Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

Mimi napenda sana vitabu tokea nikiwa mdogo, Hadi Sasa . Mtu anayesoma vitabu namheshimu sana. Na hata mtu nikikutana na mtu amebeba kitabu Nampa appreciation kimoyomoyo.. Nchi za wenzetu huko ulaya , kusoma vitabu kwao ni jadi Yao tangu zamani. Mtu anayesoma vitabu hata ku reason kwake ni tofauti sana.
IMG_20191215_230135_211_transcpr.jpg



IMG_20220118_120742_894.jpg
 
Ndiyo, kama ni story nzuri za kujenga. Lakini Mimi binafsi, kwa upande wangu, non fiction vinaweza vikawa ni vizuri zaidi.

Vitabu siyo chakula cha ubongo bali akili. Mimi siyo mtaalam wa Saikolojia lakini nafahamu kuwa ubongo siyo akili na akili siyo ubongo.

Ubongo ni kama hardware na akili ni software.

Unaposoms, yale maneno yanayoingia kwenye akili yako huweza kuathiri na utendaji kazi wa ubongo wako.

Ndiyo, maneno huweza hata kumwua mtu, ikiwa hayo maneno yataielekeza akili kufanya hivyo. Akili itakachofanya ni kuiamuru ubongo kusitisha utendaji kazi wake, na ubongo ukiacha kufanya kazi matokeo yake yanafahamika, kifo.

Lakini yakiwa chanya, yanaweza kumletea mtu manufaa makubwa sana.

Ndiyo maana ni muhimu sana kuwa makini na unachokidoma. Kitakubadilisha bila wewe kujua, sana sana ni watu wanaokufahamu ndiyo watakaobaini mabadiliko yako.

I tell you the truth, vitabu vinaweza kuathiri hata mwonekano wako wa nje. I know what I am talking about. Sijasimuliwa. Nimeiona kwa macho yangu.

Maneno humjengea mtu taswira fulani akilini mwake, na hiyo taswira hutawala matendo yake.

Maneno yanayoingia kwa wingi kwenye ufahamu wako hatimaye yatatafuta jinsi ya kujithihirisha kwa vitendo.
Aiseh

NAKUMBUKA gifte hands ya Bern carson ilinifanya nikaisoma organic chemistry advance bila tuition aiseh!!

Wakati wengi waliiona ni topic ngumu sana!!

Vitabu vina transform inner self for mutual Benefits,THINK AND GROW RICH cha napoleon Hill kilinifanya nikajenga nyumba tatu KWA space ya muda mfupi sana!!!

Siku hizi kale kautamaduni nimekaacha sana!najikuta nipo jf muda mwingi SANA!!
 
Ni kweli mkuu mi nilianza kusoma vitabu baada ya kupigwa tukio kwenye mapenzi na kitabu cha kwanza kukisoma kilikuwa kinaitwa MEN ARE FROM MARS AND WOMEN ARE FROM VENUS Pamoja na kimoja kinaitwa UNDERSTAND THE POWER AND PURPOSE OF MAN .

Sasa hivi nisiposoma vitabu naona kabisa kuna kitu hakipo sawa kuna mda nakuwa bize sana ila nimejitahidi mpaka sasa nimeshazoe na nimesoma vitabu kama NEW WORLD ORDER, THE MAGIC OF THINKING BIG, THE POWER OF POSITIVE THINKING kwa siku za karibuni nimevimaliza sasa hivi namalizia (48 Laws of power) naona kabisa nimebadilika mentally
Wazee tusome vitabu vinasaidia hasa wenye changamoto za maisha vinasaidia sana.
 
Aiseh

NAKUMBUKA gifte hands ya Bern carson ilinifanya nikaisoma organic chemistry advance bila tuition aiseh!!

Wakati wengi waliiona ni topic ngumu sana!!

Vitabu vina transform inner self for mutual Benefits,THINK AND GROW RICH cha napoleon Hill kilinifanya nikajenga nyumba tatu KWA space ya muda mfupi sana!!!

Siku hizi kale kautamaduni nimekaacha sana!najikuta nipo jf muda mwingi SANA!!
Ukisoma Rich dad poor dad na hicho ulichokitaja unakuwa bahili balaa mi nilinunua kiwanja kwasababu ya vitabu mkuu.
 
Mimi napenda sana vitabu tokea nikiwa mdogo, Hadi Sasa . Mtu anayesoma vitabu namheshimu sana. Na hata mtu nikikutana na mtu amebeba kitabu Nampa appreciation kimoyomoyo.. Nchi za wenzetu huko ulaya , kusoma vitabu kwao ni jadi Yao tangu zamani. Mtu anayesoma vitabu hata ku reason kwake ni tofauti sana.View attachment 2645904


View attachment 2645907
Vinapatikana wapi. Mf hivyo ulicyoweka hapo, eye of the needle, staying alive
 
Mkuu anzisha Group LA Whatssaap LA wasoma vitabu tujiunge,then weka Link hapa atakae kujiunga ajiunge.

Humo kutakuwa na Library ya Vitabu mbalimbali na vitawekwa kulingana na maudhui yake,yeyote atakae kwa muda wake anajipakulia anaendelea kujisomea.

Uzuri wa Group huna sababu ya kubeba kitabu popote uendapo sababu ya changamoto za kimaisha,ila Kitabu kikiwa ktk Soft copy kinarahisisha usomaji wake japo Hard copy ina raha yake ukiwa na muda mzuri na sehem sahihi ya kujiongezea kipato.

Kuna Group nilikuwemo lina utulivu sana hakuna discussion zisizo na msingi wowote zaidi ya ukimya tu kutawala,kikipostiwa kitu basi ni kitabu or Link ya kitabu or vitabu mbalimbali vinapopatikana.Baada ya kupoteza simu nimeshindwa kurudi mule tena sababu sikuwa na namba ya MTU wa mule aweze kunirudisha.
 
Share hapa vitabu ulivyosoma
Mkuu, sina uhakika kama nimekuelewa ipasavyo, na sina uhakika pia kama nitakavyojibu ndivyo inavyohitajika.

Lakini kwa kuwa hili ni jukwaa la vichwa timamu, naamini, makosa nitakayoyafanya yatarekebishwa na hivyo kuwa na manufaa kwangu na kwa wengine wengi pia.

Nimevisoma both spiritual na visivyo spiritual, lakini hapa nitagusia non spiritual pekee. Hivi ni baadhi:

1. HOW YOU CAN GET RICHER QUICKER; By M. R. Kopmeyer
Ingawa sikubaliani na kila kitu kilichoandikwa na Kopmeyer, ambaye anajiita AMERICA'S SUCCESS COUNSELOR, kitabu chake hicho ni miongoni mwa vitabu ambavyo nimetokea kuvikubali sana. Nilichojifunza kwenye Vitabu vyake, hicho kikiwemo, kimenisaidia mimi binafsi na hata kuniwezesha kuwasaidia wengine.

Ni kwenye hicho kitabu nilikutana, kwa mara ya kwanza, na neno "SUBCONSCIOUS MIND".
Nilipofahamu kuwa taarifa yoyote utakayofanikiwa kuipenyezea subconscious mind kitakachofuatia ni utekelezaji, niliamua kufanya jaribio kwa mfanyakazi mwenzangu. Nilimwaminisha kuwa ana sifa ya kuweza kupandishwa cheo, na baada ya muda, alichukua hatua iliyompelekea kuwa hivyo.

2. FAILING FORWARD; by Dr. John C. Maxwell
Kinahamasisha kutokuhofua kufeli. Kinaaminisha kwamba FAILURE IS A BLESSING IN DISGUISE. Kutokufikia matokeo uliyoyakusudia, siyo kwamba umeshindwa, bali ni ujumbe kuwa kuna mabadiliko yanayohitajika. Kwa sababu hiyo, hupaswi kumlaumu mtu yeyote, au hata kitu chochote. Ukilaumu, utakuwa umeweka sahihi kuwa umeshashindwa.

Lakini kama utauruhusu mtazamo chanya kukutawala, utajiaminisha kuwa hujashindwa ila kuna marekebisho yanayohitajika. Kwamba, umegundua njia ambayo haitakufikisha unakotaka, hivyo inakulazimu kujaribu njia nyingine mpya, ambayo huenda ikakufanikisha.

Kati ya visa vilivyonifurahisha kwenye hicho kitabu, ni habari ya mtu mmoja aliyeishia kuwa mfanyabiashara mwenye mafanikio makubwa baada ya kufukuzwa kazi ya ulinzi.

Akiwa ameajiriwa na Kanisa la Anglikana kama mlinzi nchini Uingereza, ilibainika kuwa hakuwa akijua kusoma wala kuandika, na hivyo mwajiri wake akaishia kumfukuza kazi.

Hali hiyo ilimlazimu kufungua kaduka kadogo ili kupata hela ya kujikimu, lakini miaka michache baadaye, kaduka kake kalizaa maduka mengine mengi na kumfanya kuwa miongoni mwa matajiri mtaani kwao. Hakujua kusoma wala kuandika, lakini alikuwa tajiri na maarufu.

Siku moja alipoulizwa na mwandishi wa habari kuwa ingelikuwaje kama angekuwa anajua kusoma na kuandika; alijibu, "Ningekuwa mlinzi wa Kanisa la Anglikana".

Kufukuzwa kwake kazi kwa sababu ya kutokujua kusoma na kuandika kulimchochea kugundua uwezo wake wa kufanya biashara na kumfanya kuwa tajiri kumzidi aliyekuwa bosi wake. Kuachishwa kazi kuligeuka kuwa baraka kwake. Ndiyo maana wanasema, FAILURE IS NOTHING BUT A BLESSING IN DISGUISE!

3. AWAKEN THE GIANT WITHIN; By Anthony Robbins
Miongoni mwa mambo nilivyojifunza ni umuhimu wa kuweka Lengo na kuzielekeza fikra zako zote huko kwenye hilo lengo.
Hilo lengo, ikiwa limembatana na hisia kali sana, au umelitafakari kwa muda mrefu, huishia kuwa maelekezo kwenye subconscious mind. Bila kujali kama ni zuri au baya, subconscious mind itakutengenezea mazingira ya kuwa vivyo hivyo, sawa sawa na lengo lako.


4. SNOW BALL: WARREN BUFFETT AND THE BUSINESS OF LIFE
Kitabu chake kilinihamasisha kusoma vitabu zaidi. Alinitia wivu alivyoelezea jinsi alivyoanza kusoma vitabu akiwa na umri wa miaka saba. Alipofikisha miaka tisa, alianza kufanyia kazi alichokuwa akisoma.

Tabia yake ya usomaji ilimpelekea kuwa mwekezaji mkubwa sana ndani na nje ya Marekani.

5. THE LAWS OF SUCCESS; by Dr. Napoleon Hill
Kati ya mambo ambayo nayakumbuka, ni jinsi maneno mtu anayoyasikia yanavyoweza kuitawala akili yake kulingana na asili ya hayo maneno.

Kwa mbinu ijulikanyo kama SUGGESTION, mtu anaweza kutawala fikra za mtu mwingine, na kwa AUTOSUGGESTION, humsaidia kuzitawala fikra zake binafsi.

Ikitokea subconscious mind, kwa mfano, ikaaminishwa kuwa "huyu mtu anatakiwa kufa, "itakachofanya ni kuyasimaisha mapigo ya moyo na hatimaye lengo kufikiwa.

6. HOW TO WIN FRIENDS AND INFLUENCE PEOPLE; By Dale Carnegie
Kimenisaidia kuwaelewa watu wengine na kuniepusha na uwezekano wa kukasirika kirahisi pale ninapotendewa jambo la kukwaza. Kimenisaidia kufahamu kuwa kati ya hitaji kubwa sana kwa kila binadamu, ni shauku ya kutambuliwa.

Kwa hiyo, hata inapotokea wakati mwingine mtu akanikosoa kwa namna isiyo na staha, nakumbuka kuwa huenda nafsi yake ina njaa sana ya kutambuliwa. Yeye mwenyewe anayefanya hivyo hajui hilo, ila kwa mwelewa, atajua kuwa hicho ni kilio cha ndani kinachotaka mhusika naye apewe attention! Kwa hiyo, badala ya kujibu kwa hasira, nitatenda kulingana na nitakavyoona inafaa.

7. THE RICHEST MAN IN BABYLON, By Samuel G. Classon
Huwezi kujisomea hicho kitabu na usione umuhimu wa kuweka akiba (savings)

8. STAY LOCAL AND GOING GLOBAL
Silikumbuki jina la mwandishi, ila ni Mnigeria. Ndicho kitabu cha kwanza kujifunza umuhimu wa SYSTEM (mfumo) kwenye kazi/biashara. Kwamba, kama utaanzisha biashara ambayo hutaki ubanwe na uendeshaji wake, yakupasa kutengeneza mfumo utakaoweza kumtawala kila mtu atakayekuwa akifanya kazi humo.

9. CASHFLOW QUADRANT; By Robert Kiyosaki
Kimeelezea vyanzo Vikuu 4 vya fedha/ utajiri na umuhimu wa kilia kimoja: EMPLOYMENT, SELF EMPLOYEE, BUSINESS & INVESTMENT.

The quickest of all, in most cases, katika kufikia utajiri wa haraka, ni BUSINESS. Lakini ambayo haina stress ni INVESTMENT. Ukiwekeza, fedha yako itakuwa ikifanya kazi kwa niaba yako

10. THOUGHTS TO BUILD ON; By M. R. Kopmeyer
Wazo aliwazalo mtu muda mrefu, hatimaye huishia kulitenda. Kwa hiyo, maisha ya mtu ni jumla ya mawazo aliyowahi kuwaza.

11. HOW TO START A MULTIBILLION BUSINESS IN AFRICA FROM THE SCRATCH; By Strive Masiyiwa.
Bilionea huyu mwenye uraia wa Zimbabwe na Uingereza, ameelezea jinsi MANAGEMENT ilivyo ya muhimu sana kwenye biashara. Ndiyo uti wa wa mgongo wa biashara yoyote ile.

Humo utakutana na masuala ya:
(A). Financial Management
(B). Human Resources Management,
E.t.c.

12. WHO WILL CRY WHEN YOU DIE; By Robbins Sharma
Kati ya vitu nilivyojifunza ni umuhimu wa kuwa na kauli ya kujisemesha mara kwa mara kwa lengo la kutawala fikra zako. Kwa mfano, kama unaenda kufanya presentation mbele ya watu ambao hujazoeana nao, na ukawa unahofu kuwa huenda utakosa ujasiri wa kuzungumza mbele yao, unaweza ukaamua kujisemea mara kwa mara, "KUONGEA MBELE YA UMATI WA WATU NI JAMBO RAHISI SANA". Kwa kufanya hivyo, kila seli ilyopo kwenye mwili wako itaelekezwa kukufanya ujisikie hivyo na kutenda hivyo.

Nilipompatia hicho kitabu rafiki yangu mmoja ambaye alikuwa Mwalimu wa Sekondari, aliishia kuacha ajira ya ualimu baada ya kukisoma.

Nilipokutana naye baadaye, alinieleza kuwa hicho kitabu kilimfanya afahamu kuwa alichokuwa anakifanya(ualimu wa Sekondari) sicho alichoumbiwa kufanya.

Aliacha kazi ya ualimu na kuanzisha shughuli zake binafsi.

Jamani ee, nimejaribu kwa kadiri ya ufahamu wangu, ila mpaka sasa, sijui kama ndicho kilichokuwa kinahitajika.
 
Mimi napenda sana vitabu tokea nikiwa mdogo, Hadi Sasa . Mtu anayesoma vitabu namheshimu sana. Na hata mtu nikikutana na mtu amebeba kitabu Nampa appreciation kimoyomoyo.. Nchi za wenzetu huko ulaya , kusoma vitabu kwao ni jadi Yao tangu zamani. Mtu anayesoma vitabu hata ku reason kwake ni tofauti sana.View attachment 2645904


View attachment 2645907
Mimi napenda sana vitabu tokea nikiwa mdogo, Hadi Sasa . Mtu anayesoma vitabu namheshimu sana. Na hata mtu nikikutana na mtu amebeba kitabu Nampa appreciation kimoyomoyo.. Nchi za wenzetu huko ulaya , kusoma vitabu kwao ni jadi Yao tangu zamani. Mtu anayesoma vitabu hata ku reason kwake ni tofauti sana.View attachment 2645904


View attachment 2645907
Mwezi April mwaka huu, nilimtembelea rafiki yangu ambaye sikuwa nimeonana naye kwa miaka kadhaa.

Katika siku tatu nilizokaa naye, niligundua ongea yake, hasa reasoning, imekuwa tofauti sana na nilivyokuwa nikimfahamu.

Ni kati ya marafiki zangu ambao nilijitahidi kuwahimiza wasome vitabu lakini sikufanikiwa kuwashawishi.

Kutokana na jinsi alivyokuwa akijenga hoja, nilimwumiza zaidi ya mara moja siri ya mabadiliko yake, lakini aliishia kuniambia ni kawaida tu.

Lakini Kabal ya kuondoka, nilibaini sababu ya mabadiliko niliyoyaona katika ongea yake. Naye ameshaanza kusoma vitabu. Mpaka mwezi huo wa April, alikuwa ameshasoma ya Vitabu mia moja.

Kama hiyo haitoshi, alikuwa amepanga kwa mwezi May 2023 asome Vitabu kumi.

Msomaji wa Vitabu, bila kujali kama ana cheti au hana, ndiye Msomi halisi.

Ukweli ndiyo huo.

Mtu aliyeishia darasa la pili lakini akajijengea tabia ya usomaji vitabu, atakuwa na uelewa mkubwa sana unaoweza usifikiwe hata na maprofesa.
 
Mwezi April mwaka huu, nilimtembelea rafiki yangu ambaye sikuwa nimeonana naye kwa miaka kadhaa.

Katika siku tatu nilizokaa naye, niligundua ongea yake, hasa reasoning, imekuwa tofauti sana na nilivyokuwa nikimfahamu.

Ni kati ya marafiki zangu ambao nilijitahidi kuwahimiza wasome vitabu lakini sikufanikiwa kuwashawishi.

Kutokana na jinsi alivyokuwa akijenga hoja, nilimwumiza zaidi ya mara moja siri ya mabadiliko yake, lakini aliishia kuniambia ni kawaida tu.

Lakini Kabal ya kuondoka, nilibaini sababu ya mabadiliko niliyoyaona katika ongea yake. Naye ameshaanza kusoma vitabu. Mpaka mwezi huo wa April, alikuwa ameshasoma ya Vitabu mia moja.

Kama hiyo haitoshi, alikuwa amepanga kwa mwezi May 2023 asome Vitabu kumi.

Msomaji wa Vitabu, bila kujali kama ana cheti au hana, ndiye Msomi halisi.

Ukweli ndiyo huo.

Mtu aliyeishia darasa la pili lakini akajijengea tabia ya usomaji vitabu, atakuwa na uelewa mkubwa sana unaoweza usifikiwe hata na maprofesa.
Nakubali ,ingawaje majority ya watu wakimuona mtu akisoma vitabu wanamuona kama ni old fashioned... Ndio maana kwenye jamii yetu ya ki Tz mambo ujinga unapewa kipaumbele sana. Kuna muda nikiangalia let's say movie za majuu unaweza kuona mtu sebuleni kwake Kuna shelf safi ya vitabu kadhaa SI chini ya 100 .. hayo maisha Yana ni inspire sana...
 
Mkuu anzisha Group LA Whatssaap LA wasoma vitabu tujiunge,then weka Link hapa atakae kujiunga ajiunge.

Humo kutakuwa na Library ya Vitabu mbalimbali na vitawekwa kulingana na maudhui yake,yeyote atakae kwa muda wake anajipakulia anaendelea kujisomea.

Uzuri wa Group huna sababu ya kubeba kitabu popote uendapo sababu ya changamoto za kimaisha,ila Kitabu kikiwa ktk Soft copy kinarahisisha usomaji wake japo Hard copy ina raha yake ukiwa na muda mzuri na sehem sahihi ya kujiongezea kipato.

Kuna Group nilikuwemo lina utulivu sana hakuna discussion zisizo na msingi wowote zaidi ya ukimya tu kutawala,kikipostiwa kitu basi ni kitabu or Link ya kitabu or vitabu mbalimbali vinapopatikana.Baada ya kupoteza simu nimeshindwa kurudi mule tena sababu sikuwa na namba ya MTU wa mule aweze kunirudisha.
Inaweza ikawa msaada? Labda, tuvute muda kidogo tujiridhishe kama ni jambo litakalokuwa na tija.
 
Nakubali ,ingawaje majority ya watu wakimuona mtu akisoma vitabu wanamuona kama ni old fashioned... Ndio maana kwenye jamii yetu ya ki Tz mambo ujinga unapewa kipaumbele sana. Kuna muda nikiangalia let's say movie za majuu unaweza kuona mtu sebuleni kwake Kuna shelf safi ya vitabu kadhaa SI chini ya 100 .. hayo maisha Yana ni inspire sana...
Miaka ya nyuma, niliwahi kushauriwa na mtu zaidi ya mmoja kuwa nipunguze kusoma vitabu. Japo waliamini ni ushauri mzuri, namshukuru Mungu sikuupokea huo ushauri.
 
Miaka ya nyuma, niliwahi kushauriwa na mtu zaidi ya mmoja kuwa nipunguze kusoma vitabu. Japo waliamini ni ushauri mzuri, namshukuru Mungu sikuupokea huo ushauri.
Hii nishawahi kukumbana nayo... Baada ya kutema facts ambazo hazikuwaingia akilini. Maana waliniuliza umetoa wapi ,nikawajibu ni vitu vimeandikwa... Jamaa akanijibu nipunguze kusoma vitabu ,[emoji848] I don't what's wrong with my fellow country people
 
Hii nishawahi kukumbana nayo... Baada ya kutema facts ambazo hazikuwaingia akilini. Maana waliniuliza umetoa wapi ,nikawajibu ni vitu vimeandikwa... Jamaa akanijibu nipunguze kusoma vitabu ,[emoji848] I don't what's wrong with my fellow country people
Wa kwanza kunishauri nipunguze usomaji, nilimjibu kuwa badala ya kupunguza, nitaviongeza, na ndivyo nilivyofanya.
 
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata Chuo Kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!!!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!!!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili yako.
ukitaka kumficha mtanzania, weka maandishi kwenye kitabu
 
Tupen Sasa hicho Cha Think and grow rich .
Au tupen link tudowload
 
Kwel kabisa ,kuna kipind nilikua nimekataa tamaa ya maisha ,sababu ya kero za mimba changa,yaan ile tapikatapika ,kukerwa na harufu za za karibu kila kitu iwe chakula,mafuta n.k.nikapata kwa rafik yangu kitabu kinaitwa"how to stop worries and start and start living" nikakisoma kwa utulivu mkubwa sana,aisee kilinibadilisha mind set nikapona kabisa,mate nkaacha kutema ,nkaanza kula kila kitu,nakurejea na majukumu yangu nikiwa imara kabisa.mpaka leo huwa sikisahau kuna vitu naviapply kwny maisha yng kupitia kile kitabu na majib ni mazur ,
 
Kwel kabisa ,kuna kipind nilikua nimekataa tamaa ya maisha ,sababu ya kero za mimba changa,yaan ile tapikatapika ,kukerwa na harufu za za karibu kila kitu iwe chakula,mafuta n.k.nikapata kwa rafik yangu kitabu kinaitwa"how to stop worries and start and start living" nikakisoma kwa utulivu mkubwa sana,aisee kilinibadilisha mind set nikapona kabisa,mate nkaacha kutema ,nkaanza kula kila kitu,nakurejea na majukumu yangu nikiwa imara kabisa.mpaka leo huwa sikisahau kuna vitu naviapply kwny maisha yng kupitia kile kitabu na majib ni mazur ,
Wao! Kitabu kizuri sana: HOW TO STOP WORRYING AND START LIVING by Dale Carnegie.

Asante kwa huo ushuhuda. Usomaji vitabu unalipa sana!
 
ukitaka kumficha mtanzania, weka maandishi kwenye kitabu
Nafikiri ni tabia ya Waafrika wengi. Ndiyo maana wengi wakishahitimu masomo wanaagana na vitabu.

Kwa Wazungu wengi, ni jambo la kawaida kujiwekea bajeti ya Vitabu kila mwaka.

Lakini kwa Watanzania, ni wachache sana wanaofanya hivyo.
 
Back
Top Bottom