Baada ya Malalamiko ya wananchi, Serikali yasitisha bei mpya za vifurushi

Baada ya Malalamiko ya wananchi, Serikali yasitisha bei mpya za vifurushi

Habari zilizo teka mitandao na nje ya mitandao ni taarifa ya vifurushi vilivyo badilishwa.
Hii ilinilazimu kuandaa uzi maalumu usemao Tanzania tupaze sauti kupinga mfumo wa vifurushi vipya
Kwa namna moja au nyingine nilionekana kama naropoka tu.
Lakini siku ya leo mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA wameliona hilo na kuja na taarifa hizi👇
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala, amesema matumizi ya bei mpya ya vifurushi yamesitishwa kwa muda.



Hata hivyo, amesema uamuzi huo utahusu vifurushi vya data pekee huku vile vya ujumbe mfupi wa maneno na kupiga zitaendelea kama ilivyotangazwa mapema leo Ijumaa.



“Tumesitisha matumizi ya gharama mpya za vifurushi hadi hapo itakapotangazwa baadaye. Lakini, hili litahusu vifurushi vya data pekee na vile vya sms na kupiga vitaendelea kama kawaida,” amesema Mwakyanjala alipozungumza na Mwananchi kwa njia ya simu dakika chache zilizopita.



Kanuni ndogo za gharama na tozo za vifurushi, utangazaji wa huduma na ofa maalum zilizotungwa na TCRA, zimeanza kutumika leo ambapo, matumaini ya wengi ilikuwa ni bei za vifurushi kupungua lakini ikawa tofauti.


Sauti yetu imesikika.
Habari haina ukweli wowote ipuuzwe.
Hadi muda huu tigo sh 1500 unapata mb 300
 
Hawakusikia kilio chenu.
Ni amri toka juu.
Simu moja tu jamaa walirudi ofisini japo ilikua sikukuu halafu usiku.
 
Friday April 02 2021

Mwananchi Gazeti

Dar es Salaam. Saa chache baada ya kutangazwa kwa bei mpya za vifurushi, Serikali imetangaza kusitisha kutumika kwa gharama hizo hadi hapo itakapotangazwa baadaye.

Uamuzi huo unaweza kuwa habari njema kwa watumiaji wa mitandao ya simu ambao, tangu kutangazwa kwa bei hizo mpya mapema leo Ijumaa ya Aprili 2, 2021, wamekuwa kwenye mjadala mzito kwani, matarajio ya wengi ilikuwa ni kushuka kwa gharama hizo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala, amesema matumizi ya bei mpya ya vifurushi yamesitishwa kwa muda.

Hata hivyo, amesema uamuzi huo utahusu vifurushi vya data pekee huku vile vya ujumbe mfupi wa maneno na kupiga zitaendelea kama ilivyotangazwa mapema leo Ijumaa.

“Tumesitisha matumizi ya gharama mpya za vifurushi hadi hapo itakapotangazwa baadaye. Lakini, hili litahusu vifurushi vya data pekee na vile vya sms na kupiga vitaendelea kama kawaida,” amesema Mwakyanjala alipozungumza na Mwananchi kwa njia ya simu dakika chache zilizopita.

Kanuni ndogo za gharama na tozo za vifurushi, utangazaji wa huduma na ofa maalum zilizotungwa na TCRA, zimeanza kutumika leo ambapo, matumaini ya wengi ilikuwa ni bei za vifurushi kupungua lakini ikawa tofauti.

Mwanzoni mwa Machi, 2021 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba aliahidi utekelezaji wa kanuni hizo za kukabiliana na malalamiko juu ya huduma ya vifurushi yaliyotokana na maoni 3, 278 yaliyotolewa na wananchi.

Baadhi ya changamoto ambazo watumiaji wa huduma za simu walikuwa wakikutana nazo na kuzilalamikia ni pamoja na gharama za vifurushi kuwa juu na vifurushi vya data kubadilika mara kwa mara.

Jana mitandao ya simu iliwataarifu watumiaji wake juu ya mabadiliko hayo, lakini jambo ambalo limewaibua wengi hususani katika mitandao ya kijamii ni kuminywa kwa vifurushi hivyo kuliko hata ilivyokuwa awali wakati wanatoa malalamiko hayo.

Katika makundi ya mtandao wa kijamii wa WhatsApp na mitandao mingine ya kijamii inayokutanisha watu kama Twitter, Instagram na Facebook mjadala ni vifurushi ambavyo vimebadilika katika mitandao yote ya huduma za simu wengi wanaomba walau hali irudi kama ilivyokuwa.

Mitandao mbali ya simu kama ilivyo ada katika sikukuu mbalimbali ilituma salamu zao za sikukuu kupitia kurusa zao za mitandao ya kijamii, lakini maoni ya wananchi wengi si kupokea salamu hizo bali ilikuwa ni kulalamikia mabadiliko yaliyofanywa katika vifurushi.

Zaidi, soma: Tanzania na Vifurushi vipya vya Data na Sauti (Aprili 2021) - Mwitikio wa wananchi
View attachment 1741566
Nilitaka kumsaidia huyo Waziri wa Teknolojia..... ha ha ha.... Wayonge tutaahidiwa mengi sana.... Mara Mkongo wa Taifa utashusha gharama za mtandao... Gesi ya Mtwara itapunguza gharama za gesi.... leo Bwawa la Nyerere litapunguza gharama za umeme..... Wayonge wenzangu tuendelee kusubiri.... Nashauri mwenendo huu wa kusubiri reaction ya wananchi.... mtakuwa mnajiwekea mazingira magumu kuongoza.... Hii ni zahiri kuwa wayonge hawakuhusisha ktk kutoa maoni.... Big up Wananchi Wayonge TZ.
 
Ukiangalia hizo bei zilizokuwa zianze kutumika,inabidi useme asante Mungu kwa kutuweka kwenye maombolezo
 
ME NAJIULIZA TU ILIKUWAJE MBAKA WAKAWEKA TASWIRA HII KWENYE VIFURUSHI,SABABU HASA ILIKUWA MAPATO AU KUKOMOA?
 
Na mafuta jamani,yamepotea especially ya alizeti na ukiyakuta hiyo bei balaa lita 5 elf 30 badala ya elf 22
Duh! Majuzi nimeenda dukani nimekuta lita 3 sh. 22,000! Kwa mara ya kwanza nami nikagundua kwamba "kumbe mimi ni mnyonge" manake kwa unyooonge, nikamwambia shopkeeper "nipe hayo..." nikimaanishe anipe Korie ambayo nilishayasahau yanafananaje!!
 
Baada ya serikali kutoa tangazo la kusitisha bei mpya ya vifurushi hasa vya data bado makampuni yamekaza shingo yameongeza bei na hayajarudisha kama ilivyokuwa awali huku suala hili likitafutiwa suluhisho . Je jeuri hii inatoka wapi?

Kabisa sioni kama wametekeleza agizo la serikali ,mpaka sasa bei ni ile ile ya kuumiza....Naangalia hapa voda 1000 ni 300MB.
 
Hebu acheni Upuuzi wenu na kutaka kuwapa Sifa ( Kiki ) za Kipumbavu hawa TCRA wenu.

Hivi anayesikia Kilio anatakuwa azuie ( arekebishe ) Jambo kabla halijawa katika Utekelezaji wake au anaruhusu litokee kisha likishawaumiza wengi ndiyo anajifanya Kujitokeza Kukutetea?

Msidhani Watanzania ni Wapuuzi hivyo.
Hawa TCRA wapumbavu tu. Mabadiliko ya vifurushi kwa mitandao yote hayajatokea kwa bahati mbaya, walikaa mezani wote na wakapanga hizo bei. Halafu eti leo wanajifanya wamesikia kilio chetu.
 
Hakuna utatuzi walioufanya hapo zaidi ya kurudisha tatizo la mwanzo lililokuwa linalalamikiwa.

Mh. Dr Faustine Ndugulile hajawahi kufanya jambo lolote la kuonekana katika Wizara yoyote aliyokuwa. Akiwa Wizara ya Afya huduma zilikuwa mbovu, watoa huduma ni miungu watu na wizi wa dawa kila mahali. Alikuwepo tu. Hana hata kimoja cha kuonesha alichosimamia.

Hata hii wizara mpya hatofanya lolote la maana zaidi ya kuharibu tu.
 
Mzee alisema mtanikumbuka kwa mazuri.
IMG-20210403-WA0007.jpg
 
Haya yipangwa akiwepo na sio kwa ajili ya Mama,
Hayo makubaliano na hao watu wa mitandao na TCRA yalifanyika mwezi gani!?
 
Yaani umekaa hapo unawaza upuuzi wako halafu unalazimisha huo upuuzi yawe ndio mawazo ya watu wenye akili timamu[emoji849][emoji849]

Tumkwamishe ili wewe ndio uwe rais??

Wewe ndio ulimteua kuwa makamu wa rais mara ya kwanza na ya pili? Wewe ndio uliwateua mawaziri na mabalozi waliopo?

Hebu kapambane na Tundu au tulizana.....!!

Nchi yetu iko imara sana
Chama cha mapindunzi kiko imara
Serikali ya Tanzania iko imara

Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote [emoji7][emoji1241][emoji91]

Rest well our hero President John Pombe Joseph Magufuli [emoji885]
Mlizoea kuuza maneno ya fitina, kuhakikisha kuwa hakuna amani nchini ili muendelee kujipatia ridhiki kwa unafiki wenu.

Leo hii kaingia mama wa kazi asiyeendekeza majungu na fitina hivyo nyinyi mlio zoea kuuza majungu na fitina hamna nafasi tena.

Watu hawaichukii ccm kama jina,no bali watu wanachukia wanao kiongoza hicho chama na sasa chama kimepata kiongozi mwenye maono na moyo wa upendo kwa watanzania.

Nyinyi MATAGA ebu kaeni pembeni ili msimkwamishe mama yetu maana nyinyi ni masalia na hamna nia njema kwa mama yetu.
 
Mlizoea kuuza maneno ya fitina, kuhakikisha kuwa hakuna amani nchini ili muendelee kujipatia ridhiki kwa unafiki wenu.

Leo hii kaingia mama wa kazi asiyeendekeza majungu na fitina hivyo nyinyi mlio zoea kuuza majungu na fitina hamna nafasi tena.

Watu hawaichukii ccm kama jina,no bali watu wanachukia wanao kiongoza hicho chama na sasa chama kimepata kiongozi mwenye maono na moyo wa upendo kwa watanzania.

Nyinyi MATAGA ebu kaeni pembeni ili msimkwamishe mama yetu maana nyinyi ni masalia na hamna nia njema kwa mama yetu.

Nani kakuambia alikua anauza maneno ya fitna!? Unajua mtu anayewaza mambo yasiyokuwepo na kutunga mambo na kuyashikia bango pamoja na kuyasambaza kama wewe anaitwaje!?

Wacha umbea na majungu basi, unashusha heshma yako bure
 
Sio kweli menu imebadilika imerudi kama zamani hapa
Naona Eatel inanigomea hapa kila nikitaka kuingia kwa *150*60# au *149*99# inaniandikia Not registerd on network nazan wapo kwene hayo marekebisho yavifurushi virudi kama zamani
 
Nani kakuambia alikua anauza maneno ya fitna!? Unajua mtu anayewaza mambo yasiyokuwepo na kutunga mambo na kuyashikia bango pamoja na kuyasambaza kama wewe anaitwaje!?

Wacha umbea na majungu basi, unashusha heshma yako bure
Wacha niishushe tu kama kuwasema nyinyi wanafiki wacha ishuke.
Nyinyi MATAGA ni wanafiki na hatutakubali kikundi chenu kimuharibie mama yetu .

Kama mmeona mmekwama hameni kabisa nchi.
Maana mmeshaanza kuomba samahani kwa mliyo watendea watanzania.

Mbona hamkuomba hiyo samahani kwenye utawala wa jiwe?
Naona mmeanza kujua kuwa kila mweupe siyo mzungu.
 
Back
Top Bottom