Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Hembu msituchoshe na huyo mtu wenu, nani alikuwa na ubavu wa kumshauri, yeye aliamua kuwa kama alivyokuwa akiamini hakosei na yeye ni bora kuliko Mtanzania yeyote, sasa uvundo unapanda juu, vumilieni tu awekwe wazi hakuna namna.
 
Huyu ndiye fisadi papa na kiongozi wa genge la mumiani la 'msoga gang'
 
Shida alikuwa Jiwe. Washauri CCM watenganishe, Rais asiwe Chairperson ili iwe rahisi kumdhibiti
 
CCM ivunje Serikali yake au imuwajibishe Spika wa Bunge. Ni rahisi mno, CCM iwaelekeze Wabunge wake kupiga kura ya kutokua na imani na spika kwa kuichafua Serikali au kama Spika yuko sahihi CCM iwawajibishe Wanachama wake
Hapo ndipo ukweli ulipo

Kula kichwa cha Spika

Itapunguza gharama na heshima mpya itaanzia hapo

Huko DRC Kongo ndicho kilichofanyika na nchi inasonga mbele

Who is Ndugayi kwa amani ya taifa

Nimtu asiyenafadhila Raisi alimuidhinishia mamillioni ya fedha za kigeni kuzidi zinazo ruhusiwa leo hii anamgeuka Hayati na CCM iliyomkingia kifua

Kweli CCM aliinunua Magu na ameondoka nayo safari hii kwenye uchaguzi mnaenda kuzomewa na Polisi siyo Wananchi kama 2015 mlipokuwa mnaficha magwanda yenu ya kijani.
 
Mleta mada wala usipoteze nguvu zako na akili zako kumpambania Magufuli. Wewe fahamu tu, Magufuli ameshakufa (hana kitu cha kufanya tena) na makada wa CCM waliomzunguka kipindi akiwa hai wengi kwa sasa wanafurahi na kushangilia, maana walikuwa hawampendi lakini kwa unafiki walijificha kwa kumsifia na kumpamba kwa kila ujinga na upumbavu kiasi cha kumwita mungu.

Kwa sasa wewe anza kupambana na hali yako, kuusaficha uchafu wa Magufuli hautaweza milele. Marehemu kiujumla hakuwa mtu mzuri.
 
Asingechapisha kura za bandia saa hizi angekua anakula sato Chato na kupokea pension ya mstaafu.
 
Rostam Aziz huyu huyu aliyemwambia agombee ubunge Morogoro au mwingine?!
 
Upumbavu nao no mzigo,
Ulitaka ampinge ili amsuicide?
Ulishawahi ona mtu yeyote aliyempinga Magufuli akabaki salama?

Umeshawahi jiuliza kwanini watu wamemkubali Sana huyu Rais?
1. Mcha Mungu
2. Anakugusa kero za maisha yao
3. Imani ya matendo siyo ya mdomoni, kuwaaminisha watu kumtanguliza Mungu huku unapiga watu risasi
 

Watanzania wengi akili zao ndogo hata magufuli alianza hiv na alipendwa baadae wanajua wenyewe samia ni mfumo utakaomfanya arudi kwa magufuli hawez kucheza nje zile bit kilio kipo karibu jana waandishi wamekamatwa huko ilala unategemea shetan atakuwa malaika? Haipo hiyo samia atakuwa timamu kama atakuwa nje ya ccm na katiba inayomlinda
 
Iko kwenye makaratasi....... Ni kwa sababu haijaanza kutekelezwa (ANDIKO LA MRADI). Utekelezaji hufanywa hatua kwa hatua kulingana na uwepo/upatikanaji wa fedha na kuimarika kwa uchumi ikiwa ni pamoja ya mpangilio wa vipaumbele.

Vile vile Rais alishatoa ahadi ya utekelezaji wa ilani pamoja na miradi ya kimkakati; ingawa hii pia haizui kuibuka kwa mambo mapya kwa sasa na pengine hata baadae.
 
Acheni unafiki nyie Chato! Sasa kukamatwa kwa waandishi wa habari Rais anahusikaje hapo? Kigogo2014 anawalisha matakataka!
 
Kaka, hata nyumbani kwako huwezi badiri Kila kitu kwa wakati mmoja.
Na hili ndilo kosa alilofanya Magufuli alipoingia madarakani.
Ndani ya miaka mitano alitaka haya,
1. Serikali kuhamia dodoma,
2. Kujenga bwawa na umeme
2. Kununua ndege
3. She
4. Ukuta mererani
5. Daraja kigongo
6 Airport chato
7. Ujenzi wa kivuko na Meri nk nk
HII NI AKILI?
Akasababisha maisha ya watu kuwa magumu afadhari ya wafungwa huko jela.
Maana mfungwa anachojua no kazi na muda wa kulala, hajui mwanamke, kusomesha, na kutunza familia, hajui Kodi ya nyumba Wala ardhi.

Mimi siyo muumini wa ccm islani, lakini no muumini wa viongozi toka Zanzibar, wanaharikia kwenye ccm tu.
MWACHENI MAMA AFANYEKAZI TARATIBU MSIMUINGILIE KWENYE MJUKUMU YAKE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…