Moo Click
JF-Expert Member
- Feb 18, 2015
- 3,495
- 3,236
30 jela DoneYule DC mtesaji na mporaji huenda ana mkono wake ... achunguzwe...
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
30 jela DoneYule DC mtesaji na mporaji huenda ana mkono wake ... achunguzwe...
Wakomae wapi wewe kibatala ni mwizi tu km wezi wengine wa serikali.hapo hiyo kesi nenda rudi kwake yeye ndio anataka posho.Ndo maana wakina Kibatala wamekomaa na hii kesi...
Utakuwa unakaa kwa prof.Mwaikambo.Unamjua Masorogo?Kuna siku polisi walinikamata, wakawa wanataka kunibabatiza na kesi zao za kipuuzi.
Wakawa wanataka kunipeleka kituoni.
Nikasema sawa, si tatizo. Ngoja nimpigie simu mshua nimtaarifu mmenikamata watu nyumbani wapate habari nimekamatwa na polisi. Halafu mtawaeleza kosa langu ni lipi.
Wakaniuliza kwani mshua wako nani?
Nikawaambia mshua tu.Msijali.
Nikaona wanaanza kuogopa.
Wakang'ang'ania kumjua.
Nikawatajia.
Haraka sana wakaanza kujibaraguza basi nenda tu.
Nikasema hapa kama mtu hajulikani angelala polisi.
Siku nyingine tumekaa maskani Upanga.
Tunaona polisi kama 20 wametanda mtaani wanakuja.
Mimi nikawaambia madogo fulani tumekaa nao, nikasema hapa kama mtu hawezi kuongea nao hawa ajikate kabisa, hapa tunabaki wabishi tu.
Basi wakafika mpaka pale tulipokuwa.
Mmoja akaanza kusema "hapa mnafanya nini nyie?".
Dah, kosa. Jamaa mmoja akamjibu "Hivyo ndivyo mlivyofundishwa kusalimia watu?"
Ikawa kama mzozo. Watu wakasema hapa tupo nyumbani.Polisi wakaanza kuuliza mmoja mmoja, wewe unakaa wapi? Watu wanaonesha nyumbani hapo, nyumbani hapo.
Wakamfikia jamaa mmoja tuko naye maskani.
Wewe unakaa wapi?
Jamaa akajibu "Kwa Ben".
Polisi wakawa wanashangaa, wakauliza, kwa Ben? Ben gani?
Jamaa akajibu, Ben Mkapa huyo huyo wa Jamhuri ya Muungano, kwani wewe unamjua Ben gani?
Hapo rais ni Ben Mkapa.
Askari wakastuka. Ikawa kama hawaamini.
Mmoja wao akawa kama anawanong'oneza, nikamsikia anasema "huyu namjua, nilikuwa namuona nyumbani kwa Mkapa pale Sea View kwenye lindo". Presumably wakati Mkapa akiwa Waziri.
Basi hapo hapo tukaona askari polisi walioanza kutuingia kwa inda wanabadilika mara moja.
Wakaanza kusema "mnajua wazee ni katika kufahamiana tu, hatukuwa na lengo baya, ni kufahamiana tu".
Nikasema hawa huko mitaa ya watu wasio na majina wanawakamata watu na kuwatoa upepo vizuri sana, bila kosa.
Bahati yao mbaya leo wamekutana na kisiki.
Ile maskani waliipigia alama kituoni kwao, waliambizana maskani hii msiguse, kuna mtoto wa rais anakaa hapo.
Haki ya kikatiba ya kila mtu ya kutosumbuliwa na kuchukuliwa hana hatia mpaka atakapopatikana na hatia inavurugwa na inakuwa privilege ya watu wenye majina.
Kazi ya Sabaya na Afande JumanneDuh hao polisi walimgusa mtu ambaye hawakumjua, Prof huyo lazima atakuwa na connection.
Sasa polisi hao wamembambikia nyara hizo ili wamtemeshe pesa dah.
Ova
Kwani PGO inasemaje?Hivi polisi wanapokamata mali kama hizi juwa wana utaratibu gani wa kuhifadhi? Maana juzi wamekamata heroin zaidi ya tani moja, wasije wakawa wamegawana huko.
Mabosi wenyewe wanawatuma ili wawafurahishe wateuzi.Kama waliweza kuweka pembe za ndovu kwenye mzinga ili wapige hela ya mstaafu watashidwa kutengeneza kesi kuwafurahisha maboss
Na ndio kazi ya mwanasheria. Penye kesi ndio mlo wake upo. Kwani ni tatizo?Wakomae wapi wewe kibatala ni mwizi tu km wezi wengine wa serikali.hapo hiyo kesi nenda rudi kwake yeye ndio anataka posho.
Bila kesi huyo jamaa hali.
Askari mmojawapo yupo kwenye kesi ya mbowe kama shahidi upande wa Jamhuri
mtu kakaa mpaka ikulu alafu unambambikia kesi😂 ,mzee hata hapo kawahurumia yeye ilikuwa ni simu moja tu anapiga ikuluDuh hao polisi walimgusa mtu ambaye hawakumjua, Prof huyo lazima atakuwa na connection.
Sasa polisi hao wamembambikia nyara hizo ili wamtemeshe pesa dah.
Ova
Hao polisi waliyavagaa kwelimtu kakaa mpaka ikulu alafu unambambikia kesi😂 ,mzee hata hapo kawahurumia yeye ilikuwa ni simu moja tu anapiga ikulu
na huyo Masotogo ndio wewe Boss😂Utakuwa unakaa kwa prof.Mwaikambo.Unamjua Masorogo?
intelijensia ilikwama😂Hao polisi waliyavagaa kweli
Ova
Aisee!Kwa wasiomjua huyu prof. Lile ghorofa pale Leganga ambako TRA wamepanga,NSSF etc ndio la huyo dingi.
Na lile jengo ambako Meru Community bank walikua wamepanga ni la mdogo wake huyo Prof.(ambako ndipo alipoenda kuomba hio mil 30 iliyopelea kwny ile rushwa ya mil 100).
Connection tu ndio ilimuokoa mzee na huo msala,lakini kuna wengine wengi washabambikiwa misala kama hiyo na pesa zikawatokaHao polisi waliyavagaa kweli
Ova
hapa namtetea sabaya,hakubaka ila walikuwa wanampa wenyewe tu,nasikia wengi wao ni wanachuoSabaya ni Jambazi ,alitaka kumuua Malisa GJ.....Jambazi alitoki tena kuna kesi 7 mafaili yanaandaliwa aingizwe kwenye 18 bado za ubakaji sema hizi za ubakaji hazina ushahidi wa moja kwa moja labda watumie busara ya kuwasikiliza wabakaji na kuyafanyia kazi malalamiko yao maana waliobakwa ni zaidi ya mademu 44.
Kweli kabisaConnection tu ndio ilimuokoa mzee na huo msala,lakini kuna wengine wengi washabambikiwa misala kama hiyo na pesa zikawatoka
Kuna watu wengine viherehere sanaintelijensia yao ilikwama🤣, hata mimi kuna siku naingia kambi fulani ya jeshi nikapita zangu getini fasta kumbe ka jamaa kapo kwenye kibanda cha mlinzi kakanifuata nikakapa Hi tukawa tunapiga stori kananilalamikia nimepita bila kufika pale kusalimia ni kinyume cha utaratibu nikaongea nako vizuri tu
ghafla kakaja kengine kanasema kwa sauti (apige pushapu huyo haraka,lala chini) mwenzie akakaambia huyu jamaa anaenda kwa fulani,kalinywea sana