Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

Ni sahihi zamani nilipenda sana kusomaa vitabu tofaut hata vya dini ,,nilikua tofaut kuongea kufanyaa kazi na kujiamin hata Kuna wakati nilikua namua kuruhusu kuulizwaa swali lolote na kulijibu kwa ufahasa sio kwa sababu nilikua nimesomea vitu vingi hapana ni vile uwezo wa kufikir ulikua juu,,ukitaka kua kiongozi mzuri soma vitabu vingi.
Ubongo wa mzee sana lakini msomaji wa Vitabu huendelea kuwa active ukilinganisha na wa mzee asiye msomaji. Mfano mzuri ni Donald Trump. Kwa umri wake wa miaka 92, ilitegemewa aendelee kuwa active kwenye kazi? Vitabu vinasaidia sana.
 
Nafahamu Mtanzania mmoja, lakini simtaji jina. Alishawahi kusimulia kuwa siku chache baada ya kuajiriwa kama mhudumu wa afya, akisoma kitabu cha Napoleon Hill: THINK AND GROW RICH?
Matokeo yake? Kesho yake aliacha kazi. Kitabu alichokisoma kilibadili mwelekeo wa maisha yake. Sasa hivi ni miongoni mwa wafanyabiasha wazawa Tanzania, akimiliki makampuni ndani na nje ya Tanzania.
Ni sahihi Mimi nilikua napendelea kusomaa vitabu magezeti hata barabarani nikiona kipande Cha karatasi lenye maandishi nasoma kwa sababu nilikua naamin mtu ambaye kaandika ana akili timamu ,,akili ilibadilika sana nilivo maliza chuo nikawa sitaki kuajiriwaa ,,kujiamin sana ,,shetani haogipwi ,,ikifika kipindi nikawa nalala mlango wazi nikiamin siwezi fanyiwa unyama na binadamu Wala shetani .
 
Ni sahihi Mimi nilikua napendelea kusomaa vitabu magezeti hata barabarani nikiona kipande Cha karatasi lenye maandishi nasoma kwa sababu nilikua naamin mtu ambaye kaandika ana akili timamu ,,akili ilibadilika sana nilivo maliza chuo nikawa sitaki kuajiriwaa ,,kujiamin sana ,,shetani haogipwi ,,ikifika kipindi nikawa nalala mlango wazi nikiamin siwezi fanyiwa unyama na binadamu Wala shetani .
👏👏👏

Natamani tuanzishe club ya wasoma Vitabu! Naelewa unachosema. Naelewa mnooo!!!
 
Mimi namshukuru Mungu nimeanza kusoma vitabu nikiwa mdogo Sana, nilivyojua tu kusoma na nyumbani pia wazazi walikua wasomaji yaani nilikua nasoma vitabu,magazeti,majarida yaani nikikutana na maandishi tu Mimi nasoma hahah,nakumbuka nikiwa darasa la tatu au la nne niliishiwa vitabu nikaona nyumbani biblia kuubwaa nikaisoma lile agano la kale huwa ni Kama stori nilisoma lote nikamaliza Ila nilivyofika agano jipya nikaona sielewi nikaacha.
Pia nilipata mwalimu ambaye alielewa hobbie yangu nikiwa darasa la Kwanza akawa kila wiki ananiletea kitabu kimoja Cha hadithi nikisoma nikamaliza namrudishia ananipa kingine.Mpakq nimekua mtu mzima kwakeli nimesoma vitabu vingi Sana hadithi za watoto, novels genre nyingi nyingi, vitabu mbalimbali vya personal Growth na Non fiction nyingi sana pamoja na spiritual (Christian books) bado naendelea kusoma Kama ulivyosema vitabu ni chakula Cha akili yaani Kuna vitu vingi nimejifunza na vimenisogeza hata kwenye maisha ya kawaida kupitia vitabu.
 
hii nasadiki maana hata mm nawafundisha watoto mbinu nayoitumia nafundisha kidogo wanajisomea muda mrefu
 
Kwa mwaka huu umeshasoma Vitabu vingapi?

Ni vigumu kuifahamu ladha halisi ya asali ikiwa hujawahi kuilamba.

Maadam unajua kusoma na kuandika, chukua Vitabu kadhaa uvisome, ndipo utakapokuwa na uhalali wa kupinga au kuunga mkono.

Toafuti na hapo, msomaji wa Vitabu kubishana nawe itakuwa ni sawa na kukuonea. Atakuwa akiongelea anachokijua na wewe kujitutumua kujibu usichokijua.
Sijawahi kusoma na sina ninachokijua hivyo ninauliza na unijibu
 
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata Chuo Kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!!!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!!!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili yako.
Soma na vya Kiswahili pia, utajua tofauti ya 'thamini' na 'dhamini'.
 
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata Chuo Kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!!!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!!!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili yako.


400? Too much, vya subject hiyo hiyo
 
Ni sahihi zamani nilipenda sana kusomaa vitabu tofaut hata vya dini ,,nilikua tofaut kuongea kufanyaa kazi na kujiamin hata Kuna wakati nilikua namua kuruhusu kuulizwaa swali lolote na kulijibu kwa ufahasa sio kwa sababu nilikua nimesomea vitu vingi hapana ni vile uwezo wa kufikir ulikua juu,,ukitaka kua kiongozi mzuri soma vitabu vingi.
Usomaji ulinisaidia kushinda interview zaidi ya mara moja- interview za kazi, mbili zikiwa ni za kazi ambazo hazikuwa zikiendana moja kwa moja na taalum yangu.

Ujasiri niliokuwa nao, ambao kimsingi, ulitokana na usomaji wa Vitabu, uliwashawishi waliokuwa wakinisaili wanikubali.

Fikiria, tuliofanya interview tulikuwa zaidi ya 150, tukigombea nafasi tisa tu. Halafu Sasa, wenzangu, wengi wao walikuwa na taalum za hiyo kazi.

Niliwezaje kupenya?

Vitabu vilinisaidia kujiamini na hatimaye nikapita.
 
Kwamfano mimi sijawahi kusoma ata kitabu kimoja.

Naanzaje? Nipe tips nianze mdogo mdogo.

Je, ata kusoma vitabu vya story ni msosi wa Medulla oblongata? Au lazima viwe vitabu vya "How to become Wiseman"? "You was born to win"?
Soma hata vya hadithi, kama vimeandikwa na wabobezi, utajikuta unaboresha uelewa wa lugha inayotumika n.k.
 
Hakika yake,
For wonderers and adventurers!
Vitabu vinakusafirisha kiakili utajikuta places na nyakati zisizofikika kabisa.

tuwahimize watoto wetu kusoma ni utamaduni mzuri sana, kuna majibu mengi ya changamoto zetu kwa namna ya tofauti ya kipekee sana, mimi nasoma naye page kwa page, tunaulizana tumejifunza nini? author kafail wapi, kafaulu kufikisha ujumbe gani nk
It sharpens his mind zaidi na zaidi, siyo rahisi kwa sababu ya hizi games na animated series ila tunapambana hivyo hivyo kuna kukasirikiana kabisa lakini tunasonga.
Anasoma la ngapi
 
Soma hata vya hadithi, kama vimeandikwa na wabobezi, utajikuta unaboresha uelewa wa lugha inayotumika n.k.
Exactly! Muhimu tu, ahakikishe ni chakula salama.
 
Mimi namshukuru Mungu nimeanza kusoma vitabu nikiwa mdogo Sana, nilivyojua tu kusoma na nyumbani pia wazazi walikua wasomaji yaani nilikua nasoma vitabu,magazeti,majarida yaani nikikutana na maandishi tu Mimi nasoma hahah,nakumbuka nikiwa darasa la tatu au la nne niliishiwa vitabu nikaona nyumbani biblia kuubwaa nikaisoma lile agano la kale huwa ni Kama stori nilisoma lote nikamaliza Ila nilivyofika agano jipya nikaona sielewi nikaacha.
Pia nilipata mwalimu ambaye alielewa hobbie yangu nikiwa darasa la Kwanza akawa kila wiki ananiletea kitabu kimoja Cha hadithi nikisoma nikamaliza namrudishia ananipa kingine.Mpakq nimekua mtu mzima kwakeli nimesoma vitabu vingi Sana hadithi za watoto, novels genre nyingi nyingi, vitabu mbalimbali vya personal Growth na Non fiction nyingi sana pamoja na spiritual (Christian books) bado naendelea kusoma Kama ulivyosema vitabu ni chakula Cha akili yaani Kuna vitu vingi nimejifunza na vimenisogeza hata kwenye maisha ya kawaida kupitia vitabu.
Hongera sana mkuu. Ukiweza, waambukize na wengine!

Ni baraka kushea chakula kizuri na wenzako.
 
Ukisomaa sana vitabu jamii yote itakua kiganjani unawezaa fanyaa ukitakacho wakakuelewa.
Ni kweli, maana akili ni kama kiwanda.

Taarifa unazoziingiza ni raw materials. Itazichakata na kukupa product stahiki.

Ndiyo maana, kwa wasomaji wa Vitabu, ni rahisi zaidi kuibua mawazo mapya tofauti na wasiosoma.
 
Back
Top Bottom