Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Au hao waliyokuwa wanauwa enzi za mwendazake ndio hawa panyaroad?
 
Hiyo point no 5 nakumbuka Chato ilivyokuwa ikibebwa kiupendeleo mazuzu ya Jiwe yalikuwa yakikimbilia kujibu 'kwani Chato siyo Tanzania, basi halikadhalika hata Zanzibar ni Tanzania pia'.
Zamu yao wala urojo, kutesa kwa zamu.
 
T O Z O
 
Samahani mkuu...mie sio mbishani ila nimetaka tu kuweka vitu sawa na wala sina muda wa kutupiana maneno ya hovyo na mwingine.

Huyu mama samia anajikanyaga kwa kuwa...Mara baada ya kupitishwa kuwa rais wa TZ baada ya mzee.magu kufariki ilitakiwa yeye awe raisi wa 6 awamu ya tano...Simply:-

Kwanza, Kwa kuwa hawamu hiyo haikumalizwa na ili ikamilike ni kipindi cha miaka.10.

Pili, Yeye ni member wa chama sawa ha alichotoka hayati yaani CCM.

Tatu, Hakuna Awamu za kuteuliwa au kukaimu katika kitiba ya nchi yetu...bali awamu huja baada ya chaguzi(kupigiwa kura) kufanyika na mgombea husika kupatikana, kuthibitishwa na kuapishwa.

Nne, Na ikumbukwe kila awamu(kipindi cha miaka.10)...inakuja na Ilani/Malengo yake ya utekelezaji.


Turudi kwenye mada....

Hivyo kwa kuzingatia ivyo hapo juu...YAANI MAGU HAKUMALIZA AWAMU YA 5(MIAKA.10), YEYE RAIS.SAMIA HAKUCHAGULIWA KWA CHAGUZI NA PIA BADO ANATEKELEZA ILANI YA AWAMU YA 5 YA MAGU, Hakustaili kuitwa rais wa awamu ya 6...kwa kuwa hadi ivi sasa hakuna ilani ya awamu yake bali bado ni ya magu.

Na kama wewe utaibuka kusema hii ilani iliyopo ni ya awamu ya.6 EBU TUKUMBUSHE YEYE ANAYEJIITA RAIS WA AWAMU YA.6 ALIINADI WAPI ILANI YA AWAMU YA 6?(maana ilani kabla ya kutekelezwa ni lazima inadiwe na ilani hunadiwa kipindi cha chaguzi kwa mujibu wa katiba yetu ya 1977)

Hivyo basi, alistaili kuwa raisi wa 6 katika awamu ya tano(yaani anamalizia utekelezaji wa ilani ya magu/Ya CCM 2015-2025), then kwa mujibu wa katiba kwa kuwa alikaimu muda uliosalia kwa kipindi kilichozidi miaka.3( yaani miaka.4 iliyobakia)...katiba itamruhusu kugombea miaka.5 tu inayofuata akitaka kuendelea na sio zaidi.

Lakini kama angekaimu miaka mitatu au pungufu ya hapo...katiba ingemruhusu kugombea kwa kipindi cha miaka kumi kama akitaka kugombea, yaani hiyo mitatu, miwili au mmoja isingehesabika iliyosalia kwa huyu aliyefariki isingehesabika.

Hivyo, Ata mambo mengi MNAYOSEMA AMEYAFANYA NI UONGO KWA KUWA...MASUALA HAYO YALIKUWEPO KWENYE ILANI YA CCM MWAKA.2015-2025(Awamu ya tano[miaka.10])...hivyo kwa sababu yeye ni awamu ya 6...Fanya utuletee apa ilani ya awamu ya 6 unayoijua wewe na vipaumbele vyake wote tuvichambue apa jukwaani na useme aliinadi wapi?
 
Kulazimisha kuwa Samia ni rais wa awamu ya tano ni kituko, rais wa awamu ya tano 'ameshadedi' na huyu aliyepo si kwamba anakaimu hiyo nafasi ya awamu ya tano bali ameapishwa na kuwa rais wa nchi wa awamu ya sita.
Simple and straightforward.
 
Mfumuko wa Bei kwa bidhaa Ni kero kubwa na yey ndio kasababisha na makamb na Nani huyu wa skfu ya taifa mwigulu
 
Acheni uongo...nina ndugu yangu ni mmoja wa aliyepata ajira ya afya serekalini kipindi cha mzee. Magu kupitia mkono wa taasisi ya benjamini mkapa foundation 2018.

Mpaka rais magu anafariki katika kipindi cha 2015-2020 alikuwa amekamilisha ujenzi wa vituo vya afya.498. Na vingine vikiwa bado vinaendelea kujengwa...na hivyo ndo vimekamilika kipindi hiki cha rais samia, ivyo huo sio mradi wake bali ni mpango wa utekelezaji wa awamu ya tano na sio sita(ya samia).

Ona hapo ni 2018...utekelezaji wa hiyo miradi ya Vituo vya afya, zahanati, hospitali za rufaa wilaya na mikoa. Sikumbuki idadi kamili zilikuwa ngapi(zahanati, hospitali za rufaa wilaya na mikoa). Ila ulikuwa ni mradi wa Rais.Magu na sio Samia.

President's Office - Regional Administration and Local Government

Toggle navigation

JAFO: Ukamilishaji wa Ujenzi wa vituo vya afya 210 nchini ni wa kihistoria.​

Posted On: November 9th, 2018
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema kuwa tayari serikali imeshakamilisha ujenzi wa miundombinu vituo vya afya 210 na wakati huohuo vituo vingine vipo katika hatua za ukamilishaji na kuwa najumla ya vituo 350 vilivyojengwa katika Serikali ya awamu ya Tano ya Mhe. John Pombe Magufuli.
Mhe. Jafo ameyasema hayo wakati alipokuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa vituo vya afya vya Murriet na Kaloleni vilivyopo katika Halmashauri ya Jiji la Arusha leo
Amesema vituo vya afya 350 vimejengwa ndani ya miezi kumi na nane (18) ukilinganisha na vituo vya afya 115 viliyokuwa vikitoa huduma ya upasuaji tangu uhuru hadi mwaka 2015 hivyo ni mabadiliko makubwa katika sekta ya afya.
Amewashukuru Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Kamati za Ujenzi na wananchi kwa ujumla kwa kusimamia ujenzi wa miundombinu ya vituo vya afya kwa weledi na kuhakikisha miundombinu hiyo inakamilika kwa wakati na ubora wa hali ya juu.
“Ninawashukuru Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Kamati za Ujenzi wa Vituo vya afya, wananchi kwa kuwa kazi kubwa imefanyakika katika ujenzi wa miundombinu ya afya nchini na kuweza kukamilisha ujenzi huo kwa wakati” Anasema Mhe. Jafo
Mhe. Jafo amekiri kuwepo kwa changamoto za upelekeji wa vifaa tiba kwenye Vituo vya afya vilivyokamilika na kuwaagiza MSD kuhakikisha wanapeleka haraka vifaa tiba kwenye vituo vya afya vilivyokamilika ili viweze kutoa huduma kwa jamii.
“Bado kunachangamoto katika upelekaji wa vifaa tiba katika vituo vya afya vilivyokamilika wakati katika ujenzi wa miundombinu kulikuwa na fedha zilizotengwa kwa ajili ya vifaa tiba amabazo zilipelekwa MSD lakini inasikitisha kila eninapopita kwenye vituo vya afya vifaa tiba bado havijafika, hivyo nawaagiza MSD kuhakikisha wanapeleka haraka vifaa tiba katika Vituo vya afya ili viweze kutoa huma kwa wananchi” Anasisitiza Jafo
Mhe. Jafo anasisistiza kuwa haiwezekani kuwa na miundombinu bora ya afya lakini kunakosekana vifaa tiba jambo ambalo linasababisha kukamisha maendeleo na wananchi kutokupata huduma bora za afya na kwa wakati.
Akiongelea kuhusu changamoto ya Vifaa tiba Mhe Jafo amesema kuwa bado kuna changamoto kubwa ya uwpo wa vifaa tiba hivyo amewaagiza MSD kuhakikisha wanaweledi ujenzi na ukarabaati wa vituo vya afya nchini na kuwa kazi ya mfano katika ujenzi wa miundombinu ya afya na kuwa kazi ya mfano nchini.
Wakati huohuo Mganga Mkuu wa Jiji la Arusha Dkt. Simon Chacha amesema kuwa Ujenzi na ukarabati wa Kituo cha afya cha Kaloleni umegharimu shilingi milioni 400 ambapo hadi sasa ujenzi huo umefikia asilimi 45 na tayari majengo yaliyojengwa ni jengo la X-Rays, Jengo la Wazazi na Upasuaji, jengo la Kufulia nguo na ukarabati wa miundombinu.
Dkt. Chacha anasema kwa upande wa Kituo cha afya cha Murriet jumla ya shilingi milioni 700,000 zimetumika katika ujenzi wa jengo la wagonjwa, maabara, Jengo la Wazazi, jengo la upasuaji, Chumba cha kuifadhia maiti,, kichomea taka, Mfumo wa kuifadhia maji taka na ujenzi wa barabara ndani ya site lengo likiwa ni kutoa huduma za afya katika maeneo ya jirani kwa kuzingatia idadi ya watu wanaokadiriwa kufikia takriban 56401

Video​


Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22​

More Videos

Quick Links​

Related Links​

World visitors tracker​



Location Map​


Contact us​

Other Contacts



Visitors Counter​

Counter Started on: 27th. July 2015​

click here



Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.
 
Elimu bure ililetwa tokea mwaka 2015 na sio yeye ililetwa na mwendazake na ndo alisimamia hili yeye samia hajaja na sera ya elimu bure wacha kudanganya
Naikumbuka hii ila mzee.magu alifanya adi kidato cha.4 kama sikosei...mama kaja kaongeza adi kidato cha sita.
 
Mkuu ngoja tuwekane sawa...

1. Mama ameongeza tu miaka miwili ya A'level, lakini iyo ilikuwa ni sera ya mzee magu kuwa elimu bure adi kidato cha nne.

2. Madarasa yalishajengwa miaka mingi isipokuwa labda useme ameboresha miundombinu chakavu za madarasa na kuweka vifaa kazi vya kufundishia.

3. Hapo kwenye kupandisha madaraja na mishahara nampa pongezi lakini kuna maana gani kuongeza mishahara na huku garama za maisha na mfumuko wa bei ukiongezeka pia siku hadi siku(natumai ili unalifahamu hususani katika bidhaa za madukani tuzitumiazo kila nyakati NI TATIZO KUBWA).

4. Kodi bila mtutu, sawa ni nzuri hasa kwa kuwa kuna unafuu kwetu sie masikini lakini apo ndo anapigwa na matajiri/wafanyabiashara wakubwa...kwakuwa hakuna mifumo sahihi ya kudumu ya ukusanyaji kodi isipokuwa nguvu ya ukusanyaji mapato ndo imepungua.

5. Ajira za serikali alizotoa mama tumeshuhudia wazi sanasana ni za Afya na uwalimu...unavyosema ajira za taasis zote...unamaanisha zipi mbali na izo?

6. Hapo kwenye barabara ndo kabisa labda useme tu mama ameboresha ila asilimia 99% ni miradi aliyoitekeleza magufuli...kama hutojali tuwekee hapa barabara mpya zilizoanzwa kujengwa na rais samia(sio kukamilika kipindi hiki alichokuwa yeye rais)

NB: NA MWISHO KABISA MTOA MADA HAKUONYESHA VIASHIRIA VYA UDINI NA MADA YAKE, HIVYO NA WEWE UWACHE KUHUSISHA DINI YA MTU/WATU NA UTENDAJI WAKE PIA.
 
Kulazimisha kuwa Samia ni rais wa awamu ya tano ni kituko, rais wa awamu ya tano 'ameshadedi' na huyu aliyepo si kwamba anakaimu hiyo nafasi ya awamu ya tano bali ameapishwa na kuwa rais wa nchi wa awamu ya sita.
Simple and straightforward.
Hoja hupingwa kwa hoja ndugu, kila awamu ina Ilani yake ya kutekelezeka katika kipindi cha miaka.10, Sasa ilani yake ni ipi?..Na aliinadi wapi??...

Na kama hakuna ilani ya awamu yake ya 6...sasa yawezekana vipi rais wa awamu ya sita aendelee kutekeleza ilani ya awamu ileile ya 5???(na uku ukidai awamu ya tano ishapita kwa kuwa inafahamika rais alifariki)

Nasema amekaimu kwa kuwa hajapigiwa kura(kuchaguliwa na wananchi) ila kilichotokea ni "State of emergency" kufuatia kifo cha Predecessor wake...na kupitia katiba ikampa nguvu ya moja kwa moja ya yeye kuapishwa ili akaimu kiti/mamlaka na majukumu ya Uraisi TZ.

Na Pia kama hoja yako kuwa ni wa awamu ya sita kwa kuwa aliapishwa basi nakusikitikia, KWANI WEWE ULITEGEMEA YEYE KI VYOVYOTE ASHIKE MAMLAKA YA RAIS BILA KUAPISHWA?....ULIONA WAPI HII MTU ANASHIKA KITI CHA URAIS BILA KUAPISHWA DUNIANI??

Hilo jambo nilogusia la awamu na vipindi vya utawala...lilichambuliwa vyema hadi na kina pole pole ambao pia ni CCM wenzake...mwisho wasiku wakamtuliza yule kijana.
 
Tunaangalia nchi imenufaikaje.....Watu wa chini wanatakiwa wajitahidi waje juu tujenge nchi. Magufuli alijinasibu kuwa anawajali ninyi mafukara lakini mbona maisha yalikuwa ya ovyo. Acheni hizo, mmejifanya mmesahau.
 
1. Picha ya gari yako iko wapi?!!! Kuna mtu amesema anaitaka?!!!!

2. Kwani mama ye anahitaji kupendwa na kila mtu?!!!!! Umesahau kuwa ili ufanikiwe unahitaji maadui wengi zaidi?!!! Ye hajasahau. Isitoshe, a lioness doesn't concern herself with the opinions of the sheep!

3. Kalagha baho!
 
Gari aina gani kwanza isijekuwa ni 404 ya 1982
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…