Uchaguzi 2020 Askofu Gwajima: Naimudu Kawe. Mimi sio kilaza, nilienda Marekani mwaka jana na nimeshaandika vitabu 5 kwa kijapani, vipo Amazon

Uchaguzi 2020 Askofu Gwajima: Naimudu Kawe. Mimi sio kilaza, nilienda Marekani mwaka jana na nimeshaandika vitabu 5 kwa kijapani, vipo Amazon

Waumini wake wanasali kwenye matope pale viwanja vya Mkanada Tegeta. Kwa miaka 20 ameshindwa kujenga kanisa kama Kakobe.

Halafu alinunua Chopa imezungushiwa utepe pale Airport yani haijwahi kutoka pale!
Kwa miaka 20 Chadema ni wapangaji na mnapokea ruzuku na bado mnadai mtailetea Nchi maendeleo,

Labda ya kuzungumza kingereza kama anavyodai mgombea wenu lakini si wa mabomba ya mafuta na midege na SGR.
 
Akiongea katika ufunguzi wa kampeni zake askofu Gwajima amesema jimbo la Kawe ni jepesi sana halihitaji serikali wala manispaa kujiendesha.

Gwajima amesema pindi atakapoapishwa ataanza kugawa magari ya wagonjwa kila kata yeye mwenyewe ili wananchi wakewawaishwe hospitali pindi wanapougua.

Mambo mengine mengi mazuri yatafuatia ikiwemo maboti ya uvuvi kwa ndugu zetu kule ufukweni mwa bahari.

Source: East Africa Radio.

Maendeleo hayana vyama!
Ameshindwa kujenga jengo zuri la kufanyia mazingaombwe na viini macho vyake kwa misukule wake pale Ubungo, ndio aje agawe hayo magari kwa kila kata , na anavyoongea utadhani kazi ya mbunge ni kununua hayo magari.
 
Hiyo ni Mihemko ya watoa mawaidha wala siyo mambo ya kuchukulia siliasi!
Kuna maustadhi wengi wanaongeaga maneno zaidi ya hayo lakini watu wa dini nyingine wala hawachukulii maananani wanaendelea na shughuli zao !
Kwa sababu sio dini yako ,yaseme maneno ambayo maustadhi au mashekh wanaongeaga tuyaone kama wewe sio muongo.
 
Ambulance za nini wakati anao uwezo wa kufufua waliokufa, kuponya vilema.

Si bora angesema atakuwa anawaombea hao wagonjwa waponee majumbani kwao.
Gwajima hana uwezo wa kumfufua mtu yoyote yule, labda anachoweza ni kuponya kishirikina.
 
Yaani mpaka leo watz bado tunaamini ahadi za hivyo?!? si angefanya hayo hapo kabla?!?, tunachagua wabunge/madiwani kama wawakilishi wetu serikalini wakaishauri Serikali wapeleke hoja zetu huko maana kwa hali iwayo yote hawezi kutatua matatizo ya jimbo yeye kama yeye. tatizo sio kukosekana ambulance, mfumo na sheria nalo ni tatizo, sasa kama anawaahidi ambulance na nyie mnashangilia!!! then hakuna maendeleo ya kweli yatapatikana tz
 
Wajinga ndio waliwao, waumini wake wanasalia kwenye jua, ameshindwa kuwajali ndio ataweza kununua ambulance? Hivi anadhani wananchi wa kawe ni kama hao waumini wake wanaosadiki porojo zake? Mbona hizo ahadi za kitapeli ni za enzi za watu wakiwa na ufahamu mdogo, au na yeye kaamua kuja na swagga za kuifanya Tanzania kama ulaya na Kigoma kuwa Dubai?
Kama alinunua Helkopta atashindwa kununua ambulance?
 
Hiyo ni Mihemko ya watoa mawaidha wala siyo mambo ya kuchukulia siliasi!
Kuna maustadhi wengi wanaongeaga maneno zaidi ya hayo lakini watu wa dini nyingine wala hawachukulii maananani wanaendelea na shughuli zao !
Wataje maustadhi wapi hao na maneno gani hayo?

Nani aliwahi kusema kuwa atafanya makanisa kuwa misikiti na lau angesema hivyo wangekuwa washamfungulia shitaka la ugaidi
 
Kwa miaka 20 Chadema ni wapangaji na mnapokea ruzuku na bado mnadai mtailetea Nchi maendeleo,

Labda ya kuzungumza kingereza kama anavyodai mgombea wenu lakini si wa mabomba ya mafuta na midege na SGR.
Haya jiandae kupelekwa kwa mabeberu na Gwajiboy maana ndizo ahadi zake alizotoa leo.

 
Wajinga ndio waliwao, waumini wake wanasalia kwenye jua, ameshindwa kuwajali ndio ataweza kununua ambulance? Hivi anadhani wananchi wa kawe ni kama hao waumini wake wanaosadiki porojo zake? Mbona hizo ahadi za kitapeli ni za enzi za watu wakiwa na ufahamu mdogo, au na yeye kaamua kuja na swagga za kuifanya Tanzania kama ulaya na Kigoma kuwa Dubai?
Kama hoja ni kushindwa kujenga jengo la kanisa, chadema nao wameshindwa kujenga jengo la ofisi nao tusiwachague mpaka wajenge jengo lao?
 
Huku jengo la kanisa likiwa nimemshinda kujenga anatangatanga. Lakini angeanza na kuboresha miundombinu ya shule ingefaa kuliko hayo magari.
Kama chadema walivyoshindwa kujenga jengo la ofisi licha ya kupokea ruzuku nono afu ndo wanataka tuwakabidhi nchi.
 
Wataje maustadhi wapi hao na maneno gani hayo?

Nani aliwahi kusema kuwa atafanya makanisa kuwa misikiti na lau angesema hivyo wangekuwa washamfungulia shitaka la ugaidi


Wapo wengi lakini sababu I am psychologically matured enough huwa sitilii maanani hata katika kuwakariri majina yao!

Chamsingi na cha sekondari sisi sote ni waTZ tupendane na kushirikiana!
 
Waumini wake wanasali kwenye matope pale viwanja vya Mkanada Tegeta. Kwa miaka 20 ameshindwa kujenga kanisa kama Kakobe.

Halafu alinunua Chopa imezungushiwa utepe pale Airport yani haijwahi kutoka pale!
Hilo swali umewahi kumuuliza Mbowe lini atajenga ofisi ili muhame kwenye ile servant quarter?
 
Kabisa mkuu!
Bwashe ambulance siyo maendeleo ni uchuro, mgombea gani huyo anayeombea Jimbo kuwa na wagonjwa daily? Au katumwa mauti huko anakopataga riziki yake? Gwajima ni wa kuogopwa kama jini kwa style hi ya ambulance.
 
Wajinga ndio waliwao, waumini wake wanasalia kwenye jua, ameshindwa kuwajali ndio ataweza kununua ambulance? Hivi anadhani wananchi wa kawe ni kama hao waumini wake wanaosadiki porojo zake? Mbona hizo ahadi za kitapeli ni za enzi za watu wakiwa na ufahamu mdogo, au na yeye kaamua kuja na swagga za kuifanya Tanzania kama ulaya na Kigoma kuwa Dubai?
Mkuu, nilikuwa nina hamu ya kuchangia chochote kwenye uzi huu. Lakini naona tayari umekwisha uweka mchango wangu kwenye haya maoni yako!
 
Wataje maustadhi wapi hao na maneno gani hayo?

Nani aliwahi kusema kuwa atafanya makanisa kuwa misikiti na lau angesema hivyo wangekuwa washamfungulia shitaka la ugaidi


Huwa sitilii maanani katika kushika majina yao sababu najua ni mihemko tu na wala wayasemayo hawawezi kuibadili imani ya mtu mwingine!

Mbona wengi tu wanaenda mbali hata kuthubutu kusema Yesu si Mungu?!

Hivi kuna kubwa kuliko hilo?!

Sisi sote ni waTZ tupendane tustahamiliane!
 
Kwa nni hakufanya hivo huko nyuma kama anawapenda wanakawe. Ananunua ubunge ka ambulance!
 
Gwajima smart Sana. Tukiwa na wabunge wenye kujiongeza kama hawa 100 tutapata kwa maendeleo.
 
Back
Top Bottom