Baada ya Kifo cha Rais Magufuli: Nani anafaa kuwa Makamu wa Rais Tanzania?
Bila shaka kwa nafasi hii watu hawalali, Lumumba na viunga vyake, baraza la Mawaziri nalo lipo tumbo joto maana lazima pangua pangua itakuwepo, kwa nafasi ya VP hapo January ndio chaguo la mama, kiufupi CCM ya asilia inarudi, MATAGA mwisho rasmi umefika.
Una uhakika mzee ya kwamba January ndiyo chaguo la mama ?
 
Poleni sana Watanzania wenzangu kwa kuondokewa na Rais wetu kipenzi. Mungu amlaze mahali pema peponi, Amina.

Kutokana na hali ilivyo, automatically Mama Samia aliyekuwa Makamu wa Rais ndio anakuwa Rais kamili kwa kipindi cha miaka minne iliyobaki.

Je, nani anayefaa kuwa Makamu wa Rais ukizingatia kuwa lazima atoke Bara kwani Mama Samia ametokea Zanzibar?

R.I.P Magufuli.
Doctor Slaa anafaa kabisa kuvaa viatu vya Magu, mtizamo wangu angepewa u makamu wa Rais ange endana na matakwa yetu, kwa upande Mwingine kassim majaliwa yupo vzr Sana Ila sitaki kumuondoa pale Kati maana tunahitaji mtu makini wa kusukuma jahazi Kama waziri mkuu
 
Sema kwakuwa kazi yenyewe ya umakamu wa rais kwa hapa bongo haina issue zaidi ya kukata utepe kwenye zinduzi basi. Hata awekwe nani kwa katiba hii atakuwa hana nguvu kimamlaka.
Makamu wa rais ana umuhimu mkubwa sana ila hapa bongo kwenu ndo mnam-profile kidogo kidogo
 
Hivi tunamchagua mtu kwa ajili ya uwezo wake au kwa ajili ya dini yake ?
Kigezo ni uwezo lakini vipi linapokuja kwamba wapo wenye uwezo katika dini zote hizo mbili kubwa?

Kama kuna Wakristo wengi wenye uwezo na hawapo katika nafasi zote kubwa za juu kwanini uendelee kuwaweka Waislam ambao tayari wameshikilia nafasi zote za juu kwa bara na visiwani?
 
Imfikie Mstaafu Jakaya Kikwete popote alipo,
Salaam Baba habari ya MSOGA?
Nakuletea salaam nyingi toka kwa Wananzengo, Pole sana kwa Msiba wa Rais MAGUFULI, Hakika hatutasahau kazi na historia yake katika Taifa letu.

Ni wiki sasa Tangu tupate Msiba huu mkubwa kwa Taifa letu, wiki hii pia tunatarajia kumstiri mpendwa wetu Kijijini kwao Chato, Kazi ya Bwana haina Makosa japo bado ni ngumu kuzoea.

Wiki hii pia tumempata Rais Mpya, Mama Samia Suluhu Hassan, yote kheri tunamshukuru Mungu kwa kila jambo.

Wakati tunasubilia kuzika huko chato na maombolezo ya siku 21, yameanza kusikika maneno na hakika minong'ono kuwa WEWE Jakaya Kikwete sasa unajiandaa kurudi Ikulu kwa Mlango wa nyuma kupitia neno maarufu "USHAURI".

Hakuna mtu mwenye mashaka juu ya uwezo wako Baba Kikwete, hakuna mtu asiyejua kuwa wewe ndie tunayekutegemea kumshauri Rais wetu Mama Samia, Lakini chondechonde usimpotoshe akakosea ingali ASUBUHI kabla ya Matanga kuisha.

Mama Samia kwasasa baada ya kuapa na baada ya Mazishi anatakiwa kuitisha Bunge na kupeleka jina la Makamu wa Rais baada ya kushauriana na Chama chake (CCM).
Hapa pia anatakiwa kumchagua Waziri Mkuu Mpya ( japo watu bado wanampigia chapuo Majaliwa aendelee).

Minong'ono inayotanda kuwa wewe Baba Kikwete ndie unaepanga Safu hii na kumshauri Mama Samia atekeleze, Hofu ya wengi ni kuwa unaweza kumpotosha Mama yetu na likawa kosa la kwanza la kuwavunja Moyo Watanzania katika kipindi hiki kigumu cha kuhitaji Matumaini na kutiwa Moyo.

Chondechonde Baba Kikwete usimshauri vibaya Mama Samia afanye makosa Asubuhi maana atamaliza vibaya Jioni.

Yapo mambo hayajaandikwa katika Katiba yetu ya JMT lakini yanatekelezwa kwaajili ya mtangamano wa Taifa letu, Mfano anayetakiwa kuwa Makamu wetu wa Rais kwasasa LAZIMA awe Mkiristo tena anayetoka Tanzania Bara. Katika hili yapo Majina mengi yanatajwa ambayo yanahusishwa na wewe kupenyeza majina hayo kwa Rais Mama Samia kuwa hawa ndio wanaofaa, Mshauri vizuri Rais wetu usimpotoshe na usimuingizie Wana Mtandao watamvurugia uongozi na Itawakatisha Tamaa Watanzania ambao wanayapenda Maendeleo.

Baba Kikwete, Nakukumbusha Mwaka 1985 wakati Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere anaachia Madaraka na kumkabidhi Mzee Mwinyi (anayetoka Zanzibar) Mzee Ruksa alichagua Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mzee Msuya kumsaidia Mambo ya Tanzania Bara, Baadae alimchagua Mzee Warioba kumsaidia mambo ya Tanzania Bara, Baadae alimchagua Mzee Malechela kumsaidia Mambo ya Tanzania Bara na kwa Hakika mambo yalienda vizuri.

Umuhimu wa kumchagua Makamu wa Rais Mtu mzima mwenye uzoefu wa Nchi mwenye msimamo asiyeyumbishwa na anayeweza kumshauri vizuri Rais Samia Suluhu Hassan lazima lipewe kipaumbele na kuzingatiwa, Hapa ndipo penye Hekima kubwa bila mihemko, makundi na mitandao ya wasaka urais 2025 au 2030. Baba Jakaya uwe Makini maana lawama utazibeba wewe na utamfanya Rais ashindwe kumudu kazi yake vyema, mpatie nafasi apendekeze MTU mwenye uzoefu na uwezo wa kufanya kazi mwenye maadili na anayekubalika Tanzania BARA, Mkiristo anaweza kuunganisha viongozi wa dini na anayeza kumsaidia Rais katika Majukumu ya Urais muda wote.

Baba Kikwete najua kwasasa uko katika maombolezo lakini upatapo barua hii tafadhali pokea salaamu hizi na ujue kuwa watu wanajua kuwa ushauri wako unaweza kuwavunja Moyo Watanzania au kuwatia Moyo Watanzania katika kipindi hiki cha msiba mzito tulionao.

Yapo majina yanatajwa kuwa yanaweza kupewa kipaumbele kama Mizengo Pinda, Martine Shigela, Antony Mtaka, Palamagamba Kabudi, Stephen Wasira, Emmanuel Nchimbi na Wiliam Lukuvi. Pamoja na Wazoefu hawa kutajwatajwa lakini tunaomba Mama SAMIA aachwe ama ashauriwe vizuri kupata Makamu wa Rais anayekubalika kwa Watu, Bunge na Jeshi letu.

Baada ya Mchakato wa kuunda serikali kuisha, Umshauri Rais wetu Mama Samia kuweka safu nzuri ya Chama kuanzia Makamu Mkiti Imara, Katibu Mkuu Imara, Mwenezi Imara na Idara za chama zipate viongozi shupavu, Ikumbukwe kuwa Chama Imara huzaa Serikali Imara na Chama legelege huzaa Serikali legelege. Mkiti mpya wa Chama Mama Samia usimpotoshe akaunda safu za Kimtandao Hakika zitawakatisha Tamaa wanachama ambao wana IMANI KUBWA na chama chao.

Wasalaam Baba Kikwete.

Mungu ibariki Tanzania.
Suala la dini lisipewe nafasi.
Kwani wanaenda kuhubiri huko?
Tena waislamu wangepewa nafasi zote ili kupunguza malalamiko
 
Nafasi ya VP wapewe wakongwe kama kina Mkuchika, Mathias Chikawe, Andrew Chenge, Abdul Kinana, Rose Migiro, Mama Tibaijuka, Anna S. Makinda, Balozi Ombeni Sefue, Wiliam Lukuvi, Mark Mwandosya, Balozi Kagasheki, Bernard Membe, Adadi Rajabu, Juma Mwapachu(Sio Baker, Baker ame RIP), Mama Sitta, Christopher Chiza, Balozi Philip Marmo, Lut. Gen. Samwel Ndomba, Lut. Gen. Abdulrahman Shimbo, Lut. Gen James Mwakibolwa, Gen. Davis Mwamnyange, Harrison Mwakyembe, David Mwakyusa, Job Ndugai, Dr. W. Slaa, Stephen Wasira; Orodha ni ndefu.
Hii nafasi haina ushawishi wowote.
Ni ya washika mikasi kuzindua miradi kama alivyokuwa akifanya Gharib Bilal
 
Kigezo ni uwezo lakini vipi linapokuja kwamba wapo wenye uwezo katika dini zote hizo mbili kubwa?

Kama kuna Wakristo wengi wenye uwezo na hawapo katika nafasi zote kubwa za juu kwanini uendelee kuwaweka Waislam ambao tayari wameshikilia nafasi zote za juu kwa bara na visiwani?
Kigezo cha kuwa VPURT haijawahi kuwa uwezo. Kigezo kikubwa ni upande wa Muungano anaotokea na busara za kumsaidia Rais bila kumhujumu au kutamani kuwa na mamlaka ya Rais au Maarufu kuliko Rais au kutaka kumrithi Rais.
Hivyo ndio vigezo. Na ndio maana nashawishi nafasi hiyo apewe veteran mojawapo.
 
I wish vice president awe wa kanda ya ziwa au wa pwani/Tanga


🇦🇷🇦🇷🇦🇷🔥
Ninyi ndio wale wenye roho ya mgawanyo. Je, kanda ya Magharibi nao wakisema they wish atokee Kigoma au Katavi? Wa Mtwara nao? Hili ni Taifa moja lisilo na vipande. Hata hiyo kanda ya ziwa ina kibao kama ukianza kutambua viongozi kwa kanda zao.
 
Back
Top Bottom