Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Katufanya tuuone Muungano ni wa kikuda hapo zamani,hatukuwahi kujua kuwa hawa wazanzibar,wanaitamani Tanganyika yetu, wametunyonya sasa wanataka watuuze na sisi kama Loliondo kwa waarabu na wauze nchi yetu kwaarabu,
#Muungano ni utapeli,Kataa Muungano
 
[emoji1][emoji1787][emoji38][emoji38]
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] eti uliona wapi
 
Kampa mbowe ruzuku anakula na watoto wake... Kamrudisha Lissu bongo anaishi hana pakukaa... Kamrudisha na kumlipia Lema deni la mkopo crdb alilokua amelikimbia... Kubwa zaidi nchi ipo huru wawekezaji kila kona... 💩💩💩
 
Kampa mbowe ruzuku anakula na watoto wake... Kamrudisha Lissu bongo anaishi hana pakukaa... Kamrudisha na kumlipia Lema deni la mkopo crdb alilokua amelikimbia... Kubwa zaidi nchi ipo huru wawekezaji kila kona... [emoji90][emoji90][emoji90]
Ujaelewa uzi! Hivyo vitu ni too common hata kila Rais anafanya: mfano JPM alimtoa Babu seya kifungoni. Kwa wenye akili uwezi kusema eti hilo ni jambo lenye mashiko

Lete jambo lenye mashiko ambalo amefanya hadi sasa SSH
 
Umeongea umbeya tu,
Mfano c lazima Wote tuajiriwe ,nimemaliza chuo Miaka 4,ckuwahi kuomba Ajira na sina Mpango ,niliamua kujiajir,
-Ajira cyo creativity,nchi za wenzetu watu hawawazi kuajirowa wanawaza wawe creativity ndo mana nafasi zipo.
Kumlipia sijui nani cjui,kumpa mbowe hela,
Inafaida gani kwa uchumi wetu ....!!
Hafai

Anatuuza

Mm nahisi angeanzia zanzibar kwanza,huku hapana
 
Za wengine zipi! Hii thread ni unique ndo maana mod ajaiunganisha na nyingine
 
ANAANDIKA BABA ASKOFU BAGONZA (PhD)

BANDARI: Tumefikaje? Tutatokaje?

Mjadala wa “kuuzwa”, “Kubinafsishwa”, “Kukodishwa” au vyovyote ilivyofanywa, umeonyesha nyufa za hatari katika nyumba yetu TANZANIA. Nitaje kadhaa:

1. Rushwa

Rushwa bandarini ndiyo imesababisha bandari ifanywe inachofanyiwa. Wakiishapeana rushwa, serikali inakosa mapato, mizigo inachelewa, inapotea, na bandari limekuwa pango la majizi.
Swali ni je, kila penye rushwa tuuze? Tubinafsishe? Tukabidhi sekta binafsi? Je rushwa ikishika kichwani na moyoni? Tujadili ufa huu bila jazba. Rushwa itavuruga wawekezaji wapya.

2. Umoja na Utaifa

Mjadala umeonyesha, wanaodai wanaujenga/kuutetea umoja na utaifa, ndio wanaubomoa. Wanaoonekana kuubomoa, ndio wanaujenga. Bandari imeujeruhi umoja na utaifa wetu. Hii ina gharama mbeleni. Tumejuana, tuishi kwa tahadhari.

3. Udini na Siasa Zetu

Viongozi wetu wana dini zao. Sitamani kuchagua kiongozi asiye na dini. Tatizo tunalo viongozi wa dini. Tunawakosoa viongozi wa dini ileee na kupongeza wa dini zetu. Au tunanyamaza mpaka tupigwe sindano ya kupongeza badala ya kushauri. Inapendeza kumkosoa na kumshauri kiongozi wa dini yako japo haizuiwi kumkosoa wa dini isiyo yako.

4. Ujuzi wa Sheria na Uchumi.

AJABU: Wanasheria walioongea tukaelewa ni wachache sana. Walio wengi ujanja wao unaishia Kisutu.
Wanauchumi wetu ujanja wao unaishia Kariakoo. Mkataba huu hawauelewi na wakiuelewa hawatuelezi tukaelewa. Huu ni ufa wa hatari.

5. Bunge

Hili lingebinafsishwa kabla ya bandari. Walichoongea bungeni sicho wanachoongea mitaani na kwenye baa. Wanamdanganya rais kuwa wanamuunga mkono wakati wamebeba mishale ya kumwangamiza. Mjadala wa Bandari umefanywa mgumu na bunge letu.

6. Serikali

Mjadala na tabia za watu vimeonyesha serikali hii si ya rais Samia hata kama kaiteua yeye. Hii ni mchanganyiko wa serikali zilizopita. Ina utii uliogawanyika - kiapo kimoja Chamwino na vingine huko makaburini, Msufini, na Butiama. Serikali bila “Uwajibikaji wa pamoja” ni sawa na genge la wasela. Ufa huu unadai tuanze upya.

7. Rushwa part 2.

Katika Mjadala wa Bandari tumesikia malalamiko ya rushwa za aina tatu: Wanaonufaika na uzembe wa bandari wakikazana kukwamisha mkataba; DP World wakikazana mkataba upite; na wanaoitwa wazalendo wasio wa taka DP World wala wazembe wa bandari LAKINI bila kutoa suluhisho. Ufa huu ni mgumu kuushughulikia bila kuchelewesha mkataba na kusikilizana kwanza.

8. Rais Wetu

Rais SSH ni wetu sote. Ni muhimu kama taifa kumkinga na mipasuko inayotokana na mjadala huu. Kuna maisha baada ya mjadala wa bandari. Yeye analo jukumu la kutuongoza sote na makundi yote mpaka tuvuke. Subira itatufundisha kuliko haraka. Ufa huu unazibwa kwa kusikiliza na kuchukua hatua.

9. Miafaka yetu

Mjadala huu umejeruhi miafaka yetu na kufukua baadhi ya makaburi. Baadhi ya makaburi tumekuta marehemu hawajaoza.
Katiba, maridhiano, Muungano, maelewano ya kidini, uhuru wa maoni na mamlaka ya wananchi bila bunge ni mambo muhimu sana katika kuziba nyufa zilizojitokeza.

10. Upinzani wetu

Mjadala unaonyesha aina mpya ya upinzani. Ndani ya chama tawala na serikali kuna upinzani mkali dhidi ya suala la bandari. Hii ni afya kwa nchi lakini hatari kwa utawala. Vyombo vyetu vijifunze kutotumia nguvu kupambana na maoni. Bora upinzani wa hadharani kuliko wa moyoni.

Nawashukuru wooote wanaochangia kwa hoja na kutuelimisha tulio wajinga wa sheria, uchumi, mikataba ya kimataifa na katiba yetu.
 
Du, kweli fadhila, mfadhili mbuzi hata mchuzi utakula.

Yaani yote aliyofanya SSH hata moja hulioni. Ngoja niishie hapa, maana kusema sana si kama mtu utakuelewa sana.
 
Kwangu chama chochote kikifa sawa tu, Cha msingi utanzania wetu.Mama Samia ni mzalendo wa kweli Sio yule mwenda zake
"Pendo hasegawa"

pamoja na kwamba umedandia uzi wangu nakushauri kama ungeanzisha wa kwako hizi point zingeelimisha wengi! Hapa ulipoichomeka wachache wataiona!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…