Baada ya kumsafirisha mke najisikia amani, furaha na wepesi wa kutosha. Ndoa inahitaji umakini usiomithilika

Baada ya kumsafirisha mke najisikia amani, furaha na wepesi wa kutosha. Ndoa inahitaji umakini usiomithilika

Na kuna wanaume wanaowapata wanawake ambao hawana tabia hata moja hapo halafu wao ndio wanazingua.

Maisha hayana usawa!
Kweli kabisa! Nina shemeji yangu aliukwaa mkenge akapata janaume la hovyo hovyo sijawahi kuona! Binti moja maridadi sana na ana cheo chake benki yaani sisi wanaume!!
 
Umuofia kwenu!!

Kama mada ilivyo, nimempeleka kwanza kwao kwa muda usiopungua miezi miwili.....akajifunze kitu (kama ni mwenye kujifunza). Siku moja tu baada ya kutoka kwake;

1. Leo kwa mara ya kwanza, katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu, nimefanikiwa kutulia nyumbani saa mbili usiku na kuangalia taarifa ya habari mwanzo mwisho. Kabla, ilikuwa sikai maana nikibadilisha channel tu na kuweka kituo changu pendwa cha Star TV kuangalia taarifa basi manung'uniko yenye kukera huanza kukimbizana kutoka nje ya kinywa chake.

"Tutaacha vp kubadilishiwa channel wakati TV sio yetu na hata bei yake hatuijui..."

"Hata kuzima we zima tu, nini kubalisha channel" Dah

2. Nimepumzika kushuhudia mabega na makwapa ya mke wangu yakionwa na watoto muda wote awapo nyumbani. Jitihada za kumrekebisha ili aendane na desturi yangu, daima huenda sambamba na ugomvi.

3. Nimepumzika kuona sura ya kununanuna pale ninapotoa maelekezo.

4. Udokozi wa vielfu tano tano vyangu katika tigopesa yangu utakoma kwa muda.

5. Nitapumzika kusikia matusi kama 'nyoko we' n.k yanayotolewa kwa watoto kila siku.

6. Nitafurahia vichenji vinavyobaki katika matumizi madogomadogo na kuziweka mezani. Kwa kawaida hivi hutoweka dakika moja tu baaada ya kuviweka, hata kama akiwa amelala basi huamka ghafla na kuvichukua kisha kulala tena.

Mbona nina furaha sana sasa?!!! Atarudi kweli? Arudi ili nije kupata stress tena?

Ndoa..........mh!
Huko alikoenda watoto wa mbwa watamgonga wamle hadi mifupa na akirudi kwako amechoka. Usijaribu kufanya hili sio jambo zuri. Kama unamuacha muache moja kwa moja asirudi.
 
Katika vitu nimejiandaa kuingia navyo kwenye mahusiano ni kumiliki uchumi wangu binafsi wa kifedha.
Nitazinguana na mwenzi wangu kwa issue nyingine sio za kifedha, Inshort mwenyewe najimudu. Hizo zake ni km za ziada.
Mwanamke anayesachi pesa kwenye suruali ya mumewe namshauri atoke maghetoni.
Kuchukua hela ya mwenzio owe mzazi, mume , mke bila kumuambia ni wizi . Hakuna sababu ya msingi eti ohh humpi hela. Mimi hata uache sh. ngapi, kama kuna matumizi ya lazima nitakuambia hata kabla sijachukua. Unawezaji kusachi mfuko wa mwenza wako na kuchukua hela bila taarifa?
 
Huyo mke itakuwa ulimpaa mimba ndo ukalazimishwa kuoa mkuu
Umeamua kuongeza idadi ya single mothers bila aibu?
 
Ni kuvumilia mkuu. Mimi tangu jana nina homa kali, asubuhi nimeamka nipo hovyo nikaomba wife anitengenezee tangawizi aise akaanza kurap huoni nafanya usafi! Yaani nyumba hii Kila kitu Mimi! Mtoto akaomba maji akaambiwa Kwa kufoka kanywe bombani!

Unajua usipokua mvumilivu ni unavunja mtoto wa watu.

Nikainuka nimempa mtoto maji nikajitengenezea tangawizi yangu, jioni hii yupo kawaida anaongea vizuri
 
Kuchukua hela ya mwenzio owe mzazi, mume , mke bila kumuambia ni wizi . Hakuna sababu ya msingi eti ohh humpi hela. Mimi hata uache sh. ngapi, kama kuna matumizi ya lazima nitakuambia hata kabla sijachukua. Unawezaji kusachi mfuko wa mwenza wako na kuchukua hela bila taarifa?
Tena sio tabia nzuri!!
Kwanini usimwambie naomba? Mwanaume km hataki kufanya majukumu yake na fedha anayo ni kumshtaki ebooh!!
Na kingine wanawake na sisi tufanye hata biashara ndogo ndogo, tuepuke kero na unyanyasaji wa wanaume wapumbavu.
 
Iwe jumla hiyo mkuu. Ndoa ni utapeli mkubwa ona sasa ulivyokuwa unatapeliwa mda mchache tu wa kuwa single umekuwa na amani. NDOA NI UTAPELI
 
Back
Top Bottom