Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata chuo kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili yako.
 

Attachments

Kwamfano mimi sijawahi kusoma ata kitabu kimoja.

Naanzaje? Nipe tips nianze mdogo mdogo.

Je, ata kusoma vitabu vya story ni msosi wa Medulla oblongata? Au lazima viwe vitabu vya "How to become Wiseman"? "You was born to win"?
 
Kwamfano mimi sijawahi kusoma ata kitabu kimoja.

Naanzaje? Nipe tips nianze mdogo mdogo.

Je, ata kusoma vitabu vya story ni msosi wa Medulla oblongata? Au lazima viwe vitabu vya "How to become Wiseman"? "You was born to win"?
Hadithi huandikwa katika lugha yakiufundi ambayo msomaji anapaswa kutumia akili kuelewa maudhui,sio kila mtu anaweza kuelewa
 
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata Chuo Kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!!!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!!!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili yako.
Share hapa vitabu ulivyosoma
 
Kwamfano mimi sijawahi kusoma ata kitabu kimoja.

Naanzaje? Nipe tips nianze mdogo mdogo.

Je, ata kusoma vitabu vya story ni msosi wa Medulla oblongata? Au lazima viwe vitabu vya "How to become Wiseman"? "You was born to win"?
Vyote vinaweza vikawa na msaada, lakini hasa hutegemeana zaidi na uhitaji wako wewe - sababu ya kusoma. Kwa kuwa ndiyo unaanza, visome vyote - fiction (hadithi) na non fiction, kama ulichoandika hapo juu: HOW TO BECOME...

Baada ya muda, utabaini aina ya vitabu vinavyokusaidia zaidi.

Hata hivyo, pendelea zaidi kuvisoma vitabu ambavyo ni NON FICTION
 
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata Chuo Kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!!!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!!!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili yako.
Mungu akubariki!

Umetoa msaada mkubwa sana kwa watu watakaokuelewa ulichoshauri!

Vitabu vina maarifa mengi sana!

Vina majibu yote muhimu ktk MAISHA!

Hongera sana!
 
Hakika yake,
For wonderers and adventurers!
Vitabu vinakusafirisha kiakili utajikuta places na nyakati zisizofikika kabisa.

tuwahimize watoto wetu kusoma ni utamaduni mzuri sana, kuna majibu mengi ya changamoto zetu kwa namna ya tofauti ya kipekee sana, mimi nasoma naye page kwa page, tunaulizana tumejifunza nini? author kafail wapi, kafaulu kufikisha ujumbe gani nk
It sharpens his mind zaidi na zaidi, siyo rahisi kwa sababu ya hizi games na animated series ila tunapambana hivyo hivyo kuna kukasirikiana kabisa lakini tunasonga.
 
Kwamfano mimi sijawahi kusoma ata kitabu kimoja.

Naanzaje? Nipe tips nianze mdogo mdogo.

Je, ata kusoma vitabu vya story ni msosi wa Medulla oblongata?
Ndiyo, kama ni story nzuri za kujenga. Lakini Mimi binafsi, kwa upande wangu, non fiction vinaweza vikawa ni vizuri zaidi.

Vitabu siyo chakula cha ubongo bali akili. Mimi siyo mtaalam wa Saikolojia lakini nafahamu kuwa ubongo siyo akili na akili siyo ubongo.

Ubongo ni kama hardware na akili ni software.

Unaposoma, yale maneno yanayoingia kwenye akili yako huweza kuathiri na utendaji kazi wa ubongo wako.

Ndiyo, maneno huweza hata kumwua mtu, ikiwa hayo maneno yataielekeza akili kufanya hivyo. Akili itakachofanya ni kuiamuru ubongo kusitisha utendaji kazi wake, na ubongo ukiacha kufanya kazi matokeo yake yanafahamika, kifo.

Lakini yakiwa chanya, yanaweza kumletea mtu manufaa makubwa sana.

Ndiyo maana ni muhimu sana kuwa makini na unachokidoma. Kitakubadilisha bila wewe kujua, sana sana ni watu wanaokufahamu ndiyo watakaobaini mabadiliko yako.

I tell you the truth, vitabu vinaweza kuathiri hata mwonekano wako wa nje. I know what I am talking about. Sijasimuliwa. Nimeiona kwa macho yangu.

Maneno humjengea mtu taswira fulani akilini mwake, na hiyo taswira hutawala matendo yake.

Maneno yanayoingia kwa wingi kwenye ufahamu wako hatimaye yatatafuta jinsi ya kujithihirisha kwa vitendo.
 
Kwamfano mimi sijawahi kusoma ata kitabu kimoja.

Naanzaje? Nipe tips nianze mdogo mdogo.
Kwamba unaanzaje?

Anza vivyo hivyo, papo hapo ulipo, leo. Huhitaji kufanya maandalizi, bali kuamua. Kama huna kitabu, kitafute leo, hata kama ni kwa kuazima.

FANYA kama wafanyavyo walafi wa Vitabu. Tembea na kitabu kokote uendako.

Umemtembelea ndugu au rafiki? Usipoteze muda, wakati anakuandalia chochote, soma.

Upo kwenye ndege? Ulishafundishwa kuhusu mawingu tokea ukiwa shule ya Msingi. Usiyashangae, soma kitabu!

Unaendesha gari kwenda kazini au kutoka kazini? Usikasirishwe na foleni. Dakika tano zitakutosha kuongeza kitu kwenye ufahamu wako kupitia kitabu.

Upo kwenye daladala? Ni fursa nzuri sana kwa ajili ya kusoma, labda kama unapenda kufisadi muda.

Umeenda kuonana na mkubwa fulani ofisini kwake? Wakati unasubiri kuonana naye, ni fursa nyingine ya kusoma kurasa kadhaa.

Vipi kama unapika? Unaweza kusoma pia, labda tu kama unatumia macho badala ya mwiko kusonga ugali.

Mkuu, unanipata lakini? Muhimu ni kuwa na kitabu jirani nawe, na udhamirie kutumia kila dakika huru kwa kusoma.

Na sivyo tu. Jitengenezee na muda maalum wa kujisomea pia. Unaweza ukatenga alau lisaa limoja Usiku na limoja Asubuhi kwa ajili ya kusoma.

Ukifanya hivyo kila siku, nina uhakika, mwezi hautaisha bila kuanza kuona mabadiliko.

Ila hakikisha ni Vitabu salama kwa akili. Vitabu vina nguvu sana. Ni ama chakula au sumu.

Visome vile tu ambavyo ni chakula salama.
 
Kwamfano mimi sijawahi kusoma ata kitabu kimoja.

Naanzaje? Nipe tips nianze mdogo mdogo.

Je, ata kusoma vitabu vya story ni msosi wa Medulla oblongata? Au lazima viwe vitabu vya "How to become Wiseman"? "You was born to win"?
Kwa kuongezea, usomaji wa Vitabu ni tabia. Na tabia haitokei automatically. Hujengwa.

Kwa kuwa hukuwa na tabia ya usomaji, inawezekana mwanzoni usifurahie, ingawa si lazima iwe hivyo. Unapoamua kuwa msomaji wa Vitabu, unapaswa kufanya hivyo ukiwa umedhamiria kufanikiwa kwa gharama yoyote ile, hata kama ni kwa kujichapa viboko au kutokula mpaka uwe umalize kusoma. Maana yake, uwe umenia kusoma hata kama hutakuwa ukijisikia kusoma.

Unaweza ukafanya kama alivyoshauri Winston Churchill, kwamba hata kama hujisikii hivyo, chukua Vitabu kisha ukajifungie kwenye chumba kwa masaa manne ukisoma.

Churchill alifahamu alichokuwa akishauri. Inawezekana ndivyo alivyokuwa akifanya na kuweza kuwa mmoja ya Mawaziri Wakuu maarufu wa Uingereza na mwandishi wa Vitabu vilivyotumiwa na Vyuo Vikuu mashuhuri Uingereza: Oxford University na Cambridge University. Alikuja kuwa mwandishi hodari wa Vitabu, ingawa, kipindi alipokuwa Sekondari, hakuwa mzuri sana darasani.

Vitabu vilimbadilisha, kama vitakavyokubadilisha na wewe na kuwa bora mara nyingi sana kuliko ilivyokuwa hapo awali.

Unaamini hayo? Mpira upo kwako. Ni maamuzi yako tu!
 
Sio vitabu tu, hata picha,movie,miziki,maongezi,simulizi, na vitu vyote vinavyoingia kupitia macho na masikio ni chakula cha ubongo.

Hivyo basi, imekupasa mwanadamu kuwa makini na kile unacholisha ubongo wako.
Kwakuwa You are what you eat.

Huwezi kupanda mahindi ukategemea kuvuna mpunga.
 
Hadithi huandikwa katika lugha yakiufundi ambayo msomaji anapaswa kutumia akili kuelewa maudhui,sio kila mtu anaweza kuelewa
Ni kweli! Hata tulipokuwa Sekondari, baadhi ya wenzangu walikuwa wakipata shida kwenye usomaji wa Vitabu vya FASIHI & LITERATURE, lakini kwenye Vitabu vingine kama Jiografia na Historia ilikuwa sawa. Ila kuna wengine wanaovimudu vyote, fiction and nonfiction, mimi ni miongoni mwao.
 
Mungu akubariki!

Umetoa msaada mkubwa sana kwa watu watakaokuelewa ulichoshauri!

Vitabu vina maarifa mengi sana!

Vina majibu yote muhimu ktk MAISHA!

Hongera sana!
Nilichojifunza, ambacho hakijathibitishwa na TCU ni kuwa, kusoma Vitabu vya darasani, madhalani kwa mwanafunzi, kumtamsaidia kufaulu mitihani ya darasani. Na kujisomea Vitabu mbalimbali kwa lengo la kujiongezea maarifa ya kimaisha, vitakusaidia kupata majibu ya kimaisha, na hata kuboresha utumiaji wa vyeti ulivyopewa shuleni.

Kwa hiyo, kusoma kunapaswa kuwa sehemu ya maisha. Haina kustaafu.

Ndiyo maana bilionea wa Marekani, Warren Buffett, pamoja na kuwa na umri wa miaka 92 kwa sasa, bado anasoma Vitabu kila siku.

Alipokuwa kijana, alikuwa akisoma kurasa 1,000 kwa siku. Kwa sasa, anasoma alau kurasa 500.

Halafu kuna watu bado wanashangaa kwa nini Wazungu wanaendelea kuwazidi Waafrika kwa mafanikio? Sababu mojawapo inaweza ikawa ni hiyo, VITABU!!!
 
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata Chuo Kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!!!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!!!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili yako.
Sawa mkuu
 
Back
Top Bottom