Wanabodi,
Declaration of Interest
Kumezuka huu mtindo wa mtu yoyote humu, akisifia jambo lolote kumhusu rais wa JMT, ananyooshwa vidole vya kutafuta uteuzi, niliwahi kuwafundisha watu humu, jinsi ya kutofautisha wasifiaji wa kujikombakomba na kutafuta uteuzi, na wasifiaji wa ukweli, kumsifu kiongozi anapofanya mazuri ili kumtia moyo. Wasifiaji wa kujikombakomba, wao kazi yao huwa ni moja tuu, kusifu, kuimba nyimbo za shangwe na mapambio, kawa wafanyavyo watu wanaitwa ma "chawa". Wasifuji wa ukweli, wa type yangu ni wale tunaosifu mazuri tuu, na kukitokea huyo unayemsifu akaboronga, tunamkosoa. Mtafuta uteuze kamwe hawezi kukosoa!.
Mimi Paskali, naomba ku declare interest, nansifu Rais Samia kwa mazuri yake na wala sitafuti uteuzi wowote, na kumsifu rais Samia sikuanza leo, tembelea
HAPA! na
HAPA! tena ni mimi mwaka 2015 nilimtaja Samia Suluhu Hassan kuwa na best female presidential material
HAPA!
Hivyo pongezi zangu mbalimbali kwa Rais Samia, kama hizi
PONGEZI! PONGEZI!,
SAMIA TUMAINI JIPYA! SAMIA MPONYAJI!
ndio maana naelewa kuwa Rais Samia ni binadamu, na anaweza kukosea makosa ya kibinaadamu, akikosea pia tunamkosoa humu humu kama hapa jinsi nilivyo mkosoa
RAIS SAMIA SIO MALAIKA, NI BINADAMU! na
2025 SIO LAZIMA SAMIA! na
JAPO TUMEPANGA 2025 TWENDE NA MWANAMKE, KUNA HII SAUTI!
Hata kwenye utengenezaji wa filamu ya Royal Tour, tangu mwanzo tunaiandaa, tulikosoa na kushauri, local producers wa ndani pia tushirikishwe, ili baada ya filamu ya Mama ya kizungu kwa ajili ya wazungu, local producers, tumtengenezee Mama A Tanzanian Tour, kwa Kiswahili kwa ajili ya utalii wa ndani. Kabla ya uzinduzi wa Royal Tour, wengi wameishia kusifu tuu, akina sisi ambao tuko more objective, hatukusifu tuu bali pia tumekosoa!
ROYAL TOUR TUNGE...! Hivi msifia mtafuta uteuzi, atasifu tuu, hawezi kukosoa lolote, msifia ukweli, atasifu panapostahili sifa na kukosoa panapostahili kukosolewa!
Utangulizi
Kama kawa, leo tana nimepata nafasi ya kushuka na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" leo nazungumzia kuponywa kwa taifa na trends za 2025, Rais Samia, Ameosha kwa Kauli na Matendo, Yeye ni mtu wa haki, sio tuu ni msema haki bali ni mtenda haki, tunaamini soon ataruhusu mikutano ya siasa, na kuifanyia marekebisho Tume ya taifa ya Uchaguzi kuifanya kuwa tume huru zaidi na shirikishi.
Katiba yetu ya 1977 ilitoa uhuru kwa kila mtanzania mwenye sifa na vigezo, kuwa huru kushiriki kwenye kuunda serikali toka serikali za mitaa hadi serikali kwa sheti moja tuu la Utanzania wake. Hivyo kila Mtanzania yuko ana haki na yuko huru kushiriki uchaguzi kwa kugombea nafasi yoyote na kushiriki kuwachagua viongozi wetu. Hili ndilo lilikuwa lengo la mtunga katiba. Baadae kukajitokeza "mambo", haki ya kupiga kura kuwachagua viongozi, kwa uhuru, hii ipo na inaendelea, lakini haki na uhuru wa mtu yoyote kushiriki kwenye kuunda serikali, yaani haki ya kugombea na kuchaguliwa, haki hii imeondolewa kwa ubatili fulani,
Japo Rais Samia ameunda timu ya "kikosi kazi" cha kumshauri, na hicho kikosi kazi kinaita baadhi tuu ya watu, sijasikia kama sisi wananchi wa kawaida pia tuko huru kufika mbele ya kikosi kazi, ila mimi haya mawazo yangu, nitayaandika na kuyawasilisha, ila kwa vile tayari Rais Samia ameisha onyesha kwa kauli na matendio, yeye sui tuu ni muwaza haki na msema haki, bali pia ni mtenda haki kwa matendo ya haki kuonekana, tunamuomba atutendee haki Watanzania, kwa kutuondolea ubatili huu, ndani ya Katiba Yetu!.
Angalizo
Bandiko hili, linauzungumzia ubatili fulani kwenye katiba yetu, kwa vile Watanzania wengi ni wavivu wa kusoma vitu vikubwa, virefu, vigumu, wanapenda vitu rahisi rahisi, na mabandiko mafupi mafupi, wa wa type hii, inaweza kuishia hapa, halafu mkarukia kwenye hitimisho.
Mastori ya Pasco Paskali Snr
Hitimisho
Jana kwenye mitandao ya kijamii, zimesikika habari, Tundu Lissu amelipwa haki zake, hivyo hapa ni uthibitisho tuu wa matendo ya haki na sio tuu kauli za haki.
Naamini kupitia “kikosi kazi”, soon ataruhusu mikutano ya siasa, ataifumua na kuisuka upya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kuifanya iwe shirikishi, pia tunamuomba rais Samia, auondoe na ubatili fulani ndani ya katiba yetu, inayoruhusu kila Mtanzania kuwa na haki ya kuchagua na kuchaguliwa, haki ya kuchagua bado ipo ila haki ya kuchaguliwa, imechomekewa ubatili fulani wa kudhaminiwa na chama na siasa!. Ubatili wenyewe ni huu
KATIBA YETU INA UBATILI, SHERIA YA UCHAGUZI INA UBATILI!. na SHURTI HILI KWENYE KATIBA YETU NI BATILI!
Hivyo mpaka sasa, Rais Samia, ameishathibitisha kwa kauli na matendo, kuwa yeye ni mpenda haki na mtenda haki. Analiponya taifa, hivyo kwa matendo haya ya haki, Rais Samia anayoyafanya, atabarikiwa sana, na taifa litabarikiwa na kupata ustawi wa kisiasa, kiuchumi na kijamii. Nimalizie kumshukuru Mungu kwa kutuletea Rais Samia: Ni Msema Haki na Mtenda Haki!. Soon Ataruhusu Mikutano ya Siasa na NEC Shirikishi, jee vipi kuhusu ubatili huu ndani ya Katiba yetu?
Asante Mungu kwa Rais Samia, ni Baraka kwa nchi yetu, naomba lile jicho, liuone na ubatili huu ndani ya katiba yetu.
Mungu Mbariki Rais Samia,
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali.