Baada ya kimya kingi nami nitie neno DP World, Mtazamo wangu ni Tofauti kidogo

Kwa ufupi ni kwamba DP World wamekuja kwa njia ya uani kuzuia Bagamoyo Port Project...

Na hii issue ipo Serikalini wanajua...
Alipofariki Magufuli hii project ilirudi mezani na walishaanza kurejesha mazungumzo na China na Oman kujenga Bandari kubwa sana ukanda huu wa Africa...

Kumbuka malighafi nyingi zinatoka Uarabuni na Asia kuja Africa...

Sasa Dubai anapanua Bandari yake iwe ya mfano... Kwahiyo malighafi nyingi za Uarabuni na Asia zitapitia Dubai kwanza kisha kusambazwa Africa...

Kwahiyo DP World wana ushirika mkubwa na US... Hawakutaka kamwe Bagamoyo Project Isimame...

Ndio maana utaona mkataba badala hata ya kuwa Dar Port alone... Wanasema bandari zoteeee.... Na ukitaka kujenga Port mpya Baharini omba Ruhusa Dubai... Kitu ambacho itakuwa ni ngumu sana...

Kiufupi tumeshasaini toka mwaka jana... Na kutoka huko kuna kazi ya ziada kama sio kulipa mabilioni ya dola katika mahakama za kimataifa
 
Tangu nimekufahamu, leo umeandika kwa kutuliza akili,, Naona umeacha kunywa LUBISI,,!

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Kuna kipengele muhimu sana cha DP world wanawekeza how much kwenye uwekezaji wao sababu ni
1.Tayari tumeshawekeza zaidi ya Tril 1.4 pale JPM alitoa,
2.Kama ni uwekezaji wa $400m ni pesa ambayo hata sisi kama Taifa tunaweza kuiweka kisha tukakodi kampuni ya kuendesha tu Bandari kwani tayari miaka miwili iliyopita tumeshaweka pesa zaidi ya iyo inayosemekana mwekezaji anakuja kuweka (kama sio kuendesha tu maana tayari tumeshaweka iyo ela pale )
 
Kama na wao hawakubakiani na huu "Umangungo" jee!!??
 
Shida Moja kubwa ni kwamba kwa Nini huo mkataba unahusisha bandari zote za maziwa na bahari?
Pia mkataba hauoneshi ukomo wake kwa mantiki hiyo watu tunaona tushakaribisha koloni hivi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…