Baada ya Kifo cha Rais Magufuli: Nani anafaa kuwa Makamu wa Rais Tanzania?
Kabudi hafai

Wengine ambao hawafai,Mwigulu,Jafo wizara imemzidi,Ndumbaro,Jenesta,Dr Gwajima huyu aliamua kuacha taaluma akatufanya tupige dua na kula mitishamba,ambayo haijathibitishwa popote Ili kutibu corona.
 
Sawa ila mwambieni asiwe anaongea kama anafoka yeye ni diplomatic figure.
 
Unamkusudia yule muokotwa jalalan????
Napendekeza Palamagamba Kabudi afanywe Makamu wa Rais kwa sababu zifuatazo.

Kwanza Kabudi ana maono. Pili anajiamini kama JPM.Tatu elimu inakidhi viwango

Nne na mwisho utendaji kazi wake sina mashaka nao. Hakika atainyoosha nchi hii akiwa na mama jembe Kiboko ya Vidomodomo.

#hayana chama maendeleo!![emoji23]
 
kwenye elimu achana nako elimu ya kufanya research za sheria haikusaidii chochote kwenye uongozi! Hii ni kujidanganya tu kwa waliosoma😂. Lakini atafaa umakamu kwasababu ya uzalendo
Huyu kadaharauliwa mpaka na msukuma mtu aliyefika yarasa la nne!! Vitendo vyake vay sycophancy vimefanya wasomi wasiwe na heshima katika jamii!!
 
Makamba sio mtendaji ameshawekwa kwenye wizara kadhaa hakuna cha maana alichofanya, wanaompenda sijui hutumia kigezo gani kutaka apewe madaraka ya juu serikalini, alibebwa na Magufuli hakubebeka matokeo yake akaishia kumchora kwenye vi cartoon vyake twitter.

Huyu mtu kwangu namuona kama kijana aliejikuta kwenye familia ya mkubwa hivyo hafanyi jitihada zozote kusogea mbele zaidi, anaamini na kuaminishwa na fans wake jina lake linatosha kumpa madaraka ayatakayo, kama CCM wakifanya hivyo watafanya Magufuli akumbukwe mapema zaidi, hili taifa kwasasa linahitaji watendaji, sio viongozi wa mazoea.
 
Sio top 3? Yaani kati ya hao wa 3 mmoja awe tofauti na wenzie!
 
Hebu turudi kuleee enzi za kusoma hasi na chanya.
Hasi+hasi=?
Chanya+chanya=?
Hasi-chanya?=?

Sasa ipo hivi piga ua garagaza makamo wa raisi ni lazima atofautiane na raisi katika vigezo vifuatavyo.
1.Jinsi/jinsia
Hapo lazima awe wa kiume
2. Dini
Hapo lazima atofautiane Na samia. Ikiwa samia anaingia msikitini basi lazima makamu wake awe mtu wa kuingia kanisani na kinyumechake ndio ukweli wenyewe.

Sasa nimepitia mijadala mbalimbali naona ya kwamba January makamba anatajwa kushika nafasi hiyo hilo naomba asahau.

Kuna mtu anaitwa bashiru huyo nae asahau, vigezo hapo juu vinamtupilia mbali.
Majaliwa nae vilevile hata baada ya baraza kuvunjwa(ikitokea sio waziri mkuu) naye hawezi kuwa makamu.

Utaniuliza nimepekua katiba gani kuja na maelezo haya nami nitakujibu hakuna katiba niliyopekua na pengine hayo hayamo, ila uongozi wa kitanzania tangu anzi na enzi umeangukia ktk vigezo hapo juu.
Usiku mwema poleni niliowakera.

Nipo tayari kuja kuomba radhi endapo moja ya majina hapo juu yakipitishwa.
Mbona Kikwete na Mwinyi makamu wake wote walikuwa waislamu na wanaume hawakuwa jinsia tofauti
 
Napendekeza Palamagamba Kabudi afanywe Makamu wa Rais kwa sababu zifuatazo.

Kwanza Kabudi ana maono. Pili anajiamini kama JPM.Tatu elimu inakidhi viwango

Nne na mwisho utendaji kazi wake sina mashaka nao. Hakika atainyoosha nchi hii akiwa na mama jembe Kiboko ya Vidomodomo.

#hayana chama maendeleo!![emoji23]
kwenye elimu na uweledi yuko vizuri.
Ila wasiwasi wangu ni uzoefu wake kwenye tasnia ya siasa.
Ana uwezo gani wa kupambana na wakongwe wa kwenye siasa kama wakina bernard membe na wakina lowasa,mbowe,tundulissu,kinana,makamba,nape maana hawa ni wakongwe na CCM ni kama nyumbani kwao.
 
Mbona kikwete na mwinyi makamu wake wote walikuwa waislamu na wanaume hawakuwa jinsia tofauti
Ahsante kwa fact hii tuendelee kuvuta subra. Jinsi awamu hii ilivyo naona kama mambo yamebadilika hivi.
 
Back
Top Bottom