Inashangaza Sana[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kinachonishangaza kwa herufi kubwa ni kwanini huyu mama anakubalika kwa kiwango hiki
na hawa wapinzani waliokua wanaichukia ccm kwa kiasi kile? kwanini? na kila hatua anayopiga
wapinzani wanapiga makofi na kufurahia,yani ni rahisi wa kwanza ambae wana ccm ndio tunamkosoa
na ni rais wa kwanza kutoka ccm ambae ni chaguo la upinzani,eti leo hii Mbowe ana hashtag #Samia2021-2030 kweliiiii?!!!?!?
natamani yote haya yawe ni ndoto,matamanio yangu ni mtu aniamshe aniambie Amka wewe,halafu nimsimulie nilichokua naota...
Anayeshangaaa atakua ana matatizo au ni ile hali ya kuona MPINZANI ni adui au kila anayekosa baya la ccm basi ni mpinzani.kiukweli mama ameanza vizuri...katika maisha kila mtu anapenda UTU wake uthaminiwa kwa rais aliyepita yy aliamini kwenye VITU zaidi na siyo ,Utu sasa mama Samia amekuja tofauti ndiyo maaana hata uwe mpinzani utafurahi tu.Inashangaza Sana[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Dunia haiishi maajabu.
hata kama asipokua na la maaana lakini UTU wake uwezi linganisha na aliyepita mama yupo hivi HAIBA yako inambeba.Hivi kuna watu wanadhani Samia atakuwa na lamaana kwenye Nchi kweli
Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Wale wa msibani hawakuwahi kulalamika kwamba kuna corona? Lkn hao wanaoomba kufanya mikutano wameshasema sio zaidi ya mara moja kwamba nchini kuna corona, na kuna kipindi waliwahi kutoka bungeni ili wakakae lockdown majumbani kwao. Sasa inakuaje waombe tena mkusanyiko wa mikutano? Lisu alisema mlinzi wa hayati Magufuli alikufa kwa corona, Mbowe nae alidai kuwa yeye ashapata chanjo ya corona. Sasa wanaomba mikusanyiko ya nini, kuuwa watu na hiyo corona yao au? Muda mungine unapoandika kitu jaribu kwanz kutumia akili yako kufikiri kuhusu swali lako sio unakuja na maswali kwa lengo la kutaka kumuonesha mwenyekiti kuwa unajua kuuliza na wakati ki uhalisia swali lako linakubana mwenyew kama hivi?Msibani kwa mwenda zake,mbona hawakuzuia watu kukusanyika?
Ety wamesahau , walikua wanamnanga haswa na walisema mzee wa angani na wakapiga hesabu za siku alizokaa angani , walimwita vascodagama, mara marcopolo..Hawa Wanaomsifia sasa ndo hao hao Watakaomnanga........Kama Enzi za Mzee Wa Msoga...! Tunaikumbuka ile Kauli Ya ' Raisi Dhaifu' ilitokea Wapi....!
Jamani msilazimishe mawazo ya Rais aliyetutoka yafuatwe na Rais wetu Samia Suluhu. WaTanzania tutamsupport Rais huyu hata kama ni sisi upinzani au wana CCM ili nchi yetu ipate maendeleo ya wananchi wote!! wakulima, makuli, walimu, bodaboda, wafanya biashara kubwa na ndogo, wafanya kazi serikalini na binafsi!Mama Samia achana na cheap popularity haitakusaidia lolote unatakiwa usiwe muongeaji sana maana naona unaanza kutoboa matundu ya hela wakati huo ukiwa umewekwa kwenye mtego mgumu na mzito sana wa ilani yenye kurasa 300 ya kutekeleza miradi yote iliyoko kwenye ilani.
Yaani kumbuka sasa hivi hauko kwenye meli mpya uko kwenye meli ileile sema tu imepata mawimbi katikati ya safari.
Mama nimekushangaa sana unaposema kuna miradi mingine iko kwenye makaratasi wakati wewe na Hayati Magufuli ndio mliotembea nchi nzima kuinadi kwa hiyo tunataka ahadi zilizoko kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi.
Tofauti na hapo hatutakuelewa tutanyima kura 2025 kama ukitaka kuomba ridhaa ya kugombea tena.
Jitahidi sana kwenye suala la kodi usiwalaumu tu TRA waonye hata wafanyabiashara pia maana ni wakorofi.
Unaweza ukawa sawa, lkn Rais has never raised that issue!Mkuu vyama vya upinzani kupitia wenyeviti wake kama vile Mbowe, Tundu Lisu nk, wanadai kuwa nchini kuna corona. Sasa kama kuna corona kwa mujibu wa maneno yao wenyewe. Hauoni kama wakipewa ruhusa ya kufanya mikutano watasababisha maambukizi yasio ya lazima. Usihamishie lawama kwa raisi
Na sisi tuanzishe uzi usemao "ANAEJUA FREEMAN MBOWE ANATUPELEKA WAPI"??Huu uzi mbona ni kama ule wa jpm anatupeleka wapi???
Anasikiliza pande zote na kutaka kuridhisha kila upande, (hii ni sawa akiwa kama mama lakini akiwa kama raisi anatakiwa atoe muongozo na ausimamie muongozo wake mwanzo mpaka mwisho - Alianza vizuri kwa kuapa kurudisha umoja lakini ameishia kuupotezea na hana tena mpango wa kuugusia wala kushughulikia hilo)
Aliapa ataurudisha umoja na mshikamano, na alipokuwa anaapa hata "body language" pamoja na matamshi yake yalionyesha dhahiri hakupendezwa na namna ambavyo hayati John Magufuli alivyoligawa taifa kwa vyama na ukanda. Aliongea kwa sauti ya chuki dhidi ya uonevu dhidi ya kundi flani la watanzania uliokuwa umekithiri. Lakini baada ya kukalia kiti cha uraisi kwa wiki tatu amekutana na watu ambao wamemshawishi aachane na maono yake badala yake aendeleze yale maono ya mtangulizi wake. Ukiangaliza matamshi yake na hata "body language" utaona kabis amebadili gia angani, amegeuza kutoka kwenye muelekeo mzuri na amerudi kwenye mateso ambapo hata yeye mwenyewe kule mwishoni kabisa atateseka pia.
Siku zote maneno matupu hayavunji mfupa, mpaka sasa mengi ameyatamka tu kwa kinywa lakini hakuna hata moja alilotenda yeye kama yeye. Mfano, aliposema atarejesha umoja wa kitaifa ni vyema na ilistahili ayaainishe yale makundi yote ambayo yalikuwa yamepitia katika uchungu mkubwa na kuzungumza nayo kisha waone wote kwa pamoja nini kifanyike. Kikubwa alichoweza kusema kwa mdomo tu ni kwamba ccm ni ile ile na mambo ni yale yale hivyo amepingana na kiapo alichokula siku ile alipokuwa ana fikra safi ambazo hazichafuliwa.
Ni mengi ameyasema lakini asipoweza kuondoa udhaifu huu wa kusema tu kwa maneno bila vitendo basi ataishia kuumia nafsi yake na wengine wataendelea kuumia pia.
Samia kama unasoma huu uzi tafuta sana kufanya yaliyo haki na yale yote yaliyo kwenye mawazo yako maana wote wanaokushauri wanakushauri kwa kutumia matumbo yao na sio vinginevyo na bora hata ungetenda haya kwa kushirikisha wale wanaonekana wabaya na watakupa ushauri sahihi lakini wengine wote waliokaribu yako roho zao zimeharibika na wanawaza maabaya kwa manufaa yao na sio taifa letu.
Kila mtu amejaa ubinafsi...Judgmental na full of hutred...Mama anajitahidi kuleta umoja tayari makundi yanayotaka upendeleo na uhakika wa interests zao zina mvuta huku na kule...Mpeni basi nafasi, atendee kwa kadri ya ufahamu wake. Weakness kila mtu anayo, ziacheni kwanza weakness zake kuzeni talents zake ili apate confidence ya kuongoza nchi kwa amani na upendoIpo siku wote tutakufa na tutaacha yote tulioyapigania, hivyo tupiganie kuwaachia watoto wetu na kizazi chetu kwa ujumla mambo mema na yenye kuwapa baraka na sio laana. Afrika kwa ujumla mengi tunayowaachia watoto wetu ni laana tupu
Umeongea kwa point sana lakini, natamani kama point yako ingekuwa validi lakini naomba urejee clip ya siku mama anaapishwa uitizame mwanzo mpaka mwisho kisha angalia na clip ya siku za usoni ulinganishe je, anaelekea kwema ama kubaya? Akina majaliwa, mpango, kabudi, mwigulu, umi mwalimu, jafo, na wote wengine wameshambadilishia gia zake alizokuwa ameingiza tayari kuanza safari na sasa anaenda safari yao na sio yake.Kila mtu amejaa ubinafsi...Judgmental na full of hutred...Mama anajitahidi kuleta umoja tayari makundi yanayotaka upendeleo na uhakika wa interests zao zina mvuta huku na kule...Mpeni basi nafasi, atendee kwa kadri ya ufahamu wake. Weakness kila mtu anayo, ziacheni kwanza weakness zake kuzeni talents zake ili apate confidence ya kuongoza nchi kwa amani na upendo