Andrew Chenge afika kwenye Kamati ya Katiba, awataka Wajumbe warudi kwenye Rasimu ya Warioba

Andrew Chenge afika kwenye Kamati ya Katiba, awataka Wajumbe warudi kwenye Rasimu ya Warioba

Mzee Chenge , mtu anayeaminika kuwa miongoni mwa wanaccm wachache wenye busara , leo amefika kwenye Kamati ya Rais ya kuratibu maoni ya Katiba mpya na kueleza yaliyo moyoni mwake .

Chenge ambaye pia ni Mwanasheria wa Zamani wa Serikali ya Tanzania hakumung'unya maneno , amewataka wajumbe wa Kamati hiyo kurejea kwenye Rasimu iliyopendekezwa na Wananchi , Amedai ni kweli si rahisi kumzuia Rais wa Nchi kuteua Maofisa wa Serikali , lakini anawateua kwa utaratibu gani ? ni lazima Wateuliwa Waombe nafasi na Wasailiwe , amesema utaratibu huu ndio utakoiletea heshima nchi .

Chanzo : Mwananchi
Mtu yeyote anayetaka kukwepa Rasimu ya Warioba basi ana jambo lake na hana nia na katiba mpya
 
Amedai ni kweli si rahisi kumzuia Rais wa Nchi kuteua Maofisa wa Serikali , lakini anawateua kwa utaratibu gani ? ni lazima Wateuliwa Waombe nafasi na Wasailiwe , amesema utaratibu huu ndio utakoiletea heshima nchi .
Wazee wa mtelezo a.k.a chawa wa uteuzi wakiona kauli hizi wanachachawa🤣🤣🤣
 
Kuna wakati saa mbovu ya mshale huonyesha majira sahihi. Chenge ni saa mbovu ya mshale iliyoonyesha majira sahihi.
Katika hili ninampa hongera Chenge.
Saa mbovu ni mbovu tu

Hakuna muda inasoma majira sahihi


R.jpeg
 
hakumung'unya maneno , amewataka wajumbe wa Kamati hiyo kurejea kwenye Rasimu iliyopendekezwa na Wananchi , Amedai ni kweli si rahisi kumzuia Rais wa Nchi kuteua Maofisa wa Serikali , lakini anawateua kwa utaratibu gani ?
Na mimi simung'unyi maneno, je hakuwemo kwenye BMK wakati ule!?
 
NI kweli mzee chenge amepatia.kuwa waziri wa mambo ya ndani alafu unadai katiba mpya ya warioba.anahitaji kupongezwa Sanaa mzee chenge
Kuna wakati saa mbovu ya mshale huonyesha majira sahihi. Chenge ni saa mbovu ya mshale iliyoonyesha majira sahihi.
Katika hili ninampa hongera Chenge.
 
Mzee Chenge , mtu anayeaminika kuwa miongoni mwa wanaccm wachache wenye busara , leo amefika kwenye Kamati ya Rais ya kuratibu maoni ya Katiba mpya na kueleza yaliyo moyoni mwake .

Chenge ambaye pia ni Mwanasheria wa Zamani wa Serikali ya Tanzania hakumung'unya maneno , amewataka wajumbe wa Kamati hiyo kurejea kwenye Rasimu iliyopendekezwa na Wananchi , Amedai ni kweli si rahisi kumzuia Rais wa Nchi kuteua Maofisa wa Serikali , lakini anawateua kwa utaratibu gani ? ni lazima Wateuliwa Waombe nafasi na Wasailiwe , amesema utaratibu huu ndio utakoiletea heshima nchi .

Chanzo : Mwananchi
Leo Chenge ni Mzee mwenye Busara? Hii nchi ngumu sana.... 🤣
 
Back
Top Bottom