Arusha: Hakimu Benson Ngowi(32) anashikiliwa na Polisi kwa kosa la kumlawiti kijana mwenye umri wa miaka 29

Arusha: Hakimu Benson Ngowi(32) anashikiliwa na Polisi kwa kosa la kumlawiti kijana mwenye umri wa miaka 29

Muktasari:​

  • Jeshi la Polisi Wilaya ya Ngorongoro linamshikilia Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Loliondo, Mkoa wa Arusha kwa tuhuma za za kumlawiti kijana mwenye umri wa miaka 29.
Arusha. Linaweza kuwa ni moja ya matukio ya nadra kutokea nchini, baada ya Jeshi la Polisi kumtia mbaroni hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Loliondo, Mkoa wa Arusha kwa tuhuma za kumlawiti kijana mwenye umri wa miaka 29 baada ya kumlewesha pombe.

Mbali na hakimu huyo kushikiliwa, jeshi hilo linamshikilia pia mwathirika wa tukio hilo kutokana na msimamo wa sheria unaosema kuwa mwanamume anayemruhusu mwanamume mwenzake kumwingilia, naye ametenda kosa la jinai.
Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro (DC), Kanali Wilson Sakulo, amethibitisha
"Ni kweli kuna taarifa za tukio la aina hiyo nimezipata na Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi, kwa sasa siko kwenye nafasi ya kusema tukio hilo," amesema.
Taarifa kutoka wilayani humo, zinadai hakimu huyo anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Loliondo.

Inadaiwa tukio hilo limetokea juzi Alhamisi, Februari 1, 2024 saa tatu na saa nne usiku nyumbani kwa kijana huyo ambaye hufanya kazi ya kuendesha bodaboda katika eneo la Wasso, wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha.
Chanzo hicho kilidai hakimu huyo ambaye hivi karibuni alihamia kikazi, alionekana majira ya mchana akiwa na kijana huyo na baadaye jioni walikwenda kunywa pombe nyumbani kwa kijana huyo.
"Ilipofika majira ya usiku kaka yake na kijana aliyelawitiwa (jina linahifadhiwa) alifika nyumbani kwa mdogo wake na kuwakuta wakiwa uchi, ndipo alipompigia simu hakimu mwenzake na mtuhumiwa," amedai mmoja wa chanzo chetu
"Alipokuja huyo Hakimu mwenzake, walipiga simu polisi na polisi walikuja kuwachukuwa wote wawili na hadi sasa wanashikiliwa kituoni," ameongeza
Chanzo hicho kiliendelea kueleza kijana huyo katika mahojiano ameeleza hii ni mara ya tatu hakimu huyo kumfanyia kitendo hicho na aliamua kunyamaza kwa madai aliona kutoa taarifa ingemdhalilisha na alipelekwa katika hospitali ya Wasso kwa matibabu na daktari kuthibitisha kuwa ameingiliwa.

"Kijana kwenye mahojiano alisema alikunywa sana pombe ikamzidi na kuamua kulala na aliposhtuka alikuta hakimu huyo akiwa anamwingilia kinyume na maumbile na kutokana na ukaribu wao hata kaka wa kijana alianza kuwa na mashaka," kilidai chanzo hicho
Taarifa zinadai hakimu hiyo alikuwa na mazoea na kijana hiyo kutokana na kumtuma mara kwa mara ikiwemo kumsafirisha kutoka eneo moja kwenda jingine kwa kutumia pikipiki yake.
 
Hapa ieleweke,ikiwepo penetration,hilo ndilo kosa.
Ikitokea zinaa,lakini penetration haikuwepo,hiyo pia ni zinaa,hilo pia ni kosa,lakini isiwe sababu ya kuleta shari.
Sasa toka nilipofika Arusha siku ya Christmas hili nadhqni ndilo kosa la pili la zinaa linatokea.
Kwanza ilitokea mwanamke anataka kubakwa akapiga mayowe. Jamaa alipokwenda kumsaidia,huyu jamaa akakatwa kiganja cha mkono.
Nilikuwa namsikia Mhubiri mmoja katikw redio jana ananukuu Biblia kuhusu kuwalewesha watu na kuwavua nguo. Nadhani alikuwa anaongea kuhusu tukio hili la huyu hakimu.
 
Akimu kwaiyo ndo goma lake kaamua kujilia au ndo kamtoa bik ya marinda
 
ninachokiona hapa ni,kaka wa anayeitwa mhanga kutofurshishwa na hali aliyoikuta nyumbani kwa mdogo wake.hao ni wapenzi sema bro kajua jana kwa kuwafuma🙈🙈🙈
Aki hao ni wapenzi, ila dogo kamzalilisha bro ake sana kiukweli sie tuliopitia cuba ningewawahisha kuzimu kimya kimya
 
Wanawake hawa wote? Kweli ? Na kizazi cha sasa hivi wanawake walivyo wazuri unajiingiza kwenye ushetani.

Kama ni kweli hakimu kaidhalilisha mahakama.
N.b adhabu ya Mungu ni kali hawezi kulifumbia macho hili.
 
Sasa huyo kidume aliyeliwa ndy kafa kiume sasa [emoji1][emoji1]..
 
Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Loliondo,Benson Ngowi(32) anashikiliwa na jeshi la Polisi katika kituo cha Loliondo,Wasso kwa kosa la kumlawiti kijana mwenye umri wa miaka 29 mkazi wa Wasso wilaya ya Ngorongoro Mkoani Arusha.

Hakimu huyo, ambaye pia alifanya kazi ya uwakili kwenye Kampuni ya mawakali[ jina ni la kiswahili ila hapa naandika kwa kingereza wewe utafsiri JUSTICE FIRST ] ni wakili unaweza kumuona kwenye mfumo wa mawakili, ameacha uwakili hivi miaka ya karibuni na kuwa hakimu.

Kwa mujibu wa chanzo cha Habari wilayani humo,tukio hilo limetokea jana majira ya saa tatu na saa nne usiku nyumbani kwa kijana huyo ambaye hufanyakazi ya kuendesha pikipiki maarufu bodaboda katika eneo la Wasso.

Mtoa taarifa alifafanua kwamba Hakimu huyo ambaye hivi karibuni alihamia kikazi,alionekana majira ya mchana akiwa na kijana huyo na baadaye jioni walienda kunywa pombe nyumbani kwa kijana hiyo ambaye ànaishi chumba kimoja na sebule

Alisema ilipofika majira ya usiku kaka yake na kijana aliyelawitiwa (jina linahifadhiwa) alifika katika nyumbani kwa mdogo wake na kumkuta mdogo wake wakiwa na hakimu Benson Ngowi wakiendelea kunywa pombe aina ya Safari huku hakimu ndiye aliyekuwa akimnunulia kijana hiyo kwa mshahara wake wa January.

Taarifa inasema kwamba majira ya saa tatu usiku Hakimu alimtuma kaka yake na huyo kijana kwenda kuchukua chakula na wakati aliporejea alikuta mlango umefungwa na kuamua kugonga.

"Baada ya kugonga Hakimu alienda kufungua mlango lakini chaajabu alionekama sehemu zake za siri zikiwa Imesimama ndipo kaka yake aliposhtuka na kuamua kuingia chumbani kwa mdogo wake kujua kulikoni na kumkuta akiwa amelala kitandani kifudifudi akiwa utupu hajitambui" alisema mtoa taarifa.

Alisema baada ya tukio hilo aliamua kutoa taarifa kwa watu mbalimbali ndipo hakimu Benson Ngowi wenzake na mtuhumiw walifika Eneo la tukio na baadaye polisi walikuja na kumkuta kijana hajitambui kitandani na baada ya kumwamsha na kuzinduka alihisi maumivu sehemu zake za haja kubwa ndipo askari hao walipomtia nguvuni mtuhumiwa.

Kijana huyo alipelekwa katika hospitali ya Wasso kwa matibabu na taarifa za daktari zimethibitisha kuwepo na michubuko sehemu za haja kubwa pamoja na mbegu za kiume.

Taarifa zinadai kwamba hakimu hiyo alikuwa na mazoea na kijana hiyo kutokana na kumtuma mara kwa mara ikiwemo kumsafirisha kutoka eneo moja kwenda jingine kwa kutumia pikipiki yake.

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Justin Masejo alipotafutwa alisema bado hajapata taarifa ila anafuatilia tukio hilo na atatoa taarifa.

Update 5-2-2024
#Taarifa zinasema Benson Ngowi alikuwa Wakili kwenye kampuni moja Dar es salaam na baadae kuamua kuwa hakimu ambapo alipangiwa Karagwe na kuhamishwa kwa makosa ya kinidhamu kama hili la Arusha.
Aliyelawiti miaka 32 na aliyelawitiwa miaka 29.

Hapa mi naona ni kesi ya Ushoga.
 
Aliyelawitiwa ana miaka 29, amelawitiwa nyumbani kwake. Mtuhumiwa ana miaka 32, kaka wa alielawitiwa akatumwa na mtu wa lika lake.
Maswali ni mengi sana.
 
Back
Top Bottom