Askofu Emaus Mwamakula akamatwa na Polisi kwa kuhamasisha Maandamano ya kudai Katiba Mpya

Hivi ni lini polisi wa nchi hii wataacha kufanya kazi kwa misingi ya kitutusa?
 
Yohana Mbatizaji, Alikatwa kichwa kwa kumtuhumu Mfalme Kumchukua mke wa ndugu Yake, na Yesu Akanyamaza kimya.

Unajua kwa nini Yesu Alinyamaza kimya? Tafakari utapata Majibu.

Nikwa sababu Yohana Hakutumia hekima kumweleza Mfalme juu ya Kosa la kumchukua mke wa Ndugu Yake.

Hivyo watumishi wa Mungu, wajue Hekima ni njema ikitumika kufikisha ujumbe kwa Viongozi.

Hakuna kiongozi hasiye shaurika au kuchukua Mawazo ya watu lakini inategemea na jinsi unavyotumia Hekima kuwasilisha hoja yako ndicho kilicho mponza Yohana Mbatizaji.
 
Waumuni wake ndio waandamane!?, au watanzania woote tuandamane???!!!. : Mchuma janga hula na wa kwao,
 
Hivi ni lini polisi wa nchi hii wataacha kufanya kazi kwa misingi ya kitutusa?
Kwa akili zako ulitaka polisi wamvike Nishani?,au ulitaka wampigie vinanda na vinubi?, lini watanzani tumekaa tukamtuma mwamakula kuwa tunahitaji katiba mpya?
 
Bora aliwahi kupost kabla hawajampora simu na kusepa nae. Otherwise angepotea kwa siku kadhaa huku akipokea kipondo heavy huko mafichoni

Hii “terror squad” ya mtu flani ni shida kwelikweli
Mataga mmoja amesema humu kuwa walichelewa kumkamata. Kweli, kwa kujipendekeza kwa Mambosiasa, ilitakiwa akamatwe hata kabla hajaingia mtandaoni. Kazi tukutu ya intelligensia!
Naye alijua atakamatwa. Alijua kama anatumia mtandao wa Voda, wenyewe watazima akamatwe bila taarifa kusambaa. Voda ya kazi tu yanafurahisha. Hivyo aliandika ujumbe bila ya kuweka tarehe. Kaupeleka kunako. Nao bila ajizi waliposikia tu wakatoa huo ujumbe wake. Unakuwa na uzito maradufu kusomeka NIMEKAMATWA kuliko AMEKAMATWA. Ukimwangalia na kumsikiliza anachoongea Mambosiasa unajua kabisa ni uozo mtupu. Sheria hakuna na mantiki ni mfu. Akili ni ile ya nywele tu. Tena taahira ana msitu wa nywele. Weledi, akili, busara na maarifa ni msamiati tosha. Geshi letu!
 
Akimaliza tu kusali anaota mshipa yeye mwenyewe chezea wazee wa ziwani weye
Ziwa gani hilo? Lile la moto? Wapambe hawana akili kabisa. Wachawi wanajua nguvu ya maombi. Wewe mshirikina upo upo na chezea wazee wa ziwani weye. Acha uzwazwa we mshirikina. Hakuna ujualo ziaidi ya tawire!
 
Lengo lilikuwa kukamatwa naona na si matembezi.
 
Ziwa gani hilo? Lile la moto? Wapambe hawana akili kabisa. Wachawi wanajua nguvu ya maombi. Wewe mshirikina upo upo na chezea wazee wa ziwani weye. Acha uzwazwa we mshirikina. Hakuna ujualo ziaidi ya tawire!
Si ajaribu sasa uone
 
'wakutanapo wawili na kulitaja jina langu, nami nipo'
Mkutanapo wawili kulitaja jina la Mungu si lazima mmoja wenu ajipe uaskofu. Huyu muhuni alikimbia Moravian sababu ya uaskofu.
 
Haki huinua taifa bali dhambi ni aibu na fedheha kwa taifa.
 
Mkutanapo wawili kulitaja jina la Mungu si lazima mmoja wenu ajipe uaskofu. Huyu muhuni alikimbia Moravian sababu ya uaskofu.
Mhuni ni wewe na sidhani kama una dini.Nadhani wewe ni mpagani tu kama mwenzio.................Na hii mada sidhani kama inakuhusu.Wewe umedandia tu.Muhuni mkubwa.
 
Habari nzima ya kusema maandamano ni lazima yapate kibali cha polisi ni kuvunja uhuru wa kikatiba.

#FreeMwamakula
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…