n-propanol
JF-Expert Member
- Apr 7, 2019
- 5,349
- 7,000
Bad news everywhere. Watu wameyeyuka mioyo na kukata tamaa. Mungu atusaidie watanzania.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Eti mama Ester mtunze wifi yako!!nilifikiri amefunguka A -Z kuhusu masaibu yaliyomkuta ili waliobaki wasiwe na maswali.Huo ujumbe mzito uko wapi?
[emoji28][emoji28]Bonyeza*102# utauona.
Mmh aisee!Mfanyakazi wa Benki ya DTB, Jijini Arusha, Bryson Burchad (50) mkazi wa Ngusero jijini hapa,amejinyonga hadi kufa katika chumba Cha mpangaji wake kwa kutumia Kanga ya mkewe aliyoomba kwa lengo la kwenda kuoga huku akiacha ujumbe mzito kwa mkewe.
"Mke wangu Rose nisamehe kwa uamuzi niliochukua asilaumiwe mtu yoyote kwenye tukio hili ni uamuzi wangu mwenyewe,Dada zangu na mama ester mtunze wifi yenu na watoto wangu" ujumbe wa karatasi alioacha marehemu uliokutwa ndani ya suruwali yake.
Mwili wa marehemu uligundulika mapema leo majira ya saa moja asubuhi wakati mkewe,Rose Baraza akijaribu kumtafuta marehemu ili ampeleke mtoto shule .
Akiongelea tukio hilo Mke wa marehemu,(Rose) alisema kuwa majira ya saa 11alfajiri leo marehemu mumewe ambaye alikuwa ameajiriwa kama dereva katika benki hiyo, alimwomba kanga ili akaoge kwa ajili ya kujiandaa kwenda kazini.
Alisema ilipotimu saa moja na robo asubuhi alishituka usingizini kukuta mtoto wa shule Bado yupo nyumbani wakati marehemu huwa na kawaida ya kumpeleka shule majira ya saa moja asubuhi.
"Nilishtuka saa moja na robo asubuhi kuona mtoto hajapelekwa shule niliangalia vitu vyake ikiwemo simu yake ,nguo za kazini nikaona zipo nikabaki kushangaa huyu mtu atakuwa ameenda wapi,ndo baadaye wakati namtafuta nikaona kupitia dirisha amejinyonga kwenye chumba Cha mpangaji wetu"alisema.
Alisema baada ya kushuhudia tukio hilo alipiga kelele na baadaye majirani kukusanyika na kutoa taarifa polisi ambao walifika na kushuhudia mwili wa marehemu ukining'inia ikiwemo ujumbe wa barua katika suruwali ya marehemu.
Alifafanua kuwa siku moja kabla ya tukio hilo mumewe alikuwa akilalamika kuumwa na tumbo na alienda kutibiwa hospitali na kugundulika kusumbuliwa na Amueba ,Jambo ambalo mkewe alikanusha kuwa chanzo Cha mumewe kujinyonga.
Hata hivyo mke wa marehemu alifafanua kuwa marehemu aliwahi kumweleza kuwa pale kazini anaugomvi unaotishia kibarua chake na mfanyakazi mwenzake(hakumtaja)na kumfanya akose raha, Jambo ambalo lilimsababisha marehemu awe anakunywa pombe kupita kiasi kutokana na msongo wa mawazo.
Marehemu ameacha watoto wanne akiwemo mtoto mchanga mwenye umri wa mwezi Mmoja na wiki tatu, Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba Cha maiti katika hospital ya Mkoa wa Arusha ya Mt .Meru.
View attachment 2098766
Kama roho ya mauti ikishatumwa kwako hata huwazi mara mbili !Yaani mfanyakazi mwenzako akukere mpaka uamue kujiua?....
Jamaa ameiacha familia yake kwenye wakati mgumu sana.....ni vizuri kufikiria madhara ya yatakayowapata watu wako wa karibu/familia kabla ya kuchukua uamuzi wa hatari.
Huyo pichani ni mjukuu wangu.Tuachane na hayo. Naomba kuuliza ni wewe kwenye iyo avatar picha? Kama ni wewe si tuanze tu kufahamiana.
Waangalie mwandiko, ni wake kweli?Mwanamke anajua kila kitu, wambane makalio na koleo atasema
Usikute mpangaji ndo mwenye uyo mtoto wa mwezi mmoja kwa mke wa jamaaHicho chumba Cha mpangaji Kuna uwalakini!
1. Huyo mpangaji ni jinsia Gani?
2. Huyo mpangaji hafanani na hicho kichanga Cha Mzee?
3. Huyo mpangaji alikuwa wapi?
4. Huyo Mpangaji yupo wapi sasa?
Sumu inaweza kuwa imetumika!Haya maelezo hayaendani na tukio halisi! Mtu ajinyonge na kuacha ujumbe bila sababu. Kuna namna hapo
Sawa Mkuu, ngoja yakukute!Sijui kwanini watu wengi wanaamua kunywa pombe wakiamini ndio njia ya kuondoa stress/depression
''Njooni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha''.
MATH 11:28-30
Ungewala tigo mkuuuniliwahi kufanya kazi taasisi moja ya afya iliyoko chini ya wahindi..basi receptionist mmoja alikuwa anagongwa na meneja mhindi alikuwa ananizingua balaa ili niache kazi yeye amlete ndugu yake...nikaamua asubuhi kabla sijaingia kazini navuta bangi jicho linakuwa jekunduu...wale maboya walikuwa wakiniona wananikwepa ...nilipotimiza malengo yangu nikasepa.
R.I.P Mwendazake
#wenyemapovutunzenisioJPMni huyo dereva
Mengi watoto aliozaa na Jack bado hawajaanza ila maisha yanasonga, chamsingi pesa tu ziwepoMiaka 60 mwanao hajaanza hata sekondari
Unawaachia watu mzigo.
Mmmmmh,hapa kuna mashakaYaani mfanyakazi mwenzako akukere mpaka uamue kujiua?....
Jamaa ameiacha familia yake kwenye wakati mgumu sana.....ni vizuri kufikiria madhara ya yatakayowapata watu wako wa karibu/familia kabla ya kuchukua uamuzi wa hatari.
Ukajinyonge chumba cha mpangaji????yaaan hapaHicho chumba Cha mpangaji Kuna uwalakini!
1. Huyo mpangaji ni jinsia Gani?
2. Huyo mpangaji hafanani na hicho kichanga Cha Mzee?
3. Huyo mpangaji alikuwa wapi?
4. Huyo Mpangaji yupo wapi sasa?
At 50 una mtoto ana mwezi mmoja! Mtoto akifika 10yrs tayari una 60 umestaafu akiwa na miaka 5. Kama una vitega uchumi vya kutosha sawa, vinginevyo shule ataisikia tuu.At the age of 50 anajinyonga, siku hizi kujinyonga imekua jambo la kawaida sana
Halafu ana mtoto wa mwezi mmoja maskini
Kwahiyo mke ndo kamnyonga? Acha kusingizia mke.Mke might be involved, Na Mara nyingi atakuwa kadanganywa Na mwanaume mwingine baada uchepukaji