoweka.
Nakuja kula mkuuDada ameshapika chakula tayari njoo dining tule tushibe tuje tena siting room tumkumbke raisi wetu wa wanyonge jpm
RIP [emoji3064][emoji3064][emoji3064] TZ INAANGAMIA
Walimu wa msingi kusimamia mitihani sekondari na walimu wa sekondari kusimamia msingi. Walimu wa vyuo kusimamia darasa la NNE. Hii ni hatari sana.
Laana ya Magufuli itakuandama sana nenda Chato ukatubu fasta.Huyu bibi ashafeli mapema miezi 8 tu toka awe rais keshaharibu kila kitu
Watu wanaanzaga vizuri huyu miezi 8 mambo yashakua hivi
1.Makato
2.Matozo
3.Kubomolea vibanda machinga bila utaratibu
4.Migao ya umeme
5.Migao ya maji.
6.Ufisadi serikalini
7.Tozo za mafuta.
8.Tozo za mabenk
9.Kodi ya jengo kukatwa kwenya luku
10.Mfumuko wa bei
11.Mafuta kupanda ya petrol na dizeli
12.Mikataba isiyoeleweka.
13.Urasimu kurudi serikalini
14.Vifurushi vya simu kupanda bei
15.Kusimama kwa miradi mikubwa kama nyerere
16.Kufeli na kuanza kutoendelea kwa miradi ya umma.
17.Uzembe serikalini nidhamu ya utendaji imeshuka.
18.Nchi kupoteza mwelekeo.
19.Safari za nje zisizo na tija
20.Matumizi ya mabilioni na mamikopo yasiyokua na tija kwa taifa
Kwa haya Huyu bibi ashafeli, tungekua watz wote tumeelimika na kuelewa haya huyu bibi 2025 tusingempa kura!