Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Ogopa sana mtu ambae anapenda kuongea maneno matamu na anaeyependa kumfurahisha kila mtu... watu wa aina hii hawana msimamo na ukikosa msimamo kila mtu utajikuta unafata ushauri wake na mwisho kama ni dereva mtajikuta mpo mtaroni.

Inakwenda miezi 3 niambieni ni kitu gani cha maana ambacho huyu mama amefanya ktk mavitu yote aliyoongea nitajieni kimoja tu. Ila kwa vile wanaopiga mapambio ni wengi watu hawaoni udhaifu wake ila soon mtaona baada ya pombe ya kusifu na kuabudu kuisha kichwani.
Kuondoa retention ya 6% kwa wakopaji wa loan board, kutangaza ajira, promotion,
 
Nimeanza kupata wasiwasi haswa pale anaposoma hotuba, hotuba zake, tones ya sauti yake inaonekana kama inayovizia wasikilizaji, inaonekana ya mtu aliechooka na kama haitoshi ina kapresha fulani hivi, kapumzi cha kuhema, pengine ni unene alionao au hofu.

Japo anajisifu kuwa anafuata nyayo za Rais aliefariki Marehemu Magufuli na kuyatekeleza yale yote aliyoyaacha Marehemu, nakaribia kuapa kwamba hilo haliwezi hata azikiri...!

Magufuli alikuwa na uthubutu wa papo kwa papo na hata akiwa mbali, halazi damu kwa wazembe wa mchana kweupe. (Alikuwa na kasoro zake nyingi tu, ila alikuwa anajua kusimamia uchapa kazi).

Huyu Bikashoo nahisi anaona watu wako poa na kila akiitwa mama ,anasahau kama anavishwa kilemba cha ukoka. Mpaka sasa kuna mambo yameshaanza kupwaya, bado nasubiri kuona uchapa kazi wake, ila kwa sasa naona ni mtu wa mikutano wa kupenda kuhudhuria huku na kule akitoa hotuba na matangazo.

Rais Samia bado hajaonyesha uwajibikaji wa aina yoyote ile ,yupo yupo tu ,labda tusubiri mwezi wa ramadhani uishe, hayo ya kupanga Mawaziri ,makatibu ndani ya srikali na ndani ya Chama chake,si ya kushitua ni yao hayo ,na yeyote aakiipata nafasi hiyo ,hayo anaweza kuyafanya kwa mwembwe kuliko zake.

Ni jambo gani mwananchi anaweza kusema hili limefanyika kutokana na amri au uongozi wake,mimi sijaona kama yupo alieona atuwekee, spika amewaumbua askari polisi na kimeeleweka anachokisema, japo nae hana jema hata moja.

Tanzania haitajengwa kwa hotuba nzuri zilizosheheni ahadi.
Ataweza kuiongoza JK yupo
 
Labda tume kuhusu corona,japo kuunda tume na kuwajibika ni vitu viwili tofauti,hayo mengine yoote ni ablakadabra

Tunampima hatua kwa hatua. Kwanza tuzisikie ripoti hizi. Kisha tuone hatua zinazofanywa.

Kumbuka #1, #2 na #3 zinawahusu pia #4.

Benefit of doubt. Tunampa muda.
 
Hivi kweli Mtu ambaye amehudumu katika Siasa za Tanzania ( akiwa ndani ya Chama Tawala ( CCM ) kwa zaidi ya miaka 26 na ameshika 'Nyadhifa' mbalimbali za Uongozi nchini Visiwani na Bara leo unaweza kusema hafai Kuongoza na kuwa Rais?

Yaani Mama wa Watu 'mnamuandama' kwakuwa tu ni Mwanamke na Kiasili 'Haiba' yake ni ya 'Upole' tofauti na mlivyomzoea 'Mbabe' na 'Mkorofi' wenu?

Mwacheni Mama aandike Kitabu chake.
Unaona hatareee hii ? Kama uhaki utaonywesha Chama hicho alichokuwemo kilishaanguka zamani,na ushahidi mzuri ni Zanzibar na zaidi mkowa wa pemba,tuliache hilo.
Si kila mkuu wa jeshi anaweza kuwepo front line hata awemo jeshini kwenye vikundi mbalimbali,front line ni jambo lingine kufa au kupona,kuna Raisi amefariki hivi karibuni akiwepo kwenye vita dhidi ya waasi ,sio wale vita imeisha eti ndio anakwenda mstari wa mbele na mipicha kibao ,turudi kwenye mada.

Kuuliza si ujinga na maendeleo hayana Chama...sawasawa..., Rasi Samia ameingia kwa jazba na kuwaaminisha wengi kuwa anaweza,ripoti ya CAG na yaliojiri BOT yanachemka juu ya mabega yake ,sasa kimya kimekuwa kikubwa,pengine hakujua matokeo yatamgusa aliemteua au aliowateuwa,hatuwezi kujua.

Tunaona amecheza drafti kupanga kete anavyohisi yeye atashinda, kunapotolewa maagizo halafu ukaona kimya na hakuna haua wala update basi ujue hapo kuna tatizo la piga tajame.
 
Ulipokosea ni hapo pa 'mbabe' na ' mkorofi' wenu...inaelekea ulikuwa humpendi huyo 'mbabe' na 'mkorofi' na huyu naye inaelekea hampendi 'mpole'..ngoma draw
Ila mkorofi hapana [emoji16][emoji1787]
 
Sawa nakubali lakini tumpe muda kwanza, kumbuka Rais wa Nchi ana mambo mengi sana na kila zuri na baya yote ni yake, utekelezaji wa maelekezo unaweza kuwa na changamoto pia. Nafikiri mama atalisikia hilo la msemaji wao na yataisha tu kuwa na amani
Tuko pamoja bwashee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ogopa sana mtu ambae anapenda kuongea maneno matamu na anaeyependa kumfurahisha kila mtu... watu wa aina hii hawana msimamo na ukikosa msimamo kila mtu utajikuta unafata ushauri wake na mwisho kama ni dereva mtajikuta mpo mtaroni.

Inakwenda miezi 3 niambieni ni kitu gani cha maana ambacho huyu mama amefanya ktk mavitu yote aliyoongea nitajieni kimoja tu. Ila kwa vile wanaopiga mapambio ni wengi watu hawaoni udhaifu wake ila soon mtaona baada ya pombe ya kusifu na kuabudu kuisha kichwani.
Wewe tangu mama aingie madarakani miezi yote iyo umefanya nini cha maana mpaka sasa tuanzie hapo kwanza
 
WaTZ au WANANCHI; tumekuwa na tumeshazoeshwa KUPEWA kiongozi mmoja baada ya mwingine kwa MFUMO uleule, watu walewale, na porojo zilezile!
MFUMO huu nguvu zake zinatokana na jamii iliyogawanywa katika MAKUNDI makuu machache:

1. WATAWALA; wenye mamlaka serikalini, ndani ya CCM, mahakama, ktk BUNGE na vyombo vyote vya ulinzi na usalama.

2. WANANCHI; ambao kwa faida ya WATAWALA:

a. Wamegawanywa ktk vikundi visivyo na mwelekeo:
'wazee', 'vijana', 'wanawake' wafanyabiashara wadogo na wajasiriamali; na wafanyakazi ambao pia kupitia vyama feki chini ya TUCTA hawana mwelekeo, pia wanachama na wasio wanachama wa vyama vya siasa; wote wamenyamazishwa! Pamoja na wanaojiita watetezi wa haki za binadamu kupitia viji-NGO feki.


2. WANANCHI hawa kupitia vikundi tajwa hapa juu, hawana mamlaka kwa maana ya sanduku la KURA, (wameporwa SAUTI zao kupitia MFUMO).

Kwa neno 'MFUMO' namaanisha vitu viwili: Katiba ya JMT/1977 yenye (matundu), mianya ya UDIKTETA, na WATAWALA wenyewe kama nilivyowaainisha hapa juu; ambao wapo kwa madhumuni ya kulinda na kuutetea MFUMO na usalama wa mslahi ya kundi lao.

HAKUNA uwezekano wa kuubadili MFUMO kidemokrasia hata kwa namna yeyote. Ndiyo maana tunaona 'maigizo' ya kina Nyarandu, Dr. Slaa, Lowassa na wengine kila kukicha. Hayo si maigizo ya kujitakia tusiwalaumu.

Ila tukumbushane:
The hallmarks of bad governance:
1. Ambiguousness,
2. Arbitrariness,
3. Capriciousness.
 
Aisee mi sijakuelewa, anayeweza yuko?. Mi ni nachojua na kukiona mpaka sasa ameweza na anaongonza nchi.

Kila awamu au kila kiongozi wa awamu husika lazima kuna mambo yataenda vizuri na kuna mambo hayawezi kwenda vizuri!.

Mfano huyu mama ameweza kuundoa hofu miongoni mwa wananchi yaani ule uhuru wa kujieleza tunaanza kuuona kwa mbali ukirudi, wakati mtangulizi wake uhuru huo tulikuwa tunaona unapotea taratibu na watu walikuwa wamejaa hofu na kulikuwa hakuna wa kusema!. Mi kwangu hilo naweza kusema mwendazake kuwa hakuweza kuongoza!.

All in all niulize, je twaweza kusema Mwalimu nyerere aliweza kuongoza nchi hii?, je Mzee Mwinyi aliweza kuongoza?, je Mzee Ben aliweza kuongoza?, je Mzee Jakaya Kikwete aliweza kuongoza?, je Mzee Magufuli aliweza kuongoza?.

Hivyo itoshe kusema kila awamu ya uongozi wowote lazima kutakuwa na mazuri na mapungufu ya uongozi husika. Mama nae ameweza kuongoza ndio maana unaona mambo yanakwenda.
 
Ogopa sana mtu ambae anapenda kuongea maneno matamu na anaeyependa kumfurahisha kila mtu... watu wa aina hii hawana msimamo na ukikosa msimamo kila mtu utajikuta unafata ushauri wake na mwisho kama ni dereva mtajikuta mpo mtaroni.

Inakwenda miezi 3 niambieni ni kitu gani cha maana ambacho huyu mama amefanya ktk mavitu yote aliyoongea nitajieni kimoja tu. Ila kwa vile wanaopiga mapambio ni wengi watu hawaoni udhaifu wake ila soon mtaona baada ya pombe ya kusifu na kuabudu kuisha kichwan

Hata kichaa Lissu alisema tutaokota maiti barabarani kwa wave hiyo ya India, mbona hata yeye hajatuokotea hata maiti moja?? na wewe na machadema wenzako wave ya India ikipita mniokotee maiti moja mtaani tuone basi!! wacha kututisha!!!
Wee mpumbafu na spika wako kila siku unamuota lissu tu vp unamtaka
 
Unaona hatareee hii ? Kama uhaki utaonywesha Chama hicho alichokuwemo kilishaanguka zamani,na ushahidi mzuri ni Zanzibar na zaidi mkowa wa pemba,tuliache hilo.
Si kila mkuu wa jeshi anaweza kuwepo front line hata awemo jeshini kwenye vikundi mbalimbali,front line ni jambo lingine kufa au kupona,kuna Raisi amefariki hivi karibuni akiwepo kwenye vita dhidi ya waasi ,sio wale vita imeisha eti ndio anakwenda mstari wa mbele na mipicha kibao ,turudi kwenye mada.

Kuuliza si ujinga na maendeleo hayana Chama...sawasawa..., Rasi Samia ameingia kwa jazba na kuwaaminisha wengi kuwa anaweza,ripoti ya CAG na yaliojiri BOT yanachemka juu ya mabega yake ,sasa kimya kimekuwa kikubwa,pengine hakujua matokeo yatamgusa aliemteua au aliowateuwa,hatuwezi kujua.

Tunaona amecheza drafti kupanga kete anavyohisi yeye atashinda, kunapotolewa maagizo halafu ukaona kimya na hakuna haua wala update basi ujue hapo kuna tatizo la piga tajame.
Hivi unajuwa kuwa report ya CAG hata bungeni halijajadiliwa ?!. Na Bunge ndiyo yenye kuielekeza serikali nini hatua za kuchukua kufuatia report Ile. So usiwe na haraka kama kijana wa balehe
 
Back
Top Bottom