Asante Rais kuruhusu mikutano, tunakuomba uruhusu haki nyingine ambayo imeporwa ya Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa

Asante Rais kuruhusu mikutano, tunakuomba uruhusu haki nyingine ambayo imeporwa ya Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Hii ni makala ya Leo kwenye Nipashe
Screen Shot 2023-01-08 at 8.01.34 AM.png
Screen Shot 2023-01-08 at 8.01.55 AM.png

Jumapili ya June 8, mwaka 2021, katika safu hii, niliandika makala ya kumpongeza Rais Samia, kwa kuwasisitiza watendaji wa serikali kutenda haki, kufuatia baadhi ya haki zilizotolewa na katiba yetu na kugeuzwa ni hisani, Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki Malala ya leo ni kumpongeza tena rais Samia.

Baada ya Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa, sasa ni nderemo na vifijo nchi mzima!. Na mimi kama Mtanzania mzalendo wa taifa letu, pale linapofanywa jambo jema lolote la kheri kwa mustakabali mwema kwa taifa letu, sina budi kujiunga na wengine wote wanaolitakia mema taifa hili kwa kumpongeza Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu mikutano ya siasa, kukubali kurekebisha sheria mbalimbali kandamizi na kubwa kuliko, kukubali kuendeleza mchakato wa katiba mpya.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa kwa vile mikutano hiyo ya vyama vya siasa ni jambo ambalo limeruhusiwa na katiba, hivyo vyama vya siasa kufanya mikutano ni miongoni mwa haki za vyama vya siasa zilizoainishwa na katiba, hata lile swali langu la Ikulu, kumuuliza rais wa JMT, ametumia mamlaka gani kwenye kifungu kipi cha sheria, kuzuia jàmbo lililoruhusiwa na katiba?, japo sikumbuki siku ile pale ikulu nilijibiwa nini, lakini sasa ndio Rais Samia, amemjibia.

Waswahili wana msemo, "anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga!", jambo linalozuiliwa kwa utashi tuu, bila kifungu chochote, cha katiba au sheria, sasa limeruhusiwa kwa utashi tena, bila kutumia kifungu chochote cha katiba na sheria. Jambo lolote lililozuiliwa, linaporuhusiwa, hatua ya kwanza ni kushukuru kwa jambo hilo kurusiwa, hivyo Watanzania wote tujiunge pamoja na kusema kwa kauli moja, "Asante Sana Mama".

Baada ya kushukuru, tusipojiuliza hili liliwezaje kutokea, ili lisije kujirudia kutokea tena. Sasa twende ndani kidogo zaidi ya jambo lenyewe lililoruhusiwa, kwa vile mikutano ya siasa ilizuiliwa kwa utashi tuu, na sasa imeruhusiwa kwa utashi tena, tukishukuru na kusema tuu asante bila kutia neno jingine lolote, hii inapelekea suala la mikutano ya siasa kuonekana ni kama jambo la hisani tuu ya rais aliyepo madarakani, JPM alizuia mikutano kwa utashi tuu, na leo Rais Samia ameruhusu mikutano hii kwa utashi na kwa hisani tuu!, tusipoliwekea muongozo, kesho atakuja kiongozi mwingine naye ataweza kuzuia jambo loloye kwa utashi tuu.

Kitu kama ni haki, haki hiyo ni stahili sio hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kuruhusu viongozi wetu, wazigeuze haki zetu na stahili zetu kuwa hisani mpaka lini?.

Tena afadhali ya hili la haki ya mikutano ya siasa, limefanywa kwa utashi tuu kwa kutumia kauli tuu, yaani mikutano ilizuiliwa kwa kauli, na sasa imeruhusiwa kwa kauli, lakini kuna na haki nyingine mbili ambazo ndizo haki kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, haki moja kati ya haki mbili hizo, imegeuzwa hisani!. Haki ya kuchagua yenyewe bado ipo, ila haki ya kuchaguliwa imegeuzwa hisani!.

Tunamshukuru sana Rais Samia kutuhisania Watanzania kuturudishia haki hii, Tuendelee kumuombea Rais Samia Mungu aendelee kumlinda na kumbariki, ili kufikia mwaka 2025, awe ameisha turudishia haki zote za kikatiba ziliporwa na kugeuzwa hisani. Nimeutaja mwaka 2023 japo ninaelewa Rais Samia anayo gursa ya kuendelea kuhudumu kipindi cha pili cha mwaka 2025-2030, mimi natumia mtindo wa linalowezekana leo lisingoje kesho. Sasa tuko 2025, tujipange kukamilisha ypte ya msingi, akiendelea, arndelee na mengine wakati ya msingi yamekamilika.

Watanzania tuendelee kuwa watu wa shukrani kwa kushukuru kwa yote, hata kama ni madogo ili tuweze kupatiwa makubwa, hivyo tuendelee kusema asante sana Mama Samia kwa a good political will la kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama na Watanzania kukushukuru kwa hisani yako hii, tunakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa!.

Wakati tukisubiria hisani ya Mama Samia kwenye hili, kupitia marekebisho ya sheria mbalimbali na kumruhusu kila Mtanzania kuchagua na kuchaguliwa, naendelea tuu kukumbushia kuwa

Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano na maridhiano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional bila masharti yoyote, Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, wala haibembelezewi kwa vikao vya maridhiano, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, kwa kuweka mashinikizi ya mikutano na maandamano ya kudai haki hizo na sio kuziomba, na hapa ni pale tuu inapobidi, baada ya njia nyingine zote kushindikana ni katika kuipigania huku kuna wakati machozi, jasho na damu huweza kumwagika, katika kupigania haki.

Kwa vile Rais wetu Mama Samia, keshaonyesha utashi, kwa kauli na matendo, tuzidi kumuombea ili Mungu amuwezeshe ayaweze yote haya kabla hajamaliza awamu yake hii ya kwanza, ili hata ikitokea akaendelea kwa awamu ya pili, hiyo itakuwa ni awamu ya shukrani na kumpa asante kwa aliyotatenda, na sio awamu ya kukamilisha ambayo hayakumamilika.

Mungu Mbariki Rais Samia

Mungu Ibariki Tanzania
 

Attachments

  • Screen Shot 2023-01-08 at 8.01.55 AM.png
    Screen Shot 2023-01-08 at 8.01.55 AM.png
    187.8 KB · Views: 7
hongera sana,ila ungeacha kwanza gazeti lifike jion ndio uweke huo ukurasa...mda huu ungeweka heading ya hiyo makala, umepunguza wateja wakununua gazet leo
Looooooo middle class wangu!mbona unafikiri kinyume, Adv.Mayala kuweka hii nakala yake ndio iwe kichocheo wewe ukalitafute gazeti la Nipashe leo,soma na weka kwenye maktaba yako huwezi in 50yrs thamani yake itakuaje!
 
Mbona umeshindwa kuelezea hizo haki mbili za kuchagua na kuchaguliwa zimeporwa vipi, na nini kifanyike ili kuwarudishia walioporwa haki zao?

Au ndio umeelezea mbele ya makala yako?
 
Makala nzur sana..

Ila wakati hizi haki zinadaiwa wengi wenu mlibeza na kuwatukana sana walijitoa kuzidai...

Tanzania kwa mujibu wa Katiba rais ndio mhisani wa kila kitu ndio maana hata mafuriko yakija tunamuomba Rais atuondolee!

Haki ya kuchagua na kuchaguliwa ni jambo la maana sana ikiwa litawekwa sawa kwa mujibu wa Katiba...

Ila for the time being tuendelee kuomba na ku meditate,Kwa hisani ya Rais.

Ila bila katiba mpya inayojisimamia mengine yote ni bure, Hivi unamuomba mtu namna ya kumtoa madarakani au namna ya kuwanyima washkaji zake nafasi nae akubali tu??

Aidha ni mzalendo sana kwa nchi yake au otherwise .

Shukran kwa makala mkuu Wakili Msomi.
 
Tunamshukuru sana Rais Samia kutuhisania Watanzania kuturudishia haki hii, Tuendelee kumuombea Rais Samia Mungu aendelee kumlinda na kumbariki, ili kufikia mwaka 2025, awe ameisha turudishia haki zote za kikatiba ziliporwa na kugeuzwa hisani. Nimeutaja mwaka 2023 japo ninaelewa Rais Samia anayo gursa ya kuendelea kuhudumu kipindi cha pili cha mwaka 2025-2030, mimi natumia mtindo wa linalowezekana leo lisingoje kesho. Sasa tuko 2025, tujipange kukamilisha ypte ya msingi, akiendelea, arndelee na mengine wakati ya msingi yamekamilika.
Well. Yaani leo nyuzi ni kali kali tu
 
Wanabodi,
Hii ni makala ya Leo kwenye Nipashe
View attachment 2472635View attachment 2472639
Jumapili ya June 8, mwaka 2021, katika safu hii, niliandika makala ya kumpongeza Rais Samia, kwa kuwasisitiza watendaji wa serikali kutenda haki, kufuatia baadhi ya haki zilizotolewa na katiba yetu na kugeuzwa ni hisani, https://www.jamiiforums.com/threads...tubadili-katiba-kurudisha-haki.1878656/makala ya leo ni kumpongeza tena rais Samia.

Baada ya Rais Samia kuruhusu mikutano ya siasa, sasa ni nderemo na vifijo nchi mzima!. Na mimi kama Mtanzania mzalendo wa taifa letu, pale linapofanywa jambo jema lolote la kheri kwa mustakabali mwema kwa taifa letu, sina budi kujiunga na wengine wote wanaolitakia mema taifa hili kwa kumpongeza Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu mikutano ya siasa, kukubali kurekebisha sheria mbalimbali kandamizi na kubwa kuliko, kukubali kuendeleza mchakato wa katiba mpya.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa kwa vile mikutano hiyo ya vyama vya siasa ni jambo ambalo limeruhusiwa na katiba, hivyo vyama vya siasa kufanya mikutano ni miongoni mwa haki za vyama vya siasa zilizoainishwa na katiba, hata lile swali langu la Ikulu, kumuuliza rais wa JMT, ametumia mamlaka gani kwenye kifungu kipi cha sheria, kuzuia jàmbo lililoruhusiwa na katiba?, japo sikumbuki siku ile pale ikulu nilijibiwa nini, lakini sasa ndio Rais Samia, amemjibia.

Waswahili wana msemo, "anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga!", jambo linalozuiliwa kwa utashi tuu, bila kifungu chochote, cha katiba au sheria, sasa limeruhusiwa kwa utashi tena, bila kutumia kifungu chochote cha katiba na sheria. Jambo lolote lililozuiliwa, linaporuhusiwa, hatua ya kwanza ni kushukuru kwa jambo hilo kurusiwa, hivyo Watanzania wote tujiunge pamoja na kusema kwa kauli moja, "Asante Sana Mama".

Baada ya kushukuru, tusipojiuliza hili liliwezaje kutokea, ili lisije kujirudia kutokea tena. Sasa twende ndani kidogo zaidi ya jambo lenyewe lililoruhusiwa, kwa vile mikutano ya siasa ilizuiliwa kwa utashi tuu, na sasa imeruhusiwa kwa utashi tena, tukishukuru na kusema tuu asante bila kutia neno jingine lolote, hii inapelekea suala la mikutano ya siasa kuonekana ni kama jambo la hisani tuu ya rais aliyepo madarakani, JPM alizuia mikutano kwa utashi tuu, na leo Rais Samia ameruhusu mikutano hii kwa utashi na kwa hisani tuu!, tusipoliwekea muongozo, kesho atakuja kiongozi mwingine naye ataweza kuzuia jambo loloye kwa utashi tuu.

Kitu kama ni haki, haki hiyo ni stahili sio hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kuruhusu viongozi wetu, wazigeuze haki zetu na stahili zetu kuwa hisani mpaka lini?.

Tena afadhali ya hili la haki ya mikutano ya siasa, limefanywa kwa utashi tuu kwa kutumia kauli tuu, yaani mikutano ilizuiliwa kwa kauli, na sasa imeruhusiwa kwa kauli, lakini kuna na haki nyingine mbili ambazo ndizo haki kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, haki moja kati ya haki mbili hizo, imegeuzwa hisani!. Haki ya kuchagua yenyewe bado ipo, ila haki ya kuchaguliwa imegeuzwa hisani!.

Tunamshukuru sana Rais Samia kutuhisania Watanzania kuturudishia haki hii, Tuendelee kumuombea Rais Samia Mungu aendelee kumlinda na kumbariki, ili kufikia mwaka 2025, awe ameisha turudishia haki zote za kikatiba ziliporwa na kugeuzwa hisani. Nimeutaja mwaka 2023 japo ninaelewa Rais Samia anayo gursa ya kuendelea kuhudumu kipindi cha pili cha mwaka 2025-2030, mimi natumia mtindo wa linalowezekana leo lisingoje kesho. Sasa tuko 2025, tujipange kukamilisha ypte ya msingi, akiendelea, arndelee na mengine wakati ya msingi yamekamilika.

Watanzania tuendelee kuwa watu wa shukrani kwa kushukuru kwa yote, hata kama ni madogo ili tuweze kupatiwa makubwa, hivyo tuendelee kusema asante sana Mama Samia kwa a good political will la kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama na Watanzania kukushukuru kwa hisani yako hii, tunakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa!.

Wakati tukisubiria hisani ya Mama Samia kwenye hili, kupitia marekebisho ya sheria mbalimbali na kumruhusu kila Mtanzania kuchagua na kuchaguliwa, naendelea tuu kukumbushia kuwa

Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano na maridhiano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional bila masharti yoyote, Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, wala haibembelezewi kwa vikao vya maridhiano, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, kwa kuweka mashinikizi ya mikutano na maandamano ya kudai haki hizo na sio kuziomba, na hapa ni pale tuu inapobidi, baada ya njia nyingine zote kushindikana ni katika kuipigania huku kuna wakati machozi, jasho na damu huweza kumwagika, katika kupigania haki.

Kwa vile Rais wetu Mama Samia, keshaonyesha utashi, kwa kauli na matendo, tuzidi kumuombea ili Mungu amuwezeshe ayaweze yote haya kabla hajamaliza awamu yake hii ya kwanza, ili hata ikitokea akaendelea kwa awamu ya pili, hiyo itakuwa ni awamu ya shukrani na kumpa asante kwa aliyotatenda, na sio awamu ya kukamilisha ambayo hayakumamilika.

Mungu Mbariki Rais Samia

Mungu Ibariki Tanzania
Mgombea binafsi! Hii sawa ila akina Mbowe Watanuna
 
Haki ya kuchagua na kuchaguliwa ni kipande cha fupa atakaye kuja kulitafuna hayuko kwenye kizazi hiki ninaona safari ndefu yenye shida hata kufikia tulipofika na si kwa kuzingatia sheria ni utashi tu
Screenshot_20230104-195923.jpg
 
Msukuma limbukeni huyo! What is this? Unashukuru Nini? Mtu kakunyanganya Shati lako, umefight akakurudishia /ukalichukua, halafu unashukuru.......bladimbuzi
 
Naunga mkono hoja kwa sababu wewe huwa hupapasi bali unalenga kile kinachotakiwa kulengwa.

Watanzania tuwe na mazoea ya kujenga hoja kwa ajili ya kujenga taifa letu, na sio kujenga hoja kwa ajili ya kumfurahisha mtu fulani.
Mkuu Dudumizi, thanks for this, na hiki ulichoeleza ndio essence yenyewe ya Makala za "Kwa Maslahi ya Taifa, ni kutanguliza mbele taifa kwanza, mengine yote yanafuata.
P
 
hata lile swali langu la Ikulu, kumuuliza rais wa JMT, ametumia mamlaka gani kwenye kifungu kipi cha sheria, kuzuia jàmbo lililoruhusiwa na katiba?, japo sikumbuki siku ile pale ikulu nilijibiwa nini, lakini sasa ndio Rais Samia, amemjibia.
Hapa ulikuwa Paschal Mayala na siyo Paschal njaa
 
Mkuu Bejamini Netanyahu , kauli huumba!. Hebu tuacheni hizi kauli za kukutana majina ya majanga na kutuletea majanga kweli.
P
Mkuu lakini hata wewe hujioni? swali lako lilikufanya ukawa maarufu kupita kiasi, binafsi nilikuwa sikujui hata kidogo ndiyo ilisababisha nikaanza kukufuatilia Star TV sijui wapi, ulivyokuja kuzingua mkuu tulikuambia
 
Hii makala ni ya kichochezi kivipi?
P
Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano na maridhiano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional bila masharti yoyote, Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, wala haibembelezewi kwa vikao vya maridhiano, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, kwa kuweka mashinikizi ya mikutano na maandamano ya kudai haki hizo na sio kuziomba, na hapa ni pale tuu inapobidi, baada ya njia nyingine zote kushindikana ni katika kuipigania huku kuna wakati machozi, jasho na damu huweza kumwagika, katika kupigania haki.
 
Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano na maridhiano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional bila masharti yoyote, Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, wala haibembelezewi kwa vikao vya maridhiano, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, kwa kuweka mashinikizi ya mikutano na maandamano ya kudai haki hizo na sio kuziomba, na hapa ni pale tuu inapobidi, baada ya njia nyingine zote kushindikana ni katika kuipigania huku kuna wakati machozi, jasho na damu huweza kumwagika, katika kupigania haki.
Huu ni uchochezi Mkuu
 
Back
Top Bottom