Askari wa JWTZ kizimbani kwa kukaidi amri halali ya askari wa Usalama Barabarani

Askari wa JWTZ kizimbani kwa kukaidi amri halali ya askari wa Usalama Barabarani

Dah! We sokwe mtu ni watumishi wangapi wanafanya hivi? Madaktari hawavalishi kiti clinical cot zao? Wahandisi wa ujenzi?

Hapa umepuyanga alafu kqzi hawafutwi kizembe zembe

Nazungumzia JWTZ ambao wanaofanya hivyo ni wale shuleless ,sijawahi kumuona mwenye cheo kikubwa ameweka kombati kwenye kiti cha gari.

Ukweli lazima usemwe acheni ushamba nyie shuleless ,JWTZ ni kazi kama kazi nyingine hivyo msijione mpo juu ya sheria....Mimi nina marafiki wengi wanajeshi lakini hawana tabia hizo za hao shuleless coz kidogo wamepita pita school.
 
Eti vibakuri😂, upo sahihi kabisa Mkuu, askari anayejielewa hana muda wa show off kabisa, ila hawa washamba ndio wanasumbua

Kuna jwtz mmoja hivo hivo siku moja road kagonga gari ya watu alafu akamuwahi aliyemgonga kumpiga beat,jamaa alitoka kwenye gari yake ana pingu ikabidi jwtz awe mpole

Acha tu ila wanaofanya hivyo ni wale ambao hawana shule ,mwanajeshi ambaye aliyeenda shule na vyeo vyake hauwezi kumkuta hata mara moja anafanya huo ujinga tena wapo peace sana tena wanakwambia mkuu hii ni kazi tu kama kazi nyingine.

Sijajua kwanini hawa JWTZ shuleless wanafanya mambo bila kufukiria yaani wanajua kila mtu barabarani ni raia wao ndiyo Jeshi ,yaani unamgonga mtu halafu unaleta tena ubabe,hawa daa yao ni kuchoma moto "vibakuli" vyao maana wengi hawana "MADUNGU".
 
Aisee kuna jamaa wengi baada ya kupata elimu ya kutosha na kukitambua ...wameacha hizo kazi za wenyewe..mwanaume asifiwi kazi anasifiwa pesa.

Hajielewi huyo ,inaonekana hajapita kabisa shule ,angepita vyuoni angeona wanajeshi waliokuja kusoma then baada ya kumaliza wakaachana na hiyo kazi wakafanya mambo mengine.
 
1.polisi wa vyeo vya chini wanakula laki 5 ,kinachosaidia ni ration ,uwe lindo mgodini na vi saccos
2.jwtz pia hawafiki laki 8 ,huku napo vi mikopo au uwe peace keeping missions
3.magereza pia ni kama polisi tu

Vijana stories za jeshini kuna pesa sijui huwa wanatoa wapi, hawana pesa ya kumfanyia mtu madharau
Na hata km wamgekuwa na hizo pesa bado sio tiketi ya kumdharau mwenzako.
 
Hajielewi huyo ,inaonekana hajapita kabisa shule ,angepita vyuoni angeona wanajeshi waliokuja kusoma then baada ya kumaliza wakaachana na hiyo kazi wakafanya mambo mengine.
Sasa unadhani kwanini huwa wanakuja kusoma kwenye hivyo vyuo?
 
Sasa unadhani kwanini huwa wanakuja kusoma kwenye hivyo vyuo?

Waliingia wakati wapo form six ili wapate ajira kwanza baada ya kuingia wakajionea waliyojionea wakaona bora waongeze elimu wapate degree ,baada ya kupata wakarudisha magwanda na kuendelea na kazi nyingine na baadhi wakaendelea hapo hapo! JWTZ huwe Officer na elimu ndiyo utaenjoy otherwise utafyeka nyasi sana!
 
Pamoja na Mikopo ya nyumba na magari wanayopewa?
Hakuna jeshi linatoa mkopo wa gari/nyumba hapa Tanzania mkuu bali kuna taasisi ndani ya majeshi ambazo zinatoa mikopo ya pesa ndio pesa hizi askari hujenga na kununua magari

Kila baada ya miaka mitano huwa kuna form wanajaza ku declare mali zao,usipoeleza umetoa wapi pesa unafuatiliwa ndio maana wakipiga deal wakanunua magari ya bei hawaandiki majina yao kwenye hati

Ukiwa mwanajeshi unamiliki Vanguard alafu una cheo cha chini utahojiwa kwa pesa gani umenunua hiyo gari ? Sababu hata ma afande wako wanajua mshahara wa jeshi hautoshi mtu kumiliki magari ya bei hizo bila kukopa au kulipwa na jeshi kwa kazi maalumu

Kwa mfano, polisi wenye hela ni kuanzia makamishina tena uwe RPC ndio utapata pesa, Huko JWTZ ni ma brigadier na vyeo kama hivo, hata Traffic naonaga watu humu wanadhani zile rushwa mnazowapa road wanakula, ila ukweli ni kwamba Traffic nae anapeleka pesa kwa RTO usipopeleka unatolewa hapo

Ma RPC nao hupeleka pesa kwa IGP
 
Kaka unafikiri natania? Unazijua ajira ambazo ukimaliza kidato cha nne kuna uwezekano wa kuzipata? Unazijua ajira ambazo ukimaliza kidato cha sita unaweza kuzipata? Unazijua ajira ambazo ukimaliza degree, masters, n.k unaweza kuzipata? Basi hao wote ni takataka kwa wanajeshi ukiwa tu unafikiria sawasawa
Acha maneno yako tumekulia katika kambi za jeshi wazazi wetu wapo uko tunayajua yote hayo jeshini hakuna pesa yoyote ya maana.

Usione wamevaa kombati zao za mabaka mabaka ukatishika kule kuna wacheza ngoma, vinyozi, fundi cherehani, fundi garage, sekretari, wafanya usafi wa mwagilia bustani, Dr, engineer nk.

Mishahara ya kawaida sana jeshini wazazi wetu wamestaafu na madeni +visukari.

Kitu pekee cha kujivunia jeshi ni lile gwanda tu ukilivaa tena utajivunia kwa washamba sio kwa waelewa
 
Mshahara wa mil 1 kukaa kwenye kota,kunywa bia zisizo na kodi ndio maisha mazuri?
Umesahau na kuvaa sare (wao huita uniform) kila muda kama mtoto wa primary 😂 (hapa natania)

Sibezi kazi za Jeshi na ninawaheshimu sana hawa jamaa,lakini huyu dogo inabidi tumpe ukweli kwa jinsi alivokuja

Mboga za ma askari wa majeshi yote,kambini huwa ni dagaa, maharage ,mchicha, karibu kila siku,haya ni maisha ya kawaida kabisa ya kitanzania

Sasa dogo akisema wanajeshi wana pesa na kuita watumishi wengine takataka, mimi anieleze hizo pesa huwa wanazila saa ngapi ?

Kitu kizuri jeshini kama ambacho watumishi wengine hawana ni kulewa, majeshi yote kama wewe sio dereva utakuwa unalewa kila siku na unaingia kazini ,cha muhimu usinywe pombe ile mpaka kila mtu ajue umepiga
 
Kaka unafikiri natania? Unazijua ajira ambazo ukimaliza kidato cha nne kuna uwezekano wa kuzipata? Unazijua ajira ambazo ukimaliza kidato cha sita unaweza kuzipata? Unazijua ajira ambazo ukimaliza degree, masters, n.k unaweza kuzipata? Basi hao wote ni takataka kwa wanajeshi ukiwa tu unafikiria sawasawa
Usikute basha wako mwanajeshi kaamua kukujaza uongo ili akugonge kiurahisi
 
Nazungumzia JWTZ ambao wanaofanya hivyo ni wale shuleless ,sijawahi kumuona mwenye cheo kikubwa ameweka kombati kwenye kiti cha gari.

Ukweli lazima usemwe acheni ushamba nyie shuleless ,JWTZ ni kazi kama kazi nyingine hivyo msijione mpo juu ya sheria....Mimi nina marafiki wengi wanajeshi lakini hawana tabia hizo za hao shuleless coz kidogo wamepita pita school.
Kuna mmoja asubuhi tunawahi uwanjan mida ya sasa kumi na mbili alivalishakoti kwenye kiti bahati mbaya Basi imebeba wa kubwa hili hapa linapita Kushoto kwetu. Niliona akiwa Ana haha kulitoa koti.
 
Back
Top Bottom