Kabudi hafai

Wengine ambao hawafai,Mwigulu,Jafo wizara imemzidi,Ndumbaro,Jenesta,Dr Gwajima huyu aliamua kuacha taaluma akatufanya tupige dua na kula mitishamba,ambayo haijathibitishwa popote Ili kutibu corona.
 
Sawa ila mwambieni asiwe anaongea kama anafoka yeye ni diplomatic figure.
 
Unamkusudia yule muokotwa jalalan????
 
kwenye elimu achana nako elimu ya kufanya research za sheria haikusaidii chochote kwenye uongozi! Hii ni kujidanganya tu kwa waliosoma😂. Lakini atafaa umakamu kwasababu ya uzalendo
Huyu kadaharauliwa mpaka na msukuma mtu aliyefika yarasa la nne!! Vitendo vyake vay sycophancy vimefanya wasomi wasiwe na heshima katika jamii!!
 
Makamba sio mtendaji ameshawekwa kwenye wizara kadhaa hakuna cha maana alichofanya, wanaompenda sijui hutumia kigezo gani kutaka apewe madaraka ya juu serikalini, alibebwa na Magufuli hakubebeka matokeo yake akaishia kumchora kwenye vi cartoon vyake twitter.

Huyu mtu kwangu namuona kama kijana aliejikuta kwenye familia ya mkubwa hivyo hafanyi jitihada zozote kusogea mbele zaidi, anaamini na kuaminishwa na fans wake jina lake linatosha kumpa madaraka ayatakayo, kama CCM wakifanya hivyo watafanya Magufuli akumbukwe mapema zaidi, hili taifa kwasasa linahitaji watendaji, sio viongozi wa mazoea.
 
Sio top 3? Yaani kati ya hao wa 3 mmoja awe tofauti na wenzie!
 
Mbona Kikwete na Mwinyi makamu wake wote walikuwa waislamu na wanaume hawakuwa jinsia tofauti
 
kwenye elimu na uweledi yuko vizuri.
Ila wasiwasi wangu ni uzoefu wake kwenye tasnia ya siasa.
Ana uwezo gani wa kupambana na wakongwe wa kwenye siasa kama wakina bernard membe na wakina lowasa,mbowe,tundulissu,kinana,makamba,nape maana hawa ni wakongwe na CCM ni kama nyumbani kwao.
 
Mbona kikwete na mwinyi makamu wake wote walikuwa waislamu na wanaume hawakuwa jinsia tofauti
Ahsante kwa fact hii tuendelee kuvuta subra. Jinsi awamu hii ilivyo naona kama mambo yamebadilika hivi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…