Atakayenionesha andiko linalosema mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini nampa laki 1 akale sikukuu

Atakayenionesha andiko linalosema mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini nampa laki 1 akale sikukuu

Lakini Biblia yenyewe imeandika, yaliyomo humu sio matukio yote yaloweza kutokea kipindi, bali yale tu yalionekana kuwa yafaa. huenda ilikuwa hivyo sema waandishi hawakuona umuhimu wa kuandika hayo.
Je Wayahudi utaratibu wao kuhusu ndoa ukoje?

Wayahudi Mchungaji hahusiki na mambo ya kufungisha Ndoa
 
Wakuu kwema,

Kuna laki moja hapa nataka nimpe mtu akale na wana wake. Ili uipate nahitaji uniwekee aya, mstari au sura ndani ya Quran au Biblia inayoonesha mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini au walifungishwa ndoa na Mtume, nabii au Kuhani?

Sihitaji Hadithi au andiko lisiloonyesha ninachokizungumza moja kwa moja.

Nimesema nukuu itoke kwenye Biblia au Quran si kwamba siheshimu dini zingine hapana, hivi vitabu ndivyo navifahamu.

Asante.
Ukianza kuhoji kwa namna hii, unaweza hata ukahoji ni wapi Biblia iliandika kuwa wanadamu watakuwa wanasfairi kwa usafiri wa ndege.

Kwa hali hiyo unaweza ukaanza kulazimisha waumini wote watumie usafiri wa punda kwa sababu kipindi Yesu alipokuwa yupo duninani, usafiri pekee uliokuwepo ulikuwa ni wa punda.

Mungu alimpa mwanadamu mamlaka ya kutawala dunia ikiwa ni pamoja na kuweka sheria ambazo atazitumia kwenye utawala, ili mradi tu sheria hizo hazikinzani na maandiko matakatifu
 
Kuzini ni neno linalohusiana na Sheria za dini.
Mwanaume na Mwanamke wakikubaliana kuishi pamoja tayari ni Ndoa. Hakuna nje ya hapo.
Kisheria za Mahakama hakuna msamiati Kuzini.

Ndio maana nikakuambia Kwa waumini WA dini za kanisa wao Kuzini wanamaanisha MTU kutokufunga ndoa Kanisani.
Jambo ambalo tayari nimeshasema ni uongo
Hapana, kwamba wote wanaofanya ngono ni wanandoa?
 
Ndio nakuambia kuwa Kijana akimchukua Binti wakaamua kuishi pamoja kama MKE na mume hiyo tayari ni Ndoa.

Achana na Ile kukubaliana kufanya ngono.
Hapa tunazungumzia wale wanaoitwa sogea tuishi. Hao wapo kwenye Ndoa
Mimi wa sogea tuishi siungi mkono. Labda kama sifahamu tafsiri sahihi.
 
Soma biblia kitabu cha mwanzo 2:18 kama unaamini Mungu yupo, unaamini aliumba vyote basi tafakari sana fungu hili. Ndoa ilianzia eden. Soma tena fungu hilo, unalielewaje? Unless roho mtakatifu kakupifa upofu. Mungu ndiye muasisi wa ndoa na akawafungia hao adam na Hawa. Sasa juu ya yesu au mtume kufunga Ndoa sijaona hilo. Ila Mungu kufunga ndoa kati ya Adam na Hawa lipo. Ubarikiwe rafiki . Je kwa kujua hilo litakusaidia vipi kumuona Mungu uso kwa uso?
 
Wakuu kwema,

Kuna laki moja hapa nataka nimpe mtu akale na wana wake. Ili uipate nahitaji uniwekee aya, mstari au sura ndani ya Quran au Biblia inayoonesha mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini au walifungishwa ndoa na Mtume, nabii au Kuhani?

Sihitaji Hadithi au andiko lisiloonyesha ninachokizungumza moja kwa moja.

Nimesema nukuu itoke kwenye Biblia au Quran si kwamba siheshimu dini zingine hapana, hivi vitabu ndivyo navifahamu.

Asante.
Kwenye uislam sio lazima sheikh kufungisha ndoa. Masheikh wamekuwa wakifungisha ndoa kwa niaba ya mawalii incase walii anaupunguf wa elim

Kweny uislam hizi ndo sharti za ndoa:

Mwanamke awe Muislamu au Mtu wa Kitabu (kwa maana awe Myahudi au Mkristo) mfuasi wa dini yake. Lakini Uislamu unatuhimiza kuchagua mwanamke Muislamu mfuasi wa dini, kwa sababu yeye atakuwa mama mlezi wa watoto wako, na msaidizi wako katika mambo ya kheri na msimamo wa kufuata dini. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Basi wewe mpate (muoe) mwenye dini». (Bukhariy, Hadithi Na. 4802. Muslim, Hadithi Na. 1466).

Mwanamke awe mwenye kujiheshimu, mwenye kujihifadhi. Ni haramu kumuoa mwanamke anayefahamika kwa mambo machafu na uzinzi, kama alivyosema Allah Mtukufu kuwa: «Na (mmehalalishiwa pia kuoa) wanawake waumini wenye kujihifadhi, na pia wanawake wenye kujihifadhi miongoni mwa wale ambao walipewa vitabu». (Almaaida, aya 5)

Mwanamke asiwe miongoni mwa Maharimu zake ambao ni haramu kwake kuwaoa uharamu wa kudumu Pia ni haramu kuoa kwa pamoja mtu na dada yake au mdogo wake, au shangazi yake, au mama yake mdogo au mkubwa.

Ni sharti kwa mwanaume awe Muislamu. Ni haramu katika Uislamu mwanamke wa Kiislamu kuolewa na kafiri; vyovyote dini yake iwavyo, awe Mtu wa Kitabu au sio Mtu wa Kitabu

Ndoa inakamilika kwa Walii kumtamkia mwanaume kwamba: Nimekuoza binti yangu, au dada yangu, na amtaje kwa jina lake. Na mwanaume atasema kwamba: Nimekubali au nimeafiki. Mkataba wa ndoa utakuwa umekamilika kwa kutumia maneno haya au maneno mengine yenye maana hiyo kwa lugha yoyote ambayo watu wanaifahamu.
 
Yesu alibatizwa na Yohana ndio maana kwa mkristo kubatizwa ni lazima maaana yangu ni kwamba jambo lenye umuhimu Yesu kama yupo katika ilo tukio lazima alifanye mfano aliwahi kufukuza watu wakiuza vitu katika hekalu maana yake ni kwamba ilo jambo halifai na kungekuwa na ulazima wa kila ndoa lazima afungishe padri au sheikh basi angenza na yeye mwenyew Yesu lakini alienda katika harusi tukio muhimu alilofanya ni kugeuza maji kuwa pombe msome vizuri mtoza ushuru utamuelewa
Hata Hilo andiko hulijui,umekariri tu.
 
Niraha Sana kuwasikiliza watu wanatafuta tafuta sababu ya kuhalalisha kitu badala ya kuleta kifungu ambacho kitamaliza hili jambo. Mpaka Sasa hakuna liyelet mwongozo wa ulazima wa ndoa kufungwaa kanisani au ulazima wa kanisa kuendesha mazishi. Wakristo wengi hawamiliki akili zao na wanafuata mambo ambayo ukiwauliza hawayajui Ila kwakuwa wameambiwa na kiongozi wa dini basi wanafuata tu, na ukija kuwauliza hawakupi majibu sahihi ya kibiblia. It's time to wake up guys.

Hata Mimi ni muumini wa kanisa ila Kuna mambo ambayo siyaelewi na Kila siku Huwa nayauliza Ila sipati majibu sahihi so hata mtu akiniuliza swali siwezi kumkomalia tu kwamba aamini kitu ambacho sikijui vizuri. Nashukuru Hili swala la ndoa dini yangu imelisolve kwa kukubali ndoa za kimila pamoja na kiserikali maadam tu Kuna ushahidi wa ndoa kufungwa (vyeti vya ndoa)
 
Wakuu kwema,

Kuna laki moja hapa nataka nimpe mtu akale na wana wake. Ili uipate nahitaji uniwekee aya, mstari au sura ndani ya Quran au Biblia inayoonesha mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini au walifungishwa ndoa na Mtume, nabii au Kuhani?

Sihitaji Hadithi au andiko lisiloonyesha ninachokizungumza moja kwa moja.

Nimesema nukuu itoke kwenye Biblia au Quran si kwamba siheshimu dini zingine hapana, hivi vitabu ndivyo navifahamu.

Asante.
Mwaka huu tunaanza kuish sogea tukae
 
Hoja yako ni ipi? Kua watu wajioleee tu bila kuwa na utaratibu kiimani! Assume ingekua hivyo hali ingekuaje? Nauliza tu Mtoa hoja..nothing personal!
 
Back
Top Bottom