Baada ya Kauli ya Rais Samia, Waliomtukana Dkt. Bashiru wamuombe radhi

Baada ya Kauli ya Rais Samia, Waliomtukana Dkt. Bashiru wamuombe radhi

Kiuhalisia mimi sijaona chochote cha ziada alichokifanya huyu bibi tokea awe Rais kinachopelekea baadhi ya wapumbavu kusema; eti, "anaupiga mwingi".

Ukweli ni kwamba huyu bibi ni Rais dhaifu kabisa kuwahi kutokea katika taifa hili.
 
Wana-CCM kindakindaki na machawa ambao mlijikita katika kumshambulia Dkt. Bashiru kwa kauli yake kwa Taasisi ya Wakulima juu kumsifia sifia Rais badala ya kutimiza malengo yao ya kutetea wakulima wamepigwa stop.

Akizungumza katika kufungua mkutano wa UWT Rais aliwaonya na kukataa mabango ya "TUNAKWENDA NA SAMIA" au "SAMIA ANAUPIGA MWINGI" na kusema sifa ni za Serikali sio mtu na waache mara moja.

Hii maana yake aliyosema Bashiru yalikuwa sahihi.

Je, hii aibu wanaibebaje hao wanafiki? Yuko wapi Lusinde au Msukuma waliomshambulia Bashiru? Yuko wapi Amos Makalla na wengine? AIBU KUBWA na walipaswa kusimama na kumuomba radhi Dkt. Bashiru.
Lakini kiukweli si Rais Anaupiga mwingi kweli au?
 
Kiuhalisia mimi sijaona chochote cha ziada alichokifanya huyu bibi tokea awe Rais kinachopelekea baadhi ya wapumbavu kusema; eti, "anaupiga mwingi".

Ukweli ni kwamba huyu bibi ni Rais dhaifu kabisa kuwahi kutokea katika taifa hili.
Nadhani wewe ndio mpumbavu,una hakika Hakuna alichofanya?
 
Walizidi kusifu na kuabudu ila yeye mama kawashtukia na sifa zao za kinafiki wamekatishwa tamaa sijui itakuwaje.
 
[emoji30][emoji30]
20221127_091458.jpg
 
Walikuwepo chawa wengi tu, hata Fatma Karume nae ujumbe umemfikie popote alipo.

Rais anastahili. kupongezwa kwa kugoma kufuata mkumbo wa wajinga wengi.
 
Kumezuka kundi la watu kazi yao kubwa ni kumsifia Rais Samia hata pasipostahili, kundi hili kwa lugha sahihi ni machawa. Machawa hawa wapo kwa ajili ya kuishi kwa ujanja ujanja wa kumsifia Rais hata pasipostahili mpaka inakuwa kero kwa mhusika.

Kauli mbiu yao ni “Mama anaupiga mwingi." Juzi wakati wa ufunguzi wa mkutano wa UWT taifa Rais Samia kachukizwa na sifa hizo hivyo, kwa taarifa yenu mama hataki!

Watanzania tunatakiwa kumpongeza Rais na siyo kumsifu siku zote, sifa na utukufu hupewa Mungu na siyo binadamu. Machawa wamekuwa wanampa sifa Rais za kinafiki na ndiyo maana Mama hataki sifa zenu.

Hongera sana Rais Samia kwa kuchukizwa na sifa za kinafiki, kumbuka hao hao wanaojifanya kukusifu ndiyo hao hao kesho watakusema vibaya, machawa ni wanafiki sana.

View attachment 2430489
Wapi Lucas Mwashambwa?????
 
Serikali yake inafanya majukumu ya kiserikali ya kawaida, sasa ukisema Samia anaupiga mwingi ndio hapo wengine wanajiuliza kipo cha ziada anachofanya Samia chenye kufanya mseme anaupiga mwingi?
Usibishane na hawa watu! Make utadhani Kuna serikali mbili ziko madarakani au kuna nchi mbili zinashindana! Hawa sio watu Ni mediocre
 
Back
Top Bottom