Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Education may be? Madrasa kiembesamaki Zanzibar. If I was CCM, I would have gone for Mwinyi
 
Chato gang mtajuaaje mama anawapeleka wapi na umafia wenu
 
kuna taratibu na sheria. ndio maana si kila kitu raia wanatakiwa wajue.
kuna nyaraka za siri.. na kila siri ina level nani ajue nani asijue.
Ni utaratib wa ki usalama nchi nyingi duniani.
Lakini mbona siri ishavuja? kuna habari inatrendi leo...very sad
 
Kufanya kitu gani kipya?
Alitaka awe na bashiru kama Cs wake wakati hawaendani kiitikadi?
Kusema Jodi inakusanywa kibabe ni kufanya vibaya? Kwani ni uongo?
Kufungulia vyombo vya habar ni jambo baya?
Kuteua mawazir na makatibu wakuu? Mbona hata marehemu aliteua? na kutumbua ? Tena wengine walishindwa mpaka kusoma viapo?
Kila mkuu wa taasisi lazima awe na management team yake . Hiyo inaitwa " organization"
 
Na wewe vipi kuhusu "...hizo makosa 6..."? issue ni ujumbe sahihi au niaje mkubwa!!
 
Marehemu alisema hapangiwi,acha atapangiwa kazi nyingine huko mbinguni na yeye.

Hayati Magufuli amewahi kukufuru kwa kusema ati "AKIFA HUKO MBINGUNI ATAPANGIWA KAZI YA KUWAONGOZA MALAIKA...." Ni kufuru jinsi gani mbele ya Mwenyezi Mungu...!!! Kuna vitu vingine Magufuli alijitengenezea kuondoka mapema kwa lugha alizokuwa akitumia....!!! Huwezi ,kumdhihaki Mungu ukabaki salama.
 
Na wewe vipi kuhusu "...hizo makosa 6..."? issue ni ujumbe sahihi au niaje mkubwa!!
Na wewe vipi kuhusu "...hizo makosa 6..."? issue ni ujumbe sahihi au niaje mkubwa!!
Mbona hata Hayati Jiwe alikuwa anakosea mara nyingi tu na mlikuwa hamuoni makosa kwa kuogopa kutumbuliwa au kupotezwa.
Nobody is perfect 100 percent.
Hilo la siku 14 au 21 ni UZEMBE WA IKULU maana yeye alipelekewa tu asome.
Walotakiwa kuwajibishwa ni Kurugenzi ya Habari Ikulu akiwemo Msigwa.
Mama mnataka kumpakazia tu....!!!
 
Anaturudisha kwa wapumbavu wasukuma na kutupeleka kwenye nchi ya ahadi
 
Maajabu

Baadhi ya wanaCCM kuwa wapinzani wa serikali
Baada ya kifo cha aliyekuwa ana imiliki CCM sasa mataga wamepotezana.....!!
Safari hii tutashuhudia vihoja na viroja......!!!!!CCM ndio watajua ilivyo hatari kutegemea akili za mtu badala ya Katiba na Sheria.
Hii miaka 4 hii tutaona mengi sana...!!!
 
Mama atauza nchi mapema dalili zinaonekana kabisa

Kama matarajio yako ulifikiri utawala wa mfalme Juha utaenziwa kwa maovu na makosa yake lazima upate shida kumuelewa mama. Ana siku chache sana ofisini tusilalame ovyoo
 
Kina Ndugai wameshaanza kumtongoza na miradi feki wapate mwanya wa kutupiga, hili taifa linaongozwa na mazezeta ya CCM.
 
Safari haijaanza, nyie tayari mmeshajua direction? Huu ni ufalme njozi
 
Tujikumbushe LIST OF SHAME!

1. Daniel Yona - Huyu alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu na faini ya shilingi milioni 3 kwa kulisababishia taifa hasara ya bilioni 11

2. Edward Lowassa - Kipindi akiwa waziri mkuu aliliingizia taifa hasara ya mabilioni kwa kutengeneza kampuni fake la kuzalisha umeme rejea kashfa ya richmond) Boss wake wa wakati huo Kikwete ndiye aliye ingiza taifa katika mkataba huu mbovu Lowassa alitii maagizo ya boss wake.

3. Rostam Azizi - Alijiuzulu ubunge kwa kile alichokiita siasa majitaka. Huyu ndiye yupo nyuma ya pazia kuhakikisha Lowassa anaionja Ikulu.

4. Andrew Chenge - Huyu ni mbunge wa Bariadi mashariki na aliteuliwa na CCM kuongoza tume ya kuandika katiba baada ya ile ya Tume ya Warioba kuvunjwa. Huyu pia ni mmoja wa waliopokea pesa toka Escrow kiasi cha dollar milioni 1 (Bilioni 2) kwa kile alichodai ni kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Rugemalira.

5. Daudi Balali - Huyu hajulikani alipo. Alipata kuwa gavana wa benki kuu na ndiye aliyeidhinisha wizi wa pesa kupitia akaunti ya EPA ambazo moja ya kampuni liliyokwapua pesa hizo ni Kagoda ambayo haijulikani ni ya nani,lakin kwa kupoteza ushahidi Jakaya Kikwete akamtoa Tanzania akampeleka Marekan halafu wakasema amekufa,amekufa lakini Twitter mzimu wake una chart...

6. Nazir Karamagi - Huyu alifukuzwa uwaziri baada ya kashfa ya Richmondi na anahusika pia na kufadhili mbio za Lowassa kuingia ikulu.

7. Patric Rutabanzibwa - Huyu amestaafu ukatibu mkuu

8. Nimrod Mkono - Huyu ni mbunge wa Musoma mjini na anatajwa kuwa karibu na kiongozi mkuu (Ayatollah) wa chama cha ACT.

9. Basil Mramba - Huyu alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu na faini ya shilingi milioni 3 kwa kulisababishia taifa hasara ya bilioni 11.

10. Jakaya Mrisho Kikwete-Huyu ni miongoni mwa viongozi wakuu wa nchi walio sain mikataba mibovu katika taifa hili, ndiye aliyewaingiza mtegoni mawaziri wake wengi wakasain mikataba mibovu sababu iliyopelekea hata mahakama ya mafisadi kushindwa kufanya kazi kwasababu kila mtuhumiwa mwisho wa siku anasema maagizo alipewa na"boss" Ndie mwenyekiti wa wanamtandao,anaongoza makundi ya wakwepa kodi na biashara zake nyingi halipi kodi.

#Logic unategemea Magufuli ange survive vipi katikati ya kundi kubwa la watu wenye nguvu kiuchumi na ma mastermind kama hawa? Wenye mtandao mkubwa ndani na nje ya serikali? Magufuli kwa kuwa mbabe aliwabana walipe kodi na kweli alikuwa mbabe kwasababu hawa waligeuza hii nchi shamba la bibi,madawa ya kulevya na kuiba rasilimali zetu bila huruma,wapi Magufuli angepona?

Hawa wametengeneza vijana ambao kwa macho wanaonekana ni wapinzani lakini rohoni ni watiifu wao,Zitto Kabwe is one among of them, kwa chain hii, mwema hawezi dumu ndani ya mfumo wa CCM. It's a simple logic wamemuua Magufuli, niambie CAG gani aliyeibua ripoti ya ukaguzi na madudu katika utawala wa awamu ya nne? Pamoja na Richmond et El, wapi Khan ripoti ya CAG ikielelezea madudu ya Kikwete? Who is a CAG kwa chain hii? Acheni upumbavu bhana.

Lakini sio tu kuwabana, Magufuli aliwakataa hakutaka kuambatana na hili kundi ambalo Mwl Nyerere aliwaita wanasiasa Malaya Malaya maana si heshima kuongozana nao na hawa ukishakuwa nao karibu kwanza lazima waku twist katika ishu za kodi ukishafungua milango ya kulegeza kodi jiandae kuwaabudu na kuwanyenyekea kwasababu ndio wanaojiita wanamtandao waliishika nguvu ya uchumi na siasa ya nchi. Mama Samia kazi kwako.
 
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) TUSAIDIENI.

1. Nchi imegawanywa katika makundi makubwa mawili. Kundi la kwanza linaongozwa na Viongozi wenye kuona kuwa JPM hakua mtu sahihi. Hawa wengi ni majeruhi wa Uongozi wa JPM kwa namna moja ama nyingine, wengi miradi yao haramu ilikufa. Kundi la pili linaunganisha wananchi wengi walioguswa na uongozi wa JPM. Hawa wanaona hospitali zimejengwa na huduma za afya zimesogea, watoto wanasoma bure, wanapata maji, umeme, barabara zinafikika, masoko, uhuru wa biashara. Wanaona kwa macho miradi mikubwa imejengwa ikikamilika itawasaidia na mambo mengine mengi. Nchi inakwaruzana CCM kimya, ipo kama haioni, haiwaonyi viongozi wake wala kutoa muongozo wowote. Utaratibu huu ukiendelea nchi itapasuka, wananchi hawatakubali kwa namna yoyote miradi iliyoasisiwa na JPM isifike mwisho kama anavyoshauri Muhongo, wananchi hawatakubali kunyanyaswa tena na wawekezaji kwa kisingizio cha kuwavutia kama ambavyo imeanza kutokea, Machinga na Mamantilie hawakubali shuruba katika biashara zao, nk.

Ushauri kwa CCM.

Nimekwishashauri, nashauri tena. CCM iitishe Kamati Kuu ya dharula isingoje Mkutano Mkuu wa April 30. Iitishe Kamati Kuu itoe kauli na muongozo, iwapige marufuku Viongozi wake kuendeleza mjadala huu hasa Bungeni. Serikali hii ni ya CCM, kuendelea kujibishana huku tutatofautiana kauli. Endapo Viongozi wakishinda kwa sababu ya madaraka yao wananchi tutaisubiri CCM ifikapo 2025 tuiadhibu. WanaCCM wengine tutaungana na Wananchi kuiadhibu CCM kwa sababu itakua imetaka yenyewe. JPM anaweza kuwa sababu ya CCM kufa au kubadilika, na kuimarika zaidi. Hakuna shortcut, CCM tusaidieni.

2. Serikali imekubali kuendelea kujitukana yenyewe. Bunge linaikashifu Serikali, CCM yenye Serikali na Bunge ipo kimya. Spika wa Bunge kusema kuwa Rais Magufuli hakushauriwa vizuri kuhusu mradi wa Bagamoyo maana yake Bunge limesema Rais hakushauriwa vizuri. Washauri wa Rais ni Makam wa Rais, Waziri Mkuu na Baraza la Mawaziri. Kwa kauli ya Ndugai (Bunge) maana yake ni kwamba aliyekuwa Makam wa Rais wakati wa Rais Magufuli hakutimiza wajibu wake sawasawa, aliyekua Waziri Mkuu wakati wa Rais Magufuli na Baraza lote la Mawaziri hawakutimiza wajibu wao. Huku ndiko kunaitwa kutokua na imani na Serikali kwa mujibu wa Katiba. Maana yake kwa kauli hiyo Bunge halina imani na Serikali na Serikali inapaswa kuanguka. Aliyekuwa Makam wa Rais ndie Rais sasa, aliyekua Waziri Mkuu ndie Waziri Mkuu sasa na karibia lililokua Baraza la Mawaziri lote ndilo Baraza la Mawaziri sasa. Kwa kauli ya Ndugai (Bunge) watu wote hawa hawafai, hawastahili kuwepo kwa sababu hawawezi kutumiza wajibu wao ipasavyo. Kwa nchi ya watu wastaarabu Serikali ilipaswa kuvunjika yote tangu kauli ya Spika ilipotoka au Spika wa Bunge alipaswa kuwajibika kwa kuichafua Serikali. CCM inaona vyombo vyake vinachafuana ipo kama haipo.

Ushauri kwa CCM.

CCM ivunje Serikali yake au imuwajibishe Spika wa Bunge. Ni rahisi mno, CCM iwaelekeze Wabunge wake kupiga kura ya kutokua na imani na spika kwa kuichafua Serikali au kama Spika yuko sahihi CCM iwawajibishe Wanachama wake Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Mheshimiwa Kassim Majaliwa na Waziri wa fedha wa wakati huo (Makam wa Rais wa sasa) kwa kushindwa kumshauri vizuri Rais wa Nchi na kwa uzembe huo Serikali inaweza kupata hasara kubwa. CCM ikiwawajibisha watu hawa, kwa kuwaondolea Uanachama, Serikali itaanza upya. Tume itaitisha uchaguzi mpya!! Tunafunga mjadala.

CCM ikiendelea kulea tatizo hili litakapokuwa sugu ijiandae kupata hasara kubwa mbele ya safari. Nchi haiwezi kwenda kwa namna hii ikizozana asubuhi hadi jioni, marehemu akichafuliwa bure. Nchi inajua Magufuli amefanya mambo makubwa kwa kipindi kifupi mno kuliko yeyote na haitarajiwi mwingine yeyote kumfikia. CCM ilinde heshima hii isiharibiwe. Aliyekuwepo na aliyepo wote ni CCM, Bunge na Serikali vyote ni CCM. CCM ndio yenye wajibu na Nchi hii hivyo ni lazima tuchukue hatua mapema za kudhibiti dalili hizi zenye kujenga uhasama katika Nchi. Imeandikwa; Usipoziba UFA utajenga UKUTA.
 
Ukiambiwa Walimshauri akakataa ushauri wao utasemaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…