Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

nakuunga mkono hata kama alimchukia sana mwenda zake apime kaurizake yake maana bado kuna watu wengi bado wanaona mwendazake alikuwa sahihi kwenye baadhi ya mambo, matendo yawe mengi kuliko maneno asionyeshe yeye ndo mdomo wa kikwete ni mapema sana kwa wao kutangaza ushindi.Kama alivyokuwa mnafiki kwaJPM watakuwa wanafiki kwake nawachumia tumbo walisha msoma sasa ni mwendo wa kukashifu utawala uliopita ambao kwa hakika NI huu huu wake na aliyeondoka ni , sioni tofauti maana hata yeye anatumia vitisho kwa sauti Nyororo mimi nbado nampamuda maana madaraka siku za mwanzo ni sawa na new money mpaka uzoee (New Money Spends by Trends, Old Money Spends by Tradition)
[/QUOTE]
Mwenda zake alizungukwa na wanafikiq watupu kama yeye alivyo kuwa mnafiki
 
😂😂😂😂😂
 
Unajuaje kama aliona abaki angalau hayo mapungufu tuliyoyaona ni baada ya yeye kuyapunguza ?

Yaani angeondoka hali ingekuwa mbaya maradufu..., Ni kama nyumbani kwako mwenza wako ni mchawi, unaamua kuondoka ili aroge watu zaidi au unabaki unakuwa unafichaficha baadhi ya matunguli hili madhara yasiwe lukuki
 
Mimi nasema tatizo letu kubwa tulilo nalo wafrika ni Njaa/Shida wakati wa utawala wa Donald Trump tumeona watu wengi tu wakikaa pembeni kwa hiari zao baada ya kutofautiana Itikadi na Boss wao yani Trump na mfano ni John Bolton aliyekuwa National Security Adviser ila pia kuna James Mattis Secretary of defence, Sio hao tu ni wengi tu ila huku Bongo unakutana na Takataka kama Kigwagwala ziko tayari kufanya ujinga wowote ili zibaki na vyeo vyao. Kwa mbali namshangaa mama pia ambae alikuwa Mshauri mkuu wa mzee wetu leo mzee katutoka kila cha mzee hakifai, Pumzika kwa Amani Magufuli hakika Umeacha alama ambazo kama taifa haina muda utakumbukwa, Ni kawaida ya mwanadamu kupenda Kipya ila after sometime hukichoka pia
 
".....kwani tembo na nyati wanakula hiyo helium hadi tusiichimbe(ndani ya hifadhi)?......" Nimeishasahau ni kauli ya nani, maana siku zinakimbia kwa speed ya mwanga.
Nipo naangalia upande wa kujiunga Kati ya Wafia Nchi au Wafuja Nchi.

cc mama D
Ni ushamba kyka kujisifia tuna hiki tuna kile halafu katika hicho hakuna unacho nufaika .
 
Mliua upinzani mkajua mmemaliza ...


Sasa humo humo ccm kumetokea mpasuko mkubwa sana ,mnamanguana wenyewe kwa wenyewe ...

Mama samia hakubakiana kabisa na li chama la mafisadi ccm na ndio kashikilia upanga sasa...

Lazima mchanganyikiwe ...


Mama samia kaza hapo hapo ...

Sisi watanzania wazalendo tuko pamoja ,..

Achana na hao wafia chama ,...

Hilo li chama hata likifa kama watanzania wanaishi maisha mazuri basi hakuna tatizo kabisa ....
 
Samia ni bora mara elfu 10, kuliko hayati aliyewaponda watangulizi wake waziwazi na kujisifia kwamba kila jambo yeye ndo kafanya, hata aliyoyakuta anaona anafaa kujisifia nayo.
Kama una kumbukumbu nzuri kuna wakati Benja alisema ni vema kuiita serikali ya CCM sio serikali ya mtu, alaf JK akasema viongozi wapunguze kujimwambafai.

Kwa hoja yako Hayati anastahili kuitwa mnafiki.
 
Msiwe wanafiki nyie kwa mnavyo muona huyo mungu mtu wenu alikuwa anashaurikaa?na hii ni kazi ya lile kundi tunalo ambiwa limepewa kazi maalumu kuhakikisha kila jambo la mama wanaliponda ili tu kufanya aonekane hafai.

Maana mmekazana kumlaumu mama mnasahau hata yeye magufuli kabla ya kuwa rais alikuwa waziri ndan ya serikali ya kikwete lakini alipo pata madaraka akajifanya yeye ndiye rais bora kuliko marais wote na aliwananga sana wenzie tena kwa maneno ya kejeli bora hata mama ana staha ya maneno na mlikuwa mkimshangilia sana wakati yeye katoka huko huko tena miaka mingi tu akiwa waziri.
 
Bado mdogo ukikua utaelewa
 
Umeyaweka wazi yote muhimu! What comes round go round! Mpaka sasa wateule wake wameshaanza kumng'ong'a[emoji848]! Ameanza vibaya kwa kukejeli mambo na baadhi ya maamuzi ya boss wake! Na tabia ya kuongelea mambo mazito yenye msitakabali wa taifa letu kujikomboa kiuchumi na akionyesha wazi nia ya kuvunja mageti yaliyowekwa kuzuia wezi, walanguzi, na mafisadi wa nje na wa ndani, huku akiwapa chapuo wawekezaji wa kigeni zaidi ya wa ndani, na hata kutochukulia uzito unaostahili juu ya mbuga zetu za wanyama na huku akionyesha wazi kutokuwa na taarifa sahihi na za kina kuhusu jambo lenyewe, ni hatari sana hiyo! Mtangulizi wake alifanyia homework na kupata uelewa stahiki kabla ya kufanya maamuzi! Kama rais wetu huyu mpendwa mama SSH anataka kuwainua wanawake wa Tz na Africa yote kuwa wanaweza, inabidi ajifunge mkanda kisawasawa na ahakikishe masaa24x7 yupo na Tz ili asidanganywe na yeyote yule ikiwa ni pamoja na 1st gentleman na jamaa wa karibu! Vinginevyo atakuwa amewafungia milango wanawake wote kuota ndoto za kupewa madaraka ya juu ktk dunia hii inayoongozwa na mfumo dume[emoji848]! Naamini kuwa maamuzi mengi kama siyo yote Mh. Dr. JPM aliyoyafanya hakumuhusisha mama yetu Janeth! Lakini sivyo kwa mama yetu huyu SSH, nina wasiwasi sana kama kuna uamuzi wowote ataufanya pasipo 1st gentleman hajauridhia! Hii ndio tofauti kubwa sana ambayo kama mama yetu huyu hatasimama kidete akijua kuwa nafasi aliyokilimiwa ni mtego na kipimo cha msitakabali wa uongozi wa wanawake Tz na Africa kwa ujumla, basi ataua matumaini ya mabinti wengi wanaoota kuja kushika madaraka ya juu kabisa kwenye nchi hii, maana hawataruhusiwa abidani[emoji24][emoji24][emoji24]!!
Bado anaweza kujirekebisha na kuwa the true 'Iron lady' of our time! Mungu ibariki Tanzania!
 
Mwacheni Mama afanye kazi msiwashwewashe,; hamjui jinsi watu walivyokosa matumaini chini mwenda zake; hotuba mbili tu watu wameshaanza kuresha furaha hata kama hawana fedha, lakini wanayo amani.Kaza hapo hapo mama.Kama yeye hakutaka kupangiwa maneno nawe Fanya hivyo hivyo.
 
Mama hana tofauti kubwa na mtangulizi wake, wote hawakujiandaa kuwa maRais. Imetokea tu coincidentally wamekuwa.

Utofauti wao ni kuwa Mmoja alikuwa anaamini kwenye manguvu, kukomoa na visasi huku mwingine akiamini kwenye Sheria, matumizi ya akili, taratibu za Nchi na kutopenda Dhuruma.
 

Kumpinga sio lazima uende ITV. VP alikuwa na uwezo wa kumuona wakati wowote. Kama mambo yalishindikana angeachia ngazi tungemheshimu kwa msimamo wake.
 
Tunashukuru kuwa tumetoka kwenye zama za kutishiwatishiwa na kukaripiwa kama watoto wadogo, na sasa tuko na huyu mama ambaye lugha yake ni laini. Hicho ndicho kitu pekee tulichokipata kufuatia mabadailiko haya ya uongozi. Nothing more, nothing less.

As a nation we are the same headless chickens now, just like we used to be under Magufuli. Clueless!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…