Baada ya kufanyiwa CT-Scan ya tumbo, hali imebadilika na kuwa mbaya

Baada ya kufanyiwa CT-Scan ya tumbo, hali imebadilika na kuwa mbaya

Wanapokea sema ukienda nenda kama ndo umeanza tiba kwa mara ya kwanza ila ukisha kutana na dr ndo umweleze hatua zote ulizopitia
 
Mpaka sasa nimeshafanyiwa vipimo 10,hakuna ambacho kimeshaonyesha ninaumwa nini zaidi ya hali kuzidi kuwa mbaya.Kila siku mimi ni tumbo,tumbo,tumbo.Halina maumivu isipokuwa machache hasa baada ya kula na tumbo kujaa kama mpira unaosubir mechi.
Punguza maneno au unafanya maigizo
 
Punguza maneno au unafanya maigizo
Maigizo kwenye ugonjwa?Tatizo mimi siwezi kuficha vile ninavyojihisi.Huo ndio ukweli tumbo linanijaa sana,ushuzi na kinyesi kinachotoka harufu yake hata wewe unayesema ni maigizo huwezi kuistahimili!!!
 
Nenda hindu mandal omba kukutana na dr wa matumbo ni muhindi nna imani atakusaidia coz mi alinisaidia sana. Pole kwa matatizo
Nadhani unamaanisha Dr. Kaushik. Ni kweli huyu ni mtaalam sana anaweza kuea msaada. Lakini pia ushauri wangu ni kuwa choo kinachokuwa na harufu kali mara nyingi ni case ya minyoo. Hebu tafuta wataalam wa magonjwa ya minyoo nao wakushauri. Pole sana ndg.
Ndo hiyo hiyo endoscopy, Majibu yalikuwaje? Ila kwanini walikuingiza kwenye haja kubwa? Uliogopa kuingizwa mdomoni?

Kipimo hiki binafsi niliwahi kuandikiwa ila kuna daktar mmoja akanishauri nisifanye coz kitaniongezea matatizo hasa kuumizwa kuta za tumbo niliogopa sana

Unadhani kinachofanya kuendelea KWA hari mbaya ni hiyo Scan ulofanyiwa au ugojwa ndgu Mungu atakusaidia upone ila ponguza siasa
 
Tafuta dawa ya asili inaitwa Aswat, ila utaharisha sana ila baada ya hapo unapona kabisa. Nenda kwenye misikiti humo wanzo dawa hizo afu utaleta mrejesho hapa. Ila ukiziendekeza hizo hospitali ujue unakitafuta kifo mapema sana.
Ni dawa nzuri?
 
Nadhani unamaanisha Dr. Kaushik. Ni kweli huyu ni mtaalam sana anaweza kuea msaada. Lakini pia ushauri wangu ni kuwa choo kinachokuwa na harufu kali mara nyingi ni case ya minyoo. Hebu tafuta wataalam wa magonjwa ya minyoo nao wakushauri. Pole sana ndg.
Asante kwa ushauri,nitaufanyia kazi!
 
Wanajf ni siku ya tatu leo toka nifanyiwe ct scan ya tumbo. Ajabu tumbo sasa limebadilika. Linawaka moto.Kiuno sasa kinauma sana. Tumbo linaunguruma sana utafikiri vyura vinafanya mazoezi.

Kelele zinasikika hadi nje ya tumbo. Mgongo una maumivu mpaka leo.Kichwa ndiyo usiseme. Sasa nimekuwa mchovu mno kiasi cha kushindwa kufanya hata yale masuala yetu ya usiku ya baba na mama. Jamani nisaidieni tatizo ni kipimo au ni maradhi yanayonisumbua ambayo bado sijayagundua?

Msaada tafadhari
Nawashukuru sana jf kwa mawazo na ushauri wenu.CT SCAN YANGU IMEONYESHA KUTANUKA KWA MISHIPA YANGU YA TUMBO.Dr. KANIAMBIA UGONJWA ULIOSABABISHA HILO BADO HAUJAJULIKANA.NIMEPEWA DAWA ZA KUTUMIA MWEZI MZIMA NDIYO NIRUDI HOSPITAL.
 
Tafuta dawa ya asili inaitwa Aswat, ila utaharisha sana ila baada ya hapo unapona kabisa.

Nenda kwenye misikiti humo wanzo dawa hizo afu utaleta mrejesho hapa. Ila ukiziendekeza hizo hospitali ujue unakitafuta kifo mapema sana.
Aswat inatibu nini?
 
Ndo hiyo hiyo endoscopy, Majibu yalikuwaje? Ila kwanini walikuingiza kwenye haja kubwa? Uliogopa kuingizwa mdomoni?
Hiyo aliyofanyiwa ni colonoscopy na si endoscopy. Inategemea ma maelezo yake daktari alifikia mwafaka wa kuangalia sehemu ya chini ya njia ya chakula.
 
Vp mkuu unaendeleaje tumbo halisumbui tena
Hali bado,rufaa Mbeya wanadai huenda nina vidonda vya tumbo.Toka 2017 walinianzishia clinic ya medicine ndipo nahudhuria hadi leo dawa wanazonipa ni nyingi sana kiasi kwamba nimeamua kutozimeza kwa sababu madaktari wenyewe wanapingana.Hali bado ni tete
 
Wanajf ni siku ya tatu leo toka nifanyiwe ct scan ya tumbo. Ajabu tumbo sasa limebadilika. Linawaka moto.Kiuno sasa kinauma sana. Tumbo linaunguruma sana utafikiri vyura vinafanya mazoezi.

Kelele zinasikika hadi nje ya tumbo. Mgongo una maumivu mpaka leo.Kichwa ndiyo usiseme. Sasa nimekuwa mchovu mno kiasi cha kushindwa kufanya hata yale masuala yetu ya usiku ya baba na mama. Jamani nisaidieni tatizo ni kipimo au ni maradhi yanayonisumbua ambayo bado sijayagundua?

Msaada tafadhari
Pole kwa kuumwa,

Kuna uwezekano tatizo la msingi lipo, lakini pia ukawa unapata tatizo kutokana na madhira ya dawa na vipimo vingine ulivyopitia au kukawa na matatito ya kurithi ambayo si ya kupata tiba timilifu/yakaisha. Pia, mfumo wa maisha ukayafanya matatizo yako kuwa yanajitokeza zaidi.

Kwa maelezo yako kuna vitu najifunza na naomba pia ujifunze:

1: Maelezo yako ndo mwanzo wa tiba yako sahihi.

Kwa mtoa huduma yoyote ni vyema kuanza na basic, jinsi ugonjwa ulivyoanza. Ikibidi andika dalili zako zote/maelezo kabla ya kwenda kwa mtoa hudima. Usiwe na haraka ya kumaliza kujieleza.

2: Eleza kwa ufasaha jinsi tumbo linavyouma, sehemu husika.

3: Eleza mahusiano na njaa, chakula na upataji wako wa choo na jinsi choo kinavyokuwa.

4: Eleza kama kwenye familia ndugu vs wazazi wana tatizo kama lako.

5: Eleza aina ya dawa na vipimo ulivyowahi kufanya na majibu kama unayo au unayafahamu.

6: Jibu maswali ya mtoa huduma vyema bila kujali kama kwa mtizamo wako yatamsaidia kujua tatizo au hapana.
 
Pole kwa kuumwa,

Kuna uwezekano tatizo la msingi lipo, lakini pia ukawa unapata tatizo kutokana na madhira ya dawa na vipimo vingine ulivyopitia au kukawa na matatito ya kurithi ambayo si ya kupata tiba timilifu/yakaisha. Pia, mfumo wa maisha ukayafanya matatizo yako kuwa yanajitokeza zaidi.

Kwa maelezo yako kuna vitu najifunza na naomba pia ujifunze:

1: Maelezo yako ndo mwanzo wa tiba yako sahihi.

Kwa mtoa huduma yoyote ni vyema kuanza na basic, jinsi ugonjwa ulivyoanza. Ikibidi andika dalili zako zote/maelezo kabla ya kwenda kwa mtoa hudima. Usiwe na haraka ya kumaliza kujieleza.

2: Eleza kwa ufasaha jinsi tumbo linavyouma, sehemu husika.

3: Eleza mahusiano na njaa, chakula na upataji wako wa choo na jinsi choo kinavyokuwa.

4: Eleza kama kwenye familia ndugu vs wazazi wana tatizo kama lako.

5: Eleza aina ya dawa na vipimo ulivyowahi kufanya na majibu kama unayo au unayafahamu.

6: Jibu maswali ya mtoa huduma vyema bila kujali kama kwa mtizamo wako yatamsaidia kujua tatizo au hapana.
Nashukuru kwa ushauri,nitaufanyia kazi
 
Hali bado,rufaa Mbeya wanadai huenda nina vidonda vya tumbo.Toka 2017 walinianzishia clinic ya medicine ndipo nahudhuria hadi leo dawa wanazonipa ni nyingi sana kiasi kwamba nimeamua kutozimeza kwa sababu madaktari wenyewe wanapingana.Hali bado ni tete
Pole sana, jaribu kutumia glucose uone kama utapata nafuu.
 
Kama una imani, nenda Dar Kawe Tanganyika Packers kwa Mtume Mwamposa. Piga kambj ya mwezi mmoja njoo utoe ushuhuda hapa JF
 
Back
Top Bottom