Asiyoyajua Yericko Nyerere katika utafiti wa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar

Asiyoyajua Yericko Nyerere katika utafiti wa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar

Yericko Nyerere Lete hoja kwa ushahidi Yericko ndugu yngu achana mambo kufikirika lini wapi kanisa lilikuwa bega kwa bega ktk kupingania uhuru wa nchi hii pia ktk uandishi jifunze kueleza wapi umetoa maandishi kmc utakuwa umecopy sehemu hakika khs mapinduzi kitabu cha kwakheri ukoloni kwakheri Uhuru kimemaliza kila kitu na kuthibitisha kuwa yale yalikuwa mavamizi jaribu kumsikiliza marehemu Aman Thani Ferouz kwenye yutube...
 
Nguruvi3,
Mimi nitajibu swali lako kwa kukupa kazi kidogo.

Chunguza matokeo ya uchaguzi mkuu Zanzibar toka 1995 angalia vipi Wazanzibari wanapiga kura na nini inakuwa matokeo yake.

Jibu lako liko hapo.
Hatuna haja ya kuzunguzuka zunguka na kukwepa hoja.
Mara uchaguzi wa 1995 ulifanyika miaka mingi baada ya Mapinduzi 1964! wazungu wanasema 'anachronism'

Swali lisilo na majibu kwa miaka linaendelea kwasababu hatujadili mambo kwa ukweli wa nafsi zetu

Nafasi ya weledi imechukuliwa na chuki, nafsi zetu zinaongozwa na Unafiki , tukijifaragua wakweli kwa uzandiki

Wanajamvi, Mohamed Said anasema mapinduzi yalichochewa na watu kutoka nje ya Zanzibar kwa mujibu wake
Kwa mantiki hiyo mapinduzi ni haramu. Hili halina mjadala tena

Wazanzibar, Mohamed Said anawaambia kusherehekea Januari 12 ni kutukuza haramu.
Kwa maneno mengine, ninyi mnaosema mapinduzi matukufu hamuelewi kuwa mapinduzi ni haramu

Kwa mantiki hiyo MAPINDUZI YA ZANZIBAR kwa mujibu wa Mohamed ni Haramu inayosherehekewa na WAZANZIBAR bila kujua wanasherehekea HARAM... Wazanzibar acheni kutukuza haramu kwa mujibu wa Mohamed Said
 
Lete hoja kwa ushahidi Yericko ndugu yngu achana mambo kufikirika lini wapi kanisa lilikuwa bega kwa bega ktk kupingania uhuru wa nchi hii pia ktk uandishi jifunze kueleza wapi umetoa maandishi kmc utakuwa umecopy sehemu hakika khs mapinduzi kitabu cha kwakheri ukoloni kwakheri Uhuru kimemaliza kila kitu na kuthibitisha kuwa yale yalikuwa mavamizi jaribu kumsikiliza marehemu Aman Thani Ferouz kwenye yutube...
Unataka ushahidi wa kipi ikiwa kitabu hujakisoma?

Nimekufafanulia hapo kwamba marejeo yote yamewekwa wazi, au hujui maana ya marejeo?
 
Hatuna haja ya kuzunguzuka zunguka na kukwepa hoja.
Mara uchaguzi wa 1995 ulifanyika miaka mingi baada ya Mapinduzi 1964! wazungu wanasema 'anachronism'

Swali lisilo na majibu kwa miaka linaendelea kwasababu hatujadili mambo kwa ukweli wa nafsi zetu

Nafasi ya weledi imechukuliwa na chuki, nafsi zetu zinaongozwa na Unafiki , tukijifaragua wakweli kwa uzandiki

Wanajamvi, Mohamed Said anasema mapinduzi yalichochewa na watu kutoka nje ya Zanzibar kwa mujibu wake
Kwa mantiki hiyo mapinduzi ni haramu. Hili halina mjadala tena

Wazanzibar, Mohamed Said anawaambia kusherehekea Januari 12 ni kutukuza haramu.
Kwa maneno mengine, ninyi mnaosema mapinduzi matukufu hamuelewi kuwa mapinduzi ni haramu

Kwa mantiki hiyo MAPINDUZI YA ZANZIBAR kwa mujibu wa Mohamed ni Haramu inayosherehekewa na WAZANZIBAR bila kujua wanasherehekea HARAM... Wazanzibar acheni kutukuza haramu kwa mujibu wa Mohamed Said
Nguruvi3,
Hayo maneno ni yako mimi sijasema popote maneno hayo.

Ninachokuambia ni kuwa hebu jaribu kuchunguza nini
Wazanzibari wanataka kila wanapopiga kura kuanzia 1995.

Uchaguzi wa 2015 kila kitu kilikuwa wazi hatuhitaji kuambiwa.

Nakuwekea mahojiano niliyifanya mwaka jana 2017 kuhusu
mapinduzi:

Mahojiano na Uhai FM 2017 kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ☝
MOHAMED SAID ANAYACHAMBUA MAPINDUZI NA MAANA YAKE

Mohammed Said: Radio Uhai FM

Sherehe za mapinduzi kadri tunavyoendelea kuziadhimisha vizazi vinavyokuja vinajifunza kitu gani?

JIBU
Kwanza ni kuwa watu wengi washajua ukweli wa mapinduzi. Na hayana nguvu au umuhimu kama viongozi wetu wanavyodhani. Watu wanataka maendeleo na utangamano, wamepiga kura hapa ya serikali ya umoja wa kitaifa, umeona matokeo yake, watu wengi wamepiga kura kutaka serikali ya umoja wa kitaifa.

Sasa yale mambo ya mapinduzi, ya sijui tulikuwa tukifanywa hivi na vile, hakuna mtu sasa anayetaka kusikia hivyo. Mambo hayo yanepita. Watu wanataka kutizama mbele. Na kuona nchi inatoka kwenye umasikini inakwenda kwenye maendeleo. Kadri tunavyokwenda ndio hawa wana mapinduzi wanavyozidi kupoteza nguvu.

Kama nilivyokuambia mwanzo kama kweli haya mapinduzi yana nguvu hivyo mbona wanashindwa kushinda uchaguzi huru na haki??

SWALI:
Uligusia pale mwanzo sheikh Mohammed kwamba kuna swala moja kubwa sana kila unapotazama historia ya kweli kabisa iliyoandikwa kuhusu mapinduzi yanazungumzwa masuala ya mauaji makubwa sana ambayo yalitokea. Hiyo inabaki kuwa ni kumbukumbu kubwa sana. Haya mauwaji yalitokana na msigano wankitu gani. Nini sababu hasa?

JIBU:
Ndio, Profesa Ibrahim Noor akaandika kitabu kile "Propaganda na udini Tanzania", akaonesha tarekh yake. Zile propaganda za kuwa Waarabu walikuja kukamata watumwa. Utumwa umefanywa na mataifa mengi. Hakuna utumwa mbaya kama ule wa Trans Atlantic Slave Trade - unaotoka Afrika magharibi na kuvuka bahari kwenda Marekani. Ule ndio unyama mkubwa. Hakuna utumwa mbaya kama wa Ubelgiji Kongo. Hawayasemi hayo. Wao kila siku wanawasingizia Waarabu tu. Na ukiwapeleka huko huwa hawana la kusema, wananyamaza kimya. Hizi propaganda ndizo zilizosababisha mauaji makubwa sana kutokea baada ya miaka zaidi ya 150 kuondolewa kwa biashara ya utumwa.

Miaka kama 20 iliyopita tusingeweza kufanya kitu kama hiki watu wakatusikiliza. Leo hivi tunazungumza bila ya matatizo. Na vijana wetu wanatakiwa waelezwe ukweli wa historia. Kuwa hii ni historia. Na usemwe ule ukweli. Watu wanaelewa. Na ndio maana kwa kuelewa kwao huko wanamapinduzi wanashindwa kushinda chaguzi huru.

SWALI:
Hebu nisaidie kunifumbua kidogo hata kwa jinsi ulivyosoma tu. Turudi nyuma zaidi ya 1964 kwanzia miaka ta 1952 uliozaliwa wewe kwenda nyuma, je maisha ya Zanzibar yalikuwa ni ya namna gani?

JIBU:
Nitakwambia kitu kimoja. Kulikuwa na watu wana nafasi zao katika jamii ya Waarabu hili huwezi kuliepuka. Haya yote ni katika madhara ya ukoloni. Na Sultan alikuwa hana nguvu hivyo. Nguvu zote alikuwa anazo Muingereza.

Kulikuwa na Waarabu masikini wakifanya kazi za vinyozi, wakilima, wakiuza kahawa mitaani, na wengine wakifanya kazi za utopasi zile za kutapisha choo, zamani vile vyoo vya shimo wanakuja kupakuwa na wakibeba kwa mapipa kwenda kumwaga. Si kama Waarabu wote walikuwa katika hali ya juu. Walikuwepo masikini. Wakitumikishwa kazi kama anavyotumikishwa Muafrika. Ukisoma kitabu cha Profesa Ibrahim Noor utayakuta haya yote. Na hizi chuki wanazosema ni za kupandikiza. Sultan aliondoka Zanzibar bila ya kuuwa raia wake, aliondoka mikono misafi haina damu ya mtu yeyote. Damu imeanza kumwagika baada ya hao wanaoitwa wanamapinduzi kushika serikali. Ndio wakaanza kuuwa watu na kuwaweka kwenye jela za mateso. Nadhani nimelijibu suali lako.

[HASHTAG]#Pray4Zanzibar[/HASHTAG]
 
Nikushukuru sana mzee wangu kwakunikumbusha vema,

Mohamed Said ni mmoja ya watu muhimu walionifundisha historia, nitakuwa mjinga sana nisipomshukuru na kumheshimu mzee huyu, na katika kitabu changu nimemtaja kama mmoja ya watu muhimu ambao vitabu vyao nimevirejea....

Kitabu tunachokabidhiana hapo kwenye picha ni kitabu cha majaribio tu kikiwa na sura 4 na kurasa 200 tu, lengo la kukichapa ilikuwa ni ushauri wa vyombo vya dola kuona mapokeo ya umma, baada ya mapokeo kuwa mazuri kilihaririwa upya na kuchapwa upya kikiwa na sura 6, kurasa 715, vilelezo 366, vielelezo siri 88, vielelezo huru 34, nyaraka 18 nk....

Kitabu hiki toleo la pili kimechimba historia ya mapinduzi kwa undani wake, hata yale Mzee Mohamed Said na wengine hawakuyajua yamo...

Kimechimba juu ya Abeid Karume, mauaji yake na mapito ya Zanzibar hadi leo hii.

Nje ya hapo kitabu kimebadili kabisa ngano za Mohamed Said juu ya historia ya Uhuru wa Tanganyika, Yale asiyoyapenda Mohamed yote yameletwa pamoja, hasa hasa uratibu na ushiriki wa Kanisa katoliki kupitia shirika lake la kijasusi la Jeisuti juu ya Uhuru wa Tanganyika...

Mambo haya ni mapya kwa Mohamed Said na wengine....ni lazima alipuke kwa hofu...

Mwaka 2013 tulikutana hapa jamvini katika mjadala uliochukua mwaka mzima hapa mimi nikikosoa ngano za Mzee Mohamed juu ya Uhuru akiunasibisha na uislamu wa Dar na kuwatenga waamini wengine kabisa... Nilimuonya kuwa mimi nitazifuta ngano zake na kusimama kwenye mlengo mwingine kabisa... Naam nimefanya hivyo... Leo watu wamejua nani alikuwa nyuma ya uhuru, nani alikuwa nyuma ya Julius Nyerere, nani alikuwa kiungo muhimu mpaka uhuru....

Haya ni mageni kwa Mohamed, mlipuko wake niliutaraji, hapa analipuka huku bado kabisa hata kitabu hajakisoma kabisa, ila anaona hizi dondoo tu ameanza kuja na kejeli na matusi lukuki dhidi yangu...

Kitabu kimeshapata sifa ya kitaifa na kimataifa, yeye amesema hakinunuliki, sijui anataka aje niwe namuonyesha kuwa huyu kanunua na yule kanunua....

Wataalamu na wasomi leo wanapendekeza nitunukiwe shahada mbili za uzamivu kwa kuandika kitabu kimoja tu, na wamefurahishwa sana katika historia na ujasusi.... Leo mzee wa ngano za kariakoo anakuja na matusi juu...

Katika madai ya Mzee Mohamed anasema kwamba nimenakili yaliyoandikwa, ukweli nikuwa wa wale waliobahatika kukisoma kitabu changu wataona maandishi yote yakunakili yanamarejeo na nyaraka mwishoni nyuma ya kitabu... Labda uwe mvivu na mwenye wivu uliovuka mipaka kama wa mzee Mohamed Said.

Nikushauri kama ulivyotushauri sisi kipindi kile 2013 kwamba historia yako tuipinge kwa kuandika kitabu, nawe ni wakati wakupinga kitabu cha Ujasusi wa Kidola naKiuchumi kwakuandika kitabu, nje ya hapo ni porojo tu mzee.... Na zaidi unanisaidia sana kunadi kitabu... Weekend nitakutafuta tupate sharubati na vibansi pamoja
Yericko,
Haitapendeza kwangu mimi nishindane na wewe kuhusu kitabu chako.
Uungwana unanikataza.

Kitabu kipo na kama mimi nitafanya, ''critique,'' yoyote basi iwe ya kisomi
isiwe kuishambulia kazi yako.

Kama kweli ''umechimba,'' historia ya mapinduzi hilo ni jambo jema na
wa kulisemea hilo si mimi na wewe bali ni wasomaji wa kitabu chako na
watakaokufanyia ''book review.''

Nasubiri kusoma ''reviews,'' za kitabu kama ninavyongoja kuona na kusoma
habari mpya za mapinduzi ambazo unasema Dr. Ghassany hakuziona katika
utafiti wake.

Ghassany alikuja na Mohamed Omari Mkwawa na Victor Mkello na kina
Lumumba, Aboud Mmasai na hawa wote picha zao na sauti zao zipo katika
Maktaba kwa ajili ya rejea kwa watafiti wengine siku za usoni.

Ghassany kaja na Kipumbwi, kambi ya askari mamluki waliovushwa kuingia
Zanzibar kusaidia mapinduzi.

Habari hii ya Wamakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura ambayo
haikufahamika toka mwaka wa 1964 ikaja kusomwa mwaka wa 2010 katika
kitabu cha Dr. Ghassany baada ya miaka 46 kupita.

Vumbi la habari hizi kila msomaji wa kitabu kile analijua.

Ikiwa wewe kitabu chako kina mambo zaidi ya hayo utakuwa umefanya kazi
kubwa sana ya kupigiwa mfano na itasaidia sana kukitangaza kitabu chako
kama utaeleza haya yakafahamika.

Nakushauri usiache kuonyesha na kueleza mambo kama haya ili wasomaji
wavuitiwe na ukweli uliokujanao katika kitabu chako hiki.

Itakuwa vizuri sana kama hawa wasomi wanaopendekeza utunukiwe shahada
kwanza kabla ya hayo wao kwa usomi wao ungewaomba waandike ''review,''
ya kitabu chako ili wasomaji wajue nini umeeleza katika kazi hii yako.

Nionavyo mie si busara mathalan kwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam au chuo
chochote kile kuanza kukupa shahada kabla ya kuonyesha kwanza uzito wa kazi
yako au hata kabla kitabu hakijaandikiwa, ''reviews'' na kuchapwa katika majarida
kama Cambridge Journal of African History.

Kweli unastahili sifa kubwa sana kuwa kitabu ni cha Kiswahili lakini kinasomwa
dunia nzima na watu ambao hawajui Kiswahili.

Unastahili sifa sana kwani hiki ulichofanikiwa wewe si kitu kidogo.

Nakueleza haya kutoka moyoni kwangu kwani mimi kama mtu wa vitabu naujua
vizuri ugumu uliopo katika biashara ya vitabu hasa kitabu kilichoandikwa na
mwandishi ambae hajawahi kuandika kitabu.

Umenishauri niandike kitabu nipinge kitabu chako.
Sidhani kama hili ni jambo la busara kwani huwezi kuandika kitabu juu ya kitabu.

Hakuna ''publisher,'' atakaegusa mswada kama huo kwa kuwa somo nimeshaliandika
na kitabu kipo.

Kitabu chako wewe kimekuja nyuma ya kitabu changu kwa takriban miaka 20.

Ninachoweza kufanya ni mimi kufanya ''book review,'' ya kitabu chako.

Hili ndilo muhimu na nitakuwa khasa mtu ninaestahili kufanya "review" kwa kuwa
hili somo la mapinduzi na uhuru wa Tanganyika nalijua vyema.

Hivi ndiyo baadhi ya vitu mwandishi anatakiwa awe anavijua kuepuka makosa ambayo
si ya lazima.

Umenishambulia kwa kuniita mvivu na mtu mwenye wivu.
Sidhani kama hizo sifa zinanienea mimi.

Ama hili la ''porojo,'' waliokuwa katika haya mambo ya utafiti na uandishi na baadhi ya
vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu ambao tumefanyakazi pamoja aidha kwa kuhariri
au kuandika au nilkopita na kufanya mihadhara kwenye vyuo vyao nadhani wananijua
kuwa mimi si mvivu wala si mpiga porojo.

Lakini akutukanae hakuchagulii tusi.

Inawezekana nina kasoro kama ilivyo kawaida ya binadamu yoyote, kakini hii sifa ya uvivu
si sifa yangu.

Napenda kuhitimisha kuwa kusema kuwa umeifanyia nchi yetu hisani kubwa kwa kuandika
historia ya TANU na mchango wa Jesuits katika historia hiyo.

Sasa tuna historia tatu za TANU.

Historia ya Chuo Cha Kivukoni, historia hiyo yako ya Jesuits na historia mnayoijua ya TANU
na uhuru wa Tanganyika niliyoandika
kama nilivyopokea kutoka kwa wazee wangu.
 
Hatuna haja ya kuzunguzuka zunguka na kukwepa hoja.
Mara uchaguzi wa 1995 ulifanyika miaka mingi baada ya Mapinduzi 1964! wazungu wanasema 'anachronism'

Swali lisilo na majibu kwa miaka linaendelea kwasababu hatujadili mambo kwa ukweli wa nafsi zetu

Nafasi ya weledi imechukuliwa na chuki, nafsi zetu zinaongozwa na Unafiki , tukijifaragua wakweli kwa uzandiki

Wanajamvi, Mohamed Said anasema mapinduzi yalichochewa na watu kutoka nje ya Zanzibar kwa mujibu wake
Kwa mantiki hiyo mapinduzi ni haramu. Hili halina mjadala tena

Wazanzibar, Mohamed Said anawaambia kusherehekea Januari 12 ni kutukuza haramu.
Kwa maneno mengine, ninyi mnaosema mapinduzi matukufu hamuelewi kuwa mapinduzi ni haramu

Kwa mantiki hiyo MAPINDUZI YA ZANZIBAR kwa mujibu wa Mohamed ni Haramu inayosherehekewa na WAZANZIBAR bila kujua wanasherehekea HARAM... Wazanzibar acheni kutukuza haramu kwa mujibu wa Mohamed Said

Wazanzibari hawasherekei mapinduzi. CCM ndio wanaosherekea mapinduzi. Na hebu jaribu kwenda zanzibar na ndo utajua ni asilimia ngapi ya watu wake amabao ni waumini wa kusherekea hayo mapinduzi.
 
Wazanzibari hawasherekei mapinduzi. CCM ndio wanaosherekea mapinduzi. Na hebu jaribu kwenda zanzibar na ndo utajua ni asilimia ngapi ya watu wake amabao ni waumini wa kusherekea hayo mapinduzi.
Hao CCM siyo wazanzibar?
 
Pamoja na ukweli wa hoja zako lkn unaonekana ww ni mbinafsi,mchoyo na mwenye wivu wa dhahiri...na unanisononesha zaidi kwa kua umri umeshakwenda,laiti ungelikua kijana ningesema maneno mabaya zaidi.

Mara nyingi unapoteza nguvu nyingi kubishana na kazi za Yericko kwa nukta nukta za ukweli unaoujua.
Ombi langu kwako kusanya kila unachokijua halafu tuandikie kitabu ukisambaze na tukisome kama alivyofanya Yericko kuliko hili povu lako la kila mara.

Mm binafsi nimesoma historia ya mapinduzi ya Zanzibar ktk vitabu vitatu tofauti na vyote vina vitu vinakinzana na kingine..Lkn pia nimesoma historia ya Zanzibar kupitia makala za Joseph Mihangwa ktk gazeti la RAI .Na kwa kutumia akili yangu nimekubaliana na aliyoandika Mihangwa kwa 65% zaidi ya kwenye vitabu nilivyosoma.

Sasa baba ANDIKA ..ANDIKA baba tusome.

HUU UNAFIKI WA KUJUA VITU HALAFU UNAA NAVYO MPAKA UFE NAVYO UTATUSAIDIA NINI SISI WA KIZAZI HIKI.
BILA YERICKO KUANDIKA UNGELIBISHANIA WAPI.
Nahisi yeye ndiye mvamizi, kama sivyo aandike.
Sio togwa hiyo
 
Hizo picha unazocopy kwa msisitizo wa hoja zako zitapendezesha kitabu chako kuliko hivi unavyofanya...Na kubwa zaidi Yericko hajaandika ya Zanzibar peke yake.Ameandika na mengine mengi kuhusu Tanganyika na maeneo mengine na huo ndio muundo wa kitabu chake.

WATU WEUSI TUNA TABU SANA AISEE!!
Watu weusi bana, ndio maana Trump ali...eti nini?
Andika kitabu chali tuone kama wewe ndiye
 
inanikumbusha ya Pascal Mayalla kusema kuwa KUKU si kitabu si lolote si chochote

mind you, KUKU kilisimamiwa na ma professa wa Harvard,

Kabla sijaendelea naomba CV na elimu ya Yeriko
 
TUJIKUMBUSHE NYEPESI NYEPESI KATIKA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUTOKA KALAMU YA DR. HARITH GHASSANY
Mohamed Said January 07, 2016 0

Utangulizi
Dr. Harith Ghassany ana ''sense of homour,'' kama wasemavyo Waingereza mbali ya kuwa msomi makini. Hata pale unapozungumzanae jambo zito kama la Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964 na roho zilizoteketea atakutafutia jambo akuchekeshe. Ngoja nikupe mfano mmoja.

Tuko Kipumbwi Tanga katika fukwe ya Bahari ya Hindi tumetoka kuangalia zile sehemu ambazo mamluki wa Kimakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura walipokuwa wakivushwa kwa majahazi kwenda Unguja tayari kushiriki katika kuiangusha serikali ya Waziri Mkuu Mohamed Shamte.

Siku ile daktari alikuwa na furaha kubwa sana kwa kuwa kitendawili kikubwa katika historia ya mapinduzi kilikuwa kimeteguliwa. Hakuna mtafiti yeyote katika historia ya mapinduzi aliyewahi kufika pale. Tulikuwa tushamaliza kupiga picha na zingine za video. Ile video camera kanikabidhi mimi tulipokuwa pangoni huko ambako mamluki walikuwa wakijificha na kupanda majahazi kiza kiingia wakivushwa na Mohamed Omari Mkwawa au kwa jina lingine ''Tindo,'' (jina alilopewa na Mzee Karume), kwenda Unguja wamejivika mavazi kama wavuvi wa Kidigo. Basi mimi napiga picha huku nafanya, ''narration.'' Yeye ananitia moto kwa kunisifia ati nahadithia vizuri. Nami bichwa linavimba kwa kusifiwa na msomi wa Harvard.

Sasa tuko juu pwani na upepo wa bahari unatupiga. Dakari ananiuliza, ''Guy sasa katika kazi hii nikuandike wewe nini kazi yako katika utafiti huu?'' Mimi najua daktari ananitania kwa kuwa kazi yangu yeye anaijua sana. Mimi shughuli yangu kuu ilikuwa ni dereva, nikimuendesha. Nami kwa maskhara na bila kufikiri nikamjibu, ''Mimi kazi yangu Guy ni ''Research Assistant.'' Kwa anaejua kazi hii katika utafiti atajua uzito wake.

Nimesahau ya Kipumbwi na yeye kesharudi Marekani nami nimebaki Tanga. Baada ya miaka kama miwili hivi 2010 kitabu kimechapwa. Ndani ya kitabu nakuta picha yangu na cheo changu, ''Mtafiti Msaidizi.'' Kila nikileta hii ''subject,'' kwake yeye anashikilia kuwa hiyo ndiyo ilikuwa kazi yangu na wala sikupatapo kuwa dereva wake. Mimi na yeye humaliza ubishi huu kwa vicheko na kwa kweli ''the joke is on me.''

Y1wMx38Wivnu76gF66VG3KCGrWPn6KfZJylXisH_8QCSMFyWWHuoX268T1EQYsX6cvrxmHrEOxGxYSR2h9Nd7ZrgFuleffRonAdXCnav3U3X-NUaUp6Zk63JHlT-IO4Z7rZPjztVzHoaiJVCyXdjJe3uERgE-HECRcq2HVK4lIZ2Qskc-hTKR1W1ghvuK0e_I53EFyRzjEpSoiRnOKOzbCczTNkMYBDQ_nWr16t5q6KcPupMBlF01LBwz9oz_m_kprhQQXE08EksQKOlJyw3lcgKPttbfRAz9BOUfG1ZWE6fGdWy8_V3oliP6WEdJAwYqMKsKe3DjudlbEydcDjyir4jv9NYplt8lU-1P3mp6zl2XxiOiFpNphrNM61KIoo5hBh_ifXOcMk6p91-PaccEGRz6I_irBdSvikInQ86iDG_UyZTwT8gBWzs_qhRB8WxuLf2k2yBEadIQlic0ISKq_B-1eZIK8mEVO_z6ULUkcY9gZIRjXW29GsZ3NPmiTJfYcuE_8DVICz8jfA9VMMa67OIl1A_UUU5gOyDTC2gkmu1HPqjpQzvib6bMOHi0wADKV6Qxv5phqZAKKwAn1p9HWlJno3sKGD_oHZoOVRD=w335-h252-no

Nyuma yangu ni kijiji cha Kipumbwi, Tanga
 
Watu weusi bana, ndio maana Trump ali...eti nini?
Andika kitabu chali tuone kama wewe ndiye
Kulindwa,
Umechangia mara tatu katika mjadala huu lakini maneno yako ni machache.
Nimelileta hili la ''plagiarism,'' si kwa nia ya kutaka kudai kitu mahakamani.

plagiarism
ˈpleɪdʒərɪz(ə)m/
noun
  1. the practice of taking someone else's work or ideas and passing them off as one's own.
    "there were accusations of plagiarism"
    synonyms: copying, infringement of copyright, piracy, theft, stealing, poaching, appropriation;
    informalcribbing
    "there were accusations of plagiarism"
Nimetaka tu kutahadharisha.
Ningependa ufahamu tu uzito wa jambo hili.

Yale maneno ni ya Prof. Mohamed Bakari ambayo mimi nimeyaandika
hapa JF mara nyingi na nimekuwa nikieleza wapi nimeyatoa.

Nadhani umeona kuwa Yericko mwenyewe katambua na hajasema lolote
kuhusu maneno yale aliyoandika kama vile ni yake.

Wewe unaweza kuona ni kitu kidogo lakini katika dunia ya usomi huo ni wizi
na ni kosa kubwa sana.

Ndipo mwanzo kabisa nkasema kitabu lazima kiwe na ''publisher,'' kwani hii ni
moja ya kazi zake.
 
Mzee wangu inaonesha unapenda sana wazungusha vijana vijiwe vya kahawa na kuwapa utam wa historia nusunusu.(utani )..nadhan ungekua kwe sehemu mzuri zaidi kama ungetupa link tusome hiyo historia unayoijua kwani kwa jinsi unavyojitanabaisha ni kama weye ulishushiwa hiyo historia toka mbinguni...kama ulipata bahati ya kusimuliwa kujisifu tu bila kuiweka kama ilivyo unatuchanganya sis vijana ambao hatukupata bahati ya kuiona no bora basi hata huyo yericko nyerere alijaribu kutuonjesha hata kama haikuiva kisawasawa kama unavyojaribu kutuaminisha...nawasilisha
Ndugu zangu,
Hebu someni hayo hapo chini kuna mengi mtatambua:

KUTOKA JF: HISTORIA YA TANU KAMA ILIVYOANDIKWA NA YERICKO NYERERE
Mohamed Said January 18, 2017 0

.............Jukumu la kuandaa nchi hizo kupata uhuru liliratibiwa na shirika hilo la kijasusi kwa ustadi mkubwa bila baadhi ya makoloni kujua, lakini lilikumbana na kikinza hasa kufuatia mnyumbuliko wa kiimani ndani ya ukristu kufuatia nguvu ya Cambrige (Anglikana), mgogoro huo ulikuzwa kwakuwa Anglikana nao tayari walikuwa wameaandaa taasisi yao waliyoiita Fabian Sociaty maalumu kwaajili ya kuwaandaa vijana wa kiafrika kukabidhiwa nchi zao, Barani Afrika Jeisuiti ilibadili mbinu kwakuwa dola la Kiingereza lilikuwa kikwazo kwa sehemu fulani, haikujikita kwenye dola isipokuwa ilisimama katika muundo wa shirika lifanya shughuli zake ndani ya Kanisa. Dhamiri ilikuwa lazima itimie, kama ilivyosemwna huko mwanzo kuwa hawa ndio wabobevu wa elimu ya juu kwa kila nyanja na ndio wanaotawala ulimwengu, hivyo vikwazo havikukwamisha wao kufikia malengo.

Katika Tanganyika chini ya Udhamini wa Jumuiko la Kimataifa, kulikuwa na harakati za hapa na pale za kudai haki za kiraia kwa wenyeji. Ifahamike kuwa vyama vya harakati hizo Tanganyika vilikuwa vingi sana, na vipo vilivyokuwa vikipingana vyenyewe kwa vyenyewe.

Mwaka 1927 hadi 1929 kanisa Katoliki nchini chini Joseph Gabriel Zelger, lilibainika kuingiza siasa katika utendaji kazi zake, kitendo hiki kiliwakwaza wakuu wa mamlaka ya kikoloni na kupelekea majasusi wakikoloni wapendekeze aachishwe uongozi wa kanisa nchini. Ni kweli tarehe 12 februari 1929 Zelger alistaafu wadhifawake kwa lazima. Ni mwaka huohuo wa 1927 ndio Chama cha African Assosiotion (AA) kilianzishwa na Gavana Sir David Cameron maaluma kwaajili ya kuratibu sherehe za watu weusi huko pembeni ya mji huko mtaa wa Stanley (leo Lumumba) na kuwapa ofisi mahali leo wanapojiita TANU ilizaliwa. Lakini historia ya Tanganyika haiwataji waasisi wa AA, Rais wa kwanza Mwalimu Cesil Matola (msomi wa mwanzo kabisa enzi za mjerumani kutoka kabila la Wayao), katibu mkuu wa kwanza Klest Sykes (Mzulu Baba yake alikuwa mateka wa kikoloni toka Afrika Kusini), Mwekahazina Ali Ramadhan (mzaramo na mvuvi maarufu wa pwani la Azania).

Hao ndio mwaka 1927 waliounda Chama cha kwanza kabisa cha kutetea maslahi ya weusi Tanganyika na shughuli zake zilikuwa ni kuratibu sherehe za waafrika tu. (Chama cha walevi kwa lugha nyingine). Mwaka 1933 Mwalimu Cesil Matola alifariki na nafasi yake ikakaimiwa na katibu mkuu wa chama hicho bwana Klest, mpaka ilipofika mwaka 1948 yakatokea mapinduzi yaliyoongozwa na mtoto wa Klest aliyeitwa Abdulwahid Sykes huyu alikuwa ametoka kupigana vita vya pili vya dunia huko Burma, na aliporudi alikuwa na mawazo ya ujana toka vitani, akampindua baba yake kwa kumpiga ngumi puani, mapinduzi yaliyoitwa “ondoa wazee”. Kisha AA ikabadilishwa jina na kuitwa TAA, Rais wake wa Kwanza akawa Dr Vedasto Kyaruzi (Mhaya), huyu ndie dakitari wa binadamu wa kwanza kabisa wa kiafrika Tanganyika, Katibu mkuu akawa Abdulwahid Sykes na Mweka hazina akawa Dosa Azizi, utawala huo ulienda mpaka mwaka 1953 uchaguzi ulipofanyika na Nyerere akashinda pale kwenye ukumbi wa Anautoglo Mnazimoja leo, mwaka 1954 Nyerere akabadili jina la chama na kuwa TANU jina ambalo lilibuniwa na Abdulwahid Sykes, TANU ilikwenda mpaka mwaka 1977 na kisha kikazaliwa chama kiitwacho CCM baada ya Muungano wa ASP na TANU.

Kisa hiki cha kufukuzwa kwa Kasisi huyu Bw. Zelger kinasema, Kanisa lilianzisha mafundisho yenye kuchochea fikra za kimaasi, nalilifanikiwa kuandaa wakufunzi maalumu kwenda katika majimbo yote ya kihuduma Tanganyika, hilo lilipelekea kuleta mtafaruku na dola ya mkoloni wa kiingereza ambapo ilimgharimu kiongozi huyu wa kiroho kuachia madaraka yake. Alipoingia askofu Edger Aristide Maranta mwaka 1930, ikiwa kama vile mwendelezo wa mtangulizi wake, Askofu Maranda alianzisha harakati za kuwashawishi viongozi wengine wa majimbo kuendeleza kutoa mafundisho yenye kumfanya mtanganyika ajitambue na adai uhuru wake, mfano, 23 mei 1938 wakati makanisa saba ya Kilutheri yakiwa kwenye hatua za mwanzo za mchakato wa kuungana, Askofu maranda aliomba kuhudhuria kikao cha tarehe 8 mwezi wa sita kilichofanyika Mjini Arusha, Askofu Maranda aliudokeza mpango ule wa siri wa katoliki katika kikao hicho, japokuwa kulikuwa na hofu ya kutoaminiana, lakini uthabiti wa malengo hayo ulijipembua baadae na kuwa wamafaa, ushahidi wa nyaraka za kumbukumbu za mkutano huo unaeleza.

Juhudi za kanisa kupigania mkataba wa Versailles ziliendelea kushika kasi huku zikiendeshwa kwa siri sana kwamfumo wa neno la kiroho, na ilipofikia miaka ya 1950+ kanisa sasa lilikuwa tayari linanguvu ya ushawishi kufuatia mafanikio ya harakati za kanisa katika nyanja za ukombozi barani afrika. Wakati hayo yakiendelea tayari kanisa kupitia shirika lake la kijasusi lilikuwa limewekeza kwa nguvu kubwa kumtafuta mtu imara mwenye weledi na vipawa atakayejengwa ili aje kuongoza nchi. Mtihani mkubwa kwa kanisa ilikuwa ni namna gani linaweza kuingia rasmi kudai uhuru wa Tanganyika. Katika kipindi hiki tangu harakati za kanisa zianze, Askofu Maranta pamoja na mapadre wa baadhi ya mikoa, walikuwa tayari ameshafanya juhudi kadhaa za kukutana na Mashehe waliokuwa na ushawishi mkubwa, mfano 05/02/1948, Askofu Maranda alikutana Shehe Issa bin Amir kiongozi wa kiroho katika msikiti wa Ilala - mchikichini.

Shehe Issa Bin Amir alizaliwa 1846 katika viunga vya Mzizima, mchikichini na kuhudumu katika wadhifa wa shekhe katika msikiti uliokuwa hapohapo viwanja vya nyumbani kwake na alifariki mwaka 1953 akiwa na umri 107, Shehe Issa Bin Amir kwa kabila alikuwa Mzaramo na akiishi hadi kifo chake Mchikichini pale nyuma ya kilipo kiwanda cha bia leo (TBL). Shehe Issa Bin Amir rafiki kipenzi wa Padre Maranta na mzee wa hekima za kilele cha zama hizo, mtu aliyekuwa kiungo muhimu kati ya uislamu na ukristu, Mtu ambae Mwalimu Cesil Matola rais wa kwanza wa AA na Klest Sykes katibu mkuu wakwanza wa AA, na wanachama wengine waliokuwa AA walimheshimu sana kwa hekima zake na mmoja wa wasisi wa Jumuiko la Uislamu Afrika Mashariki (EAMWS) Mazungumzo yao yalihusu harakati za ukombozi, Shehe Issa alimshauri Askofu kuwa ikiwa makanisa na misikiti yanapigwa marufuku na mkoloni kujihusisha na siasa za ukombozi basi watafute baadhi ya vyama vya harakati za ukombozi na waviunge mkono, wazo hilo lilimvutia Askofu lakini akajenga hofu kama je ndani ya vyama hivyo watapata vijana wasomi?.

Siku chache baada ya makutano yake na Shehe Issa, Askofu Maranta aliletewa mapendekezo kutoka kwa Attilio Beltramino kasisi wa katoliki aliyehudumu kule Iringa, mapendekezo ya kasisi huyu yalikuwa ni, Umishonari makao makuu uruhusu udurufu wa biblia zisomeke kwa makabila ya wahusika wa eneo, ndani ya biblia hizo yaongezwe mafundisho ya haki ya kujitambua na kujitawala wenyewe. Pendekezo hili lilimvutia sana Maranta hivyo akalipa baraka zake, kwa hakika lilifanikiwa na ndio lilizaa hisia kali za mwamko wa kudai uhuru, mfano biblia ya lugha ya kihehe ilikuwa inaeleza wazi athari za kutawaliwa.

Harakati za Ukombozi za Mwalimu Nyerere akiwa na nguvu mpya ya kifikra toka Chuo kikuu, zililivutia kanisa na uungaji mkono ukachagizwa, mfano mwaka 1953 wakati TAA kikiwa chama chenye nguvu kufuatia mabadiliko ya 1948 toka AA kwenda TAA. Askofu Maranta alimwalika ofisini kwake Mwalimu Nyerere, walizungumza mengi lakini kubwa nikuwa alimsifu kwa juhudi za kujipambanua bila kuwaogopa wakoloni, akamweleza jinsi kanisa linavyounga mkono juhudi za ukombozi wa Tanganyika, kisha akamshauri kuwa ajaribu kuvishawishi baadhi ya vyama vya harakati za kiraia viungane ili kuvipa nguvu ya kudai uhuru na kanisa litasaidia.

Wazo la Askofu Maranta lilimkaa Mwalimu Nyerere na mwaka 1954, alianza juhudi za kuwaunganisha vijana wenzake wa kariakoo ambao walikuwa ndani ya TAA na wenye nguvu ya ushawishi lakini wakikabiliwa na matatizo makubwa mawili katika lengo lao ambayo ni Elimu na Woga. Ikumbukwe kuwa mwaka 1953 baada ya harakati za ukombozi kupamba moto na kamata kamata ya wanaukombozi, Askofu Edger Aristide Maranta alihamishiwa Zanzibar na nafasi yake ikachukuliwa na Vicar Apostolic, lakini bado aliendelea kuwa mshauri imara wa Mwalimu Nyerere. Jambo la kushangaza kama si kufurahisha, mwaka huohuo mwezi wa 8, Edger Aristide Maranta alirudishwa tena Dar es Saalam, na sasa mbinyo dhidi ya ukoloni ukashika mkondo wake.

Mnamo tarehe 07/07/1954, Vijana (wazee wa kariakoo) wakiongozwa na Julius Kambarage Nyerere, walikubaliana wazo la kuhuisha chama kutoka TAA kwenda TANU, chini ya uratibu wa karibu wa Wajeisut (Askofu Maranta) na Waislamu (Shehe Issa bin Amir) ijapokuwa alikuwa amefariki mwaka mmoja nyuma, lakini hekima za Shehe huyu zilisaidia. Na zaidi ni kuwa safari ya kwanza ya Mwalimu Nyerere ya kwenda UNO 05/03/1955 Kanisa Katoliki lilitoa msaada kwa chama cha TANU wa tiketi ya ndege ya kwenda na kurudi, lilifanya hivyo kupitia shirika lake la Maryknoll Sisters la New York Marekani,

Si hivyo tu bali katika moja ya utani wa Mwalimu wenye ukweli ndani yake aliwahi kusema kuwa makasisi Walsh na Art Wille wa Shirika la Maryknoll ni maboss wake, akikumbuka malipo ya shilingi 600 angali ameacha kazi ya ualimu akiwa kijijini Butiama.Kuna ushahidi wa kihistoria pia unaochagiza habari hizi kwamba majasusi wa Kanisa walimuandaa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuja kuwa kiongoza Tanganyika mpya................

Kutoka kwenye kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.

Unaweza kupakua hapa www.simgazeti.com

Saa hebu someni niliyoandika kuhusu kitabu cha Yericko:

Wanamajlis,
Bandiko hili limeshawahi kuletwa hapa na nilieleza kuwa kuna makosa mengi.
Inaelekea mwandishi hakubali kuwa kuna makosa.

Kazi ya kisomi inahitaji rejea ili kuthibitisha kinachoelezwa.

Walimu wetu siku zile Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wakituasa kutoandika
''barua,'' yaani kuandika mada ya kisomi bila rejea.

Hicho hapo juu ni ''barua,'' siyo mada ya kisomi.
African Association haikuasisiwa 1927 bali 1929.

Anaweza kufanya rejea katika, ''Modern Tanzanians,'' John Iliffe (Ed) makala
ya Daisy Sykes Buruku, ''Kleist Sykes The Townsman,'' akipenda hata amsome
Mohamed Said, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968)...''Kleist
Sykes:
Pioneer and Man of Ideas 1894 - 1949.''

Akipenda zaidi anaweza kuingia katika Dictionary of Africa Biography, Oxford
University Press 2011, aangalie Kleist Sykes.

Anasema African Association iliassisiwa Stanley Street si kweli kwani wakati huo
1920s hiyo nyumba ya harakati za siasa ya Kleist hapo mtaani ilikuwa bado kabisa
haijajengwa.

Nyumba hiyo ilijengwa 1942.

AA iliasisiwa Mission Quarter nyumbani kwa Cecil Matola Mtaa wa Masasi, nyumba
hii baadae ilinunuliwa na John Rupia.

Kuna mengi ya kutunga mfano wa Nyerere kukusanya ''vijana wenzake wa Kariakoo,''
nk. nk. hakuna ukweli wowote Nyerere hakupatapo kuishi Kariakoo ila kwa muda
mfupi sana 1955 alipokaa nyumbani kwa Abdul Sykes Stanley Street baada ya kuacha
kazi ya ualimu.

Atakae kujua TANU iliasisiwa vipi sharti kwanza aijue Kamati ya Siasa katika TAA.

Waliokuwa katika kamati ya ndani ya kuasisi TANU ni wajumbe wa TAA Political Subcommittee
wajumbe walikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Said Chaurembo, Abdulwahid
Sykes, Dr. Vedasto Kyaruzi, Steven Mhando, Hamza Mwapachu
na John Rupia.

Safari ya Mwalimu Nyerere ya kwanza 1955 ilighariimiwa na TANU yenyewe na mratibu
wa safari ile aliyekuwa akikusanya fedha alikuwa Idd Faiz Mafongo aliyekuwa mweka
hazina wa TANU na Al Jamiatuli Islamiyya fi Tanganyika.

Hebu kwanza tusimame hapa.

Lakini kwa kulisaidia jamvi lau kwa ukumbusho kwa kuwa mada hii ilishajadiliwa miaka mingi
iliyopita nawaomba waingie hapo chini wasome niliyopata kuandika kuhusu historia ya
Tanganyika:
Mohamed Said: LIWALI AHMED SALEH NA SHEIKH SAID CHAUREMBO
Mohamed Said: KUTOKA JF: MAMA DAISY NA HISTORIA YA CHIEF DAVID KIDAHA MAKWAIA
Mohamed Said: KUMBUKUMBU ZA IDDI TOSIRI MWANACHAMA WA TANU KADI NO. 24
Mohamed Said: LAMECK BUGOHE MUASISI WA TANU 1954 KAFARIKI NA KUZIKWA KIMYA KIMYA
Mohamed Said: ZUBERI MWINSHEHE MANGA MTEMVU MZALENDO ALIYEKUWA NA MSIMAMO MKALI WA “AFRIKA KWA WAAFRIKA”
Mohamed Said: Abbas Kleist Sykes 1929 -
Mohamed Said: Idd Faiz Mafongo Mweka Hazina wa Safari ya Nyerere UNO 1955
Mohamed Said: MCHANGO WA MUFTI SHEIKH HASSAN BIN AMEIR KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA MAHOJIANO KATI YA SHEIKH RASHID SALIM NA MOHAMED SAID RADIO NUR ZANZIBAR
Mohamed Said: KUTOKA FB: VITUKO VYA YERICKO ''NYERERE''
Mohamed Said: KUTOKA JF: HISTORIA YA TANU - DK. VEDASTO KYARUZI, KASELLA BANTU NA JULIUS NYERERE
Mohamed Said: Ijue Historia ya Kweli ya Kuasisiwa kwa TANU
Mohamed Said: KUMBUKUMBU YA MASHUJAA WA UHURU WA TANGANYIKA RASHID ALI MELI
Mohamed Said: AZAM TV KIPINDI MAALUM CHA MASHUJAA WA UHURU WA TANGANYIKA
Mohamed Said: KUTOKA JF: SHEIKH HASSAN BIN AMIR ALIVYOIONGOZA TANU KUWA CHAMA CHA KISEKULA
Mohamed Said: KLEIST SYKES (1894 - 1949) KATIKA DICTIONARY OF AFRICAN BIOGRAPHY (DAB) OXFORD UNIVERSITY PRESS, NEW YORK

Wanamajlis,
Hizo hapo juu ni zaidi ya kurasa 100 za kusoma pamoja na audio za kusikiliza
na video za kuangalia.

Si lazima upitie zote chagua moja mbili tatu utakuwa ushajifunza kitu.

Waswahili tuna msemo na Mzee Ali Hassan Mwinyi akipenda kuutumia,
''Muongo muongoze.''

Chembelecho Maalim Faiza: Elimu bila Khiyana.

Huyu Jonathon Glassman ni professor wa historia Northwestern University
Evanston, Chicago alinialika nikazungumze chuoni kwake juu ya historia ya
TANU na uhuru wa Tanganyika.

Nilizungumza katika Ukumbi wa Eduardo Mondlane.

Glassman alifanya pitioa la kitabu changu katika Cambridge Journal of African
History Vol. 42 Issue 1 March 2001 halikadhalika John Iliffe.

historia
 
Ndugu zangu,
Hebu someni hayo hapo chini kuna mengi mtatambua:

KUTOKA JF: HISTORIA YA TANU KAMA ILIVYOANDIKWA NA YERICKO NYERERE
Mohamed Said January 18, 2017 0

.............Jukumu la kuandaa nchi hizo kupata uhuru liliratibiwa na shirika hilo la kijasusi kwa ustadi mkubwa bila baadhi ya makoloni kujua, lakini lilikumbana na kikinza hasa kufuatia mnyumbuliko wa kiimani ndani ya ukristu kufuatia nguvu ya Cambrige (Anglikana), mgogoro huo ulikuzwa kwakuwa Anglikana nao tayari walikuwa wameaandaa taasisi yao waliyoiita Fabian Sociaty maalumu kwaajili ya kuwaandaa vijana wa kiafrika kukabidhiwa nchi zao, Barani Afrika Jeisuiti ilibadili mbinu kwakuwa dola la Kiingereza lilikuwa kikwazo kwa sehemu fulani, haikujikita kwenye dola isipokuwa ilisimama katika muundo wa shirika lifanya shughuli zake ndani ya Kanisa. Dhamiri ilikuwa lazima itimie, kama ilivyosemwna huko mwanzo kuwa hawa ndio wabobevu wa elimu ya juu kwa kila nyanja na ndio wanaotawala ulimwengu, hivyo vikwazo havikukwamisha wao kufikia malengo.

Katika Tanganyika chini ya Udhamini wa Jumuiko la Kimataifa, kulikuwa na harakati za hapa na pale za kudai haki za kiraia kwa wenyeji. Ifahamike kuwa vyama vya harakati hizo Tanganyika vilikuwa vingi sana, na vipo vilivyokuwa vikipingana vyenyewe kwa vyenyewe.

Mwaka 1927 hadi 1929 kanisa Katoliki nchini chini Joseph Gabriel Zelger, lilibainika kuingiza siasa katika utendaji kazi zake, kitendo hiki kiliwakwaza wakuu wa mamlaka ya kikoloni na kupelekea majasusi wakikoloni wapendekeze aachishwe uongozi wa kanisa nchini. Ni kweli tarehe 12 februari 1929 Zelger alistaafu wadhifawake kwa lazima. Ni mwaka huohuo wa 1927 ndio Chama cha African Assosiotion (AA) kilianzishwa na Gavana Sir David Cameron maaluma kwaajili ya kuratibu sherehe za watu weusi huko pembeni ya mji huko mtaa wa Stanley (leo Lumumba) na kuwapa ofisi mahali leo wanapojiita TANU ilizaliwa. Lakini historia ya Tanganyika haiwataji waasisi wa AA, Rais wa kwanza Mwalimu Cesil Matola (msomi wa mwanzo kabisa enzi za mjerumani kutoka kabila la Wayao), katibu mkuu wa kwanza Klest Sykes (Mzulu Baba yake alikuwa mateka wa kikoloni toka Afrika Kusini), Mwekahazina Ali Ramadhan (mzaramo na mvuvi maarufu wa pwani la Azania).

Hao ndio mwaka 1927 waliounda Chama cha kwanza kabisa cha kutetea maslahi ya weusi Tanganyika na shughuli zake zilikuwa ni kuratibu sherehe za waafrika tu. (Chama cha walevi kwa lugha nyingine). Mwaka 1933 Mwalimu Cesil Matola alifariki na nafasi yake ikakaimiwa na katibu mkuu wa chama hicho bwana Klest, mpaka ilipofika mwaka 1948 yakatokea mapinduzi yaliyoongozwa na mtoto wa Klest aliyeitwa Abdulwahid Sykes huyu alikuwa ametoka kupigana vita vya pili vya dunia huko Burma, na aliporudi alikuwa na mawazo ya ujana toka vitani, akampindua baba yake kwa kumpiga ngumi puani, mapinduzi yaliyoitwa “ondoa wazee”. Kisha AA ikabadilishwa jina na kuitwa TAA, Rais wake wa Kwanza akawa Dr Vedasto Kyaruzi (Mhaya), huyu ndie dakitari wa binadamu wa kwanza kabisa wa kiafrika Tanganyika, Katibu mkuu akawa Abdulwahid Sykes na Mweka hazina akawa Dosa Azizi, utawala huo ulienda mpaka mwaka 1953 uchaguzi ulipofanyika na Nyerere akashinda pale kwenye ukumbi wa Anautoglo Mnazimoja leo, mwaka 1954 Nyerere akabadili jina la chama na kuwa TANU jina ambalo lilibuniwa na Abdulwahid Sykes, TANU ilikwenda mpaka mwaka 1977 na kisha kikazaliwa chama kiitwacho CCM baada ya Muungano wa ASP na TANU.

Kisa hiki cha kufukuzwa kwa Kasisi huyu Bw. Zelger kinasema, Kanisa lilianzisha mafundisho yenye kuchochea fikra za kimaasi, nalilifanikiwa kuandaa wakufunzi maalumu kwenda katika majimbo yote ya kihuduma Tanganyika, hilo lilipelekea kuleta mtafaruku na dola ya mkoloni wa kiingereza ambapo ilimgharimu kiongozi huyu wa kiroho kuachia madaraka yake. Alipoingia askofu Edger Aristide Maranta mwaka 1930, ikiwa kama vile mwendelezo wa mtangulizi wake, Askofu Maranda alianzisha harakati za kuwashawishi viongozi wengine wa majimbo kuendeleza kutoa mafundisho yenye kumfanya mtanganyika ajitambue na adai uhuru wake, mfano, 23 mei 1938 wakati makanisa saba ya Kilutheri yakiwa kwenye hatua za mwanzo za mchakato wa kuungana, Askofu maranda aliomba kuhudhuria kikao cha tarehe 8 mwezi wa sita kilichofanyika Mjini Arusha, Askofu Maranda aliudokeza mpango ule wa siri wa katoliki katika kikao hicho, japokuwa kulikuwa na hofu ya kutoaminiana, lakini uthabiti wa malengo hayo ulijipembua baadae na kuwa wamafaa, ushahidi wa nyaraka za kumbukumbu za mkutano huo unaeleza.

Juhudi za kanisa kupigania mkataba wa Versailles ziliendelea kushika kasi huku zikiendeshwa kwa siri sana kwamfumo wa neno la kiroho, na ilipofikia miaka ya 1950+ kanisa sasa lilikuwa tayari linanguvu ya ushawishi kufuatia mafanikio ya harakati za kanisa katika nyanja za ukombozi barani afrika. Wakati hayo yakiendelea tayari kanisa kupitia shirika lake la kijasusi lilikuwa limewekeza kwa nguvu kubwa kumtafuta mtu imara mwenye weledi na vipawa atakayejengwa ili aje kuongoza nchi. Mtihani mkubwa kwa kanisa ilikuwa ni namna gani linaweza kuingia rasmi kudai uhuru wa Tanganyika. Katika kipindi hiki tangu harakati za kanisa zianze, Askofu Maranta pamoja na mapadre wa baadhi ya mikoa, walikuwa tayari ameshafanya juhudi kadhaa za kukutana na Mashehe waliokuwa na ushawishi mkubwa, mfano 05/02/1948, Askofu Maranda alikutana Shehe Issa bin Amir kiongozi wa kiroho katika msikiti wa Ilala - mchikichini.

Shehe Issa Bin Amir alizaliwa 1846 katika viunga vya Mzizima, mchikichini na kuhudumu katika wadhifa wa shekhe katika msikiti uliokuwa hapohapo viwanja vya nyumbani kwake na alifariki mwaka 1953 akiwa na umri 107, Shehe Issa Bin Amir kwa kabila alikuwa Mzaramo na akiishi hadi kifo chake Mchikichini pale nyuma ya kilipo kiwanda cha bia leo (TBL). Shehe Issa Bin Amir rafiki kipenzi wa Padre Maranta na mzee wa hekima za kilele cha zama hizo, mtu aliyekuwa kiungo muhimu kati ya uislamu na ukristu, Mtu ambae Mwalimu Cesil Matola rais wa kwanza wa AA na Klest Sykes katibu mkuu wakwanza wa AA, na wanachama wengine waliokuwa AA walimheshimu sana kwa hekima zake na mmoja wa wasisi wa Jumuiko la Uislamu Afrika Mashariki (EAMWS) Mazungumzo yao yalihusu harakati za ukombozi, Shehe Issa alimshauri Askofu kuwa ikiwa makanisa na misikiti yanapigwa marufuku na mkoloni kujihusisha na siasa za ukombozi basi watafute baadhi ya vyama vya harakati za ukombozi na waviunge mkono, wazo hilo lilimvutia Askofu lakini akajenga hofu kama je ndani ya vyama hivyo watapata vijana wasomi?.

Siku chache baada ya makutano yake na Shehe Issa, Askofu Maranta aliletewa mapendekezo kutoka kwa Attilio Beltramino kasisi wa katoliki aliyehudumu kule Iringa, mapendekezo ya kasisi huyu yalikuwa ni, Umishonari makao makuu uruhusu udurufu wa biblia zisomeke kwa makabila ya wahusika wa eneo, ndani ya biblia hizo yaongezwe mafundisho ya haki ya kujitambua na kujitawala wenyewe. Pendekezo hili lilimvutia sana Maranta hivyo akalipa baraka zake, kwa hakika lilifanikiwa na ndio lilizaa hisia kali za mwamko wa kudai uhuru, mfano biblia ya lugha ya kihehe ilikuwa inaeleza wazi athari za kutawaliwa.

Harakati za Ukombozi za Mwalimu Nyerere akiwa na nguvu mpya ya kifikra toka Chuo kikuu, zililivutia kanisa na uungaji mkono ukachagizwa, mfano mwaka 1953 wakati TAA kikiwa chama chenye nguvu kufuatia mabadiliko ya 1948 toka AA kwenda TAA. Askofu Maranta alimwalika ofisini kwake Mwalimu Nyerere, walizungumza mengi lakini kubwa nikuwa alimsifu kwa juhudi za kujipambanua bila kuwaogopa wakoloni, akamweleza jinsi kanisa linavyounga mkono juhudi za ukombozi wa Tanganyika, kisha akamshauri kuwa ajaribu kuvishawishi baadhi ya vyama vya harakati za kiraia viungane ili kuvipa nguvu ya kudai uhuru na kanisa litasaidia.

Wazo la Askofu Maranta lilimkaa Mwalimu Nyerere na mwaka 1954, alianza juhudi za kuwaunganisha vijana wenzake wa kariakoo ambao walikuwa ndani ya TAA na wenye nguvu ya ushawishi lakini wakikabiliwa na matatizo makubwa mawili katika lengo lao ambayo ni Elimu na Woga. Ikumbukwe kuwa mwaka 1953 baada ya harakati za ukombozi kupamba moto na kamata kamata ya wanaukombozi, Askofu Edger Aristide Maranta alihamishiwa Zanzibar na nafasi yake ikachukuliwa na Vicar Apostolic, lakini bado aliendelea kuwa mshauri imara wa Mwalimu Nyerere. Jambo la kushangaza kama si kufurahisha, mwaka huohuo mwezi wa 8, Edger Aristide Maranta alirudishwa tena Dar es Saalam, na sasa mbinyo dhidi ya ukoloni ukashika mkondo wake.

Mnamo tarehe 07/07/1954, Vijana (wazee wa kariakoo) wakiongozwa na Julius Kambarage Nyerere, walikubaliana wazo la kuhuisha chama kutoka TAA kwenda TANU, chini ya uratibu wa karibu wa Wajeisut (Askofu Maranta) na Waislamu (Shehe Issa bin Amir) ijapokuwa alikuwa amefariki mwaka mmoja nyuma, lakini hekima za Shehe huyu zilisaidia. Na zaidi ni kuwa safari ya kwanza ya Mwalimu Nyerere ya kwenda UNO 05/03/1955 Kanisa Katoliki lilitoa msaada kwa chama cha TANU wa tiketi ya ndege ya kwenda na kurudi, lilifanya hivyo kupitia shirika lake la Maryknoll Sisters la New York Marekani,

Si hivyo tu bali katika moja ya utani wa Mwalimu wenye ukweli ndani yake aliwahi kusema kuwa makasisi Walsh na Art Wille wa Shirika la Maryknoll ni maboss wake, akikumbuka malipo ya shilingi 600 angali ameacha kazi ya ualimu akiwa kijijini Butiama.Kuna ushahidi wa kihistoria pia unaochagiza habari hizi kwamba majasusi wa Kanisa walimuandaa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuja kuwa kiongoza Tanganyika mpya................

Kutoka kwenye kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.

Unaweza kupakua hapa www.simgazeti.com

Saa hebu someni niliyoandika kuhusu kitabu cha Yericko:

Wanamajlis,
Bandiko hili limeshawahi kuletwa hapa na nilieleza kuwa kuna makosa mengi.
Inaelekea mwandishi hakubali kuwa kuna makosa.

Kazi ya kisomi inahitaji rejea ili kuthibitisha kinachoelezwa.

Walimu wetu siku zile Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wakituasa kutoandika
''barua,'' yaani kuandika mada ya kisomi bila rejea.

Hicho hapo juu ni ''barua,'' siyo mada ya kisomi.
African Association haikuasisiwa 1927 bali 1929.

Anaweza kufanya rejea katika, ''Modern Tanzanians,'' John Iliffe (Ed) makala
ya Daisy Sykes Buruku, ''Kleist Sykes The Townsman,'' akipenda hata amsome
Mohamed Said, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968)...''Kleist
Sykes:
Pioneer and Man of Ideas 1894 - 1949.''

Akipenda zaidi anaweza kuingia katika Dictionary of Africa Biography, Oxford
University Press 2011, aangalie Kleist Sykes.

Anasema African Association iliassisiwa Stanley Street si kweli kwani wakati huo
1920s hiyo nyumba ya harakati za siasa ya Kleist hapo mtaani ilikuwa bado kabisa
haijajengwa.

Nyumba hiyo ilijengwa 1942.

AA iliasisiwa Mission Quarter nyumbani kwa Cecil Matola Mtaa wa Masasi, nyumba
hii baadae ilinunuliwa na John Rupia.

Kuna mengi ya kutunga mfano wa Nyerere kukusanya ''vijana wenzake wa Kariakoo,''
nk. nk. hakuna ukweli wowote Nyerere hakupatapo kuishi Kariakoo ila kwa muda
mfupi sana 1955 alipokaa nyumbani kwa Abdul Sykes Stanley Street baada ya kuacha
kazi ya ualimu.

Atakae kujua TANU iliasisiwa vipi sharti kwanza aijue Kamati ya Siasa katika TAA.

Waliokuwa katika kamati ya ndani ya kuasisi TANU ni wajumbe wa TAA Political Subcommittee
wajumbe walikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Said Chaurembo, Abdulwahid
Sykes, Dr. Vedasto Kyaruzi, Steven Mhando, Hamza Mwapachu
na John Rupia.

Safari ya Mwalimu Nyerere ya kwanza 1955 ilighariimiwa na TANU yenyewe na mratibu
wa safari ile aliyekuwa akikusanya fedha alikuwa Idd Faiz Mafongo aliyekuwa mweka
hazina wa TANU na Al Jamiatuli Islamiyya fi Tanganyika.

Hebu kwanza tusimame hapa.

Lakini kwa kulisaidia jamvi lau kwa ukumbusho kwa kuwa mada hii ilishajadiliwa miaka mingi
iliyopita nawaomba waingie hapo chini wasome niliyopata kuandika kuhusu historia ya
Tanganyika:
Mohamed Said: LIWALI AHMED SALEH NA SHEIKH SAID CHAUREMBO
Mohamed Said: KUTOKA JF: MAMA DAISY NA HISTORIA YA CHIEF DAVID KIDAHA MAKWAIA
Mohamed Said: KUMBUKUMBU ZA IDDI TOSIRI MWANACHAMA WA TANU KADI NO. 24
Mohamed Said: LAMECK BUGOHE MUASISI WA TANU 1954 KAFARIKI NA KUZIKWA KIMYA KIMYA
Mohamed Said: ZUBERI MWINSHEHE MANGA MTEMVU MZALENDO ALIYEKUWA NA MSIMAMO MKALI WA “AFRIKA KWA WAAFRIKA”
Mohamed Said: Abbas Kleist Sykes 1929 -
Mohamed Said: Idd Faiz Mafongo Mweka Hazina wa Safari ya Nyerere UNO 1955
Mohamed Said: MCHANGO WA MUFTI SHEIKH HASSAN BIN AMEIR KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA MAHOJIANO KATI YA SHEIKH RASHID SALIM NA MOHAMED SAID RADIO NUR ZANZIBAR
Mohamed Said: KUTOKA FB: VITUKO VYA YERICKO ''NYERERE''
Mohamed Said: KUTOKA JF: HISTORIA YA TANU - DK. VEDASTO KYARUZI, KASELLA BANTU NA JULIUS NYERERE
Mohamed Said: Ijue Historia ya Kweli ya Kuasisiwa kwa TANU
Mohamed Said: KUMBUKUMBU YA MASHUJAA WA UHURU WA TANGANYIKA RASHID ALI MELI
Mohamed Said: AZAM TV KIPINDI MAALUM CHA MASHUJAA WA UHURU WA TANGANYIKA
Mohamed Said: KUTOKA JF: SHEIKH HASSAN BIN AMIR ALIVYOIONGOZA TANU KUWA CHAMA CHA KISEKULA
Mohamed Said: KLEIST SYKES (1894 - 1949) KATIKA DICTIONARY OF AFRICAN BIOGRAPHY (DAB) OXFORD UNIVERSITY PRESS, NEW YORK

Wanamajlis,
Hizo hapo juu ni zaidi ya kurasa 100 za kusoma pamoja na audio za kusikiliza
na video za kuangalia.

Si lazima upitie zote chagua moja mbili tatu utakuwa ushajifunza kitu.

Waswahili tuna msemo na Mzee Ali Hassan Mwinyi akipenda kuutumia,
''Muongo muongoze.''

Chembelecho Maalim Faiza: Elimu bila Khiyana.

Huyu Jonathon Glassman ni professor wa historia Northwestern University
Evanston, Chicago alinialika nikazungumze chuoni kwake juu ya historia ya
TANU na uhuru wa Tanganyika.

Nilizungumza katika Ukumbi wa Eduardo Mondlane.

Glassman alifanya pitioa la kitabu changu katika Cambridge Journal of African
History Vol. 42 Issue 1 March 2001 halikadhalika John Iliffe.

historia
Ndugu zangu,
Katika rejea zangu hizo hapo juu nimekuchagulieni hii moja msome:

KUTOKA FB: VITUKO VYA YERICKO ''NYERERE''
Mohamed Said April 26, 2016 0

10931175_947898611888705_4658545018381933995_n.jpg

Yericko ''Nyerere''
Hamisi O. Hanyato Mohamed Said Salum
4 hrs · BlackBerry Smartphones App ·

Kaka,tunataka verification ya hii habari. Ya Yeriko.Tafadhali sana usinyamaze Kaka.




Yericko NyerereFollow
10 hrs ·
Uongo wa Historia ya Afrika na Waafrika itajibiwa na muafrika.
Na: Yericko Nyerere
Binafsi nimejipa utaratibu kuwa vitabu vinavyohusu uafrika na waafri sitavitilia mkazo sana vile vilivyoandikwa na wazungu bali vilivyoandikwa na Waafrika wenyewe! Mfano ukisoma historia ya Mkwawa iliyoandikwa na wazungu wanasema mkwawa alijiua kwakujipiga risasi,
Ukweli wa historia ya kiafrika wazungu waliona aibu kusema walimshindwa Mkwawa, Mkwawa hakujiua bali aliwatoroka wazungu na kuelekea Songea ambapo alifia milima ya Lukumbulu kwakuliwa na Simba baada ya kuugua akiwa milimani peke yake. Nimpongeze kamanda Godwin Mwesiga huyu ni mtafiti wa mambo ya kiafrika na uafrika wetu.
Ni rahisi sana Vijana wa leo kuwadhalau wazee wanaokutana nao barabarani na kuwaona watu wasio na Elimu wakiaminishwa kuwa elimu ilianzia magharibi, Cha ajabu Ahmed Baba (1556-1627) karne ya 16 aliandika vitabu 60.Ni mingoni mwa wasomi wa Phd katika ufalme wa Mali.
Ni vizuri watu tuyasake maarifa kwakutumia maarifa, na kwakutokujua historia yetu Waafrika tumelidhika Bara letu la Afrika na yale machache tunayoyafahmu, tukidhani wazungu ndio wasomi wa mwanzo duniani kumbe wapo waliofanya mapinduzi makubwa katika Africa,ila wamefichwa na historia za kigeni zinazofundishwa mashuleni.
Ukisoma leo historia ya Tanganyika ni aibu, inaanza na Nyerere na kuishia na Nyerere jambo ambalo ni uogo mkubwa......Pamoja na kwamba 1927 Gavana Sir David Cameron kupiga marufuku mtu mweusi kukanyaga mjini (posta ya leo) hasa kwenye sherehe za wazungu ambazo zilikuwa maranyingi zinafanyikia ukumbi wao pale makao makuu ya NBC leo,
Gavana huyu aliwaundia chama cha kuratibu sherehe za weusi huko pembeni ya mji huko mtaa wa Stanley (leo Lumumba) na kuwapa ofisi mahali leo wanapojiita TANU ilizaliwa. Lakini historia ya Tanganyika haiwataji waasisi wa AA, Rais wa kwanza Mwalimu Cesil Matola (msomi wa mwanzo kabisa enzi za mjerumani kutoka kabila la Wayao), katibu mkuu wa kwanza Klest Sykes (Mzulu mateka wa vita vya kwanza vya dunia toka Afrika Kusini), Mwekahazina Ali Ramadhan (mzaramo na mvuvi maarufu wa pwani la Azania).
Hao ndio mwaka 1927 waliounda Chama cha kwanza kabisa cha kutetea maslahi ya weusi Tanganyika na shughuli zake zilikuwa ni kuratibu sherehe za waafrika tu. (Chama cha walevi kwa lugha nyingine). Mwaka 1933 Mwalimu Cesil Matola alifariki na nafasi yake ikakaimiwa na katibu mkuu wa chama hicho bwana Klest, mpaka ilipofika mwaka 1948 yakatokea mapinduzi yaliyoongozwa na mtoto wa Klest aliyeitwa Abdulwakil Sykes huyu alikuwa ametoka kupigana vita vya pili vya dunia, na aliporudi alikuwa na mawazo ya ujana toka vitani, akampindua baba yake kwa kumpiga ngumi puani. Kisha AA ikabadilishwa jina na kuitwa TAA, Rais wake wa Kwanza akawa Dr Vedasto Kyaruzi (Mhaya)huyu ndie dakitari wa binadamu wa kwanza kabisa wa kiafrika Tanganyika, Katibu mkuu akawa Abdulwakil Sykes na Mweka hazina akawa Dosa Azizi, utawala huo ulienda mpaka mwaka 1953 uchaguzi ulipofanyika na Nyerere akashinda pale kwenye ukumbi wa Anautoglo Mnazimoja leo, mwaka 1954 Nyerere akabadili jina la chama na kuwa TANU iliyokwenda mpaka mwaka 1977 na kisha kikazaliwa chama kiitwacho CCM ambacho kinalitafuna taifa leo..
Hili ndio chimbuko la AA, TAA, TANU na hii CCM.

LikeShow more reactions
Comment
Share
Comments

Jibu langu kwa msomaji na ni ndugu yangu aliyeniomba nimjibu Yericko:


Mohamed Said Salum
Hamisi huyu kijana kaa nae mbali sana. Mwenyewe anasema ni mtoto wa Mwalimu Nyerere kwa mama mwingine. Muongo sana huyu. Anamtaja Mzee Kleist kuwa mateka. Baba yake Mzee Kleist aliingia Tanganyika kama askari na alikuja na Affande Plantan kutoka Imhambane wakiongozwa na Kamanda wa Kijerumani Herman Von Wissman. Kleist alikuwa bado hajazaliwa. Kleist kaja kuzaliwa Pangani 1894. Huyu mtoto mpuuzi yeye anapita kwenye maandiko yangu kisha ananakili na kukoroga. Hii ni taarifa tu kwako kaka kwa kuwa umeniomba nimjibu. Siwezi kumjibu huyu si makamo yangu. Ikiwa unataka http://www.mohammedsaid.com/.../kleist-sykes-1894-1949... historia hii ingia katika blog yangu mohammedsaid.com. Ukitaka kumsoma Dr. Kyaruzi, Abdul Sykes, Nyerere na wengine fanya ''search'' utapata makala zaidi ya moja.





KLEIST SYKES (1894 - 1949) KATIKA DICTIONARY OF AFRICAN…
MOHAMMEDSAID.COM
 
Naendelea kushikilia msimamo wangu kuhusu yale niliyoandika mwanzo kabisa wa mjadala huu.
Wewe baba una shida zako na Yericko na wala sio makosa ya kimaudhui au kiufundi ya kitabu chake.

Yaani wewe una tatizo nae lingine kabisa.Haulali,hauogi,haundi chooni kisa kitabu cha Yericko na Yericko mwenyewe....IPO SHIDA KWAKO TENA SI NDOGO.

Ushauri wangu mwingine.
Fanya editing/hariri kitabu chote kwa kua ww ni mhariri andaa chapisho moja liweke kwenye soft copy na hard copy ili tununue tusome.
Itakua umemtendea haki yeye na wewe mwenyewe na jamii nzima ya wapenda historia.
Hii personal attack sio kitu cha maana ktk maisha yako na yake.

Jinsi unavyyojibiwa na jinsi unavyoendelea kuleta hoja zingine inaonekana moyo wako umevia,umumia,umejawa na hila kwamba kwanini sikuandika mm ninaejua kila kitu mpka aandike Yericko alieokotaokota hili na lile.

Umri wako mkubwa na utaalam ulio nao unatosha kuona kazi kubwa iliyofanywa na Yericko na kuithamini na kumtia moyo na si vinginevyo.

Aisee mwafrika mweusi na roho yake nyeusi tii!
 
Naendelea kushikilia msimamo wangu kuhusu yale niliyoandika mwanzo kabisa wa mjadala huu.
Wewe baba una shida zako na Yericko na wala sio makosa ya kimaudhui au kiufundi ya kitabu chake.

Yaani wewe una tatizo nae lingine kabisa.Haulali,hauogi,haundi chooni kisa kitabu cha Yericko na Yericko mwenyewe....IPO SHIDA KWAKO TENA SI NDOGO.

Ushauri wangu mwingine.
Fanya editing/hariri kitabu chote kwa kua ww ni mhariri andaa chapisho moja liweke kwenye soft copy na hard copy ili tununue tusome.
Itakua umemtendea haki yeye na wewe mwenyewe na jamii nzima ya wapenda historia.
Hii personal attack sio kitu cha maana ktk maisha yako na yake.

Jinsi unavyyojibiwa na jinsi unavyoendelea kuleta hoja zingine inaonekana moyo wako umevia,umumia,umejawa na hila kwamba kwanini sikuandika mm ninaejua kila kitu mpka aandike Yericko alieokotaokota hili na lile.

Umri wako mkubwa na utaalam ulio nao unatosha kuona kazi kubwa iliyofanywa na Yericko na kuithamini na kumtia moyo na si vinginevyo.

Aisee mwafrika mweusi na roho yake nyeusi tii!
Ridhwani,
Umeghadhibika.

Mtu akighadhibika hawezi kuandika vyema unanishambulia mimi binafsi
badala ya kujibu hoja zangu.

Uhariri wa kazi ya Yericko iko kwake mwenyewe.

Kuwa naifanyia hasad kazi ya Yericko si kweli mie na yeye katika kuandika
tuko mbalimbali sana.

Umefanya haraka ya kujibu soma niliyoweka itakusaidia kuelewa mengi.
Nakukumbusha mjadala huu chanzo chake ni historia ya Zanzibar.

(Unapotumia dots katika uandishi kanuni ni kuweka dots 3 ...).
Nimeona kidogo nikufunze uhariri.

impostor
ɪmˈpɒstə/
noun
noun: impostor; plural noun: impostors; noun: imposter; plural noun: imposters
  1. a person who pretends to be someone else in order to deceive others, especially for fraudulent gain.
    "the charity has warned anyone approached by the impostor to contact police immediately"
    synonyms: impersonator, masquerader, pretender, deceiver, hoaxer; More
 
Back
Top Bottom