Atakayeweza kuniloga nitamlipa Milioni 25

Atakayeweza kuniloga nitamlipa Milioni 25

Sasa kama huamini uchawi kwamba upo na unatenda hiyo imani ya kunuiza na kitu kikaja wewe umeitoa wapi.
Kwa herini maana nishawaambia mnaopinga wote ninyi kwenye masuala ya ufahamu wa mambo ni weupe tuu
Wapi nimesema ninatenda hiyo imani ya kunuiza?

Wewe unajua hata kusoma kwa ufahamu au ni ngumbaru usiyejua kusoma kwa ufahamu?
 
1.kumbe mwanamke dah! me nilijua kidume
2.yaani mpaka leo hujajua tu kwamba ulisharogwa? hebu fanya ihsani kawape mil 25 zao wale waliokufanya uhame hekalu lako
3.wachawi mnakwama wapi aisee utajiri nje nje huu
 
Hello Africans.

Hakuna binadamu ninaowadharau kama wanaoamini mauchawi na mauganga.

Huwa nawaona ni watu wenye kasoro kubwa kichwani na wameoza kiasi kwamba hata uwaambie nini huwezi kuwabadili imani.

Hizi imani pumbavu zinaonesha vile Africans tuko na IQ ndogo. Na ndio maana pamoja na utajiri uliopo ktk hili bara tunateseka na shida karne kwa karne huku wenzetu wasioamini haya maujinga wakituacha mbali kwa maendeleo. (Najua kuna wazungu wachache vichaa pia wanaamin ushirikina).

Ukweli hizi imani zinanikera sana maana mbali ya kuchelewesha maendeleo ya hili bara pia ni hatari. Tushaua sana wenzetu wasio na hatia sbb ya hizi imani pumbavu. Albino, Vipara, wazee with red ayes na wengine wengi.Upumbavu mtupu.

Mimi binafsi nilishahama sehemu kwa kusingiziwa eti mimi ni freemason. Nilifanya kosa nikaporomosha hekalu wanakoishi wajinga. Mjengo wetu uko tofaut by far na nyumba zingine zote.

Wale wapuuzi walishindwa kujua kuwa kufanikiwa hakuna uchawi bali janja janja na timing kwenye fursa, basi yenyewe yakajiongoza eti hapa ni masonic na makafara tu.

Mwanzoni niliwapuuza ila badae kuna kitu ilitokea nikaona hawa wapuuzi kuna siku wanaweza wakajiunga wakanichoma mle ndani wakiamin mie natoa damu za watu kafara.Ikabidi niondoke.

Yupo mfanyakazi wangu alinichana Live kuwa "boss najua huwez kutoa siri zako ila siwez amini umefika hapa ulipofika bila ndumba kuhusika"

Mimi siamini kama kuna mtu yeyote anayeweza fanya kitu digits zangu bank zikaongezeka. Siku zote ninaamini katika kutumia akili ktk kutafuta.

Pia siamini kama kuna mjinga yeyote anayeweza kuniloga kitu kibaya kikanipata sbb havifanyi kazi. Mnadanganywa tu.

UCHAWI NA UGANGA NI UONGO havipo na havifanyi kazi. Mpo wengi humu mnaoamini hayo matakataka sasa nawapeni ofa ya 25M kwa atakayeweza kuniloga.

Nifanyeni chochote kibaya na mhakikishe hamnisamehi mpaka nije hapa niandike uzi wa kuomba msamaha na kukiri kuwa kweli uchawi upo nimelogwa na pia nilipe hiyo 25M kwa mchawi wangu.

Mkitaka niwatukane babu na bibi zenu wanaoogopwa kwa uchawi ili hasira ziwapande mniloge vizuri semeni. Nitawavurumishia mitusi hao babu/bibi zenu hamjapata kuona. Nitawatukana na kuwakashifu ma hawatanifanya chochote wajinga hao[emoji23]

Haya kazi kwenu.

NILOGENI

UPDATE:Mnaotaka jina ili mniloge siwezi kuwapa sbb ua Privacy ila nawawekeeni picha yangu muitumie kuniloga. Kateni mikono,vidole,nifanyeni niwe na miguu 4 kama ng'ombe vyovyote.

View attachment 2615624
Jidanganye,uchawi hutumia majini ambayo husafiri.Na pia unalogeka ukiwa na sababu mda mwingine,Mara nyingi uchawi usio wa kawaida ni kuharibiana nyota,familia za kiafrika hatupendani,watakuonea wivu ili wakuibie nyota.
 
Habari za kulogana ni ujinga tu.

Na ujinga huu unaanza kuthibitika mnapoanza kuomba majina, mnathibitisha uchawi wenu hauwezi kujua watu majina.

Mngekuwa na uchawi kweli, mngenuiza tu kwenye uchawi mpewe jina la Kiranga, lingekuja kamili mpaka fingerprint mngepata.
uchawi/mchawi siyo kujua kila kitu acheni hayo mawazo, uchawi ni kufanya/kujua jambo tofauti na kawaida na huwa ni kwa msaada wa mashetani ya kijini.

huyo mchawi anachagua jambo maalumu analolitaka kisha shetani anamsaidia chap. na wala siyo kila jambo atakalotaka basi shetani ataweza kumfanyia/kulifanikisha laa! kuna mengine anapigwa puu tu ndomana mnahimizwa kujiweka safi mda wote, kujiombea dua na kuepuka mambo maovu mda wote kwani ndiyo yanayofanya shetani adunde akikujia

mfano mganga anataka kujua fulani yupoje basi shetani atakwenda kwa spidi ya mwanga kumpeleleza huyo mtu yupoje na kwa vile hiyo siyo kazi kubwa kwa haraka tu analeta majibu. watu kwa kutokuelewa wanabaki kumsifu tu mganga anajua siri kumbe hawajui kwamba kajuzwa na shetani.

wakina kiranga wao wanadhani mtu akiwa mchawi basi anaamua tu lolote na likawezekana mfano kuhack akaunt za fedha, aende popote atakapo kwa muda wowote, anajua mtu anachowaza, ajue kila siri... no huyo sasa atakuwa siyo mchawi tena bali ni mwenyezimungu


hayo mambo yote wanayofanya wachawi na mashetani yao hayafanikiwi ila kwa masharti magumu magumu wanayowekeana wao kwa wao na masharti hayo yanawagharimu/yanawadhuru hata wao wenyewe kwahiyo siyo rahisi kama mnavyodhani.

twende kwa mfano wa muvi tu mtu anataka mali fulani imefungiwa sehemu anaambiwa ramani ya kufika huko anayo fulani na fulani yupo nchi za mbali huko kisha ramani inaonesha kuna sehemu ukifika utakuta vizuizi fulani lets say wanyama wakali inabidi uende na kitu fulani kisha kuna walinzi kadhaa mbele itabidi uende na kitambulisho fulani ndo wakupokee maana yake inabidi ukakipate hiko nacho... mbele huko inabidi uwe na almasi ya kukatia kufuli nk. kwahiyo unakuta mission inahitaji pesa nyingi sana, nguvu za mwili, watu wengi na muhimu, akili nyingi, muda mwingi wa kutosha nk.

kwahiyo mtu akisema nipe jina la mama yako nikuroge ukimwambia alitafute mwenyewe maana yake unampa mission ndani ya mission. au wale wanaosema kwanini mchawi asiweze kujua na kukwapua fedha benki, kwanini asiweze kusafiri popote atakapo na kadhalika hawajui kwamba yote hayo yanagharimu? unakuta jambo lingine unaambiwa kulifanikisha itakubidi utumie miaka 20 sasa wakati huo wewe una 45 ndo unakuta mtu anakata tamaa maana hilo ni moja tu wakati inatakiwa likamilike hilo ndo likamilishe na mengine kama manne mbele
 
uchawi/mchawi siyo kujua kila kitu acheni hayo mawazo, uchawi ni kufanya/kujua jambo tofauti na kawaida na huwa ni kwa msaada wa mashetani ya kijini.

huyo mchawi anachagua jambo maalumu analolitaka kisha shetani anamsaidia chap. na wala siyo kila jambo atakalotaka basi shetani ataweza kumfanyia/kulifanikisha laa! kuna mengine anapigwa puu tu ndomana mnahimizwa kujiweka safi mda wote, kujiombea dua na kuepuka mambo maovu mda wote kwani ndiyo yanayofanya shetani adunde akikujia

mfano mganga anataka kujua fulani yupoje basi shetani atakwenda kwa spidi ya mwanga kumpeleleza huyo mtu yupoje na kwa vile hiyo siyo kazi kubwa kwa haraka tu analeta majibu. watu kwa kutokuelewa wanabaki kumsifu tu mganga anajua siri kumbe hawajui kwamba kajuzwa na shetani.

wakina kiranga wao wanadhani mtu akiwa mchawi basi anaamua tu lolote na likawezekana mfano kuhack akaunt za fedha, aende popote atakapo kwa muda wowote, anajua mtu anachowaza, ajue kila siri... no huyo sasa atakuwa siyo mchawi tena bali ni mwenyezimungu


hayo mambo yote wanayofanya wachawi na mashetani yao hayafanikiwi ila kwa masharti magumu magumu wanayowekeana wao kwa wao na masharti hayo yanawagharimu/yanawadhuru hata wao wenyewe kwahiyo siyo rahisi kama mnavyodhani.

twende kwa mfano wa muvi tu mtu anataka mali fulani imefungiwa sehemu anaambiwa ramani ya kufika huko anayo fulani na fulani yupo nchi za mbali huko kisha ramani inaonesha kuna sehemu ukifika utakuta vizuizi fulani lets say wanyama wakali inabidi uende na kitu fulani kisha kuna walinzi kadhaa mbele itabidi uende na kitambulisho fulani ndo wakupokee maana yake inabidi ukakipate hiko nacho... mbele huko inabidi uwe na almasi ya kukatia kufuli nk. kwahiyo unakuta mission inahitaji pesa nyingi sana, nguvu za mwili, watu wengi na muhimu, akili nyingi, muda mwingi wa kutosha nk.

kwahiyo mtu akisema nipe jina la mama yako nikuroge ukimwambia alitafute mwenyewe maana yake unampa mission ndani ya mission. au wale wanaosema kwanini mchawi asiweze kujua na kukwapua fedha benki, kwanini asiweze kusafiri popote atakapo na kadhalika hawajui kwamba yote hayo yanagharimu? unakuta jambo lingine unaambiwa kulifanikisha itakubidi utumie miaka 20 sasa wakati huo wewe una 45 ndo unakuta mtu anakata tamaa maana hilo ni moja tu wakati inatakiwa likamilike hilo ndo likamilishe na mengine kama manne mbele
Shetani hajawai kuwepo, hizo ni story kama story nyingine tu
 
Back
Top Bottom